Utafanyaje mkeo au mumeo au mzazi wako akiwa na mambo ya Kishirikina? Hivi ñdivyo utakavyofañya

Utafanyaje mkeo au mumeo au mzazi wako akiwa na mambo ya Kishirikina? Hivi ñdivyo utakavyofañya

Dah , ukishaona akili yako ni ndogo kuthibitisha hilo tambua kabisa Mungu hayupo labda tu ni wewe ulishindwa kuelewa walio leta hiyo nadharia ya Mungu walimaanisha nini.

Nadharia ya Mungu haijaletwa
Ila miungu imeletwa.

Duniani kote Watu huamini Mungu yupo aliyeumba mbingu na nchi.

Lakini jamii nyingi ziliamua kubuni miungu inayoonekana ili kuthibitisha yule asiyeonekana
 
Mtu yoyote ambaye haamini katika uwepo wa Ushirikina nae ni mnafiki.

Soma mada uelewe.

Kuamini ushirikina ni jambo moja.
Kutambua uwepo wa ushirikina ni jambo jingine.
Unaweza kutambua jambo fulani lipo lakini usiliamini


Soma kwa ufahamu
 
Nadharia ya Mungu haijaletwa
Ila miungu imeletwa.

Duniani kote Watu huamini Mungu yupo aliyeumba mbingu na nchi.

Lakini jamii nyingi ziliamua kubuni miungu inayoonekana ili kuthibitisha yule asiyeonekana
Watu duniani kote kuamini Mungu yupo sio uthibitisho kwamba kweli Mungu yupo .

Kuna kipindi duniani kote waliamini ugonjwa wa tauni ni laana na tanzania na Africa nzima walishaamini ukimwi ni uchawi , je ilikua ni ukweli?
 
Watu duniani kote kuamini Mungu yupo sio uthibitisho kwamba kweli Mungu yupo .

Kuna kipindi duniani kote waliamini ugonjwa wa tauni ni laana na tanzania na Africa nzima walishaamini ukimwi ni uchawi , je ilikua ni ukweli?

Ugonjwa wowote unaouona duniani ni laana.

Iwe Ukimwi, kisukari, mafua, kikohozi n.k.
Laana maana yake ni adhabu ya kuenenda kinyume na amri na maagizo ya Mungu(wanasayansi huita Nature)

Ndio nikakuambia miaka elfu ijayo Watu watakapotajiwa jina lako wengine wataamini ulikuwepo wengine watasema ni nadharia
 
Ugonjwa wowote unaouona duniani ni laana.

Iwe Ukimwi, kisukari, mafua, kikohozi n.k.
Laana maana yake ni adhabu ya kuenenda kinyume na amri na maagizo ya Mungu(wanasayansi huita Nature)

Ndio nikakuambia miaka elfu ijayo Watu watakapotajiwa jina lako wengine wataamini ulikuwepo wengine watasema ni nadharia
Fikra zako ni huru mno, kwenye hiyo nadharia yako, na unauwanja mpana mno kwenye hii nadharia ya Mungu muweza wa yote na mwenye kupenda sifa na kuabudiwa .
 
Ugonjwa wowote unaouona duniani ni laana.

Iwe Ukimwi, kisukari, mafua, kikohozi n.k.
Laana maana yake ni adhabu ya kuenenda kinyume na amri na maagizo ya Mungu(wanasayansi huita Nature)

Ndio nikakuambia miaka elfu ijayo Watu watakapotajiwa jina lako wengine wataamini ulikuwepo wengine watasema ni nadharia
Kwa nini useme ni adhabu na sio asili kwa sababu mwisho wa siku viumbe vyote hufa je ni nan asie pata hiyo adhabu?
 
Fikra zako ni huru mno, kwenye hiyo nadharia yako, na unauwanja mpana mno kwenye hii nadharia ya Mungu muweza wa yote na mwenye kupenda sifa na kuabudiwa .

miungu ndio hupenda kuabudiwa.
Kama Mungu muumbaji angekuwa na sifa ya kupenda kusifiwa na kuabudiwa angeúmba Watu kwa namna hiyo
 
Kwa nini useme ni adhabu na sio asili kwa sababu mwisho wa siku viumbe vyote hufa je ni nan asie pata hiyo adhabu?

