CONTROLA
JF-Expert Member
- Sep 15, 2019
- 7,001
- 23,449
Biashara zina mbinu nyingi sana za uendeshwaji kila mtu anatumia mbinu yake ili kupata wateja wake ila huwa nawambiaga watu kila siku ktk biashara hamna kitu kirahisi kama kupata mteja/wateja,yani katika vitu huwa virahisi hicho ni namba 1.
Shida/mtihani/mziki huja wapi unajua? Kumfanya yule mteja aliekuja kwako leo kununua sukari wiki ijayo sukari yake ikiisha arudi tena hapo hapo dukani kwako kununua sukari,Kumfanya yule mteja uliemshonea nguo leo,kesho pia akitaka kushona nguo ingine afikirie kurudi hapo hapo ofisini kwako kushona.
Kuna mambo mengi ambayo humfanya mteja arudi kupata huduma ofisini kwako,leo tuongelee hili swala la imani zetu za dini tulizonazo/tulizokuzwa nazo tangu utoto mpk sasa tumejitambua tumekua watu wazima,nitaweka tabia chache tu ambazo si nzuri kwa mfanyabiashara
Kufungulia Mahubiri/mawaidha
Ni kweli nafahamu wewe ni mlokole kweli tena umekuzwa katika maadili ya ulokole na utakatifu tangu utoto wako na najua jinsi gani unatamani kuwa karibu na Mungu wako wakati wote unapotembea/unapokaaa/unapopiita nk nk,na tena nafahamu wewe ni muislamu swafi kabisa usie na mawaa na wala hua ujinga wowote ktk maisha yako ila linapokuja swala la biashara tujue kutofautisha A na B,biashara na imani yako ni vitu viwili tofauti.
Mtu anafungua ofisi yake asubuhi na siku hizi Tangu flash ziingie ndio balaa,bora zamani ilikua mtu anaweka Radio station kuna ule muda wa matangazo hata mteja akiingia anajua hii radio,ila siku hizi unakuta mtu ana flash yake kaijaza mawaidha/mahubiri halafu sasa akiingia kazini anachomeka kwenye radio yake ofisini panageuka kanisani/msikitini kelele mwanzo mwisho,mahubiri anatoka mwakasege anaingia rwakatare,anafata gwajima,anakuja mwamposa yani Hamna Poo.
huku kwingine ni DUA au Mawaidha yanatoka ya dokta sule,anafata kipoozeo,anakuja othman maalim anakuja kishki yani ni bandika bandua ukiingia dukani/ofisini kwa mtu unakua huelewi yani unavurugwa tu yani kwa mfano mimi ninapoingia duka la mtu wa namna hii bila kujali n mkristu mwenzangu au muislamu huwa naweza jikuta naghairi natoka natafuta duka lingine.
Kufungulia Nyimbo za imani yako
Unaingia mahali unapokelewa na kaswida,kwaya,nk ki ukweli sisemi ni vibaya kuburudika ofisini kwako na nyimbo uzipendazo lakini kumbuka hapo n kwenye biashara na sio kwako,ukiwa nyumbani kwako pga kasidah/kwaya/mahubiri hadi chooni hutoskia mtu anaongea kitu kwasababu kule ni kwako,lakini tunapokuja huku kwenye biashara tambua hapo si kwako mwenye pake ni mteja wako.
Unajiskiaje mwenye eneo lake "mteja" kaingia (ni mkristu aliye kwiva kbsa) anakukuta unaskiliza mawaidha yale ya waislamu wakisema wakristu ni makafir kisha wanachangia kwa maneno yao yale ya ajabu ajabu,hv unafkiri huyu mteja akiskia unategemea next time atarudi kwenye hilo duka au hiyo ofisi kupata huduma? Sahau.
