ndukulusudicho
JF-Expert Member
- Aug 14, 2017
- 501
- 768
Shogako kamuitia ulevi RoyalAsante sana mkuu japo hii imekua fupi ila tunashukuru amatutoa Arosto
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Shogako kamuitia ulevi RoyalAsante sana mkuu japo hii imekua fupi ila tunashukuru amatutoa Arosto
Mawazo yako na akili yakomgando unadhani Ni choo Cha nje passport size.Dark world for dark people choon anahifandh wapi na watu hawaiingii au
Kumbuka siku ya kwanza alipokutana na Rehema, alisikia sauti kabla hata hajamuona Rehema.yani tumetoka kote uko kumbe sababu ni Rehema ... nmekua disappointed sana
mi nilidhani sijui ulikumbwa na balaa gani, kumhe demu ndo kakulostisha Daaah!! yani matukio yote uliopiga umeangukia pua kisa Rehema... aah umezingua sana .... Bora ingekua unatakiwa kumtoa bi Mkubwa hapo ningesapoti yani Demu mwanangu Demuuu aah nmeumia sana
We lazima utakua na la kuvunja chaga cyo kwa confidence hii
Maishani mwangu Nina beliefs kuwa ke ndio wanaoharibu maisha yetu wanaume Ilo halifichiki
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38] Vaa uhusika wa rey then rudia kauli yakoyani tumetoka kote uko kumbe sababu ni Rehema ... nmekua disappointed sana
mi nilidhani sijui ulikumbwa na balaa gani, kumhe demu ndo kakulostisha Daaah!! yani matukio yote uliopiga umeangukia pua kisa Rehema... aah umezingua sana .... Bora ingekua unatakiwa kumtoa bi Mkubwa hapo ningesapoti yani Demu mwanangu Demuuu aah nmeumia sana
thnx cwthrt [emoji8]Mbele kabisaaaaaaaaa[emoji144][emoji144][emoji144][emoji144][emoji144][emoji144]
Wapiiii Bantu Lady kitalembwa valentine Lovelovie Wigelekelo kiduku mpapaso Mafian cartel leadermoe F16 Falcon mafian Cartel Restless Hustler Antonio de Guzman National Anthem Labani og huku kwetu Joannah moneytalk
We kweli ni msumuma mwenzangu, umemfaham mpk Fr. Deo.Mkuu uchawi usukumani ni kama secret society zinavyofanya kazi forbidden knowledge zote ndio zimepelekea secret society ndio maana unasikia vikongwe wanakatwa mapanga ukihusishwa na uchawi. Uchawi pia unavyeo/ranks wale first class/highest rank ndio wanajua mambo makubwa.
Kwa walio kulia usukumani I.e mwanza, geita, shinyanga, tabora wanaweza kuwa wameskia au kushuhudia mtu aliyekufa baadae akarejea mara nyingi wanolejea hawajakatwa ulimi ndio wanasimulia mambo ya huko japo sio wote hupelekwa huko.
Sehemu niliyo kulia ilikuwa kawaida kusikia milio ya treni ikihusishwa na gamboshi.
Gamboshi ni kama taifa kule utaambiwa kuna wanasiasa wakubwa e.g Nyerere, kuna wachumi wakubwa I.e lipumba, kuna wanasayansi, walimu, shule, hospitali nk.
Nikawaida usukumani mme kuishi na mwanamke mchawi lakini asijue, usiku analala na fisi mkewe anaenda vilingeni.
Uchawi una operate kama secret society kwa sababu ya kuwakat mapanga na mara nyingi hata familia yenye uchawi unakuta anayejua ni mama na binti yake kwa sababu ndiye atakaye mrithisha na hao wengine ni ngazi ya kupanda daraja atakapo watoa kafara.
Kuna baadhi ya vijiji huko usukumani hukuti mzee(above 60) ni wabibi tu na vijana.
Ukiwa hauna kipaji unaenda kufanya manual work ndio hao wanaokatwa ulimi.
