Utakaa barabarani mpaka ufikishe miaka 90?

Utakaa barabarani mpaka ufikishe miaka 90?

Wordsworth

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2019
Posts
1,191
Reaction score
3,360
Nyerere, pamoja na matatizo yake yote alikomboa maskini kwa njia ya redistribution of resources. (ingawa angefanya kwa njia nyingine) Hakuwa na watendaji wazuri na viongozi wenzake wakati ule hawakumulewa (ni ngumu sana kumuelewa idealist na mtu mwenye vision ya miaka zaidi ya 100 ijayo).

Ninachotaka kusema kwamba yasingefanyika yale yaliyofanyika miaka hio, leo hii mwenye nacho angebaki nacho na asiyenacho asingekuwa na namna yoyote yakufanya ili na yeye awe nacho.

Pamoja na matatizo yote tuliyonayo Watanzania bado tuna uwezo wa kutafuta na kupata (social mobility). Hii ni kwa sababu rasilimali kama vile ardhi bado vipo mikononi mwa wananchi. Sisi siyo kama Kenya, Nigeria au mataifa yaliyoendelea ambapo wenye ardhi ni watu wachache sana na wanaobakia wanateseka na inabidi watafute njia nyingine ya kuingiza kipato. Ardhi ni ya thamani sana hatujui tu.

Huku Tanzania watu wengi wana ardhi za kurithi za mababu zao. Sipendi kujumlisha watu kwenye category moja lakini ukweli lazima usemwe tu. Vijana wengi wa Kitanzania na Watanzania kwa ujumla ni wavivu. Yaani wewe mtu na akili zako na nguvu zako unaondoka shambani unafuata mkumbo wa kwenda mjini eti kwa kisingizio cha kutafuta kipato. Unafika unaenda kukalisha makalio yako kibandani kwenye njia ya wapita miguu unauza dodoki. Eti na wewe unatafuta riziki. Huwezi hata kujiuliza hii shughuli ninayofanya hapa inasaidia vipi katika kuimarisha uchumi wa nchi.

Unamuacha mzee kijijini alime, wewe kijana mwenye nguvu unaenda kujikalisha mjini. Unashindwa kweli kufanya kilimo? Hapa najua majibu yenu ni kwamba kilimo ni kigumu blah blah blah nyingi. Ni hivi hakuna kitu kirahisi na kama unataka njia za mkato utaishia pabaya tu. Mpe hiyo ardhi uliyoikimbia Mnigeria au Mkenya akuoneshe. Au unyanganywe ndio utaelewa umuhimu wake?

Haya basi umelazimisha kuhamia mjini. Wakati wa Kikwete masoko ya machinga yalijengwa yakutosha ili wafanyabiashara wadogo wafanye kazi. Waliyakataa. Yaani mtu unakimbia sehemu ambayo ni rasmi ambapo ungetambulika kwenye mifumo yote ya nchi? Upo tayari kufanya biashara ambayo hata ukiumwa huwezi kuingiza kipato? Mnajua umuhimu wa kutambulika? Mnafahamu kwamba mngeweza kujikusanya na kupata mikopo ya vijana isiyo na riba halmashauri na kwenye baadhi ya mabenki?

Unakaa barabarani huna ujuzi wowote, hata kwenda VETA? Ukiingiza bando la mtandaoni ni kushinda kwenye udaku na kubeti hamna unachojifunza ili kuboresha maisha yako. Unaoa na kuolewa na unapata watoto. Unategemea kuwalisha kwa biashara za barabarani? Ukiumwa au mkitimuliwa inakuwaje? Ukizeeka utabaki kulalamika na kutamani urudishe miaka nyuma

Narudia tena hakuna kitu kirahisi lazima ujitume kimwili na kiakili. Kuwepo kwenye mifumo rasmi ni muhimu sana. Leo na kesho ukiumwa au ukifa bado biashara yako itaendelea. Watoto wako watarithi kibanda chenye uhakika. Mnafikiri familia zenye pesa (naongelea old money siyo hawa new money wanaorudi kwenye umasikini baada ya kizazi kimoja) muda wote wanapesa tu hawaishiwi? Wanaishiwa, lakini kwa sababu wanatambulika kwenye mifumo wana kopesheka na wana bima za kutosha hawawezi kuwa masikini. Uliyejikalisha hapo barabarani una hata bima ya afya?

