under timer
JF-Expert Member
- Dec 25, 2021
- 389
- 595
Umemjibu vemaNimekosa pa kunukuu mkuu kwakuwa nukuu zote zilizopo zimeandikwa na wanufaika wa sadaka. Hapa nimetumia uncommon sense, ufunuo na kutazama viumbe wengine. Hebu niambie Mungu na hela vinaendana? atanunulia nini ukimpa fedha, je ana tumbo na mdomo? je, anategemea utakachompa?
Unataka kusema yule aliyegundua kibatari alete reference alitoa wapi wazo la kutengeneza kibatari, aliyegundua gari ane alete reference, aliyegundua kuvaa chupi nae aeleze katoa wapi, wewe kaka amka.Kaleta hoja kuhusu mambo ya Mungu, halafu hana reference kutoka andiko lolote, hatuwezi kusema yupo sahihi Ila tutasema ana roho ya korosho ama mkono wa birika.
ApiaMungu wetu alishatuumba, akawakabidhi wazazi wako wakamilishe mchakato wa uliobakia wa kukuzaa, kukulisha, kukuvalisha na kukutunza kwa muda fulani kabla na wewe hujaanza kujitunza na kuzaa watoto wengine. Kama ni sadaka mpe mzazi wako anaeweza kuitumia hiyo sadaka sio Mungu kwakuwa Mungu hana matumizi ya sadaka; fedha, chakula wala mifugo yako maana vitu vyote ni vyake vinatoka kwake na anavyo vingi kuliko baba na mama yako. Wazazi wako wana matumizi, wana mwili, wana mdomo, na wana tumbo hivyo wanajua nini cha kufanya ukiwapa pesa, nguo, chakula, mifugo. Mungu wetu anataka ushukuru tu na kumsifu kama vile unavyomsifu TOYOTA kwa kutengeneza aina ya gari lako unaloliendesha. Baada ya TOYOTA kutengeneza gari lako kazi yako ni kuisifu toyota lakini sio kutoa zawadi, malipo au kuiomba toyota ikupatie mafuta ya gari lako, ukupakie rangi gari lako wala kulifanyia matengenezo gari lako.
Kuna watu wanapoteza Muda wao mwingi kwa Kuomba Mungu badala ya Kushukuru mungu, Kuna watu wanapoteza mali zao nyingi kwa kutoa sadaka kwa Mungu badala ya kuwapa wazazi wao. Wanakosea sana na hawajui walifanyalo zaidi ya kuwatajirisha watu wanaozipokea mali (sadaka) zao. Mungu hana shida lakini wazazi wako wana shida.
Anza na wazazi wako kwanza uone mambo yako yatakavyokunyookea haraka. Kama kila mtu akihangaika na wazazi wake Mungu atasikia vilio na maombi yao haraka kwakuwa wazazi ndio bomba lako linalopitisha maombi kutoka kwako kupitia kwa wazazi, mababu, mitume, kupitia kwa Adam na Hawa hadi kumfikia Mungu, kwakuwa Adam na Eva wanamfahamu Mungu zaidi kuliko wewe, na babu yako yuko karibu na Adam baba yako na baba yako yuko karibu na babu yako na wewe uko karibu na baba yako. Ndiyo maana kila anaewadharau wazazi na mababu zake hafiki mbali kwakuwa Mungu yukokaribu nao zaidi kuliko wewe. kila mtu anatoa sadaka kila siku anapomsaidia mtu mwingine jambo hata kumuonyesha njia, kumpa maji ya kunywa, kumbeba, kumpa chakula au soda, umeshalipa sadaka tayari lakini mzazi wako ni wajibu sio hiari.
Sadaka unayotoa haifiki kwa Mungu bali inaliwa tu na wajanga wanaojifanya wanaipeleka kwa Mungu. Tafuta mayatiba na wajane wape kama unataka kuwapa, lakini wajali zaidi wazazi wako, utaona mambo na miujiza wasiyoiweza "watumishi wa mungu" unaowapa hela zako kila siku. Unatapeliwa ndugu yangu, fumbua macho yako.
Nafahamu. Hii ni biashara kubwa sana ya wajinga kwa kutumia jina la mungu. We chunguza tu, kila mchunga kondoo anaposema na kutenda jambo (maombi, kuhubiri, kufynga ndoa, maziko, nk), mwishoweeee kulee ataishia na kukusanya sadaka.unaanzisha vita na wachunga kondoo
Bora wale wazee wetu.Ni kweli Mkuu
Kweli KABISA!
Sadaka KWA nyumba za ibada ni wizi uliohalalishwa KABISA na Taasisi!!
Hata zaka walizotoa Wana wa Israel zili liwa na hao watoaji na kubakiza kidogo KWA walawi AMBAO Ndio walipewa jukumu Sasa leo KILA mtu ni kuhani nani wa kumpa mwenzake sadaka!??
Tuwape WAZAZI tu Basi!
hatari sanaNafahamu. Hii ni biashara kubwa sana ya wajinga kwa kutumia jina la mungu. We chunguza tu, kila mchunga kondoo anaposema na kutenda jambo (maombi, kuhubiri, kufynga ndoa, maziko, nk), mwishoweeee kulee ataishia na kukusanya sadaka. Huyo MUNGU anatumbo gani la kula sadaka zote hizodunia nzima? ni upuuzi tu, ni heri wangeyaita malipo au ada ya kusema au kutenda jambo fulani kuliko kuita sadaka.
Hawa wa siku hizi ni wala kondoounaanzisha vita na wachunga kondoo
Wakati waliotuletea dini wakiendelea na sera za ushoga na kutengeneza mabomu makubwa ya kuuwa watu sisi tunahangaika na sadaka. Wajinga hawataisha kaka endelea kuhifadhi kucha za majogoo unaowachinja, zitapata kazi.Africa bila di....i uchuro ingefika mbali
Hiyo sasa ndio sadaka pendwa na kusudiwa, ndio maana hata mitume na mababu zetu walikuwa wanatoa vyakula na wanyama wanaokwenda kusaidia watu na wanyama wengine kuongezea kile walichopewa na Mungu ambacho hakikuwatosha au kuwafikia kwasababu mbalimbali.Sadaka ya kweli ni ile inayoliwa na wazazi wako pamoja na familia yako.
Nyingine ni ile inayoliwa na watu mbalimbali wasiojiweza
Nilikwambia hata wazungu hawatoi pesa madhabahuni kaka, ndio maana sasa hivi kule ulaya na marekani makanisa yamebaki yaleyale na hayapati watu, unaweza kutoka Kariakoo kufuata kanisa Kibaha sasa hivi kule. Wakati huku kwetu kila mtaa una makanisa 4.Sadaka ina siri kubwa katika mafanikio yako,Hata hao wazungu wanatoa sana ndio maana wanafanikiwa