Lastly Gamboshi kwa wachawi ni kama sehemu takatifu mostly wa wale wanaoenda huko ni wenye loyalty ya highest order kwa hiyo sio rahisi kukwambia habari za huko.
Kuna padre mmoja alikuwa paroko mwadui father Deo alikuwa anafanya research yake kuhusu hayo mambo ya uchawi usukumani nadhani aliandika kitabu sijajua kama alikiweka public.
Tatizo hunisalimii🙄Mkuu kuna kijiwe kingine? Niungeni na mimi [emoji120]
I thought pete haivuliki kama ile bangili so how come imevulika kirahisi hivoUtajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 26
Maisha yaliendelea kuwa matamu sana kwa wakati huo na hakuna aliyefahamu kile tulichokifanya mimi na Ally kwenye ule mgahawa,watu wengi walikuja kujipatia chakula na kuondoka,kiukweli tulikuwa tunauza sana,kuna muda tulikuwa tunauza hadi tunachoka wenyewe.
Mimi kwa upande wangu maisha yangu yalininyookea na nilikuwa nikisevu fedha kwa ajili ujenzi wa nyumba tena,pamoja na kulipwa na Ally Mshahara kama msimamizi wa ule mgahawa lakini pia nilikuwa nikipitisha panga kubwa kwenye mauzo ya siku,kiukweli nilikuwa ninapiga sana pesa na ukizingatia kila mwisho wa mwezi nilikuwa nikijipatia fedha kwa njia ile ya Pete.
Mwanamke wangu Rehema alipokuja nyumbani,mambo ni kama yakaanza kubadilika,alikuwa mkali sana baada ya kuona nikiwa mkononi nimevaa Pete na akahisi uenda nilivishwa na mwanamke mwingine,kitu ambacho haikuwa kweli.
Rehema "Unadhani naweza kukuamini kama unavyodhani?"
Aliendelea "Niliwahi kukwambia nyie wanaume huwa mnatamaa sana,sasa umeona ushanitumia vya kutosha ukaona kabisa uvishwe Pete na mwanamke wako"
Aliendelea "Basi hata ungeniheshimu tu kwa kuivua na kuificha ili nikiondoka ndipo uivae!"
Mimi "Hayo ni mawazo mfu mpenzi wangu,siwezi kuvishwa Pete na mwanamke mwingine,inapaswa uniamini!"
Rehema "Usidhani kunisomesha ndiyo kigezo cha kunifanyia ujinga wako,tunaweza kuachana vile vile!"
Mimi "Kwani Ray siwezi kununua Pete na kuivaa tu?"
Rehema "Usinifanye mimi mtoto mdogo,wewe ungekuwa wa kununua Pete nadhani mimi ndiye ningekuwa wa kwanza kuvalishwa,sasa mimi hujawahi nivalisha Pete halafu unaniambia madudu gani sijui!"
Usiku mzima ulikuwa wa kupigizana kelele na Rehema na kiukweli hakuelewa kitu pamoja na kumueleza,siku hiyo kiukweli Rehema aligoma kabisa kunipatia maji ya kunywa ijapokuwa nilikuwa nina kiu ya kufa mtu,kila nilipokuwa nikajaribu kumgusa anigeuzie mtungi nichote maji ninywe yeye alidai niende nikanywe kwa mwanamke aliyenivisha ile Pete.Kiukweli usiku ule sikufanikiwa kabisa kuchota maji ya kunywa na nilikesha na kiu hadi asubuhi.
Sasa ilipofika asubuhi wakati mimi najiandaa kuelekea kazini na yeye aliamka akasema anarudi nyumbani kwao na nikimhitaji tena nihakikishe hanioni na hiyo Pete kwenye kidole.Nilijaribu kumtuliza lakini akawa mkali sana akawa ameondoka akaelekea kuoanda daladala.
