Usiyoyajua kuhusu Biashara ya Simu za Kariakoo, ukijua haya utakuwa mjanja…
Ugomvi kati ya wateja na wauzaji wa simu, hasa hizi used za Dubai au refurbished, ni jambo linalotokea mara nyingi. Mara nyingi, chanzo kikuu ni pale simu inapoharibika, na mteja anataka kuirejesha ili abadilishiwe. Kuna wakati muuzaji anakuwa sahihi, na kuna wakati mteja anakuwa sahihi. Je, ni katika mazingira gani hali hizi hutokea?


Naitwa Mkisi

Nauza simu na laptop hapa Kariakoo kwa muda wa miaka 7 sasa. Natoa maarifa na makala kama hizi kila siku. Pia nina group WhatsApp na Telegram kwa updates za bei za jumla za simu na laptop.


Kesi za Ugomvi wa Wateja na Wauzaji wa Simu

Nina uzoefu mkubwa wa kushughulikia kesi kama hizi, hasa kwenye simu kuliko laptop. Kesi hizi hutokea pale ambapo:

  1. Mteja amenunua simu, kisha ikaharibika kwa bahati mbaya au makusudi, na anataka kuirejesha dukani ili abadilishiwe nyingine.

Mazingira Ambayo Muuzaji Anaweza Kukusaidia

  1. Simu yako ikiharibika kwa tatizo la software, kama vile:
    • Haishiki mtandao
    • Ime-corrupt
    • Inastack
    • Haipandishi mtandao
  2. Simu iliyo zima yenyewe tu bila sababu. Hii ni baada ya fundi kuthibitisha kuwa simu imezima bila sababu ya msingi.

Mazingira Ambayo Muuzaji Hataweza Kukusaidia

  1. Ukiharibu simu kwa kuidumbukiza kwenye maji.
  2. Simu ikiharibika kwa kupiga shoti kwenye motherboard.
  3. Simu ikiharibika kioo, iwe kwa bahati mbaya au makusudi (imeanguka, kugongwa, n.k.).
  4. Ukiamua kubandua sticker inayounganisha kioo na body ya simu, ambayo huonyesha kama simu imefunguliwa au la.

Shida Haswa Huwa Wapi?

Tatizo kubwa ni kwamba:

  • Wateja wengi hawasomi terms & conditions zilizowekwa kwenye warranty card.
  • Kuna dhana potofu kwamba wauzaji wote wa simu, hasa mtandaoni, ni matapeli au wanauza simu mbovu.

Mfano wa Terms & Conditions za Warranty

Kama mteja, unatakiwa kuelewa kwamba warranty haitaweza kusaidia katika hali zifuatazo:

  1. Ukiharibu kioo cha simu kwa bahati mbaya au makusudi.
  2. Ukiingiza simu kwenye maji.
  3. Simu ikiwa na tatizo lingine lakini ukairudisha ikiwa na crack kwenye kioo.
  4. Simu ikipiga shoti.

Ushauri Wangu

  1. Ili kuepusha ugomvi, ukiona ni ngumu au hatarishi, bora usinunue bidhaa hiyo, tafuta mbadala.
  2. Tafuta store nzuri ya simu ambayo inauza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu.

Wote lenu moja
 
Umetupa onyo na siri ulizotuahidi hujatupa, basi lipia hata tangazo
Ugomvi kati ya wateja na wauzaji wa simu, hasa hizi used za Dubai au refurbished, ni jambo linalotokea mara nyingi. Mara nyingi, chanzo kikuu ni pale simu inapoharibika, na mteja anataka kuirejesha ili abadilishiwe. Kuna wakati muuzaji anakuwa sahihi, na kuna wakati mteja anakuwa sahihi. Je, ni katika mazingira gani hali hizi hutokea?


Naitwa Mkisi

Nauza simu na laptop hapa Kariakoo kwa muda wa miaka 7 sasa. Natoa maarifa na makala kama hizi kila siku. Pia nina group WhatsApp na Telegram kwa updates za bei za jumla za simu na laptop.


Kesi za Ugomvi wa Wateja na Wauzaji wa Simu

Nina uzoefu mkubwa wa kushughulikia kesi kama hizi, hasa kwenye simu kuliko laptop. Kesi hizi hutokea pale ambapo:

  1. Mteja amenunua simu, kisha ikaharibika kwa bahati mbaya au makusudi, na anataka kuirejesha dukani ili abadilishiwe nyingine.

