Dr.adams faida
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 1,888
- 3,352
Kiufupi...
Wamasai ni kabila wazawa wa Afrika la watu wahamaji wanaopatikana
Kenya na kaskazini Tanzania. Kwa sababu ya mila tofauti zao na mavazi na kuishi karibu na mbuga nyingi za Afrika Mashariki, wao ni miongoni mwa mengi ya makabila yanayojulikana Afrika.
Wao wanazungumza mojawapo ya familia ya lugha ya Nilo-Sahara inayohusiana na Dinka na Nuer , na pia wameelimika katika lugha rasmi za Kenya na Tanzania: Kiswahili na
Kiingereza .
Idadi ya Wamasai inakadiriwa kuwa 377.089 kutoka Sensa ya 1989 au kama lugha ya wasemaji 453.000 nchini Kenya mwaka 1994 na 430.000 katika Tanzania mwaka 1993 kwa jumla inakadiriwa kuwa "inakaribia 900.000"ingawa sina data mpya za mwaka 2012
Makadirio hayo ya Wamasai katika nchi zote mbili huenda ikawa ni vigumu kuyathibitisha kwa sababu ya umbali wa maeneo ya vijiji vyao vingi, na asili yao ya uhamaji.
Ingawa serikali ya Tanzania na Kenya imeweka mipango kuwahimiza Wamaasai kuachana na asili yao ya jadi ya uhamaji, bado wameendelea na desturi hiyo.Hivi majuzi, Oxfam imedai kwamba mtindo wa maisha ya Wamasai lazima ikubaliwe ili kuzingatia mabadiliko ya hali ya hewa kwa sababu hawana uwezo wa kulima katika majangwa.
Historia
Maasai shujaa
Kulingana na historia simulizi yao wenyewe, asili ya Kimasai ilitoka kwenye bonde la Nile ya chini kaskazini ya Ziwa Turkana (North-West Kenya) na walianza kuhamia kusini karibu karne ya kumi na tano, wakiwasili katika shina la ardhi kutoka kaskazini mwa Kenya na Tanzania ya kati tangu karne ya kumi na saba hadi mwisho wa karne ya kumi na nane.
Makabila mengine yalilazimishwa kuyahama makazi yao Wamaasai walipohamia huko. Eneo la Wamaasai lilifika kilele cha ukubwa wake katikati ya karne ya kumi na tisa, na kuenea kwote katika Bonde la Ufa na pande za ardhi kutoka Mlima Marsabit huko kaskazini hadi Dodoma kule kusini.
Wakati huu Wamasai, na vilevile lile kundi kubwa walilokuwa wamejiunga nalo, walikuwa wakivamia mifugo hadi umbali wa mashariki ya
pwani ya Tanga huko Tanzania.
Washambulizi walitumia mikuki na ngao, lakini walikuwa wamehofiwa kwa kutupa vilabu (orinka) walivyoweza kutupa kwa usahihi kutoka umbali wa mita 100. Mwaka 1852 kulikuwa na ripoti ya msongomano wa wapiganaji 800 wa kimaasai kuhamia nchini Kenya.
Mwaka 1857, baada ya kufyeka "Nyika ya Wakuafi" katika kusini mashariki mwa Kenya, Washambulizi Wamasai wakatisha Mombasa katika pwani ya Kenya.
Maasai mashujaa katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani, c. 1906/18.
Kwa sababu hii ya uhamiaji, Wamasai ni wazungumzaji wa Kiniloti wa kusini zaidi. Kipindi cha upanuzi ulifuatwa na "Emutai" ya kimasai ya 1883-1902. Kipindi hiki kilikuwa kimetofautishwa na kuenea kwa magonjwa ya bovin pleuropneumonia, rinderpest, na smallpox.
Kisio la kwanza lilikuwa limependekezwa na mwanajeshi wa Kijerumani kaskazini magharibi ya Tanganyika, ilivyojulikana siku hizo ya kwamba asilimia 90 ya ng'ombe na nusu ya wanyama pori walikufa kutokana na ugonjwa wa rinderpest.
Madaktari wajerumani walidai kuwa katika eneo moja "kila sekunde" Afrika kulikuwa na mtoto aliyeugua matokeo ya smallpox. Kipindi hiki kiliambatana na ukame. Mvua ilikosa kunyesha kabisa katika mwaka wa 1897 na 1898.
