Hatotokea kiongozi yeyote tanzania akaachia nafasi kubwa kama hiyo kama lowasa alivyo fanya.
Aliwajibika kwa makosa ambayo hakufanya alionesha usomi na uelewa wa kiwango cha juu.
Nilimpigia kampeni ati nilitembea kata zote 19 kwa miguu kuwaelimisha wananchi kuhusu kwa nini aliachia cheo cha waziri mkuu.
Nyie zile pilikapilika za 2015 sio za kusahau.
1.Team lowassa
2. Team ulipo tupo
Lowassaaaaaaaa mabadiliko, mabadilikooooooooooooo lowasa.
Roho nyeupe, ngozi nyeupe, nywele nyeupe mapema asubuhi mpaka Ikulu.🤣
Bibi yangu mimi ilikuwa ni lazima apige kura sasa yeye alicho kuwa akijua ni ccm na nyerere,
Bibi yeye anasema atampigia kura wa chama cha nyerere, sasa tukachukuwa picha ya lowasa tukamuekeza kuwa lowasa ni mtoto wa nyerere, alivyoona zile nywele nyeupe akase, maaaaaaaawe anamfanana baba yake nyerere ona hizo nywele kweli nampigia kura🤣
Siku ya kupiga kura mapema vijana walishamfata na pikipiki mpaka kituo cha kupigia kura, si hajui kusoma, alivyouliza bibi unampigia kura nani akasema wa chama cha nyerere🤣
Wakamuuliza unamjua picha yake? , si alisha oneshwa picha ya lowasa na nywele zake akawaonesha huyu hapa mwenye nywele nyeupe🤣 imeisha hiyo.
RIP BIBI YANGU
RIP LOWASSA