USIHADAIKE: Hakuna uchawi wa kumfanya mtu akulipe deni

USIHADAIKE: Hakuna uchawi wa kumfanya mtu akulipe deni

Humu mitandaoni watu wanapigwa sana. Kuna madalali humu wamejaa shuhuda za kutunga na zinavutia sana!

Kama kungekuwa na huu ushirikina wa kumfanya mtu akulipe mahakama kusingefurika kesi za madai. Ama mahakama zetu zingekuwa na afueni kubwa sana...
Mkuu Mshana, nakubali sana michango yako sehemu nyingi, lakini kwenye hili nitatofautiana nawe kidogo!

Kwanza ifahamike Mimi sio mganga wa kienyeji na siungi mkono sana mambo hayo, hasa kwasasa ambapo nimeamua kumrudia mwenyezi Mungu muumba mbingu na ardhi.

Sisi wote ni binadamu na kwanamna Moja au nyingjne tumejikuta tumepitia au kufanya mambo ya aina hiyo kwenye maisha. Kuhusu mganga anayeweza kumfanya mdeni wako akulipe nimewahi kushuhudia kwa macho yangu hilo likitendeka tena ni mwaka huu huu mwanzoni.

Kuna jamaa mmoja alikuwa anafanya kazi kiwanda cha rasta pale Mbagala (sikumbuki kama ni kiwanda cha Angels au Darling). Kiwanda hiki kiliwasimamisha kazi wafanyakazi wengi kikiwa na lengo la kuwaachisha kazi bila ya kuwalipa mafao yao na malimbikizo yao ya mishahara kwa zaidi ya miezi 6.

Huyu jamaa alielekezwa kwa mganga mmoja Mwana mama (msukuma). Aliniomba nimsindikize kwahuyo mganga, Akampatia dawa ya kuoga, jamaa alikuwa anawasiwasi sana kama atafanikiwa, maana aliidharau sana ile dawa, baada ya kuiogea ile dawa kesho yake alipigiwa simu kuitwa kiwandani kulipwa mafao yake yote pamoja na malimbikizo yake ya mshahara. Jamaa hakuamini hata Mimi sikuamini mpaka alipokabidhiwa fedha zake.Jamaa aliniomba nimsindikize akampe shukrani yule mama mganga.

Japo siamini sana mambo ya kishirikina wala siwashauri watu waende huko lakini mambo haya yapo, na Mimi ni shaidi wa jambo hili, mwisho naomba radhi kama ushuhuda huu utamgusa mtu yeyote, lengo ni kusimulia na sio kumtaja mtu.
 
Mkuu Mshana, nakubali sana michango yako sehemu nyingi, lakini kwenye hili nitatofautiana nawe kidogo!

Kwanza ifahamike Mimi sio mganga wa kienyeji na siungi mkono sana mambo hayo, hasa kwasasa ambapo nimeamua kumrudia mwenyezi Mungu muumba mbingu na ardhi....
[emoji1545][emoji1545][emoji1545] Nimekupata vema lakini hapo umeona wazi ni madai kutokana na kazi ni sio kule kukopeshana pesa kwa watu wawili binafsi.

Mada yangu ililenga zaidi kwenye mambo ya cash..kuombwa mkopo halafu mkopaji kuwa mzito kwenye kulipa deni
 
[emoji1545][emoji1545][emoji1545] Nimekupata vema lakini hapo umeona wazi ni madai kutokana na kazi ni sio kule kukopeshana pesa kwa watu wawili binafsi
Mada yangu ililenga zaidi kwenye mambo ya cash..kuombwa mkopo halafu mkopaji kuwa mzito kwenye kulipa deni
Wengine wanakutupia jini la kukupumbaza tuu unashangaa unalipa mwenyewe deni

Hayo mambo wanafanya waislam
 
Unakuta kuna lijamaa unalidai mwaka sasa, unajiapiza mkikutana ama zake ama zangu kitachimbika, ila mkionana unasahau hata kudai tena, unakua mpole kama maji ya mtungini, unashindwa hata kumadai tena.
 
Unazunguka sana, dawa ya kukopesha ni kumiliki mali ya thamani zaidi ya mkopo kutoka kwa mkopaji na asiporudisha ndani ya muda mliokubaliana, mali unachukua moja kwa moja.
 
Sasa ulitaka asipate busha au fujo alipe? Mana kama kufuatwa vizuri mtu unamfuata kwa wema mwanzon akulipe deni anakutolea mbovu, kwanini usimpe adabu akulipe hela zako mana ni zako sio zake na alikuja akiwa na shida ukamsaidia kwa wema

Waswahel wanasema ukitaka ubaya dai chako...kuna baadhi ya wadaiwa hufikia kujenga uadui kabisa na wanaowadai
 
Humu mitandaoni watu wanapigwa sana. Kuna madalali humu wamejaa shuhuda za kutunga na zinavutia sana!