Mtafiti kutoka Austria Oscar Baumann akisafiri katika nchi ya Wamaasai 1891-1893, alieleza makazi huko katika volkeno ya Ngorongoro katika kitabu 1894 durch Massailand zur Nilquelle ("Kupitia ardhi ya Wamaasai ya chanzo ya Nile"):
"Kulikuwa na wanawake waliodhoofiwa mno waliotazama ule wazimu wa njaa ... mashujaa waliokuwa wameshindwa kutembea, wakiwa na wazee walioathirika na wasiojali kitu. Vikundi vya tai viliwafuata kutoka juu, hawa tai wakisubiri waathirika.
" Kulingana na kisio moja theluthi mbili ya Wamaasai walikufa katika kipindi hiki. Kuanzia na mkataba wa 1904, na kufuatiwa na mwingine mwaka 1911, ardhi ya wamaasai nchini Kenya Wamaasai ilipunguzwa kwa asilimia 60 wakati Waingereza walipowafukuza ili kutayarisha nafasi ya mashamba ya wakoloni, hatimaye kuwalazimu kuishi katika wilaya ya Kajiado na Narok.
Wamasai kutoka Tanzania walifukuzwa kutoka ardhi yenye rutuba kati ya
Mount Meru na Mlima Kilimanjaro, Nyanda yenye rotuba iliyo karibu na Ngorongoro katika miaka ya 1940.
Ardhi zaidi ilichukuliwa kujenga hifadhi ya wanyamapori na hifadhi za taifa: Amboseli, Hifadhi ya Kitaifa ya Nairobi , Masai Mara , Samburu, Ziwa Nakuru , na Tsavo nchini Kenya; Manyara, Ngorongoro , Tarangire na Serengeti huko Tanzania.
Wamasai ni wafugaji mifugo wanaopinga sisitizo la serikali ya Tanzania na serikali ya Kenya kuishi maisha ya kisasa. Wao wanadai haki ya kulisha mifugo katika Hifadhi za Taifa katika nchi zote mbili.
Wamasai walisimama dhidi ya utumwa na waliishi pamoja na wanyama pori wengi huku wakikataa kula wanyama pori hao wala ndege. Ardhi ya Wamaasai sasa ina Hifadhi za Wanyama pori zilizo bora kabisa kote Afrika Mashariki.
Jamii ya Wamaasai haikuwahi kukubali kamwe usafirishaji haramu wa binadamu, na wote waliotafuta watumwa walikuwa wakiwaepuka Wamasai.
ikumbukwe jina la sahihi kabila hili si masai kama tulivyozoea katika maandishi bali MAASAI
morani
Wamasai ni kabila wazawa wa Afrika la watu wahamaji wanaopatikana
Kenya na kaskazini Tanzania. Kwa sababu ya mila tofauti zao na mavazi na kuishi karibu na mbuga nyingi za Afrika Mashariki, wao ni miongoni mwa mengi ya makabila yanayojulikana Afrika.
Wao wanazungumza mojawapo ya familia ya lugha ya Nilo-Sahara inayohusiana na Dinka na Nuer , na pia wameelimika katika lugha rasmi za Kenya na Tanzania: Kiswahili na
Kiingereza .
Idadi ya Wamasai inakadiriwa kuwa 377.089 kutoka Sensa ya 1989 au kama lugha ya wasemaji 453.000 nchini Kenya mwaka 1994 na 430.000 katika Tanzania mwaka 1993 kwa jumla inakadiriwa kuwa "inakaribia 900.000"ingawa sina data mpya za mwaka 2012
Makadirio hayo ya Wamasai katika nchi zote mbili huenda ikawa ni vigumu kuyathibitisha kwa sababu ya umbali wa maeneo ya vijiji vyao vingi, na asili yao ya uhamaji.
Ingawa serikali ya Tanzania na Kenya imeweka mipango kuwahimiza Wamaasai kuachana na asili yao ya jadi ya uhamaji, bado wameendelea na desturi hiyo.Hivi majuzi, Oxfam imedai kwamba mtindo wa maisha ya Wamasai lazima ikubaliwe ili kuzingatia mabadiliko ya hali ya hewa kwa sababu hawana uwezo wa kulima katika majangwa.
Historia
Maasai shujaa
Kulingana na historia simulizi yao wenyewe, asili ya Kimasai ilitoka kwenye bonde la Nile ya chini kaskazini ya Ziwa Turkana (North-West Kenya) na walianza kuhamia kusini karibu karne ya kumi na tano, wakiwasili katika shina la ardhi kutoka kaskazini mwa Kenya na Tanzania ya kati tangu karne ya kumi na saba hadi mwisho wa karne ya kumi na nane.
Makabila mengine yalilazimishwa kuyahama makazi yao Wamaasai walipohamia huko. Eneo la Wamaasai lilifika kilele cha ukubwa wake katikati ya karne ya kumi na tisa, na kuenea kwote katika Bonde la Ufa na pande za ardhi kutoka Mlima Marsabit huko kaskazini hadi Dodoma kule kusini.
