Usitoe sadaka, umeshatoa

Usitoe sadaka, umeshatoa

Ni kweli Mkuu

Kweli KABISA!

Sadaka KWA nyumba za ibada ni wizi uliohalalishwa KABISA na Taasisi!!

Hata zaka walizotoa Wana wa Israel zili liwa na hao watoaji na kubakiza kidogo KWA walawi AMBAO Ndio walipewa jukumu Sasa leo KILA mtu ni kuhani nani wa kumpa mwenzake sadaka!??

Tuwape WAZAZI tu Basi!
sada haziendi kwa Mungu, na Mungu hali sadaka. Kila mtu anatoa na kupokea sadaka kila siku, na ukitoa zaidi utapokea zaidi, mfano kama wewe unatoa michango (sadaka) mingi ya harusi kwa watu wengi zaidi nawewe utapokea michango mingi zaidi kutoka kwa watu kama ukiwa na jambo lako, kama wewe unahudhuria misiba ya watu na wewe utapata watu wengi kwenye misiba utakayoipata. Maana sadaka ni msaada, pale zamani kulikuwa hakuna pesa hivyo sadaka ilikuwa ni chakula, wanyama, na mazao, baadae ikaongezeka nguo na fedha.

Sadaka usitoe madhabahuni kwenye vihenge, umeliwa. Anaekusanya ile sadaka pale madhabahuni kitu cha kwanza kabisa anakwenda kutoa sadaka kwa wazazi wake kwakuwa anafahamu umuhimu wa wazazi, maana kuna maandiko kabisa yanayomtaka mtu Awaheshimu Baba na mama yake ili siku zake ziwe nyingi zilizobaki anakwenda kufanyia mambo yake. Shida iko kwako ambae badala ya kumpa baba na mama yako sadaka umempa mla kondoo tu basi na kuwaacha wazazi wako.
 
Kila Mtu na life style yake, na kizuri zaidi maisha hayanaga kanuni unaweza usitoe na ukawa msindikizaji tu wa mafanikio ya wengine miaka nenda rudi [emoji124][emoji1]

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Unataka kusema yule aliyegundua kibatari alete reference alitoa wapi wazo la kutengeneza kibatari, aliyegundua gari ane alete reference, aliyegundua kuvaa chupi nae aeleze katoa wapi, wewe kaka amka. Hebu elezea namna sadaka yako ya sh. 10,000 iliyompa mtu wa Mungu itakavyomfikia Mungu huko mbinguni. Tueleze kama Mungu ana shida ya hela au nyama. Tueleze hizo sadaka Mungu anaziweka wapi kwa kazi gani.
Acha kubwia ugoro hiyo kitu huharibu kabisa akili 😜
 
Uunawaacha inamaanisha unaanza maisha mapya na mkeo haimaanishi uwadharau.... Anamalizia uishi miaka mingi na upate heri katika nchi upewayo na BWANA Mungu wako
Siwezi kuwadharau wazazi wangu ila nitaenda kuanzisha familia pasipo kuwategemea wao (kiuchumi)
 
Waheshimu baba yako na mama yako ili siku zako za kuishi ziwe nyingi.

Hakuna upinzani ktk hilo

Ila mtoa mada hajui alisemalo ktk huu uzi wake.
na heri duniani, anawasema wanaomjali pastor kuliko wazazi
 
