Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Umughaka sio kwamba hana akili ana mapungufu fulani tu kwenye kufanya maamuzi ya haraka, na kila mwanadamu ana mapungufu yake

Kwa jinsi alivyosimulia story zake zote kwa mtiririko mzuri na details nyingi kiasi hiki, inamuonyesha ni mtu mwenye akili na uwezo mkubwa wa kuweka kumbukumbu

Kitu kimoja nilichokiona kwake kama kasoro ni hana uwezo wa kujiamulia mwenyewe kwa haraka, maamuzi yake mengi ni ya kuchelewa au ya kuamuliwa na marafiki

Ngoja nitoe mifano michache, kule alipoenda kwa shemeji yake anayevua samaki, shemeji yake hakumlipa mshahara kama alivyoahidi kwa miezi kadhaa, lakini akawa anasita kumuuliza na kuondoka pale kwake

Kuna ile ya kupelekwa kwenye danguro alipofika Dar na kuomba kuonyeshwa gesti, alipoona ni Danguro palepale alitakiwa kuondoka na kutafuta gesti mwenyewe lakini akasita pia kuchukua uamuzi

Kuna hii alipoenda kwa mjomba wake na akawa anasaidia kutawaza mgonjwa, hapa alikuwa na haki ya kuondoka sababu ilikuwa inafahamika kwa wenyeji wake kuwa hakuja kukaa kwa muda mrefu na alitakiwa kuondoka baada ya siku chache tu, lakini akawa anasita tena, hadi akalazimishwa kuondoka na ile hostility aliyoonyeshwa na wenyeji wake

Kuna hili la Mpemba kumpeleka huko Chumbe, hapa alikua anajuà kabisa sio sahihi na ni hatari kwake, lakini pia akashindwa kumvaa usoni Mpemba na kuamua kumlatalia pale pale

Kuhusu kumuamini yule jamaa mlevi na kumpa milioni 9, hili hapa linaweza kumkuta yoyote, sababu ndio kwanza alikuwa ametoka kufanya biashara na Mtatiro, ambaye japo hakuwa ndugu yake walifanya kwa uaminifu mkubwa na kugawana faida, sasa saikolojia yake tayari inakuwa inawaza, kama Mtatiro ambaye sio ndugu yangu hajanitapeli, huyu ndugu wa damu moja hawezi kunitapeli, tutafanya vizuri kama Mtatiro (hapo hakuwa anajua kama ndugu ni mlevi)

Ni kasoro ambazo watu wengi tunazo, hata mimi kuna maamuzi mengi ya kipuuzi nafanya kisha najiuliza hivi kwa nini nisngeamua vile? Lakini sio kukosa akili, maana katika watu wenye akili Tanzania, mimi nipo, kwa mujibu wa NECTA

Lakini tupunguze kum judge tufurahie story, maana kila mtu akisimulia maisha yake haya, yatakuwa na blunder nyingi sana
 
Mimi nikushauri tata, leta epsode moja kila week au hata kila mwezi. Kule RFA kipindi cha sitasahau tulikuwa tunasubiri epsode moja tu week nzima. Hakuna anaekulipa, fanya mishe zako kwa uhuru mura. Umepitia mengi
Watu wa hovyo ndio hawa, kinachoongelewa hapa ni kupewa tuvtaarifa kuwa kutakuwa na episode moja tu siku ya Jumanne kila wiki. Sio unajificha huko watu wanaulizana na kutukanana hapa yeye yuko kimyaaaa.
 
Watu wa hovyo ndio hawa, kinachoongelewa hapa ni kupewa tuvtaarifa kuwa kutakuwa na episode moja tu siku ya Jumanne kila wiki. Sio unajificha huko watu wanaulizana na kutukanana hapa yeye yuko kimyaaaa.
Sikia, before hajaleta hii stori hakutoa taarifa ya lini ataileta. Uliikuta tu ukaanza kuisoma wala hakuna sehemu kamtag mtu kwenye hii story. We subscribe ili upate notification akitupia mzigo
 
Dah[emoji23][emoji23]
 
Huenda kulikua na utaratibu wa kufanya kila anapokua safarini, ikiwemo kuwasiliana na mganga wake wa kule zanzibar
Bado haileti maana hiyo dhana yako, kama ni hivyo kwanini wakati amesafiri alimwachia Umughaka kazi ya kununua mboga za huyo kiumbe, kama ni kuwasiliana na mganga wake si angewasiliana nae tu.
 
Nakuusia kijana mkakati wa kuchafua wapemba utakuletea shida. Maana naona hili unalichukulia poa. Wewe Kiarabu unakifahamu? Ulijuaje kuwa aliongea kiarabu? Hizi ni fitna na propaganda chafu sana.
We mbona ulisimulia upuuzi wako wa south Africa tulikushabikia iweje kwa jamaa iwe shida ?? Ni vile jamaa amebamba na story yake na wewe umepata wivu ?? Kausha maboya kama sisi tupunguze stress kwa simulizi za mwamba
 
Bado haileti maana hiyo dhana yako, kama ni hivyo kwanini wakati amesafiri alimwachia Umughaka kazi ya kununua mboga za huyo kiumbe, kama ni kuwasiliana na mganga wake si angewasiliana nae tu.
Kama ni mchakato ambao hata yeye ulikua kama unamgharimu au kumchosha huoni ndiyo maana aliona ni cheap kumtumia Umughaka kuliko huo mchakato?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…