Mugabonihela
JF-Expert Member
- Dec 12, 2022
- 306
- 1,784
- Thread starter
- #241
Kwa wanaotumiwa PDF wameanza kuipata harufu ya magofuMpaka saivi hatujasikia kuhusu magofu [emoji1783][emoji1783]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa wanaotumiwa PDF wameanza kuipata harufu ya magofuMpaka saivi hatujasikia kuhusu magofu [emoji1783][emoji1783]
Kabisa yani.Script ikiwekwa vizuri Hollywood wanaweza kuitengenezea movie sema bongo movie hawawezi budget yake itakuwa kubwa, hizi issue za ma drug lord Hollywood wanazipenda sana
VizurNdani ya nyumba hiyo aliyokua akiishi Catarina na Manuela mazingira yalikua mazuri ukilinganisha na zile nyumba tulizokua tunakaa sisi wengine. Japo hawakua na thamani za kutosha Lakini kimpangilio ilipendeza sana ikiwa na jiko na stores ambayo mzigo uliokua tayari kusafirishwa uliwekwa umo.
Tulifika mahari apo lakini kulikua na ukimya ambao bila Shaka kati wawili hao hakuna aliyejishughulisha na swala lolote lililohusu mapishi.
Kwa zile kelele na miguno ni dhahiri walikua kwenye dunia yao nyingine kabisa na kama mtu angefika hapo pasipo kujua kama waliokua ndani walikua na wadada watupu. Basi angedhani Ndani humo kulikua na kidume tena wale west Africans mandingo na binti kwa jinsi walivyokua waki shout kwa sterehe waliyokua wakipeana.
JAVIER: I'm seek of these mafackaz!!!!
( Nimechoshwa na hawa wajinga)
Hey ladies, we outside!!
( Javier aliongea vile ilikuwastua wajue kama tupo nje ili kama wanaweza waache upuuzi wao mara moja)
Sikuwahi kukutana wala kuona wanawake wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja hivyo nilitamani kuuliza wanafanyaje. Ila niliamini kumuuliza Javier swali hilo hakuna mantiki kwani nimemuuliza mambo mengi ambayo bado nasubiri majibu kutoka kwake, hivyo kuhusu swala lile la mapenzi kati ya Catarina na Manuela nililiweka kipolo.
Nje ya ile nyumba yao kulikua na shade (kibongobongo) ni vile vibanda vya msonge tulikaa hapo na kutulia kwa muda kisha tulimuona Catarina akitoka.
Catarina alionyesha ku mind sana na hapo nilijua kwanini siku ile alisema javier huwa anaendeshwa na njaa. Kumbe javier mara nyingi anawaaribia ratiba yao kwa sababu tu alikua akihitaji msosi kwa wakati.
Catarina alikuja na kamzigo bila shaka ndani yake kulikua na msosi, alifika na kuutupa ule msosi as if ana warushia mbwa chakula kile kisha bila kuongea na Yoyote aliondoka.
Baada ya muda alitoka Manuela akiwa na pensi ndogo sana mfano wa boxer na alikuja kukaa palepale tulipo sisi. Hakuna na chakula Chochote zaidi ya kinywaji kilichokua kwenye chupa ndogo ya kijani mfano wa chupa ya Serengeti light.
Bila shaka kilikua ni kilevi, kwa hakika level ya Manuela kwenye ulevi alikua ni chronic sana yaani alitamani muda wote awe yuko mafuta kichwani.
Ulevi wa kupindukia wa Manuela ulimfanya Javier atafakari sana kuhusu background yake. Javier aliamini kuna jambo kubwa sana nyuma ya ulevi wa Manuela.
Tukiwa tunapata chakula Manuela alikuja kwa namna Fulani romantic sana akanisogerea usoni kisha kwa kutumia sauti ndogo sana. Aliniambia usiku wa saa tano nimkute log stairs, eneo hili ni yale maeneo kwenye zile ngazi za magogo kupanda kuelekea ilipo ile maabara.
Manuela aliponisogelea karibu ilikua ni harufu ya pombe kali tu ndio iliyo tawala mwili wake, baada ya hapo aliondoka mapema ni wazi ali target muda ambao Catarina alikua bize kiasi kwamba asingeweza kujua kinachoendelea kule nje.
Wakati alipokua anaondoka Javier aliniangalia jicho moja la tahadhari ni kama vile ambavyo mama anamuangalia mtoto anaetazama soda ya mgeni.
Baada ya kuwa Manuela ametokomea ndani Javier aliongea kwa msisitizo na kwa umakini sana, " dogo tayari nimekuambia kila kitu hivyo sitarajii kuona unaingia kwenye mtego"
Kitendo alichokifanya Manuela kilinikasirisha sana kwani sikutaka Javier atambue kama nimeongea chochote na mwana dada huyo.