Mazingira Ambayo Muuzaji Anaweza Kukusaidia

  1. Simu yako ikiharibika kwa tatizo la software, kama vile:
    • Haishiki mtandao
    • Ime-corrupt
    • Inastack
    • Haipandishi mtandao
  2. Simu iliyo zima yenyewe tu bila sababu. Hii ni baada ya fundi kuthibitisha kuwa simu imezima bila sababu ya msingi.

Mazingira Ambayo Muuzaji Hataweza Kukusaidia

  1. Ukiharibu simu kwa kuidumbukiza kwenye maji.
  2. Simu ikiharibika kwa kupiga shoti kwenye motherboard.
  3. Simu ikiharibika kioo, iwe kwa bahati mbaya au makusudi (imeanguka, kugongwa, n.k.).
  4. Ukiamua kubandua sticker inayounganisha kioo na body ya simu, ambayo huonyesha kama simu imefunguliwa au la.

Shida Haswa Huwa Wapi?

Tatizo kubwa ni kwamba:

  • Wateja wengi hawasomi terms & conditions zilizowekwa kwenye warranty card.
  • Kuna dhana potofu kwamba wauzaji wote wa simu, hasa mtandaoni, ni matapeli au wanauza simu mbovu.

Mfano wa Terms & Conditions za Warranty

Kama mteja, unatakiwa kuelewa kwamba warranty haitaweza kusaidia katika hali zifuatazo:

  1. Ukiharibu kioo cha simu kwa bahati mbaya au makusudi.
  2. Ukiingiza simu kwenye maji.
  3. Simu ikiwa na tatizo lingine lakini ukairudisha ikiwa na crack kwenye kioo.
  4. Simu ikipiga shoti.

Ushauri Wangu

  1. Ili kuepusha ugomvi, ukiona ni ngumu au hatarishi, bora usinunue bidhaa hiyo, tafuta mbadala.
  2. Tafuta store nzuri ya simu ambayo inauza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu.

 
Miaka kumi iliyopita, nilinunua huawei ngoma dakika 30 inaua 100% betri. Sikutaka kurudi nikaapa sitorudia kununua simu kkoo.
I never did. Once nilimpeleka mtu nikamwambia bora ununue boxed infinix kuliko note 8 samsung ya used kkoo.
 
Hujatoa siri mkuu, waambie mnauza used nyingi ambazo IMEI number zimechezewa..wajue status ya OFFICIAL na CUSTOMIZED.

Waambie kuna samsung mnauza S8 hadi S10, nyingine zina charging port type C na nyingine port type B. Waambie zimepigwa spana sana na ndani unakuta betri ya za simu ndogo kama tecno na itel. Simu ni Samsung S9 lkn ndani unakuta betri la tecno.

Waambie simu mnazouza, circuit zimefanyiwa looping kwa waya kama redio za mwaka 90 na kusababisha kupata moto sana kama pasi. Zimevalishwa body nzuri nje na boksi nzuri zinazotengenezwa na wachina.

Waambie, mkienda dubai mnauziwa kwa mafungu na ndani yake zipo mchanganyiko wa mbovu na nzima...hakuna kuchagua.

Ongezea uhuni mwingine......
 
M
Hujatoa siri mkuu, waambie mnauza used nyingi ambazo IMEI number zimechezewa..wajue status ya OFFICIAL na CUSTOMIZED.

Waambie kuna samsung mnauza S8 hadi S10, nyingine zina charging port type C na nyingine port type B. Waambie zimepigwa spana sana na ndani unakuta betri ya za simu ndogo kama tecno na itel. Simu ni Samsung S9 lkn ndani unakuta betri la tecno.

Waambie simu mnazouza, circuit zimefanyiwa looping kwa waya kama redio za mwaka 90 na kusababisha kupata moto sana kama pasi. Zimevalishwa body nzuri nje na boksi nzuri zinazotengenezwa na wachina.

Waambie, mkienda dubai mnauziwa kwa mafungu na ndani yake zipo mchanganyiko wa mbovu na nzima...hakuna kuchagua.

Ongezea uhuni mwingine......
Machimbo ya simu za mafungu Dubai ni sehemu gani? Nitapita pale ninavorudi home,nikaangalie...au Deira?
 
Back
Top Bottom