Utaratibu wa kushusha daraja timu zilizofirisika haupo Africa ?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Tumeona timu za Ulaya zikishushwa madaraja kwa kufirisika na hasa timu inaposhindwa kulipa mshahara wachezaji wake , Portsmouth ya England na Parma ya italia ni mifano halisi .

Kwanini Yanga Pamoja na ukweli kwamba imefirisika hadi kushindwa kulipa mshahara wa wachezaji wake , huku wengine wakivunja mikataba ( jambo la aibu ambalo hatukuwahi kuliona ) bado inaachwa kushiriki ligi kuu ?
 
Ni wewe kweli au account yako imekuwa hacked?
Mpira ni uwanjani Kiongozi. Haijalishi kama ni hela za kuchangishana na za mwanaume mmoja. Kikubwa point mwisho wa msimu.
 
Kama Tanzania Football Fitna (TFF) wangekuwa wanafuata sheria za mpira badala ya kufuata njaa zao, leo hii Yanga wasingekuwa ligi kuu....wangeishashushwa daraja zamani sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wewe kweli au account yako imekuwa hacked?
Mpira ni uwanjani Kiongozi. Haijalishi kama ni hela za kuchangishana na za mwanaume mmoja. Kikubwa point mwisho wa msimu.
kule ulaya zilizoshushwa bado zilikuwa uwanjani mkuu
 
Hili suala naona linazungumziwa kiutani lakini kwa taratibu za FIFA zilivyo iwapo uongozi wa Yanga hautachukulia suala la kuvunja mikataba na wachezaji/makocha wake kwa makubaliano ya maridhiano ya pande mbili na wachezaji hao wakaenda kushtaki TFF and then madai yakafika FIFA na ikaonekana madai yao ni ya kweli na Yanga haina uwezo wa kuwalipa basi usishangae kuikuta Yanga mwakani inapambana na Mawenzi market, Ihefu, Green warriors n.k.

Kimsingi uongozi wa Dk. Msola unapaswa kutumia busara na maridhiano na wachezaji/makocha wanaovunja mikataba yao na si watumie mihemuko ili kila mtu aende zake kwa amani ya bwana akiwa ameridhika. Ni busara zaidi kwa uongozi kufanya makubaliano na wachezaji/makocha wanaowaacha kuwa siri badala ya kuwatuma wasemaji wa klabu kwenye vyombo vya habari kubwabwaja kuwa mchezaji fulani hana kiwango tumeamua kumuacha. Kwa mchezaji/kocha ambaye anaona kabisa hali ya kiuchumi ya klabu sio nzuri akielezwa vizuri na makubaliano yakawa siri ni rahisi sana kuvunja mkataba na akasamehe baadhi ya madai yake.

Kuvunja mikataba na wachezaji/makocha ni jambo la kawaida duniani kote na Yanga si wa kwanza wala hatakuwa wa mwisho. Kimsingi wawatumie wanasheria ambao ni mashabiki wa Yanga ambao wapo wengi tu nchini ili wawasaidie katika hili tena bila hata malipo ili klabu isiingie katika migogoro isiyo na tija na kuiingiza taasisi kubwa kama hii kwenye matatizo ambayo yanaweza kuzuilika.
 
Nimekubali mkuu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mifano miwili ya timu zilizoshushwa kwa njia hiyo?
Vinginevyo ni hadithi kama hadithi nyingine tu.
 
angalia hii
 

Attachments

  • VID-20191212-WA0009.mp4
    1.8 MB
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…