Utajiri wa Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na Wilaya, washtua Watetezi wa Haki za Binadamu

Utajiri wa Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na Wilaya, washtua Watetezi wa Haki za Binadamu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Ukwasi walionao baadhi ya mawaziri na wakuu wa mikoa na wilaya nchini umezua jambo: Watetezi wa haki za binadamu wamehoji walikopata ukwasi huo viongozi hao wa serikali.

Ni hoja iliyoibuliwa na watetezi hao jana jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa tafakuri ya hali ya utetezi na uenezi wa haki za binadamu nchini kwa kipindi cha miaka 40 ya uwapo wa haki hiyo kikatiba.

Hao ni pamoja na Jenerali Ulimwengu, Askofu Emmaus Mwamakula, Shehe Ponda Issa Ponda, Mpale Mpoki, Tike Mwambipile, Hellen Kijo-Bisimba, Rugemeleza Nsala na Kaiza Buberwa.

Snapinsta.app_469947469_1628284347807899_8848583550433286780_n_1024.jpg

Bila kutaja jina la waziri, mkuu wa mkoa na wilaya, Ulimwengu, mwandishi mkongwe mwenye taaluma ya sheria, aliwataka waandishi wa habari wenzake wampatie majibu kuhusu ulikopatikana ukwasi walionao baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya nchini.

"Ninyi waandishi wa habari, mmeshawahi kujiuliza mishahara ya viongozi, Mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya wanapata kiasi gani? Kile kipato chao halali! Masurufu anayopata yanayotokana na nini? Na akija madarakani, mali zake zinatokana na vyanzo gani? Au hii ni hela yetu ambayo ilipaswa kujenga barabara?

Chanzo: Nipashe
 
Hii hoja ya watetezi wa haki za binadamu inapiga kwenye mshono.
 
Wakati hao viongozi wakiwa masikini hao watetezi wa mchongo wa haki za binadamu walikua wapi kuwapigania?
:PainChamp: watakuwa walikuwa wanawafuatilia na ndio maana wameibuka leo baada ya Ukwasi wao kukua haraka kuliko uhalisia wa mishahara yao
 
Ukwasi walionao baadhi ya mawaziri na wakuu wa mikoa na wilaya nchini umezua jambo: Watetezi wa haki za binadamu wamehoji walikopata ukwasi huo viongozi hao wa serikali.

Ni hoja iliyoibuliwa na watetezi hao jana jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa tafakuri ya hali ya utetezi na uenezi wa haki za binadamu nchini kwa kipindi cha miaka 40 ya uwapo wa haki hiyo kikatiba.

Hao ni pamoja na Jenerali Ulimwengu, Askofu Emmaus Mwamakula, Shehe Ponda Issa Ponda, Mpale Mpoki, Tike Mwambipile, Hellen Kijo-Bisimba, Rugemeleza Nsala na Kaiza Buberwa.
Bila kutaja jina la waziri, mkuu wa mkoa na wilaya, Ulimwengu, mwandishi mkongwe mwenye taaluma ya sheria, aliwataka waandishi wa habari wenzake wampatie majibu kuhusu ulikopatikana ukwasi walionao baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya nchini.

"Ninyi waandishi wa habari, mmeshawahi kujiuliza mishahara ya viongozi, Mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya wanapata kiasi gani? Kile kipato chao halali! Masurufu anayopata yanayotokana na nini? Na akija madarakani, mali zake zinatokana na vyanzo gani? Au hii ni hela yetu ambayo ilipaswa kujenga barabara?
badala ya kuzidisha juhudi katika kufanya kazi, mnaendekeza uvivu na wivu kwenye jitihada na mali za watu..

hiyo ni useless na nonsense,
yaani ardhi ya kilimo imejaa tele, ardhi na nafasi ya ufugaji imejaa tele, mazingira ya biashara ni mazuri mno,

watu wazima na akili zao wanaona wivu, tamaa na chuki dhidi ya mali za watu wenye bidii zao? ni majahabu ya karne haya dah 🐒
 
Tunachezewa Sana
Tunaliwa Mno
Tunahomolwa
 
badala ya kuzidisha juhudi katika kufanya kazi, mnaendekeza uvivu na wivu kwenye jitihada na mali za watu..

hiyo ni useless na nonsense,
yaani ardhi ya kilimo imejaa tele, ardhi na nafasi ya ufugaji imejaa tele, mazingira ya biashara ni mazuri mno,

watu wazima na akili zao wanaona wivu, tamaa na chuki dhidi ya mali za watu wenye bidii zao? ni majahabu ya karne haya dah 🐒
Kuuliza si ujinga,wajitajirishe si kwa kodi za wavuja jasho. Waachie ofisi za umma wakafanye biashara.
Aliyewatangazia kula kwa urefu wa kamba zao naye anakula kwa urefu wa kamba yake, tena ana kamba ndefu kwelikweli
 
Ukwasi walionao baadhi ya mawaziri na wakuu wa mikoa na wilaya nchini umezua jambo: Watetezi wa haki za binadamu wamehoji walikopata ukwasi huo viongozi hao wa serikali.
Mbona ilani ilishatolewa kwamba kuleni kwa urefu mnaofikia
 
Kuuliza si ujinga,wajitajirishe si kwa kodi za wavuja jasho. Waachie ofisi za umma wakafanye biashara.
Aliyewatangazia kula kwa urefu wa kamba zao naye anakula kwa urefu wa kamba yake, tena ana kamba ndefu kwelikweli
Gentleman,
mawaziri na watumishi karibu wote nchi hii ni ama wakulima, wafugaji, wafanyabiashara au wawekezaji,

sasa kama amwekeza vizuri asitajirike?

