Utamkumbuka Edward Lowassa kwa mambo gani?

Utamkumbuka Edward Lowassa kwa mambo gani?

Barabara ya sinza

Akiwa PM alifika pale shekilango akapiga mkwara mzito sana; after 2 days wakaanza kuweka lami.

Barabara ilikua mbovu sana before 2006

Maybe wangeipa jina la Lowassa Road kwa heshima yake
 
Yale Maandamano ya Chadema kumpeleka Lowasa Tume ya Uchaguzi Posta house kuchukua Fomu ya kugombea uRais 2015 sijui yaliratibiwa ya nani

Yameweka rekodi Kwenye historia ya Uchaguzi wa Vyama Vingi

Mfungapo Kwaresma Msiwe kama Wanafiki 😃
 

Habari Wadau,

Leo Februari 10, 2024 Makamu wa Rais Dkt. Mpango ametangaza kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania na Mgombea Urais wa CHADEMA mwaka 2015 Edward Ngoyai Lowasa

Soma: Edward Lowassa (Waziri Mkuu Mstaafu na Mgombea Urais wa CHADEMA 2015) afariki dunia

Katika mwaka enzi za uhai wake Mzee alipata kuwa na ushawishi Mkubwa nchini kiwango cha kuweza kujaza mikutano katika Uchaguzi wa Urais mwaka 2015.

Binafsi ntamkumbuka sana kwa uthubutu wake wa kuweza kujiuzulu nafasi ya Uwaziri Mkuu alipohusishwa na tuhuma za ufisadi.

Wewe utamkumbuka Lowassa kwa mambo gani?
Ninachojua ni kuwa lowassa hakukosa urais. Bali watanzania walikosa rais.
 
Tanzanian president Jakaya Kikwete has reshuffled his cabinet after Prime Minister resignation following corruption scandal in which many of government officials received kickback.

-BBC World Service, a day after E.N Lowassa resignation.
 
Ni wewe.mzee lowasa ulietuwekea shule za sekondari za kata, hukuwa na visasi, japo walikuzushia sijui kama ni kweli au la, ila pumzika kwa amani mzee wangu, watoto wetu mamia kwa maelfu wanaenda sekondari, ni juhudi zako mzee lowasa. Pumzika kwa amani.
 
Tanzanian president Jakaya Kikwete has reshuffled his cabinet after Prime Minister resignation following corruption scandal in which many of government officials received kickback.

-BBC World Service, a day after E.N Lowassa resignation.
Kikwete Muungwana sana

nakumbuka Jan 1990 palipokithiri harufu za Rushwa kwmy Cabinet na PM akiwa Joseph Sinde Warioba Mzee Ally Hassan Mwinyi alivunja tu Cabinet hakupoteza muda kubembeleza mtu kujiuzulu

the same to 1994 baada ya mchafuko wa G55 Mzee Mwinyi hakumbembeleza John Samwel Malecela Malecela kujiuzulu, alivunja tu Cabinet na kuunda upya

ila Jk kwa upole na upendo wake kwa Rafiki yake akamwita akamwambia naomba kapumzike ya 2015 niachie mimi
 
Back
Top Bottom