Ukila uchafu ukaumwa hiyo ni adhabu ya kosa ulilofanya

Hapo kwenye kufa hapo ndio msingi mkuu wa wanaoamua kumsalimu Mungu ulipo.
 
miungu ndio hupenda kuabudiwa.
Kama Mungu muumbaji angekuwa na sifa ya kupenda kusifiwa na kuabudiwa angeúmba Watu kwa namna hiyo
Ila naona bado ume m single note katika personality katika neno asili au Mungu umetenganisha nadharia yako na binadamu ,ambapo binadamu na kila kitu mpaka mawazo yake nayo ni asili tu.
 
Ila naona bado ume m single note katika personality katika neno asili au Mungu umetenganisha nadharia yako na binadamu ,ambapo binadamu na kila kitu mpaka mawazo yake nayo ni asili tu.

Mawazo ya binadamu yapo ya asili na yapo ya kubuni
Mfano, kuwaza jambo lolote kinyume na matumizi ya asili pia ni ubunifu
 
Ila pia uchafu nao si asili pia kama nadharia yako inavyodai mkuu.
Uchafu ni asili kwa viumbe wachafu.

Ndio maana nikakuambia Mungu hakulazimisha wala sio mpenda sifa.

Tunapokunya Mavi ni uchafu lakini kwa viumbe wengine ni chakula.
Mwanadamu amepewa utashi(akili ya kufanya uchaguzi) wa kuamua kuwa mchafu/maovu au kuwa Msafi/Mwema.

Ushirikina ni uchafu na hufanywa na viumbe wachafu
Na wataishi katika ulimwengu wa viumbe vichafu.
 
Uchafu ni asili kwa viumbe wachafu.

Ndio maana nikakuambia Mungu hakulazimisha wala sio mpenda sifa.

Tunapokunya Mavi ni uchafu lakini kwa viumbe wengine ni chakula.
Mwanadamu amepewa utashi(akili ya kufanya uchaguzi) wa kuamua kuwa mchafu/maovu au kuwa Msafi/Mwema.

Ushirikina ni uchafu na hufanywa na viumbe wachafu
Na wataishi katika ulimwengu wa viumbe vichafu.
Ndio maana nikakuambia Mungu hakulazimisha wala sio mpenda sifa.

Kwa mujibu wa hii sentensi yako unamaanisha Pia huyo Mungu ana personality?
 
Ndio maana nikakuambia Mungu hakulazimisha wala sio mpenda sifa.

Kwa mujibu wa hii sentensi yako unamaanisha Pia huyo Mungu ana personality?

Personality Unazungumzia Utu au haina?
Mtu ni mfano wa Mungu.
Utu ni tafsiri nyingine ya uungu
 
Mawazo ya binadamu yapo ya asili na yapo ya kubuni
Mfano, kuwaza jambo lolote kinyume na matumizi ya asili pia ni ubunifu
Ila huo ubunifu pia umetoka kwenye kiumbe cha asili yani ni sawa ule asali iliyobuniwa kutoka kwenye mali ghafi za asili.
 
UTAFANYAJE MKEO AU MUMEO AU MZAZI WAKO AKIWA NA MAMBO YA KISHIRIKINA? Hivi ÑDIVYO UTAKAVYOFAÑYA.

Anaandika, Robért Heriel
Mtibeli.

Mtu yeyote ambaye haamini nguvu za Mungu huyo ni mshirikina.

Mtu yeyote ambaye anaamini nusu kwa nusu ñguvu za Mungu huyo ni Mshirikina.

Inaweza ikatokea kwenye maisha yako moja ya Watu wako wa karibu wakawa wanajihusisha na mambo ya kichawi au ushirikina.
Yaweza kuwa ni Mumeo au mkeo au wazazi au wazazi wa mumeo au mkeo.

