Usipuuze ndoto unazoota pindi unapokuwa umelala

Usipuuze ndoto unazoota pindi unapokuwa umelala

Mimi niliota nimetokewa na mtu mweupe pee kama theluji,alishuka kutoka mawinguni akanikabidhi kitu kama fimbo kama île Tochi ya olympic. Yaani fimbo ina moto live akanikabidhi akaniambia nimchape kwa hiyo fimbo adui yeyote yule.Yaani tokea hiyo siku niliamka na nguvu za ajabu na ninajiamini kupita maelezo ninaamini.ninaposses power ambayo hapa duniani hakuna wa kunishinda hata Putin yaani.
nzuri hongera.
 
Baada ya kumaliza chuo, nillikua naota ndoto Nimepata kazi au fursa nzuri, lakini kwenye maisha halisi Hali ilikua tofauti,,toka hapo sijawahi kuziamini ndoto tena
 
Nilishawahi kuota naongea na watu wakubwa Sana nchi hii sasa sjui bange

Nilishawahi kuota mchizi wangu mtaani anabiashara ya pool table niliota anachezesha ila kete zake zimepasuka Nini maana yake?

Leo nmeota mmeshindwa pata alama flani kwenye interview ninayoenda kufanya soon utumishi dah!

Nielezee maana zake

1) Kuota unaongea na watu wa kubwa ni hatima nzuri uliyokusudiwa kunyanyuliwa na kuketi meza moja na wakuu kwa case yako kwa vile unapambania kupata ajira.Ni kama vile unakusudiwa kupata mafanikio let say kupata hiyo kazi na utakuwa ofisi moja serikali moja au taasis moja MEZA yani inayokupatia chakula ajira

2) Hii ya pool table kete kupasuka sio sio ishara nzuri kwenye hiyo biashara yake ya hiyo mchezo ni uharibifu wa hiyo biashara kwake sio kwako

3) KUFELI interview na kupata marks ndogo ni mbaya ,unatakiwa uchukue hatua za dharura mana kufeli interview sio mpango wa Mungu mana ukitakiwa kukaa meza moja na wakuu upate kazi sasa hii ya kufeli interview unapingana na kupata kazi, unatakiwa usali tena ikibidi ufunge kuombea hiyo roho ya kufelishwa ipotee zaidi katoe na sadaka nenda kwa mtumishi wako akuombee neno la baraka madhabahuni unapopeleka sadaka yako toa, omba sana kuwq na imani usiogope Mungu atakusaidia kufaulu interview, mikwamk itaondoka utaketi meza moja na wakuu.
 
Tafasiri basi hiyo ndoto.
Mtu mweupe(mwenye mavazi meupe) kama theluji (Mweupe /mavazi meupe ni mtakatifu msafi asiye na dhambi kadiri wepe unavyozidi ku intensify ina maana utakatifu umezidi sana kiwangi cha uungu kuna waliomuona akin'gaa kama jua kiasi kwamba huwezi kumtazama au ukimtazama unaanguka chini kifudi fudi (sasa kiwangi cha kung'aa kikizidi kama jua anakuwa Yesu(tuseme huyo ni Yesu au malaika) ,ametokea mbinguni maana ufalme wa NURU wa mbinguni ,mbinguni wanaishi watakatifu.
2)amekupa zawadi zawadi kutoka mbinguni ambayo amekwambia unaweza kuitumia kushinda maadui ni (ROHO MTAKATIFU)inayowaka moto ni nguvu ya roho mtakatifu,ama neno la Mungu maandiko au neno la mungu pia ni ROHO (neno ni roho)na ni silaha ,ni moto ulao
ila fimbo pia inaweza ikawa ni ishara ya uongozi,(kwa scenario yako uongozi unaotakiwa ni kama uchungaji ,uinjilist kuhubiri neno)NENO la Mungu pia ni taa au torch inayomulika
totrch ya olympics sifahamu mana sifuatilii sana michezo ya kidunia tena kama olympics mingine ni ya kipagani ni ibada za kishetani huwa sifuatilii vitu vyenye asili ya giza(ila kama ina maana ya kombe au taji) hivi all in all umepewa kitu kizuri.
3)ukijumlisha na HISIA ya furaha,furaha ,amani,upendo hayo ni matunda ya ROHO MTAKATIFU moyoni ,kujazwa nguvu na kujiona umeongezdka nguvu ,naweza kusema umejazwa nguvu za Mungu au Roho mtakatifu,mana kila mtu ana roho wa Mungu ndani yake maana ufalme wa Mungu upo ndani yetu na huwa anatusemesha habari njema na kutukataza na kutuonya tuache mabaya na tukose amani ya kufanya mabaya.Ila kwa case yako wewe umehiishwa ROHO wako mtakatifu umejazwa zaidi.Na ukitaka aendelee kujaa zaidi ni kiendelea kupunguza mizigo ya dhambi uchafu moyoni ilia pate nafasi ya kujaaa na kutawala mpaka kufurika kadiri unavyopunguza dhambi uchafu moyoni unamuongezea room ya yeye kujaa na mpaka kufurika kama maji akifutumia mpaka kumwagika ndio nguvu huongezeka zaidi.
ANGALIZO
Hiyo state ni dyanamic yani Roho mtakatifu na hiyo hali ya furaha na hiyo nguvu inawezs ikaondoka kama utaendelea kufanya dhambi,na nguvu zikaisha.Ndio maana ni heri kumaliza vizuri kuliko kuanza vizuri na kumaliza vibaya.
HITIMISHO.
Shikilia sana hiyo imani yako na matendo yako mema ,ndoto hiyo uliyoota si rahisi mtu anayeishi maisha ya dhambi akaota ndoto nzuri kama hiyo.Hivyo shika sana ,linda sama moyo wako usianguke katika dhambi.Pia unaeweza ukatumia karama hiyo kusaidia wwngine mana umepewa fimbo uongozi uchunge kondoo sasa ili nao wafikie viwango vyako,hata kuombea wengine wakapona unaweza umejazwa nguvu nyingi ,hiyo karama isaidie sasa wengine isiishie kwako tu,mpango wa Mungu ni kuwaokoa watu wote na kiwaponya wengi(watu wote) sio wachache tu.
 
1) Kuota unaongea na watu wa kubwa ni hatima nzuri uliyokusudiwa kunyanyuliwa na kuketi meza moja na wakuu kwa case yako kwa vile unapambania kupata ajira.Ni kama vile unakusudiwa kupata mafanikio let say kupata hiyo kazi na utakuwa ofisi moja serikali moja au taasis moja MEZA yani inayokupatia chakula ajira

2) Hii ya pool table kete kupasuka sio sio ishara nzuri kwenye hiyo biashara yake ya hiyo mchezo ni uharibifu wa hiyo biashara kwake sio kwako

3) KUFELI interview na kupata marks ndogo ni mbaya ,unatakiwa uchukue hatua za dharura mana kufeli interview sio mpango wa Mungu mana ukitakiwa kukaa meza moja na wakuu upate kazi sasa hii ya kufeli interview unapingana na kupata kazi, unatakiwa usali tena ikibidi ufunge kuombea hiyo roho ya kufelishwa ipotee zaidi katoe na sadaka nenda kwa mtumishi wako akuombee neno la baraka madhabahuni unapopeleka sadaka yako toa, omba sana kuwq na imani usiogope Mungu atakusaidia kufaulu interview, mikwamk itaondoka utaketi meza moja na wakuu.
Nakushukuru Sana mkuu
 
Back
Top Bottom