Mungu wetu alishatuumba, akawakabidhi wazazi wako wakamilishe mchakato uliobakia wa kukuzaa, kukulisha, kukuvalisha na kukutunza kwa muda fulani kabla na wewe hujaanza kujitunza na kuzaa watoto wengine. Kama ni sadaka mpe mzazi wako anaeweza kuitumia hiyo sadaka sio Mungu, kwakuwa Mungu hana matumizi ya sadaka; fedha, chakula wala mifugo yako maana vitu vyote ni vyake vinatoka kwake na anavyo vingi kuliko baba na mama yako. Wazazi wako wana matumizi, wana mwili, wana mdomo, na wana tumbo, hivyo wanajua nini cha kufanya ukiwapa pesa, nguo, chakula, mifugo. Mungu wetu anataka ushukuru tu na kumsifu kama vile unavyomsifu TOYOTA kwa kutengeneza aina ya gari lako unaloliendesha. Baada ya TOYOTA kutengeneza gari lako kazi yako ni kuisifu toyota lakini sio kutoa zawadi, malipo au kuiomba toyota ikupatie mafuta ya gari lako, ukupakie rangi gari lako wala kulifanyia matengenezo gari lako.

Kuna watu wanapoteza Muda wao mwingi kwa Kuomba Mungu badala ya Kushukuru mungu, Kuna watu wanapoteza mali zao nyingi kwa kutoa sadaka kwa Mungu badala ya kuwapa wazazi wao. Wanakosea sana na hawajui walifanyalo zaidi ya kuwatajirisha watu wanaozipokea mali (sadaka) zao. Mungu hana shida lakini wazazi wako wana shida.

Anza na wazazi wako kwanza uone mambo yako yatakavyokunyookea haraka. Kama kila mtu akihangaika na wazazi wake Mungu atasikia vilio na maombi yao haraka kwakuwa wazazi ndio bomba lako linalopitisha maombi kutoka kwako kupitia kwa wazazi, mababu, mitume, kupitia kwa Adam na Hawa hadi kumfikia Mungu, kwakuwa Adam na Eva wanamfahamu Mungu zaidi kuliko wewe, na babu yako yuko karibu na Adam, baba yako yuko karibu na babu yako, na wewe uko karibu na baba yako. Ndiyo maana kila anaewadharau wazazi na mababu zake hafiki mbali kwakuwa Mungu yuko karibu nao zaidi kuliko wewe.

kila mtu anatoa sadaka kila siku anapomsaidia mtu mwingine jambo, hata kumuonyesha mtu njia, kumpa mtu maji ya kunywa, kumbeba, kumpa chakula au soda, umeshalipa sadaka tayari, lakini mzazi wako ni wajibu sio hiari kumpa sadaka zako.

Sadaka unayotoa haifiki kwa Mungu bali inaliwa tu na wajanga wanaojifanya wanaipeleka kwa Mungu. Tafuta mayatima na wajane wape kama unataka kuwapa, lakini wajali zaidi wazazi wako, utaona mambo na miujiza wasiyoiweza "watumishi wa mungu" unaowapa hela zako kila siku. Unatapeliwa ndugu yangu, fumbua macho yako.
Hivi unaamini tunapotoa sadaka tunataka akazile Mungu?

!!!!
 
Mungu anapokea dhamira na nia sio vitu na matendo yako. Unaonekana unaswali kumbe ni mchawi tu. Usikubali kumpa mtu sadaka, ni chukizo mbele ya Mungu, hahitaji chochote kutoka kwetu zaidi ya kumsifu, kumtangaza na Kumshukuru yeye baasi. Na Mungu hajibu maombi ya mtu mmoja mmoja na wewe huna hadhi ya kuongea na Mungu wala kuoona uso wa Mungu, huna uwezo na dhamani hiyo, wewe utaishia kumuomba mzazi wako tu na yeye atayapeleka maombi yako kwa baba yake na baba yake atayapeleka kwa baba yake ambae siku ya siku yatamfikia Adam na hawa ambao wao ndio wenye hadhi na sifa ya kuyawasilisha kwa Mungu, yaani protocol lazima izingatiwe. Ndiyo maana kama wewe huna mahusiano mazuri na wazazi wako unaowafahamu kwa sura usijihangaike kabisa na maswala ya Mungu ambae hujawahi kumuona.
Kwa hiyo watoto yatima wapeleke hoja zoa kwa nani?
 
Back
Top Bottom