Nimeangalia michezo mitatu ya kaiza chiefs: 1. Wa kwanza ni ule wa juzi juzi kwenye ligi yao ya ndani. Hawakucheza vizuri na huwezi kuamini kuwa hak ndio wako robo fainali ya caf champions league. 2. Wa pili ni ule waliocheza na Horoya kwenye mashindano haya ya champions league. Kwenye mchezo huu Kaizer chiefs ilikuwa kama timu nyingine kabisa! Wanacheza mpira kwa nguvu na kujituma sana. Simba watarajie kaizer chiefs kama hii!!?. 3. Mchezo wa tatu ni ule waliocheza na mamelod sundowns kwenye ligi ya ndani!! Huwezi kuamini!! Kaizer chiefs ilikuwa bora sana na mamelod sundowns waliangukia pua! Simba ategemee kukutana na Kaizer chiefs iliyochangamka!!
Kaizer chiefs ni timu ambayo hua inapania sana inapocheza na timu kubwa kwa lengo la kujitangaza. Simba wategemee upinzanj wa hali ya juu. Naamini mwisho wa siku Simba itaibuka mshindi ila si kwa mtelemko!!