Utabiri: PSG Ndio Mabingwa Wa UEFA Champions League 2021

Utabiri: PSG Ndio Mabingwa Wa UEFA Champions League 2021

Kichwa Kichafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2017
Posts
44,855
Reaction score
189,385
7kmm.jpg

Habari.

Hadi sasa zimebaki timu nne ambazo zitacheza hatua ya nusu fainali na ratiba:

Leg 1.
27 April 2021 Tuesday

Paris Saint Germain Vs Manchester City


Real Madrid Vs Chelsea


Leg 2.
04 May 2021 Tuesday

Manchester City Vs Paris Saint-Germain

Chelsea Vs Real Madrid


Hapo bila kupepesa macho mpira anaocheza Paris Saint Germain dhidi ya kocha wao Pochettino umekuwa na nidhamu ya kutafuta matokeo tu hakuna kingine.

Hivyo basiasi ubishe usibishe Paris Saint Germain atakuwa Champion wa ligi ya mabingwa ulaya.

Final itachezwa 29 May 2021 Ataturk Olympics Stadium.

Final itakuwa ni Paris Saint Germain Vs Real Madrid na bingwa atakuwa Paris Saint Germain.


Updates. 29/04/2021

Baada ya first leg matokeo yamekuwa yakishangaza kulingana na uzi wenyewe ila amini nawaambia wengi watashangazwa zaidi baada ya 2nd leg.

1st leg.

Real Madrid 1 - 1 Chelsea
✓Pulisic[emoji460]
✓Benzema[emoji460]

PSG 1 - 2 Manchester city
✓Marquinhos[emoji460]
✓De Bruyne [emoji460]
✓Mahrez [emoji460]

Hakika naendelea kuona PSG bado ana nafasi ya kusonga mbele vizuri kabisa kwa mpira niliyoona jana kwa zaidi ya dakika 50 alipiga mpira mwingi sana na hata Etihad nategemea wataweza kupindua meza vyema.

Real Madrid ana nafasi ngumu japo Chelsea waliweza kupambana na kucheza mpira mwingi ila pale darajani naona watalala na viatu pia naendelea kumpa nafasi Real Madrid kuendelea mbele.

Updates. 06/05/2021

Baada ya 2nd leg iliyochezwa tar 4th & 5th May 2021.

Hakika matokeo yamekuwa tofauti kabisa na maudhuhi ya huu uzi maana timu zote zikizopewa nafasi na huu uzi zimepokea kipigo cha mbwa mwizi yaani kipigo cha mtema-kuni.

Chelsea 2 - 1 Real Madrid
✓Timo Werner[emoji460]
✓Mason Mount[emoji460]

Manchester city 2 - 0 PSG
✓Mahrez[emoji460]
✓Mahrez [emoji460]



Hivyo kufanya vikongwe kutoka spain kulamba mwiko mkavu huku hawa wakulima kutoka ufaransa wakirudi na majembe pamoja na vifaa vyote vya shambani kwao wakiambulia patupu. Na kufanya marudio ya kuingia timu zote kutoka England.

Chelsea. Vs Manchester city

Tusubiri fainali hiyo ikiwa wengi wana prediction tofauti tofauti ila upande wangu hadi sasa sijui nani na sina prediction yeyote yangu ni macho kama ni usambuzi basi nimepiga F.

Nawasilisha Mzee Mkoloni.

Cc: Kichwa Kichafu
 
Kwenye soka lolote linaweza kutokea na hutakiwi kubeza.
Kuna mwana kakomaa kabisa anakwambia piga uwa Chealsea anabeba ubingwa,na ukimbishia anakwambia minaweka laki moja wewe weka kishkizo cha shati.

Kwa mara ya kwanza kabisa nafanana mtazamo na mbumbumbu fc!!
Naunga mkono hoja.

Natamani sana chama langu la Chelsea libebe ndoo mwaka huu! Ika tatizo lake lina watoto wengi wa chekechea na ina washambuliaji butu ukilinganisha na wakongwe wa Real Madrid, PSG na Man City.
 
PSG hawafurukuti zaidi wanategemea individual brilliance ya Mbappe, na ninavyomfahamu Guardiola atatafuta mfumo utakaomficha huyo Mbappe hataonekana uwanjani kama ilivyotokea kwa Haaland, nampa nafasi Man City kwenda fainali na ikitokea akafika fainali bado nampa City nafasi ya kuwa bingwa kama atakutana na Madrid, City wana ubora wa kikosi Madrid wanabebwa na historia tu.
 
Real madrid hua wanapandwa na mapepo ya ubingwa wakifika nusu fainali. Ukiangalia jana walicheza bila mabeki wao watatu wa kuwategemea. Sergio Ramos, Raphael Varane, Dan Carvajal. Pale katikati wana casemiro, mondrick, na Krose. Viungo wote hawa ni Seniors na wana uzoefu mkubwa sana, pamoja na kua wamechukua uefa mara nne ndani ya madrid, ila wanakua na njaa ya mafanikio vibaya mno.
Angalia jana walivyocheza, ni kama timu mbovu hivi, lakini zidane ni kocha wa matokeo, hana mpira mzuri ila...
 
Back
Top Bottom