Utaratibu wa kutoa talaka upoje?

Utaratibu wa kutoa talaka upoje?

Kiislam .
Andika barua kwa mkono wako.

Mimi fulani bin fulani , nikiwa na akili zangu timamu , na bila ya kushurutishwa wala kushawishiwa na mtu yoyote , nimeamua kukutaliki fulani binti fulani , hivyo kuanzia leo hii tareh...... wewe sio mke wangu wa ndoa.
Nakutakia maisha mema.

Jina na saini yako.

Mashahidi wawili ,
Majina yao na saini zao.

Halafu piga photocopy , original mmkabidhi yeye, copy moja mkabidhi babamkwe au walii wake ( sio lazima lakini ), copy moja ibaki kwako.
Kazi imekwisha.

Kama anaishi nyumbani kwako , akae hapo mpaka kipindi cha eda ya talaka iishe ndio anaondoka.
Ukimuingilia kwa tendo la ndoa kabla kipindi cha eda kuisha , talaka inakufa , ila itahesabika talaka moja tayari.
 
Habari hizo ni nadra sana kuzisikia na ni matokeo ya wanaume wasio na akili kuoa
Mwanaume asiye na akili hatakiwi kuoa.
Kuoa kunahitaji mwanaume mwenye akili sio jinga jinga.Hayo majinga jinga ndio huua
Au sio unataka wafikie huku
Screenshot_20221218-073737.jpg
Screenshot_20221218-073708.jpg


Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Katika Uislamu kuna talaka za aina nyingi! Kwa maelezo yako unataka uachane na huyo mwanamke

Unaweza kumtamkia maneno tu yakatosha kuwa talaka na kuanzia hapo hutakiwi kumgusa maana kufanya nae tendo unaitengua ile talaka kabla ya kipindi cha eda kuisha.

Au unaweza kumpa talaka kwa maandishi ya kumuandikia hapo tayari hyo talaka ni halali katika dini.

Baada ya kipindi cha Eda kumalizika pasi kumgusa , huyu mwanamke anakuwa sio halali yako tena na kama ukihtaji kurudiana nae mnatakiwa muaze process za barua , mahari mpk ndoa tena.

kama mna mali basi utafungua shauri bakwata kwa ajili ya mgawanyo wa mali lakini kama kapuku mpe karatasi yake ya talaka beba suruali zako anza maisha upya hiyo ni talaka tayari kwa Mujibu wa dini.
Kwenye hii sekta ya ndoa mko vizuri sana kuliko sisi Wagalatia. Na kwenye mazishi. Mambo simple kabisa. I admire you guys!
 
Mimi ndo mwenye shida katika ndoa, sitaki kumtesa mtoto wa watu
Kama shida ni wewe je yuko tayari kukuvumilia ? Kama yuko tayari kuvumilia shida zako , usimtaliki maana hapo utakuwa umemuonea sana, ila kama yuko tayari kuachwa basi sawa.
 
Kama ni muislam nenda bakwata wilaya. Kama ni mkristo nenda kanisani au ofisi ya kata kwanza.

Kama hamna mali huna haja ya talaka we beba suruali zako jiondokee.

Kwa wakristo talaka ni kwa matajiri ili wagawane mali kisheria sasa weww kapuku talaka ya nini.

Nb talaka huandiki wewe inaandikwa na hakimu based on your grounds za kuachana
Umempa ushauri wa pumba wewe na watu bado wanakupa (like) ama kweli kwnye miti hakuna wajenzi. umeanza vizuri umekuja kumaliza maneno ya pumba lohh majangaa kweli.
 
Tatizo lako umeshindwa kuelewa hiyo sheria inasimamia ndoa za kiserekali zinazo fungwa bomani.

Nifunge ndoa ya kidini, au kimila, hata bila kuarifu derikali leo, tunataka kuachana idhini mpaka waitoa wao. ndoa za kidini na kimila taratibu za kuacha zipo ndani ya dini na mila husika. Ndiyo maana hakuna alieshitskiwa kuachana na mkewe bila kupitia mahakamani.
Nafikiri umeongea kama mwana dini uliyelishwa daawa madrasa na hajaongea kama mtu aliyesoma Sheria ya ndoa ya Tanzania ambayo imejumuishwa na kufanya mjumuisho wa Sheria za kimila katika ndoa, dini zote na wale wasiofuata misingi yoyote katika hayo.