Baada ya kumaliza msosi ule ambao niliufurahia na kuuona wa kawaida tofauti na ule msosi niliopewa jana yake ambao ulinishinda. Hapo nilijua sasa kuwa kile chakula alicholeta Javier kilitokea kwa hawa mabinti.
Kwani mabinti hawa walikua independent kwenye kila kitu kuanzia utawala mpaka misosi nadhani hii Ilikua ni kwa sababu ya umuhimu na unyeti wa section yao ya kazi.
Tulirudi tena maabara ambapo Javier alifikia kulala huku akinionyesha majukumu mengine ya kuendelea nayo. Hapa ndipo nilipo prove kauli ya uvivu wa Javier ambayo iliongelewa na mwana dada Catarina.
Kufanya kazi eneo hilo ilikua ni zaidi ya kula bata ukilinganisha na namna wale jamaa wengine wanavyo chapika 24/7 (masaa 24 siku 7 za week). Nikiwa hapo sikuona kazi ngumu kabisa, kwani majukumu ya hapo yalizidiwa hata na zile duties za sengerema sekondari.
Hatukuchukua mda mrefu sikuhiyo, kabla ya jua kuzama tulikua tayari kwa kuondoka eneo hilo na kurudi camp kwa dhumuni la kupumzika.
Tukiwa njiani nilimuuliza Javier katika namna ya kumkumbusha anipe story fupi ya yule mzee wake ambaye anadai aliwahi kuishi East Africa.
Kwanza kabisa Javier alikanusha kwamba huyo aliyemtaja kama babu hakuwa babu yake wa damu. Isipokua kwa umri aliokua nao mzee yule alijikuta amejiwekea mazoea ya kumuita babu.
Hapa sasa Javier alinitajia jina ambalo halikua geni kwani nilikumbana nalo jana yake tu.
Kwa maelezo ya javier ni kwamba miaka karibia kumi (10) ilyopita akiwa yeye na rafiki ambae alimtaja kwa jina la Jamshid sharmahd wote wakiwa wana asili ya Iran.
Akiwa na rafiki ake huyo Waliwahi kufika ndani ya jiji moja huko ujerumani linalojulikana kama Düsseldorf na kilichowafikisha huko ni harakati za maisha. Hakuwa muwazi ni harakati gani na alionesha hakutaka kuulizwa chochote kuhusu harakati hizo.
Alipotaja lile jina la sharmahd nikakumbuka ile memo au messege niliyoikuta kwenye kitanda chake kwa usiku wa jana. Apo niligundua huyo sharmahd ndie mtu aliyeenda kukutana nae usiku wa jana.
Anaendelea Javier, wakiwa ndani ya jiji hilo la Düsseldorf waliwahi kukutana na veteran au mkongwe kwa jina rahisi.
Mkongwe huyu walimfahamu kwa jina moja tu na aliitwa Schulz, Schulz alikua ni veteran wa vita vya pili vya dunia akihudumu jeshi la ujerumani. Akiwa jeshini alikua na cheo cha kawaida sana alikua ni korporal tu kwa Wakati huo ( kama wanavyoita wajermani).
Bwana Schulz alishiriki vita nyingi mpaka kufikia mwaka 1943 September 9 ambapo Iran na ujerumani walipoingia kwenye mgogoro wa kivita na WA Nazi. Kabla ya mgogoro huu nchi ya Iran iliaminika kuwa neutral kabisa enzi zile za WWII ( vita ya pili).
Kabla story ya Schulz haijaisha tulikua tumeshafika nyumbani hivyo Nilijua tutaendelea lakini baada ya Javier kufungua Bible yake pale kitandani aliniaga tena.
Hapo Nilijua atakua ameenda kule alipoenda jana hivyo nilijisogeza tena kitandani kwake kuona kama kutakua messege yoyote au memo lakin haikuwepo.
Nadhani ile jana aliisahau kwa bahati mbaya inawezekana sio kawaida yake kuziacha memo hizo. Lakini pia inaonekana hawa watu wawili wana agenda ya siri ni inaonekana ni muhimu sana. Apo nilitamani kujua huyu sharmahd anapatikana wapi mashambani umo.
Kitu kilichonishangaza kingine ni namna ambavyo Javier huondoka kwa haraka pindi anapokuta memo yoyote kutoka kwa mtu huyo.
Kwakua sikuhiyo at least tulifanya kazi basi kauchovu kilikuwepo hivyo nikajilaza mapema ilinistuke baadae na kwenda kukutana na Manuela.
Nilitamani sana kujua binti huyo ana nini cha kuniambia lakini pia nilitamani kujua ni namna gani anaweza kunisaidia kutoka ndani umo. Apa nilijiambia sitakiwi kumzalau mtu anaweza kuwa na msaada hivyo sitakiwi kumpuuza kabisa.
