Utaratibu wa kutoa hela za matumizi kwa familia zetu kila siku, unafilisi

Utaratibu wa kutoa hela za matumizi kwa familia zetu kila siku, unafilisi

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Hasa sisi tunaoishi mijini, kumekuwa na changamoto katika utunzaji wa familia zetu. Kwa walio wengi, hupenda kila siku kuacha hela za matumizi kwa familia zao; wapo wanaoacha elfu kumi kwa siku, ishirini, laki n.k

Na waachapo hiyo fedha, ndio inayofanya manunuzi ya chakula kwa siku husika. Ndio maana wengine wakaamua kuibatiza na kuiita kodi ya meza, au wengine wanaiita kodi ya kitanda n.k

Kwangu binafsi nilishawahi kutumia hiyo fomula, lakini nikaona nakuwa mtumwa wa kila siku. Usipokuwa na fedha kwa siku husika au pungufu, mambo yanakuwa hayaeleweki eleweki.

Baada ya kujitafakari kwa kina, nikagundua hii njia sio sahihi kwa sababu unakuwa unahangaikia tumbo tu, na mambo ya msingi ya kimaendeleo yanakuwa hayaendi.

Kwa mtazamo wangu, pale upatapo hela, weka 'stock' ya chakula hata miezi sita kutokana na uwezo wako. Fedha ndogo ndogo za kubadilishia mboga kwa siku, mkabizi mke au mtu anayesimamia mambo ya ulaji wa familia.

Hata kama kipato chako ni kidogo, jaribu kujikusanya na uweke 'stock'. Baada ya hapo, hela utakayokuwa unaipata kutokana na jitihada zako, wekeza kwenye mambo yako ya msingi ya kimaendeleo.

Hii itapunguza msongo wa mawazo, hasa pale uchumi wako utakapokuwa unatetereka; kwa sababu familia yako haitalala njaa, lakini pia mambo yako ya msingi yanakuwa yamepiga hatua.

Kwa hali hiyo, huu utaratibu wa kutoa hela ya matumizi kwa kila siku husika, naona sio mzuri.

Njooni kwenye mjadala....
 
Kodi ya meza ipo siku itakumeza .
Yote kwa yote kipato kikiwa kuzuri hatuwezi kulalamika wala kuulizia chenji.
Binafsi nina mwaka wa 6 kwenye ndoa na utaratibu wangu ni kumpa pesa wife karibu zote ninazozipata. Kisha namwambia hii ya akiba, hii ina kazi fulani na hii tumia kwa matumizi ya nyumbani kadri utakavyo.
Usiache hela kila asubuhi you will die immediately , nadhani kuacha PESA kila asubuhi ndio chanzo cha migogoro mingi katika ndoa maana siku ukifulia si rahisi kueleweka. Pia pesa akitunza mwanamke inakuwa ina baraka na atapanga bajeti za nyumbani vizuri.
Kuhusu kuweka akiba ya chakula karibu kila mwanaume anatamani kufanya hivyo tatizo ni kipato.
 
Kodi ya meza ipo siku itakumeza .
Yote kwa yote kipato kikiwa kuzuri hatuwezi kulalamika wala kuulizia chenji.
Binafsi nina mwaka wa 6 kwenye ndoa na utaratibu wangu ni kumpa pesa wife karibu zote ninazopata. Kisha namwambia hii ya akiba, hii Ina kazi fulani na hii tumia kwa matumizi ya nyumbani kadri utakavyo.
Usiache hela kila asubuhi , nadhani kuacha PESA kila asubuhi ndio chanzo cha migogoro mingi katika ndoa.
Kuhusu kuweka akiba ya chakula karibu kila mwanaume anatamani kufanya hivyo tatizo ni kipato.
Ni kweli mkuu, ila kufanikisha hili itategemea pia na mtu uliyenaye. Kwa sababu katika mchakato wa kuweka akiba itakulazimu matumizi mengine kuyapunguza
 
Hii kitu ya kuacha kila siku inatesa sana ilinisumbua wakati fluni, nilichofanya kwanza nilimwambia wife naomba ahudumie issue ya chakula kila siku, kudumiaha nyumba kulipa mtoto wa kazi, nguo za watoto, mimi nipambane na mambo kama ada za watoto, umeme, mafuta ya gari, ujenzi na gasi.

Ingawa wakati mwingine huwa nanunua samaki, nyama nk kumpunguzia headach maana wakaati mwingine unaona wamefululiza aina fluni ya mboga hasa maharage
 
Huu ni utaratibu tuliourithi kutoka kwenye familia zetu za vipato vya kati, hata ukinunua stock ya mahitaji kama mchele,mafuta,unga na mazagazaga mengine still bado utaacha Kodi ya meza kwa matumizi kama ya aina flani za mboga ambazo hamkuziweka kwenye bajeti n.k

Lakini pia hii inategemea na kipato chenu

Sent from my Infinix X653C using JamiiForums mobile app
 
Kila siku huwa unaacha mkuu?
Nilivyo bahili mimi, naacha buku tu ya mboga za majani. Kama ni samaki, kuku, nyama nk viko kwenye jokofu.