Nilifunga mlango nikaondoka zangu kazini;Ilipofika usiku baada ya kutoka hapo kazini nilijaribu kumpigia simu Rehema lakini ilikuwa inaita tu haipokelewi,basi niliondoka hadi Ubungo msewe kwao Rehema na nilipofika nilivua ile Pete nikaiweka mfukoni kisha nikampigia simu,alipopokea nikamwambia nipo nje atoke tuzungumze!.Nilimbembeleza na nikamwambia ile Pete isije kuleta ugomvi kwani nimeivua na kuitupa,japo alinielewa lakini aligoma kabisa kuondoka na mimi akasema angekuja kesho yake,sikuwa na namna ilibidi niondoke zangu kurudi nyumbani,sasa wakati narudi nyumbani nikawa nimesahau kuivaa tena ile Pete na nilipofika nyumbani nikawa nimeingia kuoga na kulala,sasa ilipofika asubuhi wakati navaa ile jeans nilikuwa nimeivaa jana yake nilijaribu kuitafuta ile Pete mfukoni ili niivae lakini sikuweza kuiona,nilijitahidi kuitafuta sana hadi kukung'uta ile jeans lakini wapi !.
Niliamua kuondoka hivyo hivyo kuelekea job,sasa nikiwa kwenye gari Rehema akawa amenipigia simu ya kwamba anaenda nyumbani hivyo akawa anaulizia funguo nimeziweka wapi,nilipofika pale kituo cha Ngozi niliamua kushuka na kuingia upande wa pili ili nipande gari lingine nirudi nyumbani kumsubiri Rehema aliyekuwa njiani nimpatie funguo.Nilipofika nyumbani kuna hali nilianza kuhisi ambayo haikuwa nzuri,nilianza kuhisi baridi kama mtu ambaye alikuwa na malaria,kadiri muda ulivyokuwa ukienda ndipo hali yangu nayo ilikuwa mbaya sana.
Rehema alipofika nyumbani alikuta nimelala na aliniuliza kama ninamwa lakini nilimkatalia,alijaribu kunishika shingoni akakuta homa imekuwa kali,alikwenda pharmacy kuninulia dawa za kutuliza homa lakini nilipotumia bado hali haikuwa nzuri,sasa kwakuwa nilikuwa tayari nishafahamu kilichokuwa kinaendelea,nilichukua simu yangu nikawa nimempigia Ally Mpemba lakini simu ikawa inaita tu jamaa hakupokea.Baada ya muda kupita jamaa akawa amenitumia sms iliyosomeka "Wewe huna akili na utakufa kifo kibaya sana!".
Baada ya kuisoma ile sms niliifuta kabisa ili Ray atakaposhika simu yangu asije kuiona;Niliona ningeendelea kukaa kimya ningekufa kipumbavu kama alivyoniambia Ally Mpemba,nilichukua simu yangu nikampigia mama yangu Tarime pamoja na Dada yangu mkubwa wa Mwanza na nikawa nimewajulisha hali yangu haikuwa nzuri,sasa mama aliona mpaka nimempigia simu kiukweli hali yawezekana haikuwa nzuri,yeye alimpigia simu Anko wangu kitu ambacho sikutaka kabisa yeyote kutoka upande huo afahamu,na nilijua anko akifahamu ataanza ngonjera zake.Niliamua kuzima simu kabisa ili yeyote atakayenitafuta asinipate.
Hali yangu ilikuwa mbaya sana hadi Rehema akaamua kunipeleka dispensary pale Gongo la mboto kwa ajili ya kuchukua vipimo,majibu yalipotoka sikuonekana na tatizo lolote lakini kiukweli nilikuwa naumwa,sasa wakawa wameniambia ninywe maji mengi kwasababu hali kama hiyo huwa ni kawaida.