Eneo lile la kambi muda wote lipo active lakini tatizo ni moja hakukua na taa zozote za nje hivyo kulikua na giza sana nyakati za usiku. Huwa kunakua na nafuu siku za mbalamwezi, na siku hizi ndizo hufurahiwa na wengi maeneo hayo.
Kulikua na ulinzi mkali sana lakini haikua rahisi kujua na hii ilisababishwa na kutokuwepo kwa mahusiano au muingiliano wa aina yoyote kati ya walinzi na wafanyakazi wa eneo hilo.
Kabla ya saa tano kama tulivyokubaliana na Manuela nilijiandaa kutoka mapema zaidi kwani bado nilikua mgeni maeneo hayo.
Kutokana na baridi kali la maeneo hayo nilichukua blanket kubwa nikajifunika kisha nikatoka ndani taratibu. Na kuanza safari ya kushusha bonde lile ambalo kwa chini ndio kuna maabara na ndio eneo alilonipa ahadi Manuela nikutane nae.
Kabla sijafikia eneo husika niliguswa mgongoni kwa namna kama nashituliwa na wakati nageuka nilimkuta Manuela ndie aliyekua ananistua.
MIMI: you scared me
( Umeniogopesha)
MANUELA: worry not
(Usijali)
Uongeaji wa Manuela wakati huu ulikua tofauti sana na jinsi ambavyo nilimuona akiongea siku mbili nyuma na ata mchana wake. Na ata yeye aligundua nimemuona yupo tofauti kimaongezi kwani wakati huu alikua active na makini sana.
MIMI: this is not the place we planned to meet
(Hii sio sehemu tuliyopanga kukutana)
MANUELA: I know but here it is safer
( Najua lakini hapa ni salama zaidi)
Swali la kwanza la Manuela aliuliza vipi Javier ulimuacha amelala kweli, na mimi bila kufikiria mara mbili nilimjibu kuwa Javier aliondoka mara tu tulipofika ndani.
Manuela alifurahia sana jibu kwa kumuangalia usoni, lakini aliongeza swali lingine ambalo ni, mara ngapi Javier amekua akitoka usiku tangu nifike hapo?
Bila kuwaza tena nilijibu siku zote ninakua hapo amekua akitoka usiku lakini alikua akirudi usiku huohuo isipokua siku ya kwanza ndio nilimuona asubuhi. Na hiyo ilitokana na usingizi mzito niliokua nao Uliosababishwa na safari yangu ndefu ya kufika hapo.
Wakati anauliza maswali yote hayo tulikua tumesimama pembeni mwa barabara iliyokua inaelekea kwenye ile maabara. Na baada ya kumjibu alinisogeza ndani kidogo kutoka barabara ilipo, na alinisogeza katika namna ambayo nilishindwa kujua amenivuta vipi.
Na safari hii alinivuta karibu yake zaidi yaani naweza kusema tulikua zero distance kabisa na apa huyu binti alikua akinukia tofauti na vile alivyokua mchana. Bila shaka nilitamani asiniachie kutokana na hali ya hewa ya ukanda ule hivyo nilitulia tuliiiiii.
Swali la pili la Manuela lilikua simple sana kwangu japo kwake alihisi sitoweza kumpa majibu.
"Anaendaga wapi usiku huo" wakati huu akiwa amenibana vizuri na baridi lile nilijibu tena comfortably anaendaga kuonana na rafiki anaitwa sharmahd.
Baada ya kutaja sharmahd aliniachia kwanza kwa kushangaa kidogo, na akauliza tena kama namjua sharmahd.
Hapo nilimjibu simjui ila nilibahatika kukuta memo kwenye moja ya vitu vyake na memo hiyo ilielekeza akakutane na mtu ambaye chini ya memo aliandika jina sharmahd.
Apa Manuela alinisifia kwa kusema " I'm too clever, clever than Gatkuoth " huku akiendelea kusema nahitaji kila aina ya zawadi nzuri kwenye hii dunia
Sikuelewa kwanini amenilinganisha na marehemu Gatkuoth, lakini kabla sijamuuliza chochote alikua ameshafika mdomoni anaendelea kunyonya mate.
Kwa haraka haraka aliondoka na kama lita mbili hivi kutoka mdomoni kwangu, kuna maeneo kwenye mwili wangu alipitisha mikono nikajiona kama nipo kwenye zero gravity zone.
Alichokua anakifanya Manuela ni zaidi ya wale porn star, kwani within a second mashine ilikua kwenye joto la mdomoni of course ilikua ni blowjob.
Ghafla alisimama na kutaja jina ambalo sijawaza kulisikia wakati huo.
MANUELA: Ludovic you are in safe hands
Mwalimu nguli tunayemjua ni Mohamed Said bila shaka naye atatia neno utakapoanza kutema madini ya historyKama kuna mtu anamjua mwalimu nguli wa history fanya kama una mtag aje apate madini kwenye episode zinazofata.