Kwa Taarifa yako, ndoa zote zinazofungwa ziwe za kiserikali, za dini zote nk ni ndoa za kiserikali na sio Kila kiongozi wa dini anaruhusiwa kufungisha ndoa nazima wawe na kibali na kusajiliwa serikalini. Hivyo Kuna watu wanafungishwa ndoa na watu wasio na kibali, zinakuwa batili mwanzo mwisho.
Hivyo, ndoa nyingi zinavunjika kienyeji kwa hivyo mnavyoviita talaka 3 , na watu kwa ujinga wao wa kutokujia Sheria wanaishiwa kugandamizwa kwa woga wa dini. Ila akienda mahakamani ile ndoa inakuwa bado hai na Mahakama ndio Ina mamlaka ya kuvunja au kuto kuvunja na kugawa upya Mali bila ubaguzi na kutoa amri ya matunzo ya watoto kwa mujibu wa Sheria.Mifano ni mingi ya kesi za namna hiyo na haki zimetolewa.
 
Umempa ushauri wa pumba wewe na watu bado wanakupa (like) ama kweli kwnye miti hakuna wajenzi. umeanza vizuri umekuja kumaliza maneno ya pumba lohh majangaa kweli.
Pumba iko wapi hapo.
Niko sahihi talaka hawndiki yeye
Naongea kama mwanasheria sio mganga wa kienyeji
 
Kama ni muislam nenda bakwata wilaya. Kama ni mkristo nenda kanisani au ofisi ya kata kwanza.

Kama hamna mali huna haja ya talaka we beba suruali zako jiondokee.

Kwa wakristo talaka ni kwa matajiri ili wagawane mali kisheria sasa weww kapuku talaka ya nini.

Nb talaka huandiki wewe inaandikwa na hakimu based on your grounds za kuachana
hapana mkuu
ndoa za kiislamu siyo lazima BAKWATA wilaya hata ukitamka tu kwamba kuanzia leo wewe siyo mke wangu ni talaka tayar,
ukiandika zinaanzia moja mpaka 3 ila ukimpa tatu hutamrejea kirahisi
Note: ndoa zinachangamoto ila talaka siyo jambo zuri kaeni muyazungumze mkiwashirikisha wakubwa
 
Waislamu mahari huwa ndogo na ndoa hudumu muda kidogo

Mwanaume au mwanamke wa kiislamu kuomba talaka ni kitu kidogo tu

Ndoa za Kikiristo hata kuwe na changamoto wanandoa wanatakiwa kuishi hadi kifo kiwatenganishe

Wanaume wa kiislamu pamoja na kuruhusiwa kuoa wake hadi wanne kutwa husingizia changamoto na kuoa wengine.

Mtu unaruhusiwa kuoa wake wanne huyo mmoja akikupa changamoto huwezu vumilia kidume wewe?

Akili huna za kuishi na mke kwa mujibu wa Biblia

Biblia inatamka wazi kuwa wanaume wanatakiwa kuishi na wanawake kwa akili..Na unapooa huwa unaulizwa kama una akili timamù.Lengo la swali ni kujua kama una akili za kuishi na mke. Ukiona mwanaume anampa talaka mkewe au anasema mke kanishinda ujue huyo mwanaume akili timamu hana za kuishi na mwanamke.Kifupi huyo mwanaume alitakiwa kuwa padri wa kanisa katoliki ambao hawao hawaoi.

Huyo mwanamke anayetaka kupewa talaka anatakiwa kumburuza mahakamani huyo mwaname huyu.mleta mada kwa kumtapeli na kumtaka amlipe fidia kubwa sana akielezea kuwa wakati anamuoa alijifanya kuwa ana akili timamu wakati kwenye ndoa kaonyesha wazi mambo mengi nyumbani na kwenye ndoa anaonyesha wazi akili hana.Na atoe ushahidi mfano hatunzi familia nk nk
siyo vizuri kuongea mambo usiyoyajua wala kuwa na ushahidi nayo. Hapa uliandika kwa hisia tu na wala huna ukweli wowote
 
[emoji777] Kwa Sheria ya ndoa ya Tanzania , hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuandika Wala kutoa talaka tofauti na Mahakama baada ya kupitia taratibu zote na kubaini kuwa ndoa imevunjika vipande vipanda Haina spea na Wala haitawezekana tena kwa wanandoa hao kuishi pamoja.

[emoji736] Utaratibu, unasnzia kwa Baraza la usuluishi la Kata, pale ambapo mmoja wa wandoa ataoeleka malalamiko, basi Baraza litawaita na kuwasikiliza kwa lengo sii la kuvunja ndoa Bali kuwasuluisha maana kwa mujibu wa kifungu Cha 9 Cha Sheria ya ndoa na kesi ya Hyde vs Hyde lengo la ndoa ni wanandoa waishi pamoja hadi kifo kiwatenganishe. Baraza likishindwa kusuluisha litaandika certificate kwa mahakama kuwa usuluishi umeshindikana. Hivyo hakuna kesi yoyote ya maombi ya talaka yatapikelewa mahakamani kabla ya kupitia kwenye Baraza la usuluishi linambulika kisheria. Mtu mwenye dini Fulani ambapo ndoa imefungwa kwa misingi hiyo na wanayo mabaraza ya usuluishi, mabaraza hayo yanaweza kutbulika kama mbadala wa mabaraza ya Kata.