Wakati Rehema anadhani ni ugonjwa wa kawaida mimi nilikuwa nimeshafahamu tatizo ilikuwa ni ile Pete niliyoivua na kupotelea kusiko julikana,niliona nikiendelea kuzubaa naweza kupotea kabisa,tulivyorudi nyumbani mimi niliondoka nikawa nimerudi pale Msikitini Gongo la mboto(Masijid ijumaa),kuna Sheikh mmoja nilikuwa nafahamiana naye nikawa nimefika kumuulizia lakini nikaambiwa siku hiyo hajaonekana hapo,sasa kuna Sheikh mmoja sikutaka kumficha kitu chochote kwasababu niliona kabisa nikiendelea kupuuzia naweza kupoteza maisha.
Nilimwambia kuna Pete nilikuwa ninayo lakini haikuwa nzuri ilikuwa ikinisaidia kwenye mambo yangu ya biashara na baada ya kuivua tu nikaanza kuugua,yule Sheikh aliniambia nimsubiri amalize swala kisha tuondoke.Kweli,nilivumilia hadi akawa amemaliza kuswali na alipotoka nje nilimuwahi nikamwambia nilikuwa namsubiri,alinichukua tukaondoka tukawa tunapiga stori za hapa na pale hadi tulipofika kwake mitaa ya mzambarauni,tulipofika kwake namshukuru Mungu Sheikh akaanza kunisomea dua za kufa mtu,alinisomea sana na hatimaye akawa ameniambia kuna mafuta ninapaswa nikayanunue kwenye maduka ya kisuna ambayo nitakuwa ninayaweka kwenye maji kabla ya jua kuchomoza kisha nakwenda kuoga.
Yule Sheikh aliniandika jina la yale mafuta nikaenda kuyanunua na kiukweli baada ya ya kutoka pale hali yangu ikawa nzuri kiasi.
Asubuhi baada ya kupambazuka niliyatumia yale mafuta na hali yangu ikawa nzuri japo si sana lakini kiukweli nilimshukuru sana Sheikh.
Baada ya kuwa nimepata japo ahueni,niliondoka nikaelekea Kkoo kwenye mgahawa wa Ally Mpemba ili kama nikimkuta nijaribu kuzungumza nae maana nilikuwa nampigia simu zangu jamaa hapokei,nilipofika pale kuna mwanamke mmoja mwenye asili kama ya Ally nilimkuta nikawa nimeambiwa na wale wafanyakazi wa pale kwamba yeye ndiye alikuwa msimamizi wa pale.Niliwaza sana laikini sikupata majibu kwasababu haiwezekani mimi kutokuonekana siku moja tu Ally Mpemba akaamua kuniweka pembeni.
Niliondoka hadi kwenye duka lake la pale Aggrey lakini sikumkuta,nilijaribu tena kumpigia simu hakupatikana kabisa.Niliamua kwenda hadi pale kwenye duka la Gerezani kujaribu kumtafuta lakini nilipokwenda nilikuta lile duka limefungwa,sikutaka kukata tamaa kirahisi nikaona nielekee kwake Magomeni.Nilipofika Magomeni nilikuta geti limefungwa na nilipojaribu kugonga hakuna aliyekuwepo ndani,niliamua kuondoka na kurudi zangu nyumbani mdogo mdogo nikiwa nimekata tamaa kabisa.
Rehema alikaa kwangu takribani wiki moja kisha akawa amerudi kwao ili akajiandae aweze kurudi chuo.
Baada ya Rehema kuondoka mimi pia niliondoka kuelekea Sumbawanga huko Namanyere kwa mtaalamu ambaye hapo awali Mwakisaka alikuwa amenielekeza na kunipa mawasiliano yake.
Itaendelea..............
Pete inavulika,ka unakumbuka babu alompa alimsihi asije akaivua hiyo pete. Kwa kauli hyo obviously ina uwezo wa kutoka.I thought pete haivuliki kama ile bangili so how come imevulika kirahisi hivo
Pa1 sana master UMUGHAKAUtajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 26
Maisha yaliendelea kuwa matamu sana kwa wakati huo na hakuna aliyefahamu kile tulichokifanya mimi na Ally kwenye ule mgahawa,watu wengi walikuja kujipatia chakula na kuondoka,kiukweli tulikuwa tunauza sana,kuna muda tulikuwa tunauza hadi tunachoka wenyewe.