Bwana Schulz au jasusi m-Nazi wa enzi za Adolf Hitler ana nondo kali sana za history ya dunia ambayo huwezi kuisoma popote.
0623 32 95 12 WhatsApp
Mwalimu nguli tunayemjua ni Mohamed Said bila shaka naye atatia neno utakapoanza kutema madini ya hist
THE WEALTH OF RAPTA RUINS
(Get Rich or Die Tryin)
Msimuliaji: LUDOVIC MASSAWE
NB: SIMULIZI HII IMEAMBATANISHWA NA BAADHI YA PICHA ZINAZOTUMIKA KUELEZEA MATUKIO, HURUSIWI KUTUMIA PICHA HIZO MAHALI POPOTE.
PROLOGUE/DIBAJI
Mji wa rapta ni mji uliozama baharini kisiwani mafia kwa zaidi ya miaka 2000. Unaweza kua mji mgeni Kwa baadhi ya watu, lakini wengi mnaweza kua mmepata kuusikia uwepo wa mji huu wa kale pembezoni mwa pwani ya Africa mashariki. Wapo wanaodai mji huu unapatikana maeneo ya rufiji kwa sasa na wapo wanaodai mji huu unapatikana pembezoni mwa kisiwa cha mafia. Je! ni nani yupo sahihi?
Mji huu ulipata kuwepo mwanzoni mwa karne ya 1 na imepita zaidi ya miaka 1600 mpaka 2000 tangu kuwepo kwa mji huu. Unaaminika kuwa mji wa kwanza tajiri barani Africa na pia ni miongoni mwa miji kumi na tano inayopatikana chini ya maji. ukiacha miji kama vile Thonis-Heracleion na Alexandria iliyopo Egypt, Yonaguni Jima (Japan), Port Royal (Jamaica) Dwarka (India), Pavlopetri iliyopo south-western Greece, Villa Epecuen (Argentina) nk.
Tofauti na ilivyo kwa watanzania na wakazi wa Africa mashariki wakiwemo wana archeologia. Wengi wamechelewa kuzipata habari za mji huu, mimi nilizipata habari hizi nje kabisa ya ukanda huu. Nilizipata habari hizi nikiwa jiji la Tehran uko inchini Iran (uajemi ya kale) ndani ya maktaba ya taifa (National Library of the Islamic Republic of Iran) iliyoanzishwa mwaka 1937 ikiwa na zaidi ya items milion 15 ndani yake.
Wakati nafika Iran nilikua nikitokea nchini Colombia na Peru kwenye mashamba ya koka (coca plantations). kwa wasiojua koka leaf ndio mmea unaotumika kutengeneza madawa ya kulevya aina ya Cocaine kupitia mchakato mrefu. Na ugumu wa ku control uzalishaji wa cocaine unasababishwa au unatokana na kushindwa kuthibiti chemicals zinazotumitumika kwenye mchakato huo kwani ni chemicals za kawaida zinazotumiwa kila siku kwenye matumizi ya binadamu.
Mfano; ku process coca leaf kuwa coca paste mpaka kupata cocaine base na HCI zinatumika chemicals kama, Sulfuric Acid, Sodium Bicarbonate, Sodium Hydroxide, benzene, Potassium Permanganate, Dichromate, Ammonia Hydroxide, Sodium Hydroxide, Methyl Ethyl Ketone na kerosene. Tutajuzana mengi kuhusu cocaine hapo mbele tukiendelea na simulizi.
Sasa basi Niliwezaje kufika Colombia, Peru kisha Iran na miji mingine mikubwa duniani? Niliwezaje kuzisikia habari za mji wa rapta? nani alinipa habari hizi? na mji huu wa rapta una utajiri kiasi gan ndani yake? Nilifikaje rapta na kwa msaada wa technologia gan nilifanikisha zoezi langu? Kipi kilisababisha mji huu kuzama baharini?
Swali lingine la msingi, wageni wa kwanza wa pwani ya Africa mashariki walikua ni warumi na wachina kabla ya waarabu na waajemi, sasa imekuaje details za rapta zilizoandaliwa na warumi zikafika Iran (Persian gulf) zilifikaje huko?
Najua baada ya kutaja wachina wengi mtajiuliza maswali lakini msijali tutaona ushahidi wa uwepo wa wachina ndani ya mji wa rapta. 90% ya wachunguzi wa mji huu wanatumia taarifa za warumi zilizoandaliwa na Claudius Ptolemaeus (Claudio Ptolemy). Je wana fahamu kua details hizo kabla ya kuwafikia zilishatumiwa na waajemi wa kale Na kuna uwezekano taarifa hizo zilichakachuliwa!?
Je! Mzungu bwana Alan Sutton (mzamiaji) aliyegundua kuta za rapta akiwa kwenye helicopter hivi karibuni, ilikua ni bahati mbaya tu au na yeye ni moja ya wale treasure hunters ila hajaliweka hili wazi?
