Utapeli Kariakoo: Kuna tofauti kubwa sana kati ya kusoma na kuwa na akili nyingi. Kuna watu waliishia darasa la saba (7) tu kwa sababu ya umasikini

Utapeli Kariakoo: Kuna tofauti kubwa sana kati ya kusoma na kuwa na akili nyingi. Kuna watu waliishia darasa la saba (7) tu kwa sababu ya umasikini

Trump sio "Policy Maker" yeye anatekeleza sera za nchi kama mwanasiasa na haundi sera.

Tena afadhali ungetolea mfano kwa nchi za Afrika na sio wanasiasa wa Ulaya. Hapa umekosea sana...


Donald Trump ingekuwa hachangii kuunda Sera hasingekuwa tofauti Na wenzake wakina jeb bush Na marepublicer wenzake, kiongozi yeyote anachangia sana kwenye msimamo wa serikali iliyopo madarakani, msimamo wa trump unachangia sana uelekeo wa marekani hata kama sio kati ya watu waliotunga Sera au ilani,

Msimamo wa magufuli sio sawa na kikwete hata kama ilani au Sera (policy) hakutunga yeye, kiongozi aliyeko madarakani ana ushawishi mkubwa sana wa kuielekeza nchi. Hata kuiba Na kupora. Ndio maana wengi wa wafanyabiashara matajiri wanakimbilia kwenye siasa Siku hizi ili mambo yao yaenda, Na huo ndio ukweli,
 
Sawa upo sahihi ni mwanasiasa tajiri.

Mwanasiasa ni mtekeleza sera na sio muunda sera (Policy Maker)...


Na sio lazima watekeleze kwa asilimia mia, matajiri wengi wanakimbilia siasa kwaajiri ya mambo yao yaende, kutekeleza Sera ni wajibu wakila kiongozi, kusukuma mambo yao ni agenda nyingine,

Utajiri Na siasa

Ujanja wa mtaani vs elimu ya darasani
 
Unatoa mifano mingi sana mbayo ipo nje kabisa ya mada mkuu. Yaaani hoja ya KUSOMA SANA vs UTAJIRI wewe umeigeuza kuwa SIASA vs UTAJIRI? Umenishangaza sana mkuu...


Hapana nimejibu hoja yako kwamba, kwanini waliosoma sana hawafanyi vizuri mtaani?!

Nikakujibu kuwa elimu ya darasani ni tofauti Na ujanja wa mtaani,

Nikakupa mfano wa matajiri wengi sio wasomi wakubwa kama maproffesors, Na maproffesors wengi sio matajiri wakubwa!

Ukasema maproffesors wengi ndio wako serikali wakiwapangia Sera matajiri,

Nikakujibu wako serikalini kwasababu wao ni wazuri kwakazi hizi za kuajiriwa, ujanja wao ni darasani ni wazuri kwa Kazi za collar job, sio wazuri kwa ujanja wa mtaani ili waweze kupata utajiri kama matajiri wengine, maana hakuna mtu anayetaka kuajiriwa tu maisha yake yote hasitake kuwa tajiri binafsi, ukasema matajiri wengi sio wanasiasa wazuri , nikakupa mfano wa Trump, Blomberg, shinawatra, belosconi, nk

Hapo ndio tulipofikia kwenye MATAJIRI VS SIASA
KUSOMA SANA VS UTAJIRI

Ni mwendelezo wa mada tu usiogope mkuu,,,
 
Mipango hupangwa na "Policy Makers" ambao wapo wizarani na Ikulu, hao jamaa sio wanasiasa hata kidogo. Wao ni wazalendo to the fullest...


Tunarudi kulekule mkuu,, kwamba waliopo Wizarani wanaweza kwenda kinyume Na wanasiasa ambao wanaiongoza serikali?!

Tunaongozwa Na ilani ya chama au watu wa Wizarani?!

Contradiction! Antagonistic!
 
Lakini utajiri wao unasimamiwa na wasomi wa kihivyo (Financial advisors). Si ndio?...


Sawa lakini kusimamia ni tofauti na kumiliki,,,

Kwani wao wasomi wanaosimamia huo utajiri, hawataki kuwa matajiri?!

Mbona hawana utajiri sasa?! Pamoja na usomi wao wote?!

Tunarudi kulekule elimu ya darasani ni tofauti na elimu ya mtaani (ujanja),
 
Siwezi ibiwa na mtu aliyefeli shule hata siku moja.

Kwanza sipendi vitu vya bei nafuu.
Mbili nipo huru na pesa yangu, na sina tamaa.

Tatu, ninachokitaka ndio huwa, sina tabia ya kumsikiliza MTU. Mimi ni dikteta. Hunipeleki peleki.

Kabla sijanunua kitu nimeshafanya research.

Nikitembea huwezi nikaribia na kunigusa, utajuta.

Kuibiwa ni dalili ya ujinga. Kabla uniambie kufanyiwa ujambazi.

Lakini wizi kama wizi sidhani.

Usipende bwerere
Ni kweli kabsa, halafu enzi hizo kuiba ilionekana kama sifa, mwizi anamwambia nimeichomoa kwa muhindi nawe unakubali kununua mali ya wizi kisa ni bei chee.
 
Sawa lakini kusimamia ni tofauti na kumiliki,,,

Kwani wao wasomi wanaosimamia huo utajiri, hawataki kuwa matajiri?!

Mbona hawana utajiri sasa?! Pamoja na usomi wao wote?!
Utajiri wanao ndani ya vichwa vyao mkuu...
 
Tunarudi kulekule mkuu,, kwamba waliopo Wizarani wanaweza kwenda kinyume Na wanasiasa ambao wanaiongoza serikali?!

