Usidhani shetani ni mdogo kama unavyofikiri

Usidhani shetani ni mdogo kama unavyofikiri

Hoja yangu ni hivi, kwakua Yesu alisulubishwa vibaya alipokuwa akijaribu kumpinga Shetani basi Shetani sio wa kuingia nae vitani, Ikiwa Yesu pamoja na nguvu zake zote alipata adhabu yote ile basi sisi binadamu ni akina nani hata tuthubutu kuanzisha vita na Shetani?
Hukunielewa mkuu. Ninajaribu kukutahadharisha kwamba wapo watu wengine wanaofuatilia na kusoma haya mahojiano baina yangu na wewe.

Wasomaji hao wengine(sio mimi tu) humpima mtu kwa jinsi anavyojibu maswali au hoja zinazoelekezwa kwake (vijana wa cku hizi wanaita Kumchora mtu).

Mwisho wa siku wanahitimisha kwa kuku-grade kwamba huyu jamaa ni e.g. jembe, ana madini, boya, kilaza, waKupuliza, domo zege, n.k. ndo maana nikasema chukua Tahadhari.
 
Kuna baadhi ya watu wanadhani shetani ni jambo dogo, ile ni nguvu kubwa iliyoshinda binadamu wote. Utakapojaribu kuingia kwenye ugomvi na yeye ndipo utatambua kuwa unajaribu kupigana na jambo usiloweza. Kwa reference fupi, wapo mitume waliojaribu kupambana naye wakaishia kupata adhabu kali zisizoelezeka.

Wakwanza ni Yesu, mwana wa Mungu alipojaribu kupambana nae aliishia kusulubishwa. Ayubu mcha Mungu alipata kipigo kikali sana alipomcha Mungu, Adam na Hawa pamoja na utashi wao wote walitiwa kwenye 18, mitume ikiwemo Stephano walipigwa na mawe mpaka kufa walipoingia kwenye vita na shetani.

Unaposema unataka vita na shetani labda pepo ila sio shetani aliyemsulubisha Yesu, vinginevyo utaishia kuchapwa kipigo kitakatifu.
Jiulize je, kama Yesu na nguvu zake zote alisulubishwa vibaya sana wewe atakufanyia jambo gani?
Vp kuhusu mtume Muhammad (S.A.W)? Ajapambna na shetani
 
Vp kuhusu mtume Muhammad (S.A.W)? Ajapambna na shetani
Mtume Muhammad alitumia busara kubwa sana kufundisha mema, alikua mjanja sana hakutaka vita na Shetani, wala binadamu muovu yeye alikua anawaeleza watu habari nzuri za Mungu wala hakutaka vita nao.

Ndio maana katika mahubiri yote yanayofanywa na Waislamu, yanaeneza amani hutawahi kusikia Imamu wala Sheikh akisema anampiga Shetani lakini hawa wengine mfano wachungaji wanadai kuwa wanampiga Shetani katika mahubiri yao, wewe unampigaje? kwanza hulingani nae kwa chochote, yupo tangu binadamu wa kwanza hajaumbwa, leo hii uzaliwe wewe umpige? Haingii akilini hata kidogo.

Natoa mfano rahisi- Jeshi la Tanzania linapigana na Jeshi la nchi nyingine na hutawahi kuona Jeshi la Tanzania likipigana na mgambo wa mtaa. Yaani Jeshi la Tanzania liwashe vifaru vyote na mizinga yote likapigane na mgambo wa mtaa? Huo utakuwa ni ujinga uliopitiliza na wala hutawahi kuona popote pale.
Binadamu akisimama na Shetani ni sawa na tembo na kuku.

Labda niseme hivi, nikwasababu tu Shetani anaona hawa hakuna wajuacho na wala hapigani vita na kuku lakini angeamua kuwamaliza ni kitendo cha dakika sifuri. Nasema hivi kwasababu kama Yesu alimalizwa wao ni akina nani awashindwe.

Yesu alieneza habari za Mungu kwa hasira kubwa ndio maana alichukua kiboko akawatandika wale wote waliokuwa wakifanya biashara kwenye hekalu la Mungu na kutangaza vita na Shetani hapo ndipo wazee wa mahekalu wakajawa na hasira kali na kumkamata.
 
Mtume Muhammad alitumia busara kubwa sana kufundisha mema, alikua mjanja sana hakutaka vita na Shetani, wala binadamu muovu yeye alikua anawaeleza watu habari nzuri za Mungu wala hakutaka vita nao.

Ndio maana katika mahubiri yote yanayofanywa na Waislamu, yanaeneza amani hutawahi kusikia Imamu wala Sheikh akisema anampiga Shetani lakini hawa wengine mfano wachungaji wanadai kuwa wanampiga Shetani katika mahubiri yao, wewe unampigaje? kwanza hulingani nae kwa chochote, yupo tangu binadamu wa kwanza hajaumbwa, leo hii uzaliwe wewe umpige? Haingii akilini hata kidogo.

Natoa mfano rahisi- Jeshi la Tanzania linapigana na Jeshi la nchi nyingine na hutawahi kuona Jeshi la Tanzania likipigana na mgambo wa mtaa. Yaani Jeshi la Tanzania liwashe vifaru vyote na mizinga yote likapigane na mgambo wa mtaa? Huo utakuwa ni ujinga uliopitiliza na wala hutawahi kuona popote pale.
Binadamu akisimama na Shetani ni sawa na tembo na kuku.

Labda niseme hivi, nikwasababu tu Shetani anaona hawa hakuna wajuacho na wala hapigani vita na kuku lakini angeamua kuwamaliza ni kitendo cha dakika sifuri. Nasema hivi kwasababu kama Yesu alimalizwa wao ni akina nani awashindwe.

Yesu alieneza habari za Mungu kwa hasira kubwa ndio maana alichukua kiboko akawatandika wale wote waliokuwa wakifanya biashara kwenye hekalu la Mungu na kutangaza vita na Shetani hapo ndipo wazee wa mahekalu wakajawa na hasira kali na kumkamata.
Mkuu, naomba nikunukuu ......hutawahi kusikia Imamu wala Sheikh akisema anampiga Shetani lakini hawa wengine mfano wachungaji wanadai kuwa wanampiga Shetani katika mahubiri yao,................. Yesu alieneza habari za Mungu kwa hasira kubwa ndio maana alichukua kiboko akawatandika wale wote waliokuwa wakifanya biashara kwenye hekalu la Mungu na kutangaza vita na Shetani hapo ndipo wazee wa mahekalu wakajawa na hasira kali na kumkamata.
Naomba unifafanulie haya yafuatayo:
1. Hivi wale mahujaji (Hija)kuna siku hufanya Ibada ya kutupa jiwe/mawe (kokoto saba)katika bonde la Minah. Hapo huwa wanamrushia nani hayo mawe?

2. Hebu chukulia kwamba wewe ungekuwa ni Yesu. Katika Hekalu au mahali pa kuabudia huwa kuna Taratibu za kuzingatia uwapo mahali hapo na pia ni mahali panapostahili Heshima ya kipekee(Hii hata katika Misikiti ipo na inazingatiwa ipasavyo).

Sasa ikitokea watu kwa makusudi wanakiuka utaratibu huo na wala hawaheshimu mahali hapo panapotumika kumwabudu Mungu wewe kama Yesu Ungelifanyaje kwa sababu pameshakuwa au pamegeuzwa ni kama sokoni, gulioni au mnadani - hata ukipaza sauti hutosikika.

Hatua ya Yesu kuchukua kiboko ichukuliwe kama inavyokuwa kwa mzazi anayemuonya mwanae ampendaye au mwalimu anayefundisha wanafunzi wake.

****Kuna Upotoshaji mkubwa katika maelezo yako unapotumia neno Hasira Kubwa.
Mkuu hebu soma tena Marko 11: 15-24 Hakuna neno au haijaandikwa kwa Hasira kubwa.

"Yesu aliingia Hekaluni akaanza kuwafukuza watu waliokuwa wakifanya biashara humo. Akapindua meza za waliokuwa wakibadilisha fedha na viti .."
Kwa hiyo hata leo ingekuwa ni Msikiti halafu wakatokea watu fulani wakaanza kufanya biashara humo, Unadhani Sheikh au Imamu au kiongozi wa Msikiti mahalia angelikaa kimya?. Je, utasema anahasira?

3. Yesu hakukamatwa na Wazee. Yesu alikamatwa na kikosi cha Askari (Yohana 18:3-12) na kundi la watu wakiongozwa na Yuda Iskariote (Marko 14:43-49).