Ungana nami kwenye simulizi hii ya kuvutia ili kupata majibu ya maswali yote na kwa hakika utajifunza mambo mengi ndani yake.
SEHEMU YA 01
Mgomo sengerema secondary
Wakati unajiuliza Niliwezaje kufika Colombia, Peru na kisha Iran unatakiwa kujua safari yangu ya jasho na damu pamoja na misukosuko mingi ilianzia shule ya sekondari ya sengerema nikiwa kidato cha sita. Kwa waliopata kupita shule hii wanaweza kua mashihidi kwa namna shule hii ilivyokua ya kikomando yaan wenyewe tulikua tunaita late-summer boot camp.
Kwa haraka haraka tu ni shule aliyowahi kufundisha hayati magufuli kabla hajawa waziri na kisha raisi. Nadhani umeanza kupata picha ilikua shule ya aina gani, Ni shule ambayo kila mtu alikua jeuri kuanzia headmaster mpaka mpishi wa jikoni. Wakati nikiwa hapo tuliwahi kushuhudia kesi nyingi ngumu na za ajabu kama wanafunzi kukutwa na kombati za jeshi full set. Kuna mengi kuhusu sengerema ambayo hatuyajui nitawaeleza machache tu na ni kwa namna gani safari yangu ilianzia hapo.
Nilifika hapo kwa mbinde huku o'level nikitokea Ngerengere kizuka sekondari baada ya kufukuzwa MAKOKO SEMINARY, kiukweli nilikua mtoto mtukutu na jeuri ilifika hatua mzee wangu mzee MASSAWE alisema hizi tabia nimeridhi kutoka kwa babu yangu. Ambae alikimbia nchi baada ya kuhusika kwenye matukio mawili, lile la utekaji wa ndege ya ATC mwaka 1982 February kwa makusudi ya kushinikiza mwalimu ajiuzulu na lile jaribio la kuangusha serikali ya mwalimu Nyerere la mwaka 1980's. Babu Yangu alikua ni miongoni mwa wale maafisa wakuu waliosuka ule mpango, Tuachane na babu na tuludi zetu sengerema.
Tukio la mgomo ndio lililoanzisha safari yangu Na lilipangwa usiku baada ya mlo wa jioni, vidume baada ya kushiba dona maharage pamoja na nchima boyo akili zikatutuma tufanye mgomo usiku wa siku hiyo. Sababu za mgomo zilikuwepo japokua hazikua na mashiko sana naweza sema ni ujana tu ndio ulikua unatusumbua ukiongeza na zile bangi zakuvutia maporini (chaka).
Kama kawaida mzee baba siku hiyo ya mgomo niliwekwa kitengo cha TANESCO, yani niliambiwa ikifika saa 2 kamili usiku ni hakikishe shule nzima umeme umezima. Hii ilitokana na ujuzi wangu wa mambo ya electronics na wiring za ujanja ujanja za mabwenini especially bweni la kimweri na sokoine.
Basi ilipotimu saa 2 kamili nilihakikisha Giza limetanda shule nzima kasoro nyumba za walimu tu, na kazi yangu iliishia hapo na Majukumu mengine yaliyobaki yalikua kwa wenzangu wahamisishaji kuhakikisha kila mmoja anashiriki. Lakini pia kuna jamaa mmoja wa mwananyamala yeye alikua na dumu la petrol lita 5 sijui alilitolea wapi usiku ule huyu bwana kazi yake ilikua kuhakikisha moto unawaka maeneo yote yaliyopangwa kuchomwa.
Mpaka kufika saa nne usiku stationary ya mwalimu wetu siwezi kumtaja jina ilikua haitamaniki na baadhi ya walimu walikimbiza familia zao mjini. 90% ya wanafunzi tulikua michepuo ya sayansi yani PCM, PCB na combination nyingine hivyo tulikubaliana kutokugusa maabara wala library wala darasa, wachache sana walikua arts na cha ajabu kwenye hii shule watu wa arts walikua wamestaarabika ukilinganisha na sayansi.
Shule imejengwa mlimani kabisa kiasi kwamba ilipofika saa 4 na nusu usiku defender ilionekana ikipandisha na wote tukapotelea maporini. Jambo la kufurahisha ni kwamba askari hawakufanikiwa kukamata ata mwanafunzi mmoja kati ya wanafunzi 800. Wengi waliishia kulala kwenye miembe na majaruba ya mpunga kwa usiku huo kwani shule ilizungukwa na makachero wakutosha. Lakini massawe nikasema siwezi lala juu ya mti Kama tumbili, usiku ule ule nikaanza safari ya kuelekea mjini mitaa ya soko mjinga.
Pale mjini kuna binti alikua anasoma shule ya jilani inaitwa NTUNDURU alikua amepanga ghetto. Can you imagine!!! Shule ya boarding na bado amepanga mtaani! asee!!... Merry alikua ni hatari sana mnyaturu yule wa singida.