Ninachosema hapa hakiwezi kutatua tatizo la umaskini katika jamii, umasikini ni mfumo na kinachohitajika ni jitihada za kutosha zikiongozwa na serikali kulitatua tatizo hili.

Ninachosema ni hatua mtu binafsi anazoweza kuchukua ili kuhakikisha anaboresha maisha yake yeye na ya watoto wake. Mifumo inafanya tajiri aendelee kuwa tajiri na masikini aendelee kuwa masikini. Hakikisha unakuwa katika mfumo rasmi ili uondokane na hili janga la umasikini. Tupo kwenye nchi ambayo bado matabaka kwenye jamii hayajakomaa. Huko baadaye yakikomaa utajutia kweli ujana wako na kwa nini hukutaka kuhangaika.

Na serikali nayo imelala sijui imekufa. Mipango miji ilitenga maeneo ya huduma za jamii ikiwemo masoko madogo kwenye maeneo ya makazi ya watu. Hayo maeneo yako wapi? Mliwauzia watu binafsi au?
Mwenye masikio na asikie.
 
Kama ulishawahi kusikia ule msemo, sungura kambeba tembo ndo hii sasa!
 
Lack of exposure ni tatizo kubwa kwa Watanzania. Niliangalia documentary ya Mghana alikwenda kutafuta maisha Ulaya, alizamia meli akaishia Italy. Alipata kazi kwenye mashamba ya nyanya.

Alibeba idea ile ya kilimo, alipotoboa alikwenda Ujerumani, alinunua matrekta na lorry. Amerudi Ghana sasa hivi anafanya commercial farming ya nyanya.
 
Lack of exposure ni tatizo kubwa kwa Watanzania. Niliangalia documentary ya Mghana alikwenda kutafuta maisha Ulaya, alizamia meli akaishia Italy. Alipata kazi kwenye mashamba ya nyanya.

Alibeba idea ile ya kilimo, alipotoboa alikwenda Ujerumani, alinunua matrekta na lorry. Amerudi Ghana sasa hivi anafanya industria farming ya nyanya.
Huo mstari wa kwanza umemaliza kila kitu.
 
Lack of exposure ni tatizo kubwa kwa Watanzania. Niliangalia documentary ya Mghana alikwenda kutafuta maisha Ulaya, alizamia meli akaishia Italy. Alipata kazi kwenye mashamba ya nyanya.

Alibeba idea ile ya kilimo, alipotoboa alikwenda Ujerumani, alinunua matrekta na lorry. Amerudi Ghana sasa hivi anafanya industria farming ya nyanya.
Lack of exposure!! Hii ndo main point.
Lakini watu wana smartphone na wanamitandao. Wanashinda kwenye udaku. Hawawezi kujifunza? Kuna makala kibao, video kibao. Wanashindwaje kupata exposure?
Wanataka wabebwe?
 
Umeongea vizuri, tuna mengi ya kujifunza kama taifa na kama individuals.

Inasikitisha sana mwenye nchi/raisi ndio anakuwa advocate mkubwa wa kutandaza biashara pembezoni kwa barabara. Yaani inasikitisha sana!
 
Trust me nakomaa na barabarani nasiji kuzeeka kidenzi my big dream is to become dollars billionaire
Kwa ufupi uko mashambani kama auna mpunga wa maana ni kama unacheza kamari usione watu wanatoka nduki kote uko watu washapita
 
Trust me nakomaa na barabarani nasiji kuzeeka kidenzi my big dream is to become dollars billionaire
Kwa ufupi uko mashambani kama auna mpunga wa maana ni kama unacheza kamari usione watu wanatoka nduki kote uko watu washapita
Utakuwa billionaire kwa kukaa barabarani?
😂😂😂😂😂😂
Labda kama una njia nyingine haramu ya kukuingizia kipato.
Tafuta shughuli rasmi ya kufanya yenye kukuingizia kipato. Nenda hata VETA.
Au unasubiria serikali ikulimie shamba?
 