Mkuu, katika hali ya kawaida, Wazee na uzee wao wasingeliweza hiyo shughuli ya kukamata au sio ?

4. Mtume Mohammad(s.aw.) alitoka (alikimbia) Makka kwenda Madina......... Je, unadhani waliokuwa wakimfutilia walikuwa ni kwa jambo la Kheri au ni kwa shari?

Ni nani (Roho gani) aliyewahamasisha watu hao kuwa wakorofi vile? unadhani sio Ibilisi / Shetani? By the way, mm siijui (ni mjinga kabisa) inapokuwa ni hoja za Quran.
 
Mkuu, naomba nikunukuu ......hutawahi kusikia Imamu wala Sheikh akisema anampiga Shetani lakini hawa wengine mfano wachungaji wanadai kuwa wanampiga Shetani katika mahubiri yao,................. Yesu alieneza habari za Mungu kwa hasira kubwa ndio maana alichukua kiboko akawatandika wale wote waliokuwa wakifanya biashara kwenye hekalu la Mungu na kutangaza vita na Shetani hapo ndipo wazee wa mahekalu wakajawa na hasira kali na kumkamata.
Naomba unifafanulie haya yafuatayo:
1. Hivi wale mahujaji (Hija)kuna siku hufanya Ibada ya kutupa jiwe/mawe (kokoto saba)katika bonde la Minah. Hapo huwa wanamrushia nani hayo mawe?
2. Hebu chukulia kwamba wewe ungekuwa ni Yesu. Katika Hekalu au mahali pa kuabudia huwa kuna Taratibu za kuzingatia uwapo mahali hapo na pia ni mahali panapostahili Heshima ya kipekee(Hii hata katika Misikiti ipo na inazingatiwa ipasavyo). Sasa ikitokea watu kwa makusudi wanakiuka utaratibu huo na wala hawaheshimu mahali hapo panapotumika kumwabudu Mungu wewe kama Yesu Ungelifanyaje kwa sababu pameshakuwa au pamegeuzwa ni kama sokoni, gulioni au mnadani - hata ukipaza sauti hutosikika. Hatua ya Yesu kuchukua kiboko ichukuliwe kama inavyokuwa kwa mzazi anayemuonya mwanae ampendaye au mwalimu anayefundisha wanafunzi wake.
****Kuna Upotoshaji mkubwa katika maelezo yako unapotumia neno Hasira Kubwa.
Mkuu hebu soma tena Marko 11: 15-24 Hakuna neno au haijaandikwa kwa Hasira kubwa.
"Yesu aliingia Hekaluni akaanza kuwafukuza watu waliokuwa wakifanya biashara humo. Akapindua meza za waliokuwa wakibadilisha fedha na viti .."
Kwa hiyo hata leo ingekuwa ni Msikiti halafu wakatokea watu fulani wakaanza kufanya biashara humo, Unadhani Sheikh au Imamu au kiongozi wa Msikiti mahalia angelikaa kimya?. Je, utasema anahasira?
3. Yesu hakukamatwa na Wazee. Yesu alikamatwa na kikosi cha Askari (Yohana 18:3-12) na kundi la watu wakiongozwa na Yuda Iskariote (Marko 14:43-49).
Mkuu, katika hali ya kawaida, Wazee na uzee wao wasingeliweza hiyo shughuli ya kukamata au sio ?
4. Mtume Mohammad(s.aw.) alitoka (alikimbia) Makka kwenda Madina......... Je, unadhani waliokuwa wakimfutilia walikuwa ni kwa jambo la Kheri au ni kwa shari?
Ni nani (Roho gani) aliyewahamasisha watu hao kuwa wakorofi vile? unadhani sio Ibilisi / Shetani? By the way, mm siijui (ni mjinga kabisa) inapokuwa ni hoja za Quran.
Kitendo cha kutupa mawe katika bonde la Minah kinamaanisha kuwa mtu amechoka dhambi anajaribu kuvua madhambi yake na kutupilia mbali.

Baada ya Yesu kueneza habari za Mungu kwa muda mrefu, wakosefu hao walikerwa na kitendo chake cha kuwagusa kila mara kwa maneno makali yanayopinga matendo yao, hapo ndipo walipoanza kujawa na hasira na hata kuanza kumdharau na kubehi nyingi.

Lengo la watu wale walitaka Yesu asiwakanye wala asibadilishe yale waliyokuwa wakifanya ikiwemo kunywa vilevi, kuishi na wake wasio rasmi nakadhalika.

Bila shaka ndugu yangu nakupa tafakuri, leo hii nenda kasimame mbele ya watu uwakanye kuachana na starehe, uwazuie kunywa, kushiriki mapenzi, kumiliki mali na pesa alafu uone mapokeo yake, mimi nina uhakika watu hao hawatakuacha uishi, ndio maana vita ya kukosoa ni ngumu kuliko vita yeyote ile.

Hao utakaokuwa ukiwapiga vita lazima watahakikisha kuwa wanakushuhulikia ipasavyo ili waendelee kuishi kama watakavyo.
 
Kuna baadhi ya watu wanadhani shetani ni jambo dogo, ile ni nguvu kubwa iliyoshinda binadamu wote. Utakapojaribu kuingia kwenye ugomvi na yeye ndipo utatambua kuwa unajaribu kupigana na jambo usiloweza. Kwa reference fupi, wapo mitume waliojaribu kupambana naye wakaishia kupata adhabu kali zisizoelezeka.

Wakwanza ni Yesu, mwana wa Mungu alipojaribu kupambana nae aliishia kusulubishwa. Ayubu mcha Mungu alipata kipigo kikali sana alipomcha Mungu, Adam na Hawa pamoja na utashi wao wote walitiwa kwenye 18, mitume ikiwemo Stephano walipigwa na mawe mpaka kufa walipoingia kwenye vita na shetani.

Unaposema unataka vita na shetani labda pepo ila sio shetani aliyemsulubisha Yesu, vinginevyo utaishia kuchapwa kipigo kitakatifu.
Jiulize je, kama Yesu na nguvu zake zote alisulubishwa vibaya sana wewe atakufanyia jambo gani?
Ni wapi kwenye maandiko inasema Yesu alitaka kupambana na shetani?

Yohana10:17 - 18
Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.

Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.
 
Kitendo cha kutupa mawe katika bonde la Minah kinamaanisha kuwa mtu amechoka dhambi anajaribu kuvua madhambi yake na kutupilia mbali.

Baada ya Yesu kueneza habari za Mungu kwa muda mrefu, wakosefu hao walikerwa na kitendo chake cha kuwagusa kila mara kwa maneno makali yanayopinga matendo yao, hapo ndipo walipoanza kujawa na hasira na hata kuanza kumdharau na kubehi nyingi.

Lengo la watu wale walitaka Yesu asiwakanye wala asibadilishe yale waliyokuwa wakifanya ikiwemo kunywa vilevi, kuishi na wake wasio rasmi nakadhalika.

Bila shaka ndugu yangu nakupa tafakuri, leo hii nenda kasimame mbele ya watu uwakanye kuachana na starehe, uwazuie kunywa, kushiriki mapenzi, kumiliki mali na pesa alafu uone mapokeo yake, mimi nina uhakika watu hao hawatakuacha uishi, ndio maana vita ya kukosoa ni ngumu kuliko vita yeyote ile.

Hao utakaokuwa ukiwapiga vita lazima watahakikisha kuwa wanakushuhulikia ipasavyo ili waendelee kuishi kama watakavyo.
Exactly. Hapo Mkuu umenena UKWELI. Maelezo yako yamekaa kiuhalisia zaidi - Nimeyapenda. Hata wahenga waliwahi kusema "Wema hawadumu".

Asante kunifafanulia sababu za kutupa mawe bonde la Minah - nilikuwa sijui- nasikia ya mitaani tu. Leo nimejua ukweli.
 
Binadamu wote ni sawa ila daraja/division za kiroho kwa Mungu ni tofauti na hii hutokana na kila jitihada ya kila mmojawapo ya kumuelekea Mungu.

Binadamu ni kiumbe dhaifu na shetani ni mwenye nguvu. Ni mwenye nguvu za maumbile na ni mwenye nguvu ya kielimu; ana elimu kubwa. Binadamu hawezi kushindana na huyu!

Lakini binadamu amepewa siri; siri pekee hakuna anayeijua isipokuwa yule pekee atakayeingia kwenye mlango huo wa siri. Nabii Hizqil A.S (Ezekiel) aliaambiwa na Mungu ya kuwa yeye Mungu hatoshi kukaa kwenye mbingu saba na kwenye ardhi saba ila anatosha kukaa kwenye moyo wa binadamu na hii ndiyo siri.