Mishale ya saa tano usiku nilikua mlangoni kwa merry nabisha hodi, baada ya dikaka 3 alifungua mlango nikaingia. Walikua wawili yeye na mwenzie anaitwa jane. Ndani kulikua na chupa za safari na mzinga mkubwa wa konyagi, nilipoingia nilihisi uwepo wa mwanaume mule ndani na baadae niliona funguo za sun LG na vipisi vya sigara. Ila sikujali sana nilijitupa kitandani nikapitiwa na usingizi mzito uliotokana na uchovu wa mgomo na mbio za kuwakimbia field Force.
Nilikuja kustuka saa kumi alfajiri na mlio wa pikipiki uliokua unamrudisha merry ambae alikuja yupo hoi na kwa haraka niligundua jane amebaki na yule kidume wa jana.
Merry akilewa bia hua zinashuka chini, waliosoma cuba wamenielewa hapa. Hivyo baada ya kuingia ndani hakutaka story zaidi ya kutupa nguo kwenye kila kona ya chumba hicho kama mwehu. Na mimi kutokana na nilikua namjua vizuri haikusumbua kujua anataka nini zaidi ya kuanza mtanange wa kukata na shoka uliochukua zaidi dakika 90 kama finally ya Argentina vs France kule Qatar.
Tulikuja kuamshwa na mwanga mkali wa jua la saa 4 asubuh uliokua unapita dirishani Huku merry akiwaza supu. Ilituchukua muda mfupi kujiandaa kwenda maeneo ya stendi kupata supu, nilishangaa baada ya kufika stendi nilikutana na wanafunzi wenzangu wakiwa na mabegi wengine ma tranka. Nilipowauliza walijibu shule imefungwa kwa muda wa week 3 na tutapewa utaratibu wa jinsi ya kurud tukiwa nyumbani. Hapo nilianza kuwaza namna ya kurud nyumbani huku mizigo yangu yote imebaki shule na hakuna mwanafunzi anaeruhusiwa kwenda tena shule kwa muda huo.
Basi bwana tulipata supu na mrembo merry kisha tukarud zetu ghetto kupumzika, nakumbuka ilikua siku ya alhamisi hivyo merry hakuenda shule kutokana na hangover na tulishinda ndani siku nzima mpaka kesho yake asubuhi.
Siku ya pili akili ilivurugika zaidi baada ya kupata habari kwenye vituo vya habari viwili tofauti kuhusu mgomo wa sengerema, kituo cha kwanza ni redio sengerema ilitangaza wanafunzi kumi na tisa (19) wamefukuzwa na wengine kusimamishwa masomo kwa muda usiojulikana. Hivyo hivyo kwa redio free Africa na gazeti la mwananchi, gazeti hili lilitoa majina ya waliofukuzwa na mimi nilikua jina la kwanza kwenye ile list.
Niliwaza namwambia nini mzee massawe ambae alichoshwa na tabia zangu.
Akili ikanituma kuangalia upande wa pili wa maisha na sio kukomaa na shule, niliamini siku Moja nikiludi home na pesa nyingi mzee massawe atanikubali sana jembe lake.
Baada ya kupata wazo la kutoendelea na shule nikaanza kuwaza natakiwa nianzie wapi kutafuta pesa. Apo apo akili ikaniambia dar ndio sehemu pekee naweza tengeneza pesa nyingi, lakin kwa bahati mbaya sikua mzoefu wa mji huo na wala sikutakiwa kufikia kwa ndugu yoyote na bado sina nauli ya kufika huko. Niliamini nikifika Mwanza kwenda dar itakua rahisi hivyo nikaanza mchakato wa kufika mwanza (nyegezi).
Nilimshirikisha merry kwa makusudi ili anisaidie nauli ya kufika nyegezi kwani kutoka sengerema hadi nyegezi ni kiasi cha shilingi 4000 tu. Na kwa maelezo ya merry aliniomba tufike stendi kuna mtu atampatia tukifika hapo.tukiwa stendi Merry alimfuata jamaa mmoja bonge hivi anadeal na tickets pale stendi, Kwa haraka niligundua huyo ndio sponsor waliekua nae jana. Sikujua waliongea nini na merry ila merry aliniambia tusubiri kuna coaster inatokea katolo ndio tutaenda nayo mwanza.
Haikuchukua muda mrefu ile coaster ilifika na walipanda abiria kadhaa kisha bonge akamwambia konda hawa ndio wadogo zangu wanaoenda nyegezi. na sisi tulipanda tukaanza safari, nilishangazwa na uwepo wa Merry kwenye safari sikujua na yeye anaelekea wapi kwani hakua na sababu ya kutoka sengerema siku hiyo kwani masomo kwa upande wake yalikua yanaendelea. Merry alikua mwanafunzi wa kidato cha nne NTUNDURU sekondari na ile siku tumeshinda ote ndani nilitumia fursa kumfundisha almost topics tatu za msingi.