Si hakima bali ni hekima.
Mwenye masikio na asikie.
Siwezi kubishana na mtu asiye na idea yeyote kuhusu history, economics, sociology na anthropology.
Ciao[emoji111]
Pamoja na kwamba umeandika uzi mzuri ila una ujuaji mwingi na kujifanya mkorofi bila sababu. Huu mtazamo hauwezi kuutumia shambani uko unakosema kulimia mafenesi na mchaichai. Be humble, na kwa hali hii hutokuwa na maajabu zaidi ya kutishia watu. Ukiendeleza ligi mimi sitahusika.

Sasa ulitaka huyo alete idea za Economics, History, Anthropology kwani huu uzi una idea gani kati ya hizo. Hivi vitu ni common sense, hakuna special field.
 
Uko sawa wa bongo % kubwa hatupendi kujiibidisha tunapenda sna vitonga pasipo kupiga hesabu ya kesho yake.sehemu yoyote utakayo jikita vizuri jipe miaka 3 lazima utoboe sema sasa zile akikukuta mwenzio anakukatisha tamaa then unaacha mnajiunga ktk kundi la usengenyaji, Mara siku hizi anajisikia sna baada ya kupata vihela ...pumb@v Fanya kazi kiumbe
 
Pamoja na kwamba umeandika uzi mzuri ila una ujuaji mwingi na kujifanya mkorofi bila sababu. Huu mtazamo hauwezi kuutumia shambani uko unakosema kulimia mafenesi na mchaichai. Be humble, na kwa hali hii hutokuwa na maajabu zaidi ya kutishia watu. Ukiendeleza ligi mimi sitahusika.

Sasa ulitaka huyo alete idea za Economics, History, Anthropology kwani huu uzi una idea gani kati ya hizo. Hivi vitu ni common sense, hakuna special field.
Lazma niwe mjuaji kwasababu ninajua haswa.

Wewe ardhi unayoiona haina thamani mwenzako anaitamani. Fungua akili acha kulegalega. Unataka kulimiwa shamba?

Unaelewa application ya history? Economics? Anthropology? Hujui. Hiki ndio ninachokiongelea hapa.

Au ulitaka nianze uzi na "Good morning class today I will teach you anthropology ..."

Changamka una mtandao, jifunze!
 
Umeandika ya maana lakin umeandika kijuaji sana na kwa kiburi

Halaf weng wanaoandikaga hiv huwa si lolote si chochote..wao ni wajuz sana wa ku preach ila wao hawatendi...yaan mnakuaga vzur kwenye kuongea lakin hata income ya maana huna..uwekezaj wako ni wakuhangaika hangaika
Or else ni mdada umeolewa bwana anakuhudumia kakupa ka mtaj ka mini supermarket hapo bas unajiona umewin maisha....

Umeongea ya maana ila presentation ya hovyo inatufanya sis ambao ni go getters tukuone una bwabwaja tu

Huko barabaran kuna watu wanatengeneza mamilion ya pesa..bakhresa anauzia ukwaju na ice cream wap...bidhaa zote unazoziona barabaran behind the scenes kuna mwamba anaingiza 500k a day..wengne had 30m a day....kuna mzee hapo kkoo ambae ni mentor wangu anaingiza karibu 10m a day kwa hzo bidhaa za barabaran hapo kkoo..kwahyo tizama maisha kwa pande nne wew binti.
 
Uko sawa wa bongo % kubwa hatupendi kujiibidisha tunapenda sna vitonga pasipo kupiga hesabu ya kesho yake.sehemu yoyote utakayo jikita vizuri jipe miaka 3 lazima utoboe sema sasa zile akikukuta mwenzio anakukatisha tamaa then unaacha mnajiunga ktk kundi la usengenyaji,Mara siku hizi anajisikia sna baada ya kupata vi hela ...pumb@v Fanya kaz kiumbe
Ni sawa kabisa ulichosema.
Peer pressure ni janga lingine. Mtu hawezi kujiona yeye kama yeye aangalie future yake anaogopa wenzake watamuonaje utafikiri atazeeka nao.
 
Back
Top Bottom