Usipokuwa Rais huwezi kuwa Mwenyekiti wa CCM!!??

Usipokuwa Rais huwezi kuwa Mwenyekiti wa CCM!!??

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Historia inaonesha kuwa hakuna Mwenyekiti wa CCM aliyedumu kwenye nafasi hiyo akiwa nje ya Urais.

Mwalimu alipotoka madarakani harakaharaka akamuachia Ally Hassan Mwinyi uenyekiti wa CCM akiwa Rais.

Mwinyi naye alipotoka kwenye Urais akamwachia Benjamin William Mkapa uenyekiti wa CCM ambaye wakati huo alikuwa Rais wa Tanzania.

Mkapa bila ya kupoteza muda Jakaya Mrisho Kikwete alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanzania, akamwachia uenyekiti wa CCM Jakaya.

Jakaya naye akafuata nyayo za watangulizi wake kumuachia uenyekiti wa CCM John Pombe Magufuli.

Magufuli alipokutana na faradhi ya kifo, CCM haraka haraka wakamkabidhi Samia Suluhu Hassan uenyekiti wa chama Chao.

Kwa mtiririko huo inaonesha shayiri dhahiri kwamba wanachama wengine woote wa CCM hawatakiwi hata kwa bahati mbaya, kuwaza kuwa siku moja wanaweza kuwa mwenyekiti wa CCM Taifa.

Kwanza mfumo wa kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa hakuna kugombea. Kamati Kuu huteua mtu ambaye hupitishwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.

Kwa ivo wenye chama chao ( Kamati Kuu na Halmashauri) wameshaamua kuzuia wanachama wengine wote kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa mpaka wawe Rais. Tena Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania. Rais wa Zanzibar haruhusiwi.
 
Nyerere alibaki kuwa mwenyekiti wa ccm kwa miaka 5 toka alipostaafu urais 1985 hadi 1990 ndipo alipostaafu uenyekiti wa ccm.
Ni kweli. Lakini unajua sababu yake?

Halmashauri Kuu ya CCM ilikuja na hoja ya "ujenzi wa chama" ambapo ilisemwa Mwalimu angeondoka ghafla CCM ingetikiswa.

Kwa ivo Mwalimu alichelewa kuondoka ili amalize Program ya Ujenzi wa chama.
 
Historia inaonesha kuwa hakuna Mwenyekiti wa CCM aliyedumu kwenye nafasi hiyo akiwa nje ya Urais.

Mwalimu alipotoka madarakani harakaharaka akamuachia Ally Hassan Mwinyi uenyekiti wa CCM akiwa Rais.

Mwinyi naye alipotoka kwenye Urais akamwachia Benjamin William Mkapa uenyekiti wa CCM ambaye wakati huo alikuwa Rais wa Tanzania.

Mkapa bila ya kupoteza muda Jakaya Mrisho Kikwete alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanzania, akamwachia uenyekiti wa CCM Jakaya.

Jakaya naye akafuata nyayo za watangulizi wake kumuachia uenyekiti wa CCM John Pombe Magufuli.

Magufuli alipokutana na faradhi ya kifo, CCM haraka haraka wakamkabidhi Samia Suluhu Hassan uenyekiti wa chama Chao.

Kwa mtiririko huo inaonesha shayiri dhahiri kwamba wanachama wengine woote wa CCM hawatakiwi hata kwa bahati mbaya, kuwaza kuwa siku moja wanaweza kuwa mwenyekiti wa CCM Taifa.

Kwanza mfumo wa kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa hakuna kugombea. Kamati Kuu huteua mtu ambaye hupitishwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.

Kwa ivo wenye chama chao ( Kamati Kuu na Halmashauri) wameshaamua kuzuia wanachama wengine wote kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa mpaka wawe Rais. Tena Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania. Rais wa Zanzibar haruhusiwi.
Ni utamaduni wa CCM
Ni kweli kwamba huo ndio utamaduni wa CCM ambao wameiga kutoka kwa Watawala wadhalimu wa Kikomunisti/Ujamaa, hususani kutoka kwa Chama Cha Kikomunisti Cha China kilipokuwa chini ya Mwenyekiti wake Mao, ambaye pia ni Mwanzilishi wa chama hicho.

Hapo ndipo ilipoanzia falsafa potofu na ya kidhalimu ya 'Zidumu Fikra za Mwenyekiti.'

Chini ya Falsafa hii potofu na ya kidhalimu, Wakomunisti wanaamini kwamba 'Mwenyekiti wa Chama Tawala' ndiye mtu pekee katika nchi ambaye mwenye akili nyingi na akili kubwa zaidi kuliko mtu mwingine yoyote yule. Hivyo, hapaswi kukosolewa.
Aidha, chini ya falsafa hii Wakomunisti watawala wanaamini kwamba 'raia wote katika nchi ni kama mateka wa Mwenyekiti.'
 
Ni kweli. Lakini unajua sababu yake?

Halmashauri Kuu ya CCM ilikuja na hoja ya "ujenzi wa chama" ambapo ilisemwa Mwalimu angeondoka ghafla CCM ingetikiswa.

Kwa ivo Mwalimu alichelewa kuondoka ili amalize Program ya Ujenzi wa chama.
Sawa,lakini mimi nimejibu lile ulilodai,"Historia inaonesha kuwa hakuna Mwenyekiti wa CCM aliyedumu kwenye nafasi hiyo akiwa nje ya Urais."
 
Sawa,lakini mimi nimejibu lile ulilodai,"Historia inaonesha kuwa hakuna Mwenyekiti wa CCM aliyedumu kwenye nafasi hiyo akiwa nje ya Urais."
Ya Mwalimu ilikuwa "Mahsusi" na alipomaliza alichotumwa akatoka.
 