[emoji736] Kesi ikifika mahakamani, baada ya kuwasikiliza itsona kama kweli haiwezekani wanandoa Hawa kuendelea kuishi pamoja na kabla haijatoa talaka lazima itoe muda wa kisheria wa wanandoa kujitafakari hii order ni separation ambayo ni decree nisi.

[emoji736] Baada ya muda wa separation kuisha mahakama itawasikilizs tena kama bado mambo ni magumu basi itatoa talaka na amri za matunzo ya watoto ( kama wapo) na mgawanjo wa Mali walizochuma pamoja .

[emoji777] Hivyo, kwa Sheria zetu, makatatasi wanaojiandikia watu kwa kusema mara ni talaka tatu, mara talaka rejea kimsingi Yale sii talaka na hayana effect ya kuvunja ndoa, mmoja wao akienda mahakamani kesi inasikilizwa upya kwa mujibu wa Sheria na haki inatolewa. CHOMBO CHENYE MAMLAKA YA KUVUNJA NDOA KISHERIA TANZANIA NI MAHAKAMA TUU
Unaongea kulingana na uwelewa wako.Inategemea walifunga ndoa ya aina gani
 
Unaongea kulingana na uwelewa wako.Inategemea walifunga ndoa ya aina gani
Sio uelewa wangu ni sheria ya ndoa ya Tanzania ya mwaka 1971 wewe ndio umejaza kichwani propaganda ambazo sio za kisheria na yawezekana Kuna sehemu umekaririshwa ukayameza kama yalivyo, na umeendelea kuamini yapo hivyo.
 
hapana mkuu
ndoa za kiislamu siyo lazima BAKWATA wilaya hata ukitamka tu kwamba kuanzia leo wewe siyo mke wangu ni talaka tayar,
ukiandika zinaanzia moja mpaka 3 ila ukimpa tatu hutamrejea kirahisi
Note: ndoa zinachangamoto ila talaka siyo jambo zuri kaeni muyazungumze mkiwashirikisha wakubwa
Labda muowane kwa kutamkiana hivyo hivyo. lakini mkisaini vyeti vya serekali hamuchani kienyeji namna hiyo
 
Kwema humu,

Nisiwachoshe nimeishi na mke wangu kwenye ndoa mpaka sasa ni miaka mitano ila kutokana na changamoto za ndoa nilikuwa nahitaji tuachane kwa amani na mke wangu pasi kugombana, kwahiyo nilikuwa nahitaji kumpa talaka.

Msaada wenu taratibu za kuandika talaka upoje?

Inanisikitisha sana; Kwani imeshindikana kabisa kumaliza mgogoro wenu kwa amani mkaendelea kufurahia maisha yenu.Mbona maisha yetu hapa duniani ni mafupi sana.Kwa nini kugombana gombana
 
Kiislam .
Andika barua kwa mkono wako.

Mimi fulani bin fulani , nikiwa na akili zangu timamu , na bila ya kushurutishwa wala kushawishiwa na mtu yoyote , nimeamua kukutaliki fulani binti fulani , hivyo kuanzia leo hii tareh...... wewe sio mke wangu wa ndoa.
Nakutakia maisha mema.

Jina na saini yako.

Mashahidi wawili ,
Majina yao na saini zao.

Halafu piga photocopy , original mmkabidhi yeye, copy moja mkabidhi babamkwe au walii wake ( sio lazima lakini ), copy moja ibaki kwako.
Kazi imekwisha.

Kama anaishi nyumbani kwako , akae hapo mpaka kipindi cha eda ya talaka iishe ndio anaondoka.
Ukimuingilia kwa tendo la ndoa kabla kipindi cha eda kuisha , talaka inakufa , ila itahesabika talaka moja tayari.
VIP akienda mahakamani unadhani mahakama itapokea icho kikaratasi Chako unachoita talaka.jamani mue na uwelewa ndoa Ni Mali ya serikali mahakama peke yake ndio imepewa mamlaka ya kuvunja ndoa
 
Siku hizi mahakama nasikia hazicheleweshi kesi za talaka .

Kwa jinsi wanandoa wanavyoumizana na kuuana naona wamehamasika
Ku-facilitate kesi kuisha haraka.
 
Kama nafsi imekataa usilazimishe kuishi nae maijepata matatizo bure!
 
VIP akienda mahakamani unadhani mahakama itapokea icho kikaratasi Chako unachoita talaka.jamani mue na uwelewa ndoa Ni Mali ya serikali mahakama peke yake ndio imepewa mamlaka ya kuvunja ndoa
Hiyo ni kwenu !
 
Back
Top Bottom