Unajiskiaje mwenye eneo lake "mteja" kaingia (ni muislamu wale wa itikadi kali) anakuta unaskiliza mahubiri ya hawa wahubiri wasio na break midomoni anasema "waislamu wote wana mapepo,waje kwa yesu awaokoe" hivi huyu mteja akaingia akakutana na hiki kipande unafikiri kesho yake kama anataka sukari imeisha kwake atarudi hapo kwako? sahau Anaweza kunywa hata maji na mkate nakuhakikishia.
Kuchoma/kufukiza UDI
Hii sijui maana yake nini lakini kusema ukweli ktk vitu nachukia mpaka nashkwa na kitu kooni ni pale ninapoenda sehemu ya mtu ya biashara halafu nasikia harufu za namna hii ki ukweli inakera inaboa na inaudhi,kama ni masharti ya waganga hebu ombeni waganga wawabadilishie hayo masharti maana ki ukweli wateja wengi huchukizwa na hicho kitu ni basi tu hawawezi kukwambia.
Imani zetu tujaribu kuzitenganisha na biashara zetu,tufahamu kwamba biashara si mali zetu,una duka la TV fahamu kwamba hizo TV si zako n za wateja zingekua zako ungezipeleka kwako lakini kwakua umefahamu sio zako umeamua kufungua frem ili mwenye tv yake aje ifata siku atakayoamua yeye,sasa kwanini unatengeneza mazingira ya ki ubaguzi kwenye ofisi yako?
unajua kuna watu hawapendi hata kuwasiliana na mtu ambae ni tofauti nae kiimani achilia mbali kununua bidhaa yake,humjui mteja wako n wa aina gani na atakuja vipi nadhani ni vyema unapokua ktk biashara uwe Neutral,simama kati kati akija muislamu msalimie kiislamu kama unajua kusalimia,akija mkristo msalimie ki kristo kama n mtu mpenda hzo salamu,kaa hapo kati kati.
Usiwatenge wateja wako na imani yako,wewe amini unachokiamini,Muamini unaemuamini lakini unapokuja kazini STAY NEUTRAL epuka kuweka/kuonyesha alama zozote za dini flani ktk eneo lako la biashara,usije ukasema hukuambiwa na kama unaona nina gubu sawa kama haikufai iache hapa hapa. END.
Shida/mtihani/mziki huja wapi unajua? Kumfanya yule mteja aliekuja kwako leo kununua sukari wiki ijayo sukari yake ikiisha arudi tena hapo hapo dukani kwako kununua sukari,Kumfanya yule mteja uliemshonea nguo leo,kesho pia akitaka kushona nguo ingine afikirie kurudi hapo hapo ofisini kwako kushona.
Kuna mambo mengi ambayo humfanya mteja arudi kupata huduma ofisini kwako,leo tuongelee hili swala la imani zetu za dini tulizonazo/tulizokuzwa nazo tangu utoto mpk sasa tumejitambua tumekua watu wazima,nitaweka tabia chache tu ambazo si nzuri kwa mfanyabiashara
Kufungulia Mahubiri/mawaidha
Ni kweli nafahamu wewe ni mlokole kweli tena umekuzwa katika maadili ya ulokole na utakatifu tangu utoto wako na najua jinsi gani unatamani kuwa karibu na Mungu wako wakati wote unapotembea/unapokaaa/unapopiita nk nk,na tena nafahamu wewe ni muislamu swafi kabisa usie na mawaa na wala hua ujinga wowote ktk maisha yako ila linapokuja swala la biashara tujue kutofautisha A na B,biashara na imani yako ni vitu viwili tofauti.
