Oltung'anyi
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 284
- 196
- Thread starter
-
- #61
Ndio maana yake. Kwa mfano, kama una nyumba, ukishakufa, hebu tupe namna ambayo utahakikisha kuwa nyumba yako ipo.Ina maana mie nikifa hapa vitu ambavyo sasa vipo vitakuwa havipo?
Mbona watu wanakufa mungu yupo tu
Mungu atakapokua akiandaa kuni za kuchoma wenye dhambi wala hata hatosumbuka kuzitafuta, maana zipo tu plenty available
Suala sio aina ya kuhakikisha ila ni uwepo wa hiyo nyumba,kiuhalisia kifo changu hakiondoi uwepo wa nyumba yangu.Ndio maana yake. Kwa mfano, kama una nyumba, ukishakufa, hebu tupe namna ambayo utahakikisha kuwa nyumba yako ipo.
Suala sio aina ya kuhakikisha ila ni uwepo wa hiyo nyumba,kiuhalisia kifo changu hakiondoi uwepo wa nyumba yangu.
Twende taratibu mkuu. Huwezi kusema kitu fulani hakipo kwa sababu tu huna njia ya kuweza kujua kama kipo au hakipo, unachozungumza wewe ni kinadharia ila katika uhalisia kukosekana uwepo wako hauondoi uwepo wa vitu vyengine.Usingekuwepo, hakuna namna ambavyo nyumba yako ingekuwepo. Sawa mkuu? Kwa hiyo nyumba yako ipo kwa kuwa upo. Siku usipokuwepo, kwako hakuna kitakachokuwepo tena. Nyumba itaendelea kuwepo kwa atakayekuwepo tu. Hakuna namna utaendelea kufahamu kuwa nyumba yako ipo ikiwa haupo.
Usipokuwepo hakuna namna unaweza kusema una ndugu, jamaa wala rafikiri. Kwa hiyo, kutokuwepo kwako kunasababisha kila kitu kisiwepo, hadi Mungu.
Twende taratibu mkuu. Huwezi kusema kitu fulani hakipo kwa sababu tu huna njia ya kuweza kujua kama kipo au hakipo, unachozungumza wewe ni kinadharia ila katika uhalisia kukosekana uwepo wako hauondoi uwepo wa vitu vyengine.
Umesema kuwa kama mie sipo siwezi kuendelea kujua kama nyumba yangu ipo ila nyumba yangu itakuwepo kwa wale watakao kuwepo,kwahiyo hapo kiuhalisia sijaondoa uwepo wa nyumba yangu bali nimeondoa tu uwepo wangu.
Na hivyo kabla ya wewe kuwepo mungu alikuwepo(maana kulikuwa na waliyokuwepo kabla yako) na hata baada ya yeye kutowepo tena pia mungu ataendelea kuwepo.
Sitaweza kwa sababu sipo,ni sawa na wewe utoke zako nyumbani na kwenda kazini,wakati ukiwa kazini huwezijua nini kinaendelea nyumbani kwa sababu haupo ila kukosekana uwepo wako hapo nyumbani hakufanyi iwe hakuna kinachoendelea.Ni kweli ndugu, twende taratibu. Hebu fikiria, kama wewe hukuwepo, unaweza kuniambia ni kitu gani kingekuwepo?
Hujui nini kinaendelea nyumbani, ila kwa kuwa upo, unafahamu kuwa kuna nyumbani. Ukirudi nyumbani, hali yoyote utakayoikuta, ni kwa sababu upo. Ikiwa hukuweza kurudi nyumbani, kama bado upo, utakuwa unafahamu kuna nyumba uliacha, labda na familia na unaweza kutafuta namna ya kufika kuangalia nyumba au ukapiga simu kujua hali ya nyumbani. Ila usipokuwepo kabisa, usipoishi, hakuna namna yoyote utafahamu kuwa ulikuwa na nyumba. Kimsingi, kwako, hakuna kitu kama nyumba, wala familia, wala Mungu. Vitu tinavyoviona kuwa vipo, vitaendelea kuwepo ikiwa nasi tupo. Tusipokuwepo, hakuna chochote na wala hakikukaa kutokea kuwepo, hadi utakapokuwepo.Sitaweza kwa sababu sipo,ni sawa na wewe utoke zako nyumbani na kwenda kazini,wakati ukiwa kazini huwezijua nini kinaendelea nyumbani kwa sababu haupo ila kukosekana uwepo wako hapo nyumbani hakufanyi iwe hakuna kinachoendelea.
Lakini pia kama mimi kutowepo kunafanya nisiweze kujua kilichopo basi hata kujua visivyokuwepo sitoweza kujua kwa sababu sipo.
Mkuu tunaenda mbele na kurudi.Hujui nini kinaendelea nyumbani, ila kwa kuwa upo, unafahamu kuwa kuna nyumbani. Ukirudi nyumbani, hali yoyote utakayoikuta, ni kwa sababu upo. Ikiwa hukuweza kurudi nyumbani, kama bado upo, utakuwa unafahamu kuna nyumba uliacha, labda na familia na unaweza kutafuta namna ya kufika kuangalia nyumba au ukapiga simu kujua hali ya nyumbani. Ila usipokuwepo kabisa, usipoishi, hakuna namna yoyote utafahamu kuwa ulikuwa na nyumba. Kimsingi, kwako, hakuna kitu kama nyumba, wala familia, wala Mungu. Vitu tinavyoviona kuwa vipo, vitaendelea kuwepo ikiwa nasi tupo. Tusipokuwepo, hakuna chochote na wala hakikukaa kutokea kuwepo, hadi utakapokuwepo.
baada ya kifo hutojua lolote mkuu, kwani kabla ya kuzaliwa unajua ulikuwa wapi?Siku tukifa ndo tutajua ukweli..nakisubiri kifo kwa hamu ili kijibu maswali haya yoote.
