Utajiri wa siri wa mchoma mahindi

Utajiri wa siri wa mchoma mahindi

Nilikoma kula mahindi dar yanawekewa mpaka chachandu na limao kwani wanakula wajawazito
 
c9885274c5f532a7e2870521eea787da.jpg

UGUMU WA MAISHA HUANZIA AKILINI MWAKO.

Ebu fikiria Dada anayechoma mahindi maeneo ya Manzese Darajani kuanzia saa 12 jioni mpaka SAA 2 usiku, kwa siku moja anauwezo wa kuchoma mahindi .50. Kila hindi moja ananunua shambani kwa shilingi 100/- Na Anauza kwa sh.600/-

Hiyo ina maana mahindi 50 ananunua kwa shilingi 5000/- akichoma na kuuza anapata sh.30,000/-. Akitoa pesa ya mtaji (5000/- ya mahindi na 1500/- ya mkaa) anabakiwa na sh.23,500/- kwa siku.
af8b3165183b82485f76c4c664fad30f.jpg

Hivyo kwa mwezi huyu mchoma mahindi atakuwa ameingiza kiasi cha sh.705,000/-

Mwalimu mwenye Degree anayeanza kazi analipwa 584,000/- akikatwa kodi pamoja na makato mengene ya mifuko ya jamii anabakiwa na sh.425,000/.

Tofauti ya Mwalimu wa degree na Muuza mahindi ni

Kuwa Mwalimu kanaajiriwa,

muuza mahindi kajiajiri.
4629b3787c92b1fe414bcc6c0e84aaef.jpg

Mwalimu anafanya kazi masaa 9 kwa siku (saa2 asubuh hadi 11jioni)

muuza mahindi anafanya kazi masaa matatu kwa siku (saa 12 jioni hadi 2 usiku).

Mwalimu anatumia muda wake wa ziada kusahihisha mitihani na homework,

mchoma mahindi anatumia muda wake wa ziada kutafuta fursa nyingine za kupata hela zaidi..

UOGA WAKO NDIO UMASKINI WAKO..
Mnaongeaga kirahisi sana na mnakuwa na mawazo makubwa sana ya biashara yenye ndoto za "faida" tu hamkadirii risks zinazoambatana na biashara husika na dynamics za soko. Kwamba mtu akichukua mahindi 400 atauza amalize yote siku hiyo hiyo, na itakuwa hivyo daily? Kayasafirisha vipi? Kayachoma juani hajatumia mkaa? Bei yake huwa hiyo hiyo throughout the year nq hayaadimiki? Unauzia wapi na je unalipia eneo/ ushuru? Unauza peke yako (ushindani) kama upo? Nk. Nk.

Ndugu zangu maisha yangekuwa kama mnavyowaza nyie mnaojiita "motivational speakers" ambao infact mna-deliver utopian thoughts kwa vitu ambavyo hamkuwahi vifanya basi hakuna ambaye angelia shida na sisi wote wenye kima cha chini tungeenda kuuza mahindi.

Biashara sio mteremko wa maisha kwamba ukishindwa vyooote basi unafanya tu simply "unafanikiwa". Inahitaji kutulia kifikra, uzoefu na kazi ngumu kama kazi zingine zote tu otherwise utakesha kwa masangoma uchanjwe hadi sehemu za kukalia na ufanye vitu vya ajabu.
 
Back
Top Bottom