Mimi kwa upande wangu maisha yangu yalininyookea na nilikuwa nikisevu fedha kwa ajili ujenzi wa nyumba tena,pamoja na kulipwa na Ally Mshahara kama msimamizi wa ule mgahawa lakini pia nilikuwa nikipitisha panga kubwa kwenye mauzo ya siku,kiukweli nilikuwa ninapiga sana pesa na ukizingatia kila mwisho wa mwezi nilikuwa nikijipatia fedha kwa njia ile ya Pete.
Mwanamke wangu Rehema alipokuja nyumbani,mambo ni kama yakaanza kubadilika,alikuwa mkali sana baada ya kuona nikiwa mkononi nimevaa Pete na akahisi uenda nilivishwa na mwanamke mwingine,kitu ambacho haikuwa kweli.
Rehema "Unadhani naweza kukuamini kama unavyodhani?"
Aliendelea "Niliwahi kukwambia nyie wanaume huwa mnatamaa sana,sasa umeona ushanitumia vya kutosha ukaona kabisa uvishwe Pete na mwanamke wako"
Aliendelea "Basi hata ungeniheshimu tu kwa kuivua na kuificha ili nikiondoka ndipo uivae!"
Mimi "Hayo ni mawazo mfu mpenzi wangu,siwezi kuvishwa Pete na mwanamke mwingine,inapaswa uniamini!"
Rehema "Usidhani kunisomesha ndiyo kigezo cha kunifanyia ujinga wako,tunaweza kuachana vile vile!"
Mimi "Kwani Ray siwezi kununua Pete na kuivaa tu?"
Rehema "Usinifanye mimi mtoto mdogo,wewe ungekuwa wa kununua Pete nadhani mimi ndiye ningekuwa wa kwanza kuvalishwa,sasa mimi hujawahi nivalisha Pete halafu unaniambia madudu gani sijui!"
Usiku mzima ulikuwa wa kupigizana kelele na Rehema na kiukweli hakuelewa kitu pamoja na kumueleza,siku hiyo kiukweli Rehema aligoma kabisa kunipatia maji ya kunywa ijapokuwa nilikuwa nina kiu ya kufa mtu,kila nilipokuwa nikajaribu kumgusa anigeuzie mtungi nichote maji ninywe yeye alidai niende nikanywe kwa mwanamke aliyenivisha ile Pete.Kiukweli usiku ule sikufanikiwa kabisa kuchota maji ya kunywa na nilikesha na kiu hadi asubuhi.
Sasa ilipofika asubuhi wakati mimi najiandaa kuelekea kazini na yeye aliamka akasema anarudi nyumbani kwao na nikimhitaji tena nihakikishe hanioni na hiyo Pete kwenye kidole.Nilijaribu kumtuliza lakini akawa mkali sana akawa ameondoka akaelekea kuoanda daladala.
Nilifunga mlango nikaondoka zangu kazini;Ilipofika usiku baada ya kutoka hapo kazini nilijaribu kumpigia simu Rehema lakini ilikuwa inaita tu haipokelewi,basi niliondoka hadi Ubungo msewe kwao Rehema na nilipofika nilivua ile Pete nikaiweka mfukoni kisha nikampigia simu,alipopokea nikamwambia nipo nje atoke tuzungumze!.Nilimbembeleza na nikamwambia ile Pete isije kuleta ugomvi kwani nimeivua na kuitupa,japo alinielewa lakini aligoma kabisa kuondoka na mimi akasema angekuja kesho yake,sikuwa na namna ilibidi niondoke zangu kurudi nyumbani,sasa wakati narudi nyumbani nikawa nimesahau kuivaa tena ile Pete na nilipofika nyumbani nikawa nimeingia kuoga na kulala,sasa ilipofika asubuhi wakati navaa ile jeans nilikuwa nimeivaa jana yake nilijaribu kuitafuta ile Pete mfukoni ili niivae lakini sikuweza kuiona,nilijitahidi kuitafuta sana hadi kukung'uta ile jeans lakini wapi !.