yaani azubae kwenye kazi ya uteuzi tena ya uma bila kujishughulisha na mambo mengine baada ya kazi zake?

wivu chanzo chake ni uvivu tu na si vinginevyo 🐒
 
Kuuliza si ujinga,wajitajirishe si kwa kodi za wavuja jasho. Waachie ofisi za umma wakafanye biashara.
Aliyewatangazia kula kwa urefu wa kamba zao naye anakula kwa urefu wa kamba yake, tena ana kamba ndefu kwelikweli
Gentleman,
mawaziri na watumishi karibu wote nchi hii ni ama wakulima, wafugaji, wafanyabiashara au wawekezaji,

sasa kama amwekeza vizuri asitajirike?

yaani azubae kwenye kazi ya uteuzi tena ya uma bila kujishughulisha na mambo mengine baada ya kazi zake?

wivu chanzo chake ni uvivu tu na si vinginevyo 🐒
 
badala ya kuzidisha juhudi katika kufanya kazi, mnaendekeza uvivu na wivu kwenye jitihada na mali za watu..

hiyo ni useless na nonsense,
yaani ardhi ya kilimo imejaa tele, ardhi na nafasi ya ufugaji imejaa tele, mazingira ya biashara ni mazuri mno,

watu wazima na akili zao wanaona wivu, tamaa na chuki dhidi ya mali za watu wenye bidii zao? ni majahabu ya karne haya dah 🐒
“No country can progress, if its politics is more profitable than its industries. In a country where politicians are richer than entrepreneurs, they manufacture poverty.” - Peter Obi
 
Kuuliza si ujinga,wajitajirishe si kwa kodi za wavuja jasho. Waachie ofisi za umma wakafanye biashara.
Aliyewatangazia kula kwa urefu wa kamba zao naye anakula kwa urefu wa kamba yake, tena ana kamba ndefu kwelikweli
Gentleman,
mawaziri na watumishi karibu wote nchi hii ni ama wakulima, wafugaji, wafanyabiashara au wawekezaji,

sasa kama amwekeza vizuri asitajirike?

yaani azubae kwenye kazi ya uteuzi tena ya uma bila kujishughulisha na mambo mengine baada ya kazi zake?

wivu chanzo chake ni uvivu tu na si vinginevyo 🐒
“No country can progress, if its politics is more profitable than its industries. In a country where politicians are richer than entrepreneurs, they manufacture poverty.” - Peter Obi
he is politician for more than twenty years now but not rich.

I think he is a liar🐒
 
Ukwasi walionao baadhi ya mawaziri na wakuu wa mikoa na wilaya nchini umezua jambo: Watetezi wa haki za binadamu wamehoji walikopata ukwasi huo viongozi hao wa serikali.

Ni hoja iliyoibuliwa na watetezi hao jana jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa tafakuri ya hali ya utetezi na uenezi wa haki za binadamu nchini kwa kipindi cha miaka 40 ya uwapo wa haki hiyo kikatiba.

Hao ni pamoja na Jenerali Ulimwengu, Askofu Emmaus Mwamakula, Shehe Ponda Issa Ponda, Mpale Mpoki, Tike Mwambipile, Hellen Kijo-Bisimba, Rugemeleza Nsala na Kaiza Buberwa.
Bila kutaja jina la waziri, mkuu wa mkoa na wilaya, Ulimwengu, mwandishi mkongwe mwenye taaluma ya sheria, aliwataka waandishi wa habari wenzake wampatie majibu kuhusu ulikopatikana ukwasi walionao baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya nchini.

"Ninyi waandishi wa habari, mmeshawahi kujiuliza mishahara ya viongozi, Mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya wanapata kiasi gani? Kile kipato chao halali! Masurufu anayopata yanayotokana na nini? Na akija madarakani, mali zake zinatokana na vyanzo gani? Au hii ni hela yetu ambayo ilipaswa kujenga barabara?

Chanzo: Nipashe
HILI NI GENGE LA WAHUNI TU YAAANI KIN AMWAMAKULA UNAITA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU? WAMEENDA KUPIKA MAJUNGU TU WAWATAJE HAO WALIONA UKWASI KUPITILIZA TUONE NA TUAMINI VINGINEVYO NI ROHO ZA KWANINI TU ZINAWASUMBUA NDIYO MAANA HAWANENEPI WAMEKONDEANAAAA KAMA KIMWAMAKULA
 
mshara wa mkuu wa mkoa 9m. marupurupu 5m
9+5 =14m
Hiyo 9m ni taxable?

Kama ni 14m kwa mwezi, iwe ndo basic, kusiwe na marupurupu mengine yoyote ya cash ila huduma tu kwaajili ya kutekeleza majukumu.

Na hiyo 14m iwe taxed, na sio hao tu, wabunge na watumishi wooote, kama ni exemption, wapewe wale top 3 tu!

Sio serikali inalazimisha kuwa kima cha chini ni 270k halafu unawapa watumishi hao pengine 270k nyingine kama marupurupu, kisa unakwepa wage bill kubwa; kiufupi, serikali inakwepa kulipa paye kubwa na 5% kubwa ya mifuko ya jamii kwa watumishi wake kwa kushusha basic salary na kuongeza michakato ya pembeni.
 
Back
Top Bottom