Historia inaonesha kuwa hakuna Mwenyekiti wa CCM aliyedumu kwenye nafasi hiyo akiwa nje ya Urais.

Mwalimu alipotoka madarakani harakaharaka akamuachia Ally Hassan Mwinyi uenyekiti wa CCM akiwa Rais.
Hapa Umedanganya Mkuu..
Mwisho kakabidhiwa Nchi mwaka 1985..
Ila Nyerere kaachia Uenyekiti wa CCM mwaka 1992 miaka sita mpaka 7 baada ya Mwinyi kuwa Rais..

Jakaya naye akafuata nyayo za watangulizi wake kumuachia uenyekiti wa CCM John Pombe Magufuli.
Kikwete Aliachia Nchi mwaka 2015 aliposhinda Magufuli ila Kikwete ameachia Chama mwaka 2017 na Magufuli ameanza kuwa Mwenyekiti wa CCM miaka 2 Baada ya Kuwa raisi..
 
Hapa Umedanganya Mkuu..
Mwisho kakabidhiwa Nchi mwaka 1985..
Ila Nyerere kaachia Uenyekiti wa CCM mwaka 1992 miaka sita mpaka 7 baada ya Mwinyi kuwa Rais..


Kikwete Aliachia Nchi mwaka 2015 aliposhinda Magufuli ila Kikwete ameachia Chama mwaka 2017 na Magufuli ameanza kuwa Mwenyekiti wa CCM miaka 2 Baada ya Kuwa raisi..
Maudhui ya bandiko umeielewa!!??
 
Maudhui ya bandiko umeielewa!!??
Ooh Sawa sasa....
UNajua kwanini?
Mwenyekiti wa Chama Ni Mwamuzi wa wanachana wote, Sasa Imagine kama Mtu mwenye Power Kiasi Hicho hatoweza kuwa Nje ya Mfumo wa Serikali anaweza kwa matakwa yake aka Sabotage Baadhi ya Mipango ya Serikali, Sasa Ili kuepusha Hilo Ni lazima Awe Ni kiongozi wa Serkali pia Kwa hiyo TOP AT PARTY (Chama) TOP AT GAVOO
 
Ooh Sawa sasa....
UNajua kwanini?
Mwenyekiti wa Chama Ni Mwamuzi wa wanachana wote, Sasa Imagine kama Mtu mwenye Power Kiasi Hicho hatoweza kuwa Nje ya Mfumo wa Serikali anaweza kwa matakwa yake aka Sabotage Baadhi ya Mipango ya Serikali, Sasa Ili kuepusha Hilo Ni lazima Awe Ni kiongozi wa Serkali pia Kwa hiyo TOP AT PARTY (Chama) TOP AT GAVOO
Sasa umeelewa...

Kwa ivo CCM haiko imara kiasi kwamba mtu mwingine akiwa mwenyekiti na mwingine akiwa Rais itavurugika!!??
 
CCM ni dhaifu sana endapo itaondoka madarakani kwa kuwa kinachowaweka wamoja ni dola. Bila nguvu ya dola watagawana mbao na ndiyo sababu wanatumia nguvu kubwa ikiwa ni pamoja na ujambazi, mauaji na wizi wa rasilimali za umma kubaki madarakani!
 
Ooh Sawa sasa....
UNajua kwanini?
Mwenyekiti wa Chama Ni Mwamuzi wa wanachana wote, Sasa Imagine kama Mtu mwenye Power Kiasi Hicho hatoweza kuwa Nje ya Mfumo wa Serikali anaweza kwa matakwa yake aka Sabotage Baadhi ya Mipango ya Serikali, Sasa Ili kuepusha Hilo Ni lazima Awe Ni kiongozi wa Serkali pia Kwa hiyo TOP AT PARTY (Chama) TOP AT GAVOO
Mkuu sio kweli, kwani nchi nyingine ambazo kuna utengano kwenye nafasi ya Rais na mwenyekiti wa chama tawala mbona hakuna sabotage au watanzania pekee yao ndio hawaaminiki???
 
Mkuu sio kweli, kwani nchi nyingine ambazo kuna utengano kwenye nafasi ya Rais na mwenyekiti wa chama tawala mbona hakuna sabotage au watanzania pekee yao ndio hawaaminiki???
Tanzania Hatuaminiani Ndugu yangu Hebu fikiria Kwa matukio yanayoendelea Chadema..

Lets Say Mbowe akawa mwenyekiti Halafu lissu akawa ndo Rais unafikir Kingetokea Nini?

Mbowe angemfuta Lissu uanachama na Akawa ndo amekoma kuwa Rais..

Ukiacha Hivyo Fikiria Kuwa Mpina Ndo angekuwa Mwenyekiti wa CCM halafu mama Samia ndo Rais Unafikiri Angeshindwa Kumpa Onyo Rais??
 
Tanzania Hatuaminiani Ndugu yangu Hebu fikiria Kwa matukio yanayoendelea Chadema..

Lets Say Mbowe akawa mwenyekiti Halafu lissu akawa ndo Rais unafikir Kingetokea Nini?

Mbowe angemfuta Lissu uanachama na Akawa ndo amekoma kuwa Rais..

Ukiacha Hivyo Fikiria Kuwa Mpina Ndo angekuwa Mwenyekiti wa CCM halafu mama Samia ndo Rais Unafikiri Angeshindwa Kumpa Onyo Rais??
Kwa ivo tuna mfumo dhaifu (Fragile) wa siasa zetu.
 
Back
Top Bottom