Niliamua kuondoka hivyo hivyo kuelekea job,sasa nikiwa kwenye gari Rehema akawa amenipigia simu ya kwamba anaenda nyumbani hivyo akawa anaulizia funguo nimeziweka wapi,nilipofika pale kituo cha Ngozi niliamua kushuka na kuingia upande wa pili ili nipande gari lingine nirudi nyumbani kumsubiri Rehema aliyekuwa njiani nimpatie funguo.Nilipofika nyumbani kuna hali nilianza kuhisi ambayo haikuwa nzuri,nilianza kuhisi baridi kama mtu ambaye alikuwa na malaria,kadiri muda ulivyokuwa ukienda ndipo hali yangu nayo ilikuwa mbaya sana.
Rehema alipofika nyumbani alikuta nimelala na aliniuliza kama ninamwa lakini nilimkatalia,alijaribu kunishika shingoni akakuta homa imekuwa kali,alikwenda pharmacy kuninulia dawa za kutuliza homa lakini nilipotumia bado hali haikuwa nzuri,sasa kwakuwa nilikuwa tayari nishafahamu kilichokuwa kinaendelea,nilichukua simu yangu nikawa nimempigia Ally Mpemba lakini simu ikawa inaita tu jamaa hakupokea.Baada ya muda kupita jamaa akawa amenitumia sms iliyosomeka "Wewe huna akili na utakufa kifo kibaya sana!".
Baada ya kuisoma ile sms niliifuta kabisa ili Ray atakaposhika simu yangu asije kuiona;Niliona ningeendelea kukaa kimya ningekufa kipumbavu kama alivyoniambia Ally Mpemba,nilichukua simu yangu nikampigia mama yangu Tarime pamoja na Dada yangu mkubwa wa Mwanza na nikawa nimewajulisha hali yangu haikuwa nzuri,sasa mama aliona mpaka nimempigia simu kiukweli hali yawezekana haikuwa nzuri,yeye alimpigia simu Anko wangu kitu ambacho sikutaka kabisa yeyote kutoka upande huo afahamu,na nilijua anko akifahamu ataanza ngonjera zake.Niliamua kuzima simu kabisa ili yeyote atakayenitafuta asinipate.
Hali yangu ilikuwa mbaya sana hadi Rehema akaamua kunipeleka dispensary pale Gongo la mboto kwa ajili ya kuchukua vipimo,majibu yalipotoka sikuonekana na tatizo lolote lakini kiukweli nilikuwa naumwa,sasa wakawa wameniambia ninywe maji mengi kwasababu hali kama hiyo huwa ni kawaida.
Wakati Rehema anadhani ni ugonjwa wa kawaida mimi nilikuwa nimeshafahamu tatizo ilikuwa ni ile Pete niliyoivua na kupotelea kusiko julikana,niliona nikiendelea kuzubaa naweza kupotea kabisa,tulivyorudi nyumbani mimi niliondoka nikawa nimerudi pale Msikitini Gongo la mboto(Masijid ijumaa),kuna Sheikh mmoja nilikuwa nafahamiana naye nikawa nimefika kumuulizia lakini nikaambiwa siku hiyo hajaonekana hapo,sasa kuna Sheikh mmoja sikutaka kumficha kitu chochote kwasababu niliona kabisa nikiendelea kupuuzia naweza kupoteza maisha.
Nilimwambia kuna Pete nilikuwa ninayo lakini haikuwa nzuri ilikuwa ikinisaidia kwenye mambo yangu ya biashara na baada ya kuivua tu nikaanza kuugua,yule Sheikh aliniambia nimsubiri amalize swala kisha tuondoke.Kweli,nilivumilia hadi akawa amemaliza kuswali na alipotoka nje nilimuwahi nikamwambia nilikuwa namsubiri,alinichukua tukaondoka tukawa tunapiga stori za hapa na pale hadi tulipofika kwake mitaa ya mzambarauni,tulipofika kwake namshukuru Mungu Sheikh akaanza kunisomea dua za kufa mtu,alinisomea sana na hatimaye akawa ameniambia kuna mafuta ninapaswa nikayanunue kwenye maduka ya kisuna ambayo nitakuwa ninayaweka kwenye maji kabla ya jua kuchomoza kisha nakwenda kuoga.