Mafuta nina galon ya 20ltrs kutoka Singida, unga upo kiroba, mchele kilo 30, na umeme unit kama zote.

Wote wana bima za afya. Gari yangu yenyewe naitumia mara moja tu kwa wiki kubana matumizi ya mafuta, matairi, kuokoa km 3000 za service nk.

Mbaya zaidi sitajiriki, kwanini? Au nimekufa hamtaki kuniambia?
 
Kodi ya meza ipo siku itakumeza .
Yote kwa yote kipato kikiwa kuzuri hatuwezi kulalamika wala kuulizia chenji.
Binafsi nina mwaka wa 6 kwenye ndoa na utaratibu wangu ni kumpa pesa wife karibu zote ninazozipata. Kisha namwambia hii ya akiba, hii ina kazi fulani na hii tumia kwa matumizi ya nyumbani kadri utakavyo.
Usiache hela kila asubuhi you will die immediately , nadhani kuacha PESA kila asubuhi ndio chanzo cha migogoro mingi katika ndoa maana siku ukifulia si rahisi kueleweka. Pia pesa akitunza mwanamke inakuwa ina baraka na atapanga bajeti za nyumbani vizuri.
Kuhusu kuweka akiba ya chakula karibu kila mwanaume anatamani kufanya hivyo tatizo ni kipato.
Wewe umebahatika mke Mwenye akili. uliza wenzio kama hujakuta kanunua vijora yotee.
 
Nilivyo bahili mimi, naacha buku tu ya mboga za majani. Kama ni samaki, kuku, nyama nk viko kwenye jokofu.

Mafuta nina galon ya 20ltrs kutoka Singida, unga upo kiroba, mchele kilo 30, na umeme unit kama zote.

Wote wana bima za afya. Gari yangu yenyewe naitumia mara moja tu kwa wiki kubana matumizi ya mafuta, matairi, kuokoa km 3000 za service nk.

Mbaya zaidi sitajiriki, kwanini? Au nimekufa hamtaki kuniambia?
😂😂
 
Nilivyo bahili mimi, naacha buku tu ya mboga za majani. Kama ni samaki, kuku, nyama nk viko kwenye jokofu.

Mafuta nina galon ya 20ltrs kutoka Singida, unga upo kiroba, mchele kilo 30, na umeme unit kama zote.

Wote wana bima za afya. Gari yangu yenyewe naitumia mara moja tu kwa wiki kubana matumizi ya mafuta, matairi, kuokoa km 3000 za service nk.

Mbaya zaidi sitajiriki, kwanini? Au nimekufa hamtaki kuniambia?
Umenichekesha sana eti ajabu sitajiriki au nmekufa
 
Me nampa hela ya matumizi ya mwezi mzima 400k. Huwa tunalima pia tunao mpunga wa tangu mwaka juzi na mwaka jana hivyo stoo iko vizuri. Mke ni mtumishi pia ila kipato chake anajua mwenyewe anafanyia nini huwa siulizii, nalipa ada za watoto lakini kwenye kujenga ni kama 50/50 kila mmoja alichangia na tupo kwenye nyumba yetu.
 
Nilivyo bahili mimi, naacha buku tu ya mboga za majani. Kama ni samaki, kuku, nyama nk viko kwenye jokofu.

Mafuta nina galon ya 20ltrs kutoka Singida, unga upo kiroba, mchele kilo 30, na umeme unit kama zote.

Wote wana bima za afya. Gari yangu yenyewe naitumia mara moja tu kwa wiki kubana matumizi ya mafuta, matairi, kuokoa km 3000 za service nk.

Mbaya zaidi sitajiriki, kwanini? Au nimekufa hamtaki kuniambia?

Hahaha!!
 
Hii kitu ya kuacha kila siku inatesa sana ilinisumbua wakati fluni, nilichofanya kwanza nilimwambia wife naomba ahudumie issue ya chakula kila siku, kudumiaha nyumba kulipa mtoto wa kazi, nguo za watoto, mimi nipambane na mambo kama ada za watoto, umeme, mafuta ya gari, ujenzi na gasi.

Ingawa wakati mwingine huwa nanunua samaki, nyama nk kumpunguzia headach maana wakaati mwingine unaona wamefululiza aina fluni ya mboga hasa maharage
Wiki nzima ni haragwe kwa kwenda mbele!!!
 
Back
Top Bottom