Sasa tukiwa ndani ya coaster kuelekea nyegezi nilimuuliza kwanini na yeye ameamua kusafiri, majibu yake yalikua ni kwamba ana muda mrefu hajafika mjini mwanza hivyo alitaka kwenda kuosha macho kwa muda kisha baadae ataludi sengerema.
Nilipata nafasi ya kupiga stories na konda ndipo niligundua wametokea geita walipeleka msiba na hapo wanarudi dar es salaam. Niliamini safari yangu kufika Dar es Salaam imerahisishwa nachotakiwa ni kuwaza namna gani naweza kushawishi jamaa ili aniruhusu nisafiri nae.
Majadiliano na konda yalikua hivi.
Konda:"dogo! we ni mwanafunzi Nini? Jana tukiwa na msiba tulibeba madogo kama watatu hivi wakiwa na suruali nyeusi na tishet za bluu kama ulivyovaa wewe"
Merry alijibu fasta kama ameulizwa yeye,
Merry: ndio sisi ni wanafunzi, ila tumerudishwa nyumbani ghafla sababu ya mgomo wa juzi usiku.
(konda hakujua kama sengerema ni shule ya wavulana pekee)
Konda: kama wanafunzi wenyewe ndio nyinyi hiyo shule kazi ipo. Kwaiyo nyumbani ni wapi??
Nilitumia swali hilo kama fursa ya kufanikisha misheni yangu.
Mimi: home dar na hatujatumiwa nauli sijui tunafikaje?
Konda: we mtoto wa kiume jitahidi upambane.
Jibu lile lilinikatisha tamaa ya kuendelea na maongezi yale.
Haikuchukua muda tulikua tumefika kivukoni busisi. Abiria wote tulishuka na kupanda kivuko, lakini nilifurahi baada ya kumuona konda anajisogeza kwa merry na kujiongeresha. nilijua kwa ujanja wa merry anaweza kufanikisha safari yangu kirahisi sana.
Baada ya kufika upande wa pili tulirudi ndani ya coaster na kuendelea na safari na wakati huu merry aliniambia ameshampanga konda hivyo tutafika wote dar es salaam.
Merry alikua binti mjanja sana na anamacho Fulani akikuangalia tu unajua atakua fundi, hahahahahaha kwa wale tuliopita sengerema miaka ile najua mtakua mnamkumbuka kwani alikua maarufu sana. Especially tukienda shuleni kwao kwa ajili ya michezo wengi walimtolea macho, nitakuja kueleza nilimpataje hapo baadae.
Baada ya kufika nyegezi tukijiandaa na safari ya kuanza kuitafuta dar es salaam nilishangaa konda aliniita na kunipa buku tano nikatafute msosi. Na kisha konda na merry walipotelea kusiko Julikana, Nilijua merry ameshafanya yake tayar niliishia kuitunza ile buku tano nikiamini itanisaidia mbele ya safari kwani sikua na chochote mfukoni.
Baada ya nusu saa merry na konda walirudi huku nikimuona merry na vifurushi vya kutosha bila shaka ilikua ni misosi na kimoyomoyo nikasema merry hajawahi kuniangusha ata siku moja. Tulikaa kwenye siti na kuendelea na safari Huku tukipiga msosi mzito nakumbuka ilikua ni Sato na chipsi kavu za kutosha.
Mimi: merry ulisema unaishia nyegezi vipi mbona unaendelea na safari???
Merry: sijawahi kufika Dar es Salaam, nadhani hii ni fursa ambayo sitakiwi kuichezea. Najua nipo na wewe hakuna kitachoharibika nitakaa week moja kisha nitarudi shule.
Daaaaah!!!!! Nilihisi mwili unakufa ganzi nilitaman kumwambia Mimi mwenyewe sina pa kufikia ila nikapiga moyo konde. tukaendelea na safari yetu huku stories zikiwa nyingi. Merry pekee ndio alikua na simu Mimi kilichokua mfukoni ni ile buku tano, kibiriti cha gesi na scientific calculator tu.
Baada ya safari ya muda mrefu wote tulipitiwa na usingizi, safari ile ni ya kutwa nzima kwani nakumbuka tuliingia morogoro usiku wa saa tano tena hiyo ilikua ni baada ya abiria kulalamikia speed ya gari ilikua kali mno. Tulipotoka moro baada ya kufika maeneo ya chalinze nilipitiwa tena na usingizi mzito. Nilikuja kushtuliwa na konda akidai alitusahau tumeshaingia mjini mda mrefu.
Konda: nyie mnashukia wapi tumeingia Dar es Salaam tayari.
Lile swali lilikua gumu kwangu kwani sikua ata najua tunapoelekea baada ya kufika dar. Kwa Dar es Salaam nachojua ni ubungo tu hivyo nilimjibu tunashuka ubungo.