Wakati huu Wamasai, na vilevile lile kundi kubwa walilokuwa wamejiunga nalo, walikuwa wakivamia mifugo hadi umbali wa mashariki ya
pwani ya Tanga huko Tanzania.
Washambulizi walitumia mikuki na ngao, lakini walikuwa wamehofiwa kwa kutupa vilabu (orinka) walivyoweza kutupa kwa usahihi kutoka umbali wa mita 100. Mwaka 1852 kulikuwa na ripoti ya msongomano wa wapiganaji 800 wa kimaasai kuhamia nchini Kenya.
Mwaka 1857, baada ya kufyeka "Nyika ya Wakuafi" katika kusini mashariki mwa Kenya, Washambulizi Wamasai wakatisha Mombasa katika pwani ya Kenya.
Maasai mashujaa katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani, c. 1906/18.
Kwa sababu hii ya uhamiaji, Wamasai ni wazungumzaji wa Kiniloti wa kusini zaidi. Kipindi cha upanuzi ulifuatwa na "Emutai" ya kimasai ya 1883-1902. Kipindi hiki kilikuwa kimetofautishwa na kuenea kwa magonjwa ya bovin pleuropneumonia, rinderpest, na smallpox.
Kisio la kwanza lilikuwa limependekezwa na mwanajeshi wa Kijerumani kaskazini magharibi ya Tanganyika, ilivyojulikana siku hizo ya kwamba asilimia 90 ya ng'ombe na nusu ya wanyama pori walikufa kutokana na ugonjwa wa rinderpest.
Madaktari wajerumani walidai kuwa katika eneo moja "kila sekunde" Afrika kulikuwa na mtoto aliyeugua matokeo ya smallpox. Kipindi hiki kiliambatana na ukame. Mvua ilikosa kunyesha kabisa katika mwaka wa 1897 na 1898.
Mtafiti kutoka Austria Oscar Baumann akisafiri katika nchi ya Wamaasai 1891-1893, alieleza makazi huko katika volkeno ya Ngorongoro katika kitabu 1894 durch Massailand zur Nilquelle ("Kupitia ardhi ya Wamaasai ya chanzo ya Nile"):
"Kulikuwa na wanawake waliodhoofiwa mno waliotazama ule wazimu wa njaa ... mashujaa waliokuwa wameshindwa kutembea, wakiwa na wazee walioathirika na wasiojali kitu. Vikundi vya tai viliwafuata kutoka juu, hawa tai wakisubiri waathirika.
" Kulingana na kisio moja theluthi mbili ya Wamaasai walikufa katika kipindi hiki. Kuanzia na mkataba wa 1904, na kufuatiwa na mwingine mwaka 1911, ardhi ya wamaasai nchini Kenya Wamaasai ilipunguzwa kwa asilimia 60 wakati Waingereza walipowafukuza ili kutayarisha nafasi ya mashamba ya wakoloni, hatimaye kuwalazimu kuishi katika wilaya ya Kajiado na Narok.
Wamasai kutoka Tanzania walifukuzwa kutoka ardhi yenye rutuba kati ya
Mount Meru na Mlima Kilimanjaro, Nyanda yenye rotuba iliyo karibu na Ngorongoro katika miaka ya 1940.
Ardhi zaidi ilichukuliwa kujenga hifadhi ya wanyamapori na hifadhi za taifa: Amboseli, Hifadhi ya Kitaifa ya Nairobi , Masai Mara , Samburu, Ziwa Nakuru , na Tsavo nchini Kenya; Manyara, Ngorongoro , Tarangire na Serengeti huko Tanzania.
Wamasai ni wafugaji mifugo wanaopinga sisitizo la serikali ya Tanzania na serikali ya Kenya kuishi maisha ya kisasa. Wao wanadai haki ya kulisha mifugo katika Hifadhi za Taifa katika nchi zote mbili.
Wamasai walisimama dhidi ya utumwa na waliishi pamoja na wanyama pori wengi huku wakikataa kula wanyama pori hao wala ndege. Ardhi ya Wamaasai sasa ina Hifadhi za Wanyama pori zilizo bora kabisa kote Afrika Mashariki.
Jamii ya Wamaasai haikuwahi kukubali kamwe usafirishaji haramu wa binadamu, na wote waliotafuta watumwa walikuwa wakiwaepuka Wamasai.
ikumbukwe jina la sahihi kabila hili si masai kama tulivyozoea katika maandishi bali MAASAI
morani