Utajuaje kama sehemu uliyopo ni Bush?

Utajuaje kama sehemu uliyopo ni Bush?

Si lazima Kwenda shambani, mfano dar wanaamka mapema kuwahi soko la samaki,na ni kawaida kupanda na ndoo za samaki kwenye usafiri wa uma.
Lakini mimi nazungumzia vijijini sasa huko ferry ndio shambani mkuu?
 
1.Watu wengi wanajishughulisha na kilimo wanaamka saa 10 alfajiri kwenda mashambani.Pia ng'ombe zinatumika kulima

2.Ni kawaida kukutana na wazee mababu na mabibi

3.Watu wengi wanaongea lugha za makabila

4.Wanawake/wamama wengi wanavaa khanga

5.Ukipanda daladala kwenda Town mfano ahsubuhi unapanda na watu wanaopakia matenga ya mazao wanayotoka kuyanunua ili wakayauze huko waendako

6.Kujaa kwa nyumba za tope

7. Wenyeviti wa mitaa,vitongoji/ vijiji wanaogopeka kana kwamba ndio Marais

8.Kukitokea Msiba wanatangaza na vipaza sauti

9.Wasichana wengi wadogo kuwa na watoto pia wanawake wengi kubeba watoto migongoni

10.Watoto wengi kutomaliza la saba au wakimaliza hawaendelei.

11.Vikosi vya ng'ombe vinapita kwa wingi vikipelekwa machungani hasa ile ming'ombe yenye nundu

Nitaongezea mengine kadri nitakavyokuwa nayasoma mazingira ya huku bushi nawe waweza kuongezea yako unayoyafahamu kuhusu mbwinde.
Kwa vile kiswahili ni lugha ya kikabila kwa Dar es salaam na mengi kati ya uliyoorodhesha yanapaitika hapo, bas sehemu kubwa ya Dar es Salaam ni Bush;
 
Umefika mikoa mingapi ?
Nimetembea hii bongo yapata zaidi ya mikoa 20, bado Mara, Tanga, Manyara na Katavi. Unafahamu kuwa mpaka huko Daslam kwenu Kuna vijiji? Angalia Hapa chini:
1. Kijiji cha Kawe - Kijiji hiki kipo katika eneo la Kinondoni, magharibi mwa jiji la Dar es Salaam.
2. Kijiji cha Kibada - Kijiji hiki kipo katika eneo la Temeke, mashariki mwa jiji.
3. Kijiji cha Bunju - Kijiji hiki kipo kaskazini mwa jiji, katika eneo la Kinondoni.
4. Kijiji cha Kigamboni - Kijiji hiki kipo katika eneo la Kigamboni, kusini mwa jiji.
5. Kijiji cha Mbweni - Kijiji hiki kipo katika eneo la Temeke, mashariki mwa jiji.
6. Kijiji cha Kunduchi - Kijiji hiki kipo katika eneo la Kinondoni, magharibi mwa jiji.🤣
 
1.Watu wengi wanajishughulisha na kilimo wanaamka saa 10 alfajiri kwenda mashambani.Pia ng'ombe zinatumika kulima

2.Ni kawaida kukutana na wazee mababu na mabibi

3.Watu wengi wanaongea lugha za makabila

4.Wanawake/wamama wengi wanavaa khanga

5.Ukipanda daladala kwenda Town mfano ahsubuhi unapanda na watu wanaopakia matenga ya mazao wanayotoka kuyanunua ili wakayauze huko waendako

6.Kujaa kwa nyumba za tope

7. Wenyeviti wa mitaa,vitongoji/ vijiji wanaogopeka kana kwamba ndio Marais

8.Kukitokea Msiba wanatangaza na vipaza sauti

9.Wasichana wengi wadogo kuwa na watoto pia wanawake wengi kubeba watoto migongoni

10.Watoto wengi kutomaliza la saba au wakimaliza hawaendelei.

11.Vikosi vya ng'ombe vinapita kwa wingi vikipelekwa machungani hasa ile ming'ombe yenye nundu

Nitaongezea mengine kadri nitakavyokuwa nayasoma mazingira ya huku bushi nawe waweza kuongezea yako unayoyafahamu kuhusu mbwinde.
Umesahau ukiona pia matela ya punda na ng'ombe,
Kukutana na ma pawatila
 
-Kanisani na misikitini baadhi ya watu wanaenda na jezi za mpira
-Mzazi akiwa na mtoto ni mwalimu wa shule ya msing au mtendaji atajitamba kijiji kizima, Maana mwalimu kijiji ana heshimika Mno.
- Ukiwa mgeni ukipita mtaani kila Mtu anakutolea mi macho
-kijana au binti mlie pishana nae miaka 2 anakusalimia shikamoo.
 
-Kanisani na misikitini baadhi ya watu wanaenda na jezi za mpira
-Mzazi akiwa na mtoto ni mwalimu wa shule ya msing au mtendaji atajitamba kijiji kizima, Maana mwalimu kijiji ana heshimika Mno.
- Ukiwa mgeni ukipita mtaani kila Mtu anakutolea mi macho
-kijana au binti mlie pishana nae miaka 2 anakusalimia shikamoo.
Mbona huku mpaka mi mama na mibaba mizima inatoage shikamoo
 
Taja sifa nyingine kama vile kule mtama ambapo akinamama wapigakura wanalala chini wakanyagwe na mgombea
 
Back
Top Bottom