Yule Sheikh aliniandika jina la yale mafuta nikaenda kuyanunua na kiukweli baada ya ya kutoka pale hali yangu ikawa nzuri kiasi.
Asubuhi baada ya kupambazuka niliyatumia yale mafuta na hali yangu ikawa nzuri japo si sana lakini kiukweli nilimshukuru sana Sheikh.
Baada ya kuwa nimepata japo ahueni,niliondoka nikaelekea Kkoo kwenye mgahawa wa Ally Mpemba ili kama nikimkuta nijaribu kuzungumza nae maana nilikuwa nampigia simu zangu jamaa hapokei,nilipofika pale kuna mwanamke mmoja mwenye asili kama ya Ally nilimkuta nikawa nimeambiwa na wale wafanyakazi wa pale kwamba yeye ndiye alikuwa msimamizi wa pale.Niliwaza sana laikini sikupata majibu kwasababu haiwezekani mimi kutokuonekana siku moja tu Ally Mpemba akaamua kuniweka pembeni.
Niliondoka hadi kwenye duka lake la pale Aggrey lakini sikumkuta,nilijaribu tena kumpigia simu hakupatikana kabisa.Niliamua kwenda hadi pale kwenye duka la Gerezani kujaribu kumtafuta lakini nilipokwenda nilikuta lile duka limefungwa,sikutaka kukata tamaa kirahisi nikaona nielekee kwake Magomeni.Nilipofika Magomeni nilikuta geti limefungwa na nilipojaribu kugonga hakuna aliyekuwepo ndani,niliamua kuondoka na kurudi zangu nyumbani mdogo mdogo nikiwa nimekata tamaa kabisa.
Rehema alikaa kwangu takribani wiki moja kisha akawa amerudi kwao ili akajiandae aweze kurudi chuo.
Baada ya Rehema kuondoka mimi pia niliondoka kuelekea Sumbawanga huko Namanyere kwa mtaalamu ambaye hapo awali Mwakisaka alikuwa amenielekeza na kunipa mawasiliano yake.
Itaendelea..............
Hii stori imenifanya nichelewe kazini
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]yani tumetoka kote uko kumbe sababu ni Rehema ... nmekua disappointed sana
mi nilidhani sijui ulikumbwa na balaa gani, kumhe demu ndo kakulostisha Daaah!! yani matukio yote uliopiga umeangukia pua kisa Rehema... aah umezingua sana .... Bora ingekua unatakiwa kumtoa bi Mkubwa hapo ningesapoti yani Demu mwanangu Demuuu aah nmeumia sana
Waswahili hamna jema aisee
Uyo mdau @lwandamagele nakumbuka anao uzi kabisa anaelezea story ya maisha yake kule entertainment lakini haikuisha ilifika ep ya 50.Sahihi lakini pia hawa jamaa kwenye ulimwengu wao wa roho wakishakuchoka watakutengenezea zengwe ili ushindwe kutimiza masharti.
Kama unakumbuka magere aliambiwa alipe gharama kwa kumtoa kafara mkewe na hiyo ni baada ya mkewe kumpa funguo dada wa kazi asafishe kile chumba ambacho magere aliambiwa haitakiwi mtu yeyote kuingia humo isipokua yeye tu.
Kuna namna hawa jamaa wanakusahaulisha, si unakumbuka magere alivyosahau ile funguo hadi mkewe akaiona na kumpa dada wa kazi akafanye usafi kweye ile room. From there magere akatakiwa amtoe mkewe na aligoma mwisho mke wakamuua kwa ajali ya kimazingira.
Hii dunia ina mambo meusi hatari