Ikitokea ukajua kuwa moja ya Watu wako wa karibu ni wachawi au washirikina iwe kwa wao kujionyesha waziwazi au kwa kificho.
Au wanakushauri mambo ya kishirikina au uchawi wakisema kuwa huenda mambo yako hayaendi sawasawa kwa sababu kuna vitu haujafanya. Na vitu hivyo ambavyo haujafanya wàkakuambia ni kwenda kwa waganga wa kienyeji, kwenda kufanya mambo ya kishirikina iwe ya kimila au kiutamaduni.

Ikiwa ni Baba au Mama ndiye anayekushauri mambo hayo jitenge naye. Wala usiwe karibu na yeye. Tena asije nyumbani kwako akakaa kwa muda mrefu asije akawafundisha familia yako elimu yake ya kipumbavu.

Nawe usiende kwa baba au mama yako ukakaa kwa siku nyingi zizidizo siku saba. Na mkeo asikae kwa wazazi wako ikiwa unajua ni washirikina na wanamawazo ya giza.
Na watoto wako wasikae kwa wazazi wako(Bibi na Babu zao) ambao ni washirikina na wachawi.
Watakapokuuliza kwa nini unafanya hayo. Waambie ni kwa sababu wao ni washirikina na wachawi ndio maana unafanya hayo.

Kwa sababu mshirikina hana elimu nyingine ya kumpa mwanao wala binti yako au mkeo zaidi ya kumpotosha.

Ikiwa mkweo ni mshirikina au mchawi usiruhusu wanao wakakae huko. Wala wao wasijekukaa hapo kwenu kwa muda mrefu usiozidi siku saba.

Elewa, mzazi wako anaweza kumpotosha mkeo na kumfundisha mambo ya kishirikina.
Anaweza kumfundisha kwenda kwa waganga ili wakudhibiti wewe au kukupa sumu ambazo hawazijui wao wenyewe.

Hakuna mafanikio ya maana yanayotokana na ushirikina na uchawi. Ni akheri uwe maskini na wakuone hauna muelekeo kuliko kufuata njia zao.
Ni akheri ufe kuliko kupata msaada wowote, nasisitiza wowote kutoka kwenye uchawi na ushirikina.

Waambie wewe hutaki mafanikio kutoka kwenye uchawi na ushirikina.
Waambie wao wakifanikiwa kwa njia hiyo inatosha. Wafanikiwe wao kwa mambo hayo na sio wewe.

Ikiwa mkeo au mumeo anamambo ya kishirikina au kichawi vunja hiyo ndoa na familia siku hiyohiyo usisubiri. Wala usiweke mjadala wa kumbadilisha.

Kabla hujaoa wala kuolewa, hakikisha unamwambia mwenza wako kuwa siku utakayojihusisha na ushirikina na uchawi ndio siku ambayo mahusiano haya yatafika mwisho na hakutakuwa na mjadala na hakuna atakayesikilizwa.

Ikiwa mtoto wako ulimfundisha kutojihusisha na mambo ya ushirikina au uchawi lakini kwa hiyari yake akakaidi na kufuata maamuzi yake. Waeleze Ndio siku hiyohiyo hautakuwa mzazi wao, hautakuwa Baba yao, hautakuwa Mama yao.

Wasitajwe kwa jina lako. Na wala usiwape urithi wowote ule.
Na wala wasije ukajihisi vibaya kuona wengine watakuwa wamefanikiwa na hawategemei urithi au chochote cha kuwapa.
Wasije nyumbani kwako wala wewe usiende kwao.
Usichukue chochote kutoka kwao wala wao wasichukue chochote kutoka kwako.
Kwa maana waliamua kukudharau na kukaidi.

Hivyo ndivyo Watibeli walivyo.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Unaandika kwasababu hayajakukuta. My friend, mambo hayo ni mazito sana hasa yanapomhusisha mzazi. Yaache tu kama yalivyo.
 
Back
Top Bottom