Ikiwa kama unahitaji kumuweka Mungu moyoni inakubidi ufahamu utamuweka vipi! Njia pekee ni ya elimu. Elimu pekee kutoka kwa Mungu ndiyo itakayokuokoa. Maadamu yeye ndiye aliyeumba na anafahamu siri ya viumbe vyake alivyoviumba basi elimu yake itakuhabarisha kwa namna gani walivyo!

Maadamu shetani amechagua uasi elimu ya Mungu yenye siri itakufahamisha namna ya kupambana naye na ya kumdhibiti. Shetani ni mwenye nguvu kwa binadamu lakini si mwenye nguvu kwa Mungu. Hivyo, ukitaka kumshinda shetani yafuate maamrisho ya Mungu kwa maana elimu yake na utamshinda pakubwa na mifano ipo!

Kwa sababu moyo wako ukiwa safi unatakasika mpaka unafikia hatua unaungana na mwili na kuwa kitu kimoja na ukifikia hii hali unabakia kwa Mungu. Lakini yote ifahamike si kazi rahisi inahitaji kujitoa kiuhakika.

Kwa sababu binadamu amepewa mtego wa matamanio. Kwa misingi hiyo, kabla ya kuishika njia ya Mungu inakubidi uikane nafsi yako mwenyewe, uwe kama mtoto mdogo! Ukubali kuelimishwa na kuelekezeka na kuyaacha yale utakayoambiwa. Na ndiyo maana ufalme wa Mungu unahitaji watu mfano wa watoto wadogo.
 
Shetani yuko overrated sana zaid ya kutumia ujanja ujanja na utapeli hana jambo
 
Shetani ni mtu poa sana watu wanashindwa kumuelewa kuna kitu mungu anatuficha shetani anajaribu kutuambia ukweli kuhusu binadamu ni nani na kwanini tupo duniani na huu ndio ugomvi ambao mungu anamsakizia shetani
 
Mtume Muhammad alitumia busara kubwa sana kufundisha mema, alikua mjanja sana hakutaka vita na Shetani, wala binadamu muovu yeye alikua anawaeleza watu habari nzuri za Mungu wala hakutaka vita nao.

Ndio maana katika mahubiri yote yanayofanywa na Waislamu, yanaeneza amani hutawahi kusikia Imamu wala Sheikh akisema anampiga Shetani lakini hawa wengine mfano wachungaji wanadai kuwa wanampiga Shetani katika mahubiri yao, wewe unampigaje? kwanza hulingani nae kwa chochote, yupo tangu binadamu wa kwanza hajaumbwa, leo hii uzaliwe wewe umpige? Haingii akilini hata kidogo.

Natoa mfano rahisi- Jeshi la Tanzania linapigana na Jeshi la nchi nyingine na hutawahi kuona Jeshi la Tanzania likipigana na mgambo wa mtaa. Yaani Jeshi la Tanzania liwashe vifaru vyote na mizinga yote likapigane na mgambo wa mtaa? Huo utakuwa ni ujinga uliopitiliza na wala hutawahi kuona popote pale.
Binadamu akisimama na Shetani ni sawa na tembo na kuku.

Labda niseme hivi, nikwasababu tu Shetani anaona hawa hakuna wajuacho na wala hapigani vita na kuku lakini angeamua kuwamaliza ni kitendo cha dakika sifuri. Nasema hivi kwasababu kama Yesu alimalizwa wao ni akina nani awashindwe.

Yesu alieneza habari za Mungu kwa hasira kubwa ndio maana alichukua kiboko akawatandika wale wote waliokuwa wakifanya biashara kwenye hekalu la Mungu na kutangaza vita na Shetani hapo ndipo wazee wa mahekalu wakajawa na hasira kali na kumkamata.
sasa nimeelewa kwanini wanajiunga na matakwa ya shetan wanafanikiwa.
kiuhalisia wa ndani kanuni za Mungu haziishiki zaidi ya nadharia. ndo maana tunaambulia maisha ya unafiki na uzugaji kuwa tuko pamoja na Mungu.

hadi leo sielewi kwanini Mungu alimtupa shetan dunian akatawale baada ya vita kuu.

kitendo cha kuwepo VITA KALI kati ya Mungu na Bwana Shetani manake kweli sisi hatuna ubavu kwake!