Mkuu tunaenda mbele na kurudi.
Ok,kuna kutokuwepo kwa aina mbili kwa maana ya ulikuwepo na ukapoteza uwepo wako (kufa) na kuna kutowahi kuwepo kabisa. Sasa suala la kufa tumeshajadili kuwa hata ukifa kama ulikuwa na nyumba basi nyumba yako itaendelea kuwepo haitopoteza uwepo wake kisa tu wewe haupo(kufa) hata kama wewe hutokuwa ukijua nini kinaendelea.
Je,hapo tulielewana kwanza?
baada ya kifo hutojua lolote mkuu, kwani kabla ya kuzaliwa unajua ulikuwa wapi?
Mkuu tunaposema kuwepo tunazungumzia uwepo wa hapa duniani, Mimi na wewe tunayajua mambo ya hapa duniani na tunaona yanayoendelea,tunaona watu wakizaliwa(kuja duniani) na tunaona watu wakifa(kuondoka duniani).Nimekuelewa mkuu, nyumba itaendelea kuwepo, hili halina ubishi. Ila itaendelea kuwepo kama yupo atakayekuwepo. Kumbuka mada ni Kuwepo. Alimradi mtu atakuwepo, itaendelea kuwepo. Sasa wewe ambaye haupo, unawezaje kufahamu kuwa kuna uwepo na kwa hiyo nyumba yako ipo?
Kwa mfano, mara baada ya wewe kutokuwepo, nyumba yako ikabomolewa, ni nini ambacho utakijua kuhusu nyumba yako? Hali hiyo lazima ataijua atakayekuwepo tu. Kwamba, kwa sasa nyumba haipo tena. Ninafurahi kuwa umefafanua vyema kutokuwepo kwa aina mbili, kabla ya kuwepo (kabla ya kuzaliwa) na baada ya kuwepo(baada ya kuishi). Maisha haya hayana utofauti. Kwa kuwa hakukuwa na kitu kabla ya kuishi, hakutakuwa na chochote baada ya kuishi, hata Mungu hatakuwepo. Kwa hiyo, ili kuwepo kwa vilivyopo( na vinavyotarajiwa kuwepo), lazima wewe au mimi tuwepo.
Mkuu tunaposema kuwepo tunazungumzia uwepo wa hapa duniani, Mimi na wewe tunayajua mambo ya hapa duniani na tunaona yanayoendelea,tunaona watu wakizaliwa(kuja duniani) na tunaona watu wakifa(kuondoka duniani).
Hivyo tunajua kuwa mtoto anapozaliwa anakuwa amekuja duniani yani umeonekana uwepo wake duniani na si kwamba amesababisha kuwepo dunia wala vilivyopo,kwa sababu hii dunia na mambo yote tunayoyajua huku duniani yalikuwepo kabla uwepo wake hapa duniani. Na hivyo hivyo tunajua kuwa mtu akifa(kuondoka duniani) pia anaiacha dunia na mambo yake,hivyo kutokuwepo kwake hakufanyi dunia na mambo yake yasiendelee kuwepo.
Kwa hiyo hata mie nisipokuwepo duniani kiuhalisia hayo ndiyo yatakuwa yakiendelea duniani bila kujari huko niliko mimi najua au sijui,hivyo si sawa kusema usipokuwepo hakuna kilichopo hivyo kama hatupo basi uwepo wetu haupo duniani tu ila mambo ya duniani yatakuwepo na yenye kuendelea yataendelea kama tunavyojua na kushuhudia hivi sasa.
Mkuu tunaposema kuwepo tunazungumzia uwepo wa hapa duniani, Mimi na wewe tunayajua mambo ya hapa duniani na tunaona yanayoendelea,tunaona watu wakizaliwa(kuja duniani) na tunaona watu wakifa(kuondoka duniani).
Hivyo tunajua kuwa mtoto anapozaliwa anakuwa amekuja duniani yani umeonekana uwepo wake duniani na si kwamba amesababisha kuwepo dunia wala vilivyopo,kwa sababu hii dunia na mambo yote tunayoyajua huku duniani yalikuwepo kabla uwepo wake hapa duniani. Na hivyo hivyo tunajua kuwa mtu akifa(kuondoka duniani) pia anaiacha dunia na mambo yake,hivyo kutokuwepo kwake hakufanyi dunia na mambo yake yasiendelee kuwepo.
Kwa hiyo hata mie nisipokuwepo duniani kiuhalisia hayo ndiyo yatakuwa yakiendelea duniani bila kujari huko niliko mimi najua au sijui,hivyo si sawa kusema usipokuwepo hakuna kilichopo hivyo kama hatupo basi uwepo wetu haupo duniani tu ila mambo ya duniani yatakuwepo na yenye kuendelea yataendelea kama tunavyojua na kushuhudia hivi sasa.
Aueleweki ..... nonsense