Utamaduni; Ndugu wanisihi nikawawekee wanangu kinga kama desruri, nipo njia panda

Utamaduni; Ndugu wanisihi nikawawekee wanangu kinga kama desruri, nipo njia panda

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Nipo njia panda wakuu,

Zamani enzi zetu miaka ya nyuma kidogo kuna baadhi ya makabila kwenye koo flani ilikuwa ni lazima upewe kinga, haya mambo yalianza zamani sana tunaambiwa ni baada ya wahamiaji wapya, kuowa nje ya ukoo, kuchanganyana na koo mpya kukaanza kujitokeza mambo ya teknolojia ya giza kwa hio ndo hizi kinga zikaanza kutengenezwa na baadhi za koo kwenye kabila.

nakumbuka nikiwa mdogo mimi na watoto wa rika langu wa kwenye ukoo tulipashiwa maji yamoto kwenye chungu wajaweka dawa wakaanza kutumbukiza matawi ya mti flani tukaambiwa tuvue nguo zote tukaanza kama kuchapwa na hayo matawi mwili mzima, baada ya hapo tulichanjwa na nyembe na kuwekwa dawa na kupewa masharti tusije kula maini, tusije kula nguruwe, tusije kukalia kinu.

Kwangu binafsi nmeskia stori nyingi za shuhuda za hii ila kwa mimi kama mimi nilichoshuhudis ni watu wa karibu waliowahi kuniibia vitu hasa vya gharama nliwakuta navyo kabla hawajaviuza mara kadhaa, pia kuna mtaa niliwahi kupanga uswazi nikiwa chuo ili nibane pesa, ile nyumba baada ya siku 2 nikaanza kusikia vishindo darini, asubuhi wapangaji wakaniambia ni tatizo la muda, baada ya wiki 2 tatizo likajirudia, baada ya fujo za vishindo kwa dakika 5, kishindo kikubwa mno kililia batini mithiri ya mtu kudondoka na wapangaji wote tulitoka nje kuangalia juu kuna nini huku tukiwa na hofu ila hatukuona kitu, siku inayofata mtoto wa mama mwenye nyumba alikuwa kanikunjia sura huku mama yake hajatoka nje tangu asubuhi, nikahama siku hio hio na kuacha kodi yangu.

Ila masharti yake kiukweli ni mzigo, hutakiwi kukalia kinu, hutakiwi kula nguruwe na hutakiwi kula maini. ukienda kinyume na hapo ndo basi umeifuta na unatakiwa uende ku renew upya.

Sasa shida zote za nini hizi, Ninataka kujenga hoja ya namna ya jisi ya kuwaambia hao ndugu kwamba haya mambo kwa watoto wangu yatakuwa magumu, maana hata mama yao tu hachangamani kabisa na haya mambo,

sijui nifanye nini
 
Kinga za kabia gani hizo Mkuu?
Btw waruhusu wanao wakafanyiwe, hakuna kitu kinachorudisha maendeleo nyuma kwa Afrika kama uchawi.
Kwangu mimi bora mwizi kuliko mchawi.
kabila ntaweka siri ila haya mambo yapo kiukoo zaidi kuliko kikabila, sisi hii dawa ni maalum kwajili ya ukoo wetu na koo nyingine ndogo zilizikua zikiishi karibu ambazo ni kama zilimezwa na ukoo wetu ama tufanye ni watani, nje ya hapo huwezi ni ngumu.

kuhusu wanangu kufanyiwa nsona kama ni mzigo tu maana sikuhizi kuna ukiwa na imani na maombi basi hizi dawa zinakua mizigo tu.
 
kabila ntaweka siri ila haya mambo yapo kiukoo zaidi kuliko kikabila, sisi hii dawa ni maalum kwajili ya ukoo wetu na koo nyingine ndogo zilizikua zikiishi karibu ambazo ni kama zilimezwa na ukoo wetu ama tufanye ni watani, nje ya hapo huwezi ni ngumu.

kuhusu wanangu kufanyiwa nsona kama ni mzigo tu maana sikuhizi kuna ukiwa na imani na maombi basi hizi dawa zinakua mizigo tu.
Sawa Mkuu, kinga ni muhimu hata kama kuna maombi unayosemea sababu imani inahitaji kujitoa 100% na huwezi jua watoto watajitoaje kiimani.
 
Shtuka wanao wanaingizwa kwenye network ya wachawi na mizimu. Kuna familia zinakufa vifo vya kufanana, magonjwa ya kufanana, shida za kufanana ie, hawaolewi, hawafaulu, umasikini etc ni maagano ya kiukoo. Huko ndiko unapeleka wanao
 
kabila ntaweka siri ila haya mambo yapo kiukoo zaidi kuliko kikabila, sisi hii dawa ni maalum kwajili ya ukoo wetu na koo nyingine ndogo zilizikua zikiishi karibu ambazo ni kama zilimezwa na ukoo wetu ama tufanye ni watani, nje ya hapo huwezi ni ngumu.

kuhusu wanangu kufanyiwa nsona kama ni mzigo tu maana sikuhizi kuna ukiwa na imani na maombi basi hizi dawa zinakua mizigo tu.
Ni mambo ya imani tuu,Sasa sisi yatima tunachanjwa na nani?!
 
Fata mila zenu acha ujinga, ya wazungu watajifunzia wenyewe wakikuwa.
 
Shtuka wanao wanaingizwa kwenye network ya wachawi na mizimu. Kuna familia zinakufa vifo vya kufanana, magonjwa ya kufanana, shida za kufanana ie, hawaolewi, hawafaulu, umasikini etc ni maagano ya kiukoo. Huko ndiko unapeleka wanao
Hapo kwenye “hawaolewi” nadhani haihitaji rocket science kujua ni “network” ya uchawi ama la. We unaona tu hata kwao kupika/ kufanya kazi anaona kazi ambapo yupo chini ya utawala wa mtu, huyo mwanadada atahitaji rocket science kujua amelogwa ili asiolewe?!
 
Back
Top Bottom