Mtu anafungua ofisi yake asubuhi na siku hizi Tangu flash ziingie ndio balaa,bora zamani ilikua mtu anaweka Radio station kuna ule muda wa matangazo hata mteja akiingia anajua hii radio,ila siku hizi unakuta mtu ana flash yake kaijaza mawaidha/mahubiri halafu sasa akiingia kazini anachomeka kwenye radio yake ofisini panageuka kanisani/msikitini kelele mwanzo mwisho,mahubiri anatoka mwakasege anaingia rwakatare,anafata gwajima,anakuja mwamposa yani Hamna Poo.
huku kwingine ni DUA au Mawaidha yanatoka ya dokta sule,anafata kipoozeo,anakuja othman maalim anakuja kishki yani ni bandika bandua ukiingia dukani/ofisini kwa mtu unakua huelewi yani unavurugwa tu yani kwa mfano mimi ninapoingia duka la mtu wa namna hii bila kujali n mkristu mwenzangu au muislamu huwa naweza jikuta naghairi natoka natafuta duka lingine.
Kufungulia Nyimbo za imani yako
Unaingia mahali unapokelewa na kaswida,kwaya,nk ki ukweli sisemi ni vibaya kuburudika ofisini kwako na nyimbo uzipendazo lakini kumbuka hapo n kwenye biashara na sio kwako,ukiwa nyumbani kwako pga kasidah/kwaya/mahubiri hadi chooni hutoskia mtu anaongea kitu kwasababu kule ni kwako,lakini tunapokuja huku kwenye biashara tambua hapo si kwako mwenye pake ni mteja wako.
Unajiskiaje mwenye eneo lake "mteja" kaingia (ni mkristu aliye kwiva kbsa) anakukuta unaskiliza mawaidha yale ya waislamu wakisema wakristu ni makafir kisha wanachangia kwa maneno yao yale ya ajabu ajabu,hv unafkiri huyu mteja akiskia unategemea next time atarudi kwenye hilo duka au hiyo ofisi kupata huduma? Sahau.
Unajiskiaje mwenye eneo lake "mteja" kaingia (ni muislamu wale wa itikadi kali) anakuta unaskiliza mahubiri ya hawa wahubiri wasio na break midomoni anasema "waislamu wote wana mapepo,waje kwa yesu awaokoe" hivi huyu mteja akaingia akakutana na hiki kipande unafikiri kesho yake kama anataka sukari imeisha kwake atarudi hapo kwako? sahau Anaweza kunywa hata maji na mkate nakuhakikishia.
Kuchoma/kufukiza UDI
Hii sijui maana yake nini lakini kusema ukweli ktk vitu nachukia mpaka nashkwa na kitu kooni ni pale ninapoenda sehemu ya mtu ya biashara halafu nasikia harufu za namna hii ki ukweli inakera inaboa na inaudhi,kama ni masharti ya waganga hebu ombeni waganga wawabadilishie hayo masharti maana ki ukweli wateja wengi huchukizwa na hicho kitu ni basi tu hawawezi kukwambia.
Imani zetu tujaribu kuzitenganisha na biashara zetu,tufahamu kwamba biashara si mali zetu,una duka la TV fahamu kwamba hizo TV si zako n za wateja zingekua zako ungezipeleka kwako lakini kwakua umefahamu sio zako umeamua kufungua frem ili mwenye tv yake aje ifata siku atakayoamua yeye,sasa kwanini unatengeneza mazingira ya ki ubaguzi kwenye ofisi yako?
unajua kuna watu hawapendi hata kuwasiliana na mtu ambae ni tofauti nae kiimani achilia mbali kununua bidhaa yake,humjui mteja wako n wa aina gani na atakuja vipi nadhani ni vyema unapokua ktk biashara uwe Neutral,simama kati kati akija muislamu msalimie kiislamu kama unajua kusalimia,akija mkristo msalimie ki kristo kama n mtu mpenda hzo salamu,kaa hapo kati kati.
Usiwatenge wateja wako na imani yako,wewe amini unachokiamini,Muamini unaemuamini lakini unapokuja kazini STAY NEUTRAL epuka kuweka/kuonyesha alama zozote za dini flani ktk eneo lako la biashara,usije ukasema hukuambiwa na kama unaona nina gubu sawa kama haikufai iache hapa hapa. END.