Hata hivyo inafurahisha kuona hizi huwa ni story za kusadikika
 
Mkuu YESU hakuumba bali aliumbwa , Yesu Kristo ni mwana wa Mungu siyo Mungu,aliyeumba ni Mungu.

Soma vizuri hapa utaelewa:​

Yn 1:1-14​

Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza. Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana. Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye.

Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru. Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu. Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua. Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.

Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.

Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.
 
Kuna baadhi ya watu wanadhani shetani ni jambo dogo, ile ni nguvu kubwa iliyoshinda binadamu wote. Utakapojaribu kuingia kwenye ugomvi na yeye ndipo utatambua kuwa unajaribu kupigana na jambo usiloweza. Kwa reference fupi, wapo mitume waliojaribu kupambana naye wakaishia kupata adhabu kali zisizoelezeka.

Wakwanza ni Yesu, mwana wa Mungu alipojaribu kupambana nae aliishia kusulubishwa. Ayubu mcha Mungu alipata kipigo kikali sana alipomcha Mungu, Adam na Hawa pamoja na utashi wao wote walitiwa kwenye 18, mitume ikiwemo Stephano walipigwa na mawe mpaka kufa walipoingia kwenye vita na shetani.

Unaposema unataka vita na shetani labda pepo ila sio shetani aliyemsulubisha Yesu, vinginevyo utaishia kuchapwa kipigo kitakatifu.
Jiulize je, kama Yesu na nguvu zake zote alisulubishwa vibaya sana wewe atakufanyia jambo gani?
Hujasoma neno la Mungu na kulielewa kusudi lake.
1.Soma vuzuri ujue kusudi la Yesu Kristo kuja duniani.
2.Soma vizur kitabu cha Ayubu ujue alikutwa na majanga yale kwa sababu gani na mwishoni ikawaje.

Sio unasimuliwa juujuu halafu unakuja kwenye hadhila hii na povu pomoni unataka ubishani.

Soma Biblia yako vzr,tafakari neno na Muombe Mungu akufunulie kile umesoma ukielewe ipaswavyo.
Ni vizuri ukiaattend na kanisani.

UTUKUFU NI WA MUNGU TU.
 
Mpaka Mungu, muumba wa vyote ameshindwa kumuangamiza. Kwa taarifa yako Dunia yote imetekwa na shetani. Fanya utafiti, " kila penye mafanikio (hasa ya chapchap) yupo shetani".
 
Kuna baadhi ya watu wanadhani shetani ni jambo dogo, ile ni nguvu kubwa iliyoshinda binadamu wote. Utakapojaribu kuingia kwenye ugomvi na yeye ndipo utatambua kuwa unajaribu kupigana na jambo usiloweza. Kwa reference fupi, wapo mitume waliojaribu kupambana naye wakaishia kupata adhabu kali zisizoelezeka.

Wakwanza ni Yesu, mwana wa Mungu alipojaribu kupambana nae aliishia kusulubishwa. Ayubu mcha Mungu alipata kipigo kikali sana alipomcha Mungu, Adam na Hawa pamoja na utashi wao wote walitiwa kwenye 18, mitume ikiwemo Stephano walipigwa na mawe mpaka kufa walipoingia kwenye vita na shetani.

Unaposema unataka vita na shetani labda pepo ila sio shetani aliyemsulubisha Yesu, vinginevyo utaishia kuchapwa kipigo kitakatifu.
Jiulize je, kama Yesu na nguvu zake zote alisulubishwa vibaya sana wewe atakufanyia jambo gani?
Umetumia kigezo gani kujua uwezo wa huyo shetani? Au na wewe unadhani shetani ana uwezo mkubwa?

Kama unadhani tu bila ya kuwa na uthibitisho kamili wa uwezo wa huyo shetani..haya yanabaki mawazo yako na mtazamo wako.
 
Mpaka Mungu, muumba wa vyote ameshindwa kumuangamiza. Kwa taarifa yako Dunia yote imetekwa na shetani. Fanya utafiti, " kila penye mafanikio (hasa ya chapchap) yupo shetani".
Una uhakika Mungu muumba wa vyote ameshindwa kumu angamiza shetani?Yani Mungu aweze kumu umba shetani halafu ashindwe kumu angamiza? Ni Mungu gani huyo?

Na uwezo wake huo uko wapi kama anashindwa kuangamiza kitu alicho umba mwenyewe?
 
Back
Top Bottom