Usiombe uende hospitali ukafanyiwa kipimo hiki cha OGD

Usiombe uende hospitali ukafanyiwa kipimo hiki cha OGD

shaks001

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2014
Posts
1,246
Reaction score
1,070
Jana nilienda hospitali moja kubwa hapa jijini Dar.Nilikuwa nasumbuliwa na homa ikiambatana na maumivu ya mara kwa mara ya tumbo.Kwa maelezo ya Dr. ilibidi aniandikie kipimo flani hivi kinaitwa OGD.

Mungu wangu!Katika siku nilihisi roho yangu inatengana na mwili ilikuwa jana, hicho kipimo unaingizwa "li-mpira"jeusi kubwa mdomoni linasokomezwa mpaka tumboni kwa muda kama wa dakika mbili au tatu.Kwa kipindi hicho huwezi kupumua vizuri, huwezi kuongea, huwezi kutema wala kumeza mate, macho yanakutoka kama fundi saa kapoteza nati.Yaani ni mateso jamani.Hayo yote yanafanyika baada ya kupuliziwa dawa ya ganzi lakini wapi bwana, hakuna ganzi kwenye kukata roho.

Na ndio maana kipimo hiki unatakiwa ufanyiwe kabla hujala chochote maana ukitumbukizwa ule mpira ni lazima utapike.Yaani leo hii nahisi ile mikwaruzo ya ule mpira bado ipo kuanzia kooni mpaka kwenye utumbo.Aisee sitakubali nifanyiwe hii kitu labda niwe mahututi sijitambui.

Labda wataalamu wa mambo haya mnijuze, je hata huko kwa wenzetu kwenye nchi zilizoendelea wanatumia njia hii ya kutumbukizana madude haya tumboni au kuna njia nyingine? Maana siamini kama mzungu anaweza kuvumilia mateso haya.
 
Jana nilienda hospitali moja kubwa hapa jijini Dar.Nilikuwa nasumbuliwa na homa ikiambatana na maumivu ya mara kwa mara ya tumbo.Kwa maelezo ya Dr.ilibidi aniandikie kipimo flani hivi kinaitwa OGD.

Mungu wangu!Katika siku nilihisi roho yangu inatengana na mwili ilikuwa jana,hicho kipimo unaingizwa "li-mpira"jeusi kubwa mdomoni linasokomezwa mpaka tumboni kwa muda kama wa dakika mbili au tatu.Kwa kipindi hicho huwezi kupumua vizuri,huwezi kuongea,huwezi kutema wala kumeza mate,macho yanakutoka kama fundi saa kapoteza nati.Yaani ni mateso jamani.Hayo yote yanafanyika baada ya kupuliziwa dawa ya ganzi lakini wapi bwana,hakuna ganzi kwenye kukata roho.

Na ndio maana kipimo hiki unatakiwa ufanyiwe kabla hujala chochote maana ukitumbukizwa ule mpira ni lazima utapike.Yaani leo hii nahisi ile mikwaruzo ya ule mpira bado ipo kuanzia kooni mpaka kwenye utumbo.Aisee sitakubali nifanyiwe hii kitu labda niwe mahututi sijitambui.

Labda wataalamu wa mambo haya mnijuze,je hata huko kwa wenzetu kwenye nchi zilizoendelea wanatumia njia hii ya kutumbukizana madude haya tumboni au kuna njia nyingine?Maana siamini kama mzungu anaweza kuvumilia mateso haya!
ulikuwa unapimwa ulcers hapo, mi nilikataa nikaomba dawa tu kwa kuzingatia dalili za ugonjwa
 
Nishawah kisikia hiko kipimo, ni shida. Kama sikosei ni cha vidonda vya tumbo
Pamoja na kusokomezwa hilo li-mpira lakini majibu ya kipimo yalionyesha sina Ulcers.Ndio maana nikajiuliza hakuna njia nyingine za kitaalamu kugundua tatizo hilo bila kutumbukiziana hayo mavitu tukatiana mikwaruzo tu,halafu mwisho wa siku majibu yanaonesha "Normal".
 
Wanasema hichi kipimo ni accurate ukifananisha na cha kupima damu. Iko kipimo kinapiga picha eneo lote la tumbo na kubainisha tatizo.
 
Kuna kipimo kingine huwa kinaingizwa huko nyuma kina kamera mbele hicho nadhani kina afadhali
 
Pamoja na kusokomezwa hilo li-mpira lakini majibu ya kipimo yalionyesha sina Ulcers.Ndio maana nikajiuliza hakuna njia nyingine za kitaalamu kugundua tatizo hilo bila kutumbukiziana hayo mavitu tukatiana mikwaruzo tu,halafu mwisho wa siku majibu yanaonesha "Normal".
Hahaha pole sana Mkuu maana mpaka nmecheka aise,hicho kipimo au Labda dokta alikuwa anataka kukukomoaaa....
 
M nilifanyiwa Hindu mandal na selian hospital yan sitaman tena maana kipimo hk n kipya kwny baadhi ya hospital kW hyo wana force kumpima MTU ili wapate faida maana selian Nili waeleza tayar nimepma 3wek agos wakasema subir tuhakik lol yan sikutaman nirudiwe ila shida ugonjwa auna adabu
 
Sasa si ndo kipimo jamani? Utaponaje bila kupimwa? Btw ungeenda kule mbadala hawatumii mpira just mashine tu wanaona ka unavidonda au la! Pole! Kuna vipimo vinatisha loh!
Kuuliza c ujinga Btw ndio nini? Nimehis labda ni between akili ikakataa, but hyo w isingekuwepo
 
Sasa si ndo kipimo jamani? Utaponaje bila kupimwa? Btw ungeenda kule mbadala hawatumii mpira just mashine tu wanaona ka unavidonda au la! Pole! Kuna vipimo vinatisha loh!
Au ni by the way? Naona inakubali
 
Back
Top Bottom