Konda: ubungo tumepita tayari sisi tunaelekea mbagara, shukeni hapa mrudi vertinary mkapande gari za ubungo.
Kiukweli sikumuelewa konda ata kidogo kila alichonambia kilikua kipya ila sikutaka kuonyesha kutokujua mbele ya Merry hivyo tulishuka. Tulishushwa eneo moja lina mataa na ilikua saa saba na nusu usiku, nikiwa sijui cha kufanya Merry alianza kulalamika maumivu makali ya tumbo.
Nilijua tu itakua njaa kwani ni muda mrefu hatujapata chakula, baada ya kupepesa macho huku na kule niliona sehemu kwa mbaali kuna watu na mataa mengi yanawakawaka nikajua fika hapo patakua na bar hivyo hatuwez kosa msosi.
"Massawe hapa na kwenu kuna umbali gani?" Lilikua ni swali la Merry na mimi sikuona haja ya kuendelea kumficha ukweli, nilimueleza kila kitu kama nimeenda huko kutafuta maisha na nimeachana rasmi na masomo baada ya kufukuzwa shule na nilimueleza siwezi kurudi moshi kwa mzee massawe hatonielewa kabisa.
Kwa maumivu ya tumbo aliyokua anapitia Merry hakutaka kuendelea na mjadala nilimuona akiongoza kwenye lile eneo tuliloliona likiwa na watu wengi usiku ule.
Baada ya kufika eneo Hilo niliona maandishi makubwa yakiwakawaka yameandikwa SUGAR REY. Ni dhahiri ilikua ni bar, nilishangazwa na mavazi ya wadada wa eneo hilo na sio mimi tu ata merry pia.
"Hhhmmm kweli hii ndio dar es salaam ninayoisikia kila siku" yalikua ni maneno ya Merry. Tukiwa bado tumeduwaa alikuja bodaboda
Bodaboda: vipi mnaenda?
Mimi: hapana tumefika bro.
Bodaboda: punguzeni kushangaa basi.
Tulisogea mpaka eneo lile nikiamini hatuwezi kukosa chakula ukizingatia nilikua bado na lile buku tano la konda.
Tulipofika tu merry alimfuata Binti mmoja aliekua amekaa pembeni akiwa kwenye pozi Kama anamsubiri mtu na waliongea baadae wakafatana sikujua wameenda wapi. Nilijisogeza kwa jamaa wa bodaboda wakiwa na makoti makubwa nikajiunga kupiga nao story huku nikimsubiri Merry.
Mimi: bro samahan hawa wadada mbona wapo wengi na wana mishe gani apa mbona wamevaa kiasala asala?
Bodaboda: hao wanajiuza mjomba. We mgeni nini?
Mimi: ndio mi mgeni.
Bodaboda aliniangalia tu na hakuendelea kuongea chochote Zaidi ya kuwafata abiria wawili waliokua mbele yake.
Baada ya muda kidogo hivi nilimuona merry akiludi eneo nililokuwepo.
Mimi: merry punguza kujifanya unamjua kila mtu apa sio singida hii dar rafiki angu.
Merry: lile tumbo lilikua ni la siku zangu na sio njaa kama ulivyohisi hivyo nilienda kwa yule mdada kuona kama ata nipa msaada wowote si unajua sijatembea na chochote. Lakini pia nimemueleza changamoto niliyonayo kwamba hatuna pa kulala na ndio tumefika mjini.
Mimi: akasemaje?
Merry: kasema atanisaidia kwa leo sehemu ya kulala ila kuanzia kesho nitajua pa kwenda, lakini pia amenieleza kama sina ndugu kabisa atanionyesha kazi ya kufanya na tutakua tunachangia wote kulipa pango la nyumba hivyo mi nimeona niende nae tu.
Kiukweli sikutamani merry aondoke na yule dada lakini sikua na jinsi kwani hata hivyo sikua na sehemu yoyote ya kumpeleka. Merry alinikabidhi simu yake ili iwe rahisi kunipata siku inayofuata kwani alikua anajua sikua na simu. Tuliagana na merry na mimi nikabaki eneo hilo nikiwaza naelekea wapi kwa usiku huo wala sikutaka kujutia maamuzi yangu ata kidogo niliamini nipo sahihi kabisa.
Tunaendelea baadae usikae mbali.View attachment 2583318
seeafricatoday.com
Pengine Manuela ndio kamsaidia kutoka huko, tuvute subiraUmemsaliti Javier mapema.Kumbe imani ya weupe juu ya waafrika ni kweli, yani siku ya pili tu tayari dushes ishasimama.Kwa nini hukuwa kama Yusufu, ukatae kubakwa au ndio mtu mweusi hajawahi shinda majaribu ya wanawake?
Angefikaje Iran ambapo Javier ni mwenyeji?Pengine Manuela ndio kamsaidia kutoka huko, tuvute subira