Utaratibu wa kuishi na ndugu baada ya ndoa unafaa uwe vipi?

Utaratibu wa kuishi na ndugu baada ya ndoa unafaa uwe vipi?

Tatizo kubwa ni mkeo ,yeye ndo anatakiwa akae nao chini awaelimishe hawawezi kuja kwako kama hajawakari isha ,sikuingine acha kuoa wadada wa tandika kwa mtogole
 
.........Ugumu wa maisha unasababisha watu wafanye vitu vya aibu sana.
 
Duniani huwezi ukamfurahisha kila mtu mtu anakuja kukaa tu nyumbani hana kazi anatafta nini?sijawahi fuga mtu kwangu et aamke anakula na kuangalia tv kwangu ni big no?mtu wa hivyo humsaidii bali unamlemaza
 
Duniani huwezi ukamfurahisha kila mtu mtu anakuja kukaa tu nyumbani hana kazi anatafta nini?sijawahi fuga mtu kwangu et aamke anakula na kuangalia tv kwangu ni big no?mtu wa hivyo humsaidii bali unamlemaza
Watu wataprefer bure kuliko kazi ,mm hutoa mtaji sio matumizi ,mtaji ni one time hatujuani ,matumizi ni maisha ,mungu ndo atakupa matumizi au wewe mwenyewe ,wengine ni tukijaaliwa ni mtaji tuu
 
Zaburi 133:1-3 BHN

Ni jambo zuri na la kupendeza sana ndugu kuishi pamoja kwa umoja.

1 Timotheo 5:10 BHN

na awe mwenye sifa nzuri: Aliyewalea watoto wake vizuri, aliyewakaribisha wageni nyumbani kwake.....

1 Petro 4:9 BHND

Muwe na ukarimu nyinyi kwa nyinyi bila kunung'unika.


1 Timotheo 5:13 SRUV

Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizungukazunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa.


1 Wathesalonike 4:11-12 BHN

Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali. Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
 
Habari za siku nyingi watu wa Mungu.

Hivi ni utaratibu gani unafaa kufuatwa katika kuchagua ndugu wa kuishi nao baada ya ndoa. Nakumbuka mwanzo kabisa kipindi namuoa mke wangu nilimjulisha kuwa napenda sana ndugu ila kuishi na ndugu ni mtihani kama mtu ana uhitaji na tuna uwezo wa kumsaidia bora tumsaidie huko huko aliko kukiwa na ulazima sana ndipo ataishi kwetu.

Bahati mbaya huyu mwenzangu na ndugu zake wamefanya nyumba yangu kijiwe ndugu zake wote wapo hapa hapa mjini sasa imekuwa anakuja huyu anakaa wiki anaondoka wanapokezana , likizo watoto zao wanawaleta kwangu na wana vurugu kweli ile likizo ya mwaka mpya walinivunjia side mirror ya gari ikabidi niwafukuze manake walikuwa wakiaanza kukimbizana wanapita mpaka juu ya makochi ilibaki kidogo wakanyage kompyuta niliwafukuza siku hiyo hiyo.

Tatizo la pili kuna ndugu zake hawa watu wazima wakike ambao ni dadazake ni wakubwa kiasi mmoja binti yake ndiyo mwenye watoto niliowafukuza, hawa wanakaa tu nyumbani hawafanyi chochote ni kuangalia tu tamthiliya mpaka kurudi nyumbani sasa naona kero mimi na wife hatujajaliwa watoto sasa hapo nyumbani kuna familia ya watu 4 na wote wanatokea hapo mabibo yaani mimi ndio nimekuwa kama mgeni kwenye familia.

Nikimuambia hawa watu kwanini wasirudi kwenu kwenye nyumba ya familia wakae sisi tutakaa nao mpaka lini anasema soon wataondoka toka mwezi wa pili anasema hivyo soon wataondoka, karibuni mama anataka kuja kwenye matibabu MOI ila kagoma kufikia kwangu hawezi lala kitanda kimoja na mtu mwingine anashida na mifupa.

hapo bado kuna ndugu zake wanakuja tu wikend wakijisikia na wakiondoka hawana nauli wanakuomba tena shemeji nauli hasa namuuliza hawa nao wanakuja kila wikend kufanya nini, anasema kama sitaki ndugu zake waje atawaambia ila tatizo sio kuja tatizo hata nauli hawana ukiwapa ndogo wanakuimbia kuna sehemu ya kupanda bodaboda.

Ajabu wao wenyewe kwa wenyewe hawatembeleani ni kama vile wanaamua kunimalizia pesa hivi. Nipeni busara kudeal na hawa watu nahisi kuanza kukata mahitaji.
Kaa nao waambie kesho ondokeni tunaishi kwa bajeti hapa mjini period.
 
Hakuna formula !
muhimu upendo wa Mungu utawale na husuda zisiwepo hata tone moja hapo itakuwa Baraka na kustawi kwingi na neema.
 
Tatizo unaweza ukawependa lakini wakaishia kutafuta kukuangamiza Na kukuharibia !

Lakini Imeandikwa; “Tusichoke katika kutenda mema maana tutavuna kwa wakati wake tusipozimia mioyo”
 
Mkuu kosa la kiufundi unaonekana unakaa nyumba kubwa ila upo ww na Mkeo tu, kuwa na hesabu za kifedha kidogo kutatua hilo tatizo.
Pangisha hiyo nyumba kisha nenda kapange chumba kimoja hizo kenge haziwezi kujileta maana watakuwa hawana pa kulala. Kwahy utakuwa umetatua tatizo huku unakunja noti kiulaini kabisa

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom