Utapeli wa “Chumvi na Mafuta ya Upako” Wafichuliwa

Utapeli wa “Chumvi na Mafuta ya Upako” Wafichuliwa

Ushauri wako ni upi maana utapeli umeenea hata kwa makanisa yasiyouza hivyo vitu sadaka zimekuwa nyingi mno mtu unakamuliwa mpaka Senti ya mwisho uliyo nayo je tukasali wapi sasa maana tunampenda Mungu
Swali zuri.
Ni kweli utapeli umeenea, lakini Mungu hajawahi kukosa Watumishi wake waaminifu. Kama umehakikisha kabisa pasina shaka kwamba hapo unaposali kuna ujanja ujanja, ni heri utafute kanisa jingine linalohubiri Injili kamili ya Kristo bila kulazimisha watu kwa hila. Soma Biblia, muombe Mungu akupe hekima, na umshirikishe Roho Mtakatifu akuelekeze mahali sahihi pa kuabudu.

Sadaka inayompendeza Mungu ni sadaka inayotolewa kwa hiari si kwa kulazimishwa.
2 Wakorintho 9:7
"Kila mtu na atoe kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.
 
Mkuu, Pascal Mayalla , wewe ni Great Thinker na Biblia unaijua. Kwakuwa Biblia ndio mwongozo wa maisha ya Wakristu(Zaburi 119:105; 2 Timotheo 3:16-17), naomba unitajie mistari ya Biblia inayoagiza hayo uliyoyasema yafanyike. In other words, wanaofanya hayo, wanafanya kwa kuegemea Maandiko yapi ya Biblia.

Nimekuuliza hivyo kwa sababu Yesu alisema tukiwa na chembe ndogo tu ya imani tunaweza kuuambia mkuyu huu ng'oka ukaote baharini(Luka 17:6). So, kwanini tuhangaike tena kutafuta majivu na kuharibu mazingira?

Vile vile Biblia inasema imani huja kwa kusikia ujumbe unaotokana na Neno la Kristo(Rum 10:17), sio kwa kutumia natural elements.
Mkuu Seti, Setfree , japo mimi nimefika St. Peter Basilica, na The Holly Bible, nimeisoma yote, mimi sio mtu wa vifungu kihivyo!, ndio maana nilitoa angalizo hili, Angalizo: Kuna Wengi Wanamwabudu Shetani Wakidhani ni Mungu!. Jee Wewe Unajijua?, Jitambue!.
P
 
Washenzii wajipatia fursa ni kuzoa mijihela kwa wauumini, wanakondoo wa Bwana.

Wanafaata nyayo za nabii Tb Joshua.
 
Swali zuri.
Ni kweli utapeli umeenea, lakini Mungu hajawahi kukosa Watumishi wake waaminifu. Kama umehakikisha kabisa pasina shaka kwamba hapo unaposali kuna ujanja ujanja, ni heri utafute kanisa jingine linalohubiri Injili kamili ya Kristo bila kulazimisha watu kwa hila. Soma Biblia, muombe Mungu akupe hekima, na umshirikishe Roho Mtakatifu akuelekeze mahali sahihi pa kuabudu.

Sadaka inayompendeza Mungu ni sadaka inayotolewa kwa hiari si kwa kulazimishwa.
2 Wakorintho 9:7
"Kila mtu na atoe kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.
Asante sana na Mungu akubariki kwa somo zuri ila hii vita na hawa manabii feki na matapeli wengine wa kiroho ni ngumu maana watu wengi wanazidi kuwaamini na kuwafuata
 
Washenzii wajipatia fursa ni kuzoa mijihela kwa wauumini, wanakondoo wa Bwana.

Wanafaata nyayo za nabii Tb Joshua.
Tusaidiane kupiga kelele watu wajihadhari
 
Back
Top Bottom