USIIGE: Kila Mtu ana mwendo wake barabarani na sababu zake

USIIGE: Kila Mtu ana mwendo wake barabarani na sababu zake

πŸ™‹β€β™‚οΈβœοΈπŸ“πŸŽ―πŸ’―%πŸ‘ŒπŸ‘πŸ‘ŠπŸ‘πŸ€πŸ™πŸ’πŸŽπŸ—ΌπŸŽ–οΈπŸ†πŸ‘‘πŸ›‘οΈ
 
Ligi za barabarani kati ya madereva nyingi zimesababisha majanga mengi kwa:

Madereva,

Abiria,

Waenda kwa miguu,

Magari,

Na uharibifu wa mali.


Kuna watu leo hii ni marehemu, wakiwa wameacha wajane na yatima kwa sababu ya hizi ligi. Kuna watu leo hii ni walemavu na wamegeuka tegemezi kwa asilimia mia kwa sababu ya hizi ligi. Hasara ni nyingi, na madhara ni mengi pia.

Lakini je, ulishawahi kujiuliza hao wanaokimbia sana barabarani wanakimbilia nini? Wanawahi nini? Wao sio polisi kwamba wanawahi eneo la tukio; sio fire kwamba wanawahi kuzima moto mahali; sio ambulance kwamba wanawahi kuokoa uhai mahali.

Katika maisha yao yote wamekimbia, lakini hawana walichotuzidi... labda ajali! Walikowahi hawakupata kikubwa zaidi... labda fumanizi!

Barabarani, nenda mwendo wako. Usiige, usifanye ligi za bure. Hazina mwamuzi, hazina kombe.

Unayefanya naye ligi:

Hujui uzima wa gari yake,

Hujui uzima wa tairi zake,

Hujui umahiri wake kwenye usukani na pedeli,

Hujui changamoto zake kwenye maisha.

Sasa unashindana naye ili iweje?

Maisha yako ni muhimu zaidi ya ligi zisizo na faida. Una wapendwa wanakusubiri nyumbani. Wafikirie hao kwanza kabla hujaamua kukoleza mwendo ili kuonesha ushujaa usio na pongezi.

Jioni njema, Tanganyika!
Mimi nina maneno yangu nikiwa nadrive kwamba kila mtu ana safari yake,hata nikiwa nafanya jogging hvyohvyo akitokea jogger mwenzangu na mimbio yake namuacha aende zake wala simfuatishi,imenisaidia sana mentality hiyo
 
Asante ndugu yangu kwa ukumbusho murua hakika vijana wana la kujifunza.......

Nilipewaga lift na bwana mdogo mmoja nilikuwa naenda mazikoni huko upareni......ilikuwa ni hizi Prado Tx......

Kati kati ya safari akaja kupitwa na jamaa mwenye Mark X.....mzozo ukaanzia hapo..... ilikuwa mshike mshike....mtu mzima nimeshikilia roho....

Dua zangu ilikuwa tufike salama Korogwe tu niamuachie gari yake maana vurugu ilianzia Kabuku kuitafuta Segera.........

Nikashukia Korogwe nikawaacha na ligi yao.....

Lakini nilikuwa najisemea moyoni kuwa huyu bwana mdogo hana siku nyingi za kuishi....
 
Asante ndugu yangu kwa ukumbusho murua hakika vijana wana la kujifunza.......

Nilipewaga lift na bwana mdogo mmoja nilikuwa naenda mazikoni huko upareni......ilikuwa ni hizi Prado Tx......

Kati kati ya safari akaja kupitwa na jamaa mwenye Mark X.....mzozo ukaanzia hapo..... ilikuwa mshike mshike....mtu mzima nimeshikilia roho....

Dua zangu ilikuwa tufike salama Korogwe tu niamuachie gari yake maana vurugu ilianzia Kabuku kuitafuta Segera.........

Nikashukia Korogwe nikawaacha na ligi yao.....

Lakini nilikuwa najisemea moyoni kuwa huyu bwana mdogo hana siku nyingi za kuishi....
Lakini nilikuwa najisemea moyoni kuwa huyu bwana mdogo hana siku nyingi za kuishi....πŸ₯ΊπŸ₯ΊπŸ₯Ί
 
Wengine hatuhitaji ligi kwenda kasi kubwa. Imo tu katika damu.

Ila ushauri wa kupunguza kuendesha kwa kasi kubwa kiujumla una mantiki kubwa.
 
Ligi ka ligi kuuu baraaa
Yaaanii ka wewe ni dereva endesha ukitambua wewe ndo mwenye akili awo wengine ni hawaelewi chochote
Barabara Kuna maeneo yanatambulika kwa kafaraaa
Get prepared
Sala/ibada muda wote
Hii akili ingelikuwa na madreva woteingelipunguza kiasi kikubwa cha ajari barabarani
 
Kuna bodaboda alinipita mwendo Sana kumbe anaenda sherry.

Ahsante mshana jr Kwa ushauri mzuri
Naongezea, ukiwa barabarani tembea mwendo wako usiende sawa na wanyuma yako AU mbele yako mana kama unawai hospital kuna anae wahi kufumania kuna anaewai Mahakamani kifupi huwezi kumridhisha Toyote barabarani
 
Hii ni kweli kabisa,
Ni mashindano ambayo hayana pongezi zaidi ya kuiridhisha nafasi ya mkimbiaji wakati hakuna hata anayekufahamu.
 
Mimi nina maneno yangu nikiwa nadrive kwamba kila mtu ana safari yake,hata nikiwa nafanya jogging hvyohvyo akitokea jogger mwenzangu na mimbio yake namuacha aende zake wala simfuatishi,imenisaidia sana mentality hiyo
FB_IMG_1730949616466.jpg
 
majuzi tu hapa nimeipeleka familia Mkuranga usiku wakati wa kurudi daah mimi nipo makini ila dereva mwenzangu akataka kusababisha majanga, too bad, andiko zuri sana kaka yangu Mshana!
 
Mkuu mshana huwa naelewa sana mabandiko yako hapa jukwaani, juzi kati tumepoteza bodaboda wawili wamegongana uso kwa uso wote wameaga dunia chanzo ni mwendokasi kama kawaida, watanzania tatizo ni kupuuzia mambo sana ndio mana ajali kila siku hazikomi
 
Back
Top Bottom