Unaposema nicotinic, una maana gani? Definition yake; nicotinic /nic·o·tin·ic/ (nik″o-tin´ik) denoting the effect of nicotine and other drugs in initially stimulating and subsequently, in high doses, inhibiting neural impulses at autonomic ganglia and the neuromuscular junction.
2- Tende husaidia kuuimarisha moyo. Iloweke tende kwenye maji kwa usiku mmoja na asubuhi kunywa maji hayo pamoja na tende zilizolewekwa baada ya kuondoa mbegu, ukifanya hivyo mara mbili kwa wiki, moyo wako utakuwa imara.
Mkuu hebu tufafanulie vizuri, moyo unaimarishwa ki namna gani? Ninachojua ni nkuwa moyo" huundwa" na misuli ya moyo, mishipa ya damu, neva za fahamu na kiwambo chembamba kikiufunika kwa nje. Sasa ni nini kilichopo katika tende kinachoimarisha moyo; ama nini kinaimarisha sehemu gani ya moyo.
3- Tende husaidia pia kwenye mambo ya malavi davi. Iloweke tende kwenye maziwa ya mbuzi usiku, asubuhi changanya maziwa hayo na asali kisha kunywa, njia hii husaidia kuongeza nguvu na stamina za kufanya mapenzi.
Hili nalo linaleta kizungumkuti. Kama tende pekee ingekuwa inasaidia kupata hizo nguvu na stamina kwanini isilowekwe kwenye maji peke yake au kumung'unywa halafu ikupe matokeo uliyoyasema? Kwanini tusifikiri kuwa hizo nguvu zinatokana na maziwa ya mbuzi ama asali?. Maana hata maziwa halisi ya ng'ombe tunajua yanampatia mtu nguvu.
Jambo linalozidisha vurugu kwa kichwa ni hilo la kuibandika asali halafu hutaki kuipa sifa yake bali umekimbilia kwenye tende. Tunajua na imethibitishwa kuwa asali ina-free glucose, hivyo unapoila jua unapata free glucose, ikimaanisha haihitaji digestion.(Kumbuka end products of digestion of carbohydrates ni glucose that has to absorbed and later be assimilated by the body)
4- Utafiti umeonyesha kuwa tende husaidia kutanua misuli ya mji wa mimba wakati mwanamke anapokaribia kujifungua, hii husaidia kumfanya mwanamke asipoteze damu nyingi wakati wa kujifungua.
Hapa tunadanganyana kweupe.
Ili mwanamke ajifungue anahitaji sana misuli ya mji wa mimba (uterine muscles) ibane ile mtoto aweze kutoka tena ikisaidiana na misuli ya tumbo, wewe unaleta habari ya ajabu sana.Basi kuna haja gani ya kuwapatia wakina mama pitocin, ikiwa tunahitaji misuli ya mji wa uzazi/mimba ilegee ndipo ajifungue? Kuna umuhimu gani wa kuwataka wakina mama wajawazito wafanye mazoezi? Nani analiyekwambia ili damu isitoke sana basi misuli na itanuke,isibane?
5- Wataalamu wa vyakula, wanazichukulia tende kama chakula bora kwa wanawake wanaonyonyesha kwani husaidia kuyapa maziwa virutubisho muhimu vinavyomfanya mtoto awe na afya njema.
Mwanzoni, umetueleza nini kimo/kipo ndani ya tende. Ili kiwe chakula cha kupewa hadi uliyoitaja hapo juu utusaidie kwa kutuonyesha food value, its contents, in percentage.
Kwa mtazamo wangu, sidhani kama tende yaweza fikia hata maharage, soya, ama mtama. Prove me wrong kwa kutupa taarifa sahihi.
6- Tende husaidia kupunguza kiwango cha kilevi (alcohol) kwenye damu. Maji ya kunywa ambayo tende imelowekwa ndani yake husaidia kuondoa haraka alcohol mwilini.
Mmmh!! Sijui tunaweza tukafika, ila tukiwa tumechoka saaana.
7 - Tende husaidia kuchelewesha dalili za uzee na pia husaidia kurekebisha ngozi na huondoa mabaka ya kuungua na jua.
Ni kilichopo ndani ya tende mpaka kikawa kina-retard ageing? Ni kipi kilichomo ndani ya tende kinachosaidia kuondosha mabaka yatokanayo na kuungua na jua?
8- Kutokana na madini ya chuma kwenye tende, watu wenye upungufu wa damu hupata ahueni.
Mkuu, mbona unachanganya madesa kihivyo, hapo awali umesema tende lina vitu vinne, na sasa
unachomekea cha tano kiaina. Tukueleweje?
9- Vitamin B1 na B2 vilivyopo kwenye tende husaidia kuyapa nguvu maini.
Hapa sihitaji uthibitisho kwa kumtafuta mwalimu wangu wa Biology aliyenifundisha" Food Substances" katika topic ya Nutrition (as one the characteristic features of living organisms) wakati niko form II, bali nitakwenda kwa mwalimu wangu wa Sayansi Kimu wakati niko darasa la tatu.
Hivi kweli vitamini ni chanzo cha nguvu ambayo pia inaitwa nishati? Vitamini B1 and B2,you are so lucky to honoured that you are also the source of energy to liver. Oh My God!!
Mzizimkavu, hebu tufafanulie hoja nilizoziweka katika mfumo wa maswali ili isioneka ulichokileta hapa ni upupu.