Kama kungekuwa na huu ushirikina wa kumfanya mtu akulipe mahakama kusingefurika kesi za madai. Ama mahakama zetu zingekuwa na afueni kubwa sana...
Kwenye madeni mtu ukijichanganya kwa waganga lazima upigwe tu.

Ila kuna mambo mengine wengine huwa hatupendi kutoa confession ngoja nitulie sitaki comments za kuitwa tapeli.
 
Hapo mwisho nimekupata jamaa nimemkopesha bado hajanilipa deni langu anakuja tena nimkopeshe kwa mara nyingine....Kuna watu sijajua wameumbwaje...
 
Mkuu kwa heshima naomba nikujibu, sio kwamba waganga wa kweli hawapo, wapo sana, suala ni kuwafikia au kuwapata, sio watu wengi wanatoa SIRI za walipo, wengi wana roho za kwanini, na pia inategemea unayemuomba....
Haya tupe mrejesho, ndagu ulifanikiwa?
 
Hapo mwisho nimekupata jamaa nimemkopesha bado hajanilipa deni langu anakuja tena nimkopeshe kwa mara nyingine....Kuna watu sijajua wameumbwaje...
[emoji3][emoji3][emoji3]duh.. Hawa watu wapo!
 
Kwenye madeni mtu ukijichanganya kwa waganga lazima upigwe tu.

Ila kuna mambo mengine wengine huwa hatupendi kutoa confession ngoja nitulie sitaki comments za kuitwa tapeli.
Hapana usiogope watu walio kizani hawa wapo tu mbona.. Andika mwanaone
 
Humu mitandaoni watu wanapigwa sana. Kuna madalali humu wamejaa shuhuda za kutunga na zinavutia sana!

Kama kungekuwa na huu ushirikina wa kumfanya mtu akulipe mahakama kusingefurika kesi za madai. Ama mahakama zetu zingekuwa na afueni kubwa sana.

Sikiliza nikwambie kuna uchawi moderate tu tena wa kumfanya mtu akopesheke hata kama ananuka madeni na ukishampa pesa yako kumdai unaogopa. Hawa ndio maisha yao japo nao pesa wanayopata hawaifanyii chochote cha maana wanaishia kustarehe na kufanya mambo mengine ya kipuuzi kabisa.

Kuna makabila hutajwa kuwa ni kiboko ya wadeni, yani hao ukiwakopa tafadhali lipa, la sivyo litakupata la kukupata. Lakini nao uwezo wao ni kukuharibu na kukuumiza tu lakini sio kukufanya ulipe.

Kuna njia tano za kushughulika na mdeni sugu:

1. Kama una ushahidi wa maandishi fuata mkondo wa sheria. Lakini makinika deni lisiwe na riba kwakuwa sheria haitambui riba binafsi kama huna leseni ya kufanya biashara ya kukopesha
2. Pata mganga mwenye uwezo wa kumuangamiza. Njia rahisi zaidi ni kuua..ishu za kumpiga vimavi zina michakato mirefu
3. Malizana naye kihuni. Tafuta genge la wana wenye shughuli zao. Wape kazi wakamalizane naye kibingwa. Tit for tat is a fair deal!
4. Mwachie Mungu akupiganie. Kama ni mwamini lakini. Yeye ndio mkuu wa yote atatenda kwa wakati wake.
5. Samehe na sahau uiachie karma ifanye kazi yake! Pambana usimame tena..lakini ukiwa umepata funzo kwa njia ngumu

Usihangaike kutafuta mganga atakayemfanya mdeni/wadeni wako wakulipe. Kumbuka wakati unamtafuta mganga wa kumfanya mdeni akulipe , mdeni naye wakati huo huo anatafuta mganga amsaidie usimdai au usahau deni. Mbaya zaidi mnaweza kumtumia mganga mmoja bila kujijua wote.

Ukipigwa na waganga wa kienyeji kwenye ishu za madeni usije ukalalama hasa kama utakuwa umepitia huu uzi. Kumpeleka mdeni kwa mganga akulipe ni sawa na kupigwa mara mbili. Unaneemesha wezi wawili kwa wakati mmoja na kama kati yao kuna dalali kakutambulisha unaongeza wigo wa kupoteza.

NB: Kuna watu wana ukarimu wa kiMungu, hawajui kumnyima mtu kama wanacho na kuna watu nyuso zimeumbwa bila haya.

Kakukopa hajakulipa lakini bado anakurudia akihitaji msaada wako tena na tena. Lakini sote sie ni waja wa Mola wetu. Yeye ndie ajuaye zaidi yetu sote.
Ila uchawi wa kumfelisha mtu asilipe upo ili umdhulum alichoweka bondi
 
Back
Top Bottom