Tunaongozwa Na ilani ya chama au watu wa Wizarani?!

Contradiction! Antagonistic!
Wanasiasa wanaandaa Ilani ya chama baada ya kupata muongozo kutoka kwa wataalam wa nyanja husika kama afya, uchumi, foreign policy, elimu, etc
 
Na sio lazima watekeleze kwa asilimia mia, matajiri wengi wanakimbilia siasa kwaajiri ya mambo yao yaende, kutekeleza Sera ni wajibu wakila kiongozi, kusukuma mambo yao ni agenda nyingine,
Hii sina uhakika nayo kwa maana moyo wa mtu ni kichaka kinene...
 
Donald Trump ingekuwa hachangii kuunda Sera hasingekuwa tofauti Na wenzake wakina jeb bush Na marepublicer wenzake, kiongozi yeyote anachangia sana kwenye msimamo wa serikali iliyopo madarakani, msimamo wa trump unachangia sana uelekeo wa marekani hata kama sio kati ya watu waliotunga Sera au ilani,
Trump hana msimamo, bali ule ni msimamo wa nchi. Kumbuka Rais ni taasisi na sio mtu mmoja kama Trump...
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa JamiiForums.

Ndugu zangu Watanzania;

Kuna tofauti kubwa sana kati ya kusoma na kuwa na akili nyingi. Kuna watu waliishia darasa la (7) tu kwa sababu ya umasikini wa nyumbani kwao wakashindwa kuendelea na masomo.

Kuna watu hawajasoma sana (unakuta mtu ameishia darasa la saba tu mwaka 1991) ila wana akili sana hata ukikutana nao mtaani katika maisha ya kila siku, na kwa namna wanavyopangilia kazi zao au hata ratiba zao za kila siku, unajua kabisa huyu mwamba aliishia darasa la 7 kwa sababu ya umasikini tu na kama angesoma sana angekuwa mtu mmoja hatari kweli kweli.

Wewe jenga picha wale wezi wa pale kariakoo wanakuibia mfukoni bila hata wewe kujua kama kuna mkono umeingia ndani ya mfuko wako wa suruali na kuchukua pesa yako ya dagaa. Zile ni akili nyingi sana sema tu zimeelekezwa pahala pasipo stahili.

KISA KIDOGO CHA MIMI KUUZIWA KIPANDE CHA SABUNI KWA 20,000/= NIKIDHANIA NI SIMU
===========
Nikiwa kidato cha 6 miaka hiyo ya 2000 na kitu, niliahi kuuziwa kipande kidogo cha sabuni nikidhani kuwa ni simu. Nilikuwa ninatoka Tabata Segerea nyumbani mama yangu mkubwa nilienda kumtembelea siku ya ijumaa jioni sasa nikawa ninarudi jumapili mchana ili nifanye maandalizi ya usafi wa nguo kwa ajili ya shule kesho yake ambayo ni Jumatatu.

Baada ya kushuka kutoka katika daladala pale mtaa wa Kongo akatokea jamaa mmoja rika langu akiwa ameshika simu aina ya nokia zile za jeneza za zamani akawa ananioneshea kwa ukaribu basi mimi nikaichukua ile simu nikaikagua vema kisha nikamuuliza bei gani, yeye akasema ni 20,000/=. Nikasema kimoyomoyo poa ngoja nichukue hii ngoma ili na mimi nikatambe huko mitaani.

Alafu hiyo pesa yenyewe sasa ndio nilikuwa nimepewa kama pocket money ya mwezi mzima na huyo mama yangu mkubwa. Yule jamaa rika langu kabisa akaniambia mwamba njoo huko hapo barabarani sana, basi mimi nikaenda, akanipa tena simu nikaikagua kwa mara ya pili, simu ipo sawa haina tatizo.

Sawa. Basi mwamba akaichukua simu akaiweka katika bahati fulani hivi ya kaki kisha na mimi nikampa pesa yake 20,000/= huyo nikaondoka. Kabla sijaenda mbali, baada ya kupanda daladala za kwenda home kwetu kurasini, nikaona ngoja nifungue bahasha nitoe simu yangu walau nicheze hata game la nyoka niji-keep busy, halooooo!

Nilikutana na kipande cha sabuni ya kodrai hahahahahaaaaa size ile ile kama simu ya Nokia ya jeneza (3310) kikiwa kinaniangalia tu. Kwa kweli roho iliniuma sana.

Ukizingatia 20,000/= ni pesa nyingi sana kwa miaka ile alafu mimi bado mwanafunzi sina majukumu mengi. Basi sikuwa na jinsi zaidi ya kuvumilia hasira nilizokuwa nazo na nilipofika home nikafua nguo zangu kwa kutumia sabuni ya kipande ya 20,000/= hahahahaaaaa.
===========

Kuna watu wenye akili nyingi lakini hawajasoma sana hususan huko vijijini. Unakuta mwanakijiji yeye hawajawahi kuwa na njaa bomani kwake. Miaka yote anavuna mahindi mengi, anafuga ng'ombe wake vizuri na anasomesha watoto kwa kuuza maziwa tu mpaka watoto wanamaliza form six. Siku akiamua kukuandikia barua, huo muandiko wake utadhani labda ni mwalimu wa secondary.

Kuna watu hawajasoma sana ila wana akili nyingi kweli. Je, ulishawahi kukutana nao (mbali na wizi) katika maisha yako?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Lissu alikuwa anawatetea Mabeberu bungeni waendelee kuchimba madini yetu huku Rais Magufuli akitutetea sisi wanyonge.
 
Back
Top Bottom