Utaratibu wa mwanamke kupewa pasu kwa pasu baada ya talaka bila wao kuchangia ni wa Hovyo na kandamizi kwa wanaume?

Namsubiri huyo wa kuniambia nigawane naye pasu kwa pasu, jela baada ya kitendo nitakachomfanya.
 
Huko ni kufilisika ki mawazo, kama huoni faida ya ke acha kuoa ubaki na Mali zako, nyie ndio mna Ile usemi "kwani kaja na nini hadi tugawane"
 
Hebu tufafanulie

Hebu tufafanulie sheria inasemaje kuhusu kugawana Mali.
Mali kweli mnagawana kutokana na kuangalia ni nini mlipata mkiwa pamoja lakini haya mambo ya kugawana nusu kwa nusu hayapo kisheria. Mnaweza gawana lakini sio nusu kwa nusu.... yani akae tu nyumbani nimpe mali zangu nusu haitakuja tokea
 
We kichwa chako naona ndo kimejaa funza. Eti akutunzie watoto wako (as if wewe mwanamke watoto sio wa kwako)

Mnasema watoto wako (mume) wakati kila siku mnaimba mtoto ni wa mama. Na mmekoleza kamsemo nani kama mama. Wajinga sana.

Tukiachana ndo watoto wanakuwa wangu ila tukiwa pamoja ni wa kwako??

Kama watoto ni wa kwetu sote, basi kihalali ilitakiwa tukiachana mali tulizochuma wote wagawiwe watoto, sisi tukaanze upya kila mtu kivyake.


Au kama tutapata kidogo cha kuanzia maisha sawa ila sehem kubwa ni ya watoto.
 
Nini pasu kwa pasu, kuna watu vichwa. Anamwachia nyumba, gari, sijui shamba, mahouse boy & girls, huyooo,!! anaenda zake. Amani ya akili ni bora Mara 100 kuliko mali.
I assure you, utakuwa very peaceful and happy if you even forget obout her existence.
 
Bado unaongea tu hujui uchungu wake hayajakukuta wewe
 
Akili za Ngaramtoni hizi
 
Ukimfanya mke akawa tu nyumbani akikuondolea stress na kukuzalia watoto,
Kwani watoto ni kwa ajili ya baba pekee au na mama anahesabika ni wake ?

Kama watoto ni mali ya baba na mama sio baba peke yake,na kuhudumia pia ni jukumu la baba kwa muda wote wa maisha.

Sasa unaposema kuwa mwanamke kanizalia kwa nini isiwe na yeye kajizalia wakati hao watoto nae ni wake pia.

Suala la kuzaa watoto hayo ni matokeo ya ndoa,na mtoto ni mali ya mke na mume sio mume peke ake.

Labda uje na hoja mpya kwamba katika familia watoto ni mali ya baba peke yake.
 
Kwa mama wa nyumbani ninaweza kumpa hamsin au pasu pasu ila si kwa mwanamke ambaye ni mfanyakazi. Wanawake wanaofanya kazi hawachangii chochote, na pia mwanamme hupati haki yako kama mme sasa swala la pasu ni ujinga
 
Hii naona inaegemea sana kwa wamama wa nyumbani ambae anamtegemea mume kwa kila kitu hapo pasu kwa pasu inaweza ikawa ngumu.
Lakini huyu mwanamke ambaye yupo kazini weka mia aweke mia mnunue kiwanja,mara mnunue tofali au mshahara wako kopea wangu utahudumia familia hapo pasu kwa pasu itahusika.
 
Pasu kwa pasu ikiwa mke nae alichangia kama mume wakastruggle wote wakasimamisha mali hiyo haina shida.

Lakini kwamba mama yeye aliplay part ya kule familia na baba naye akaplay part ya kutafuta alafu mwisho wa siku eti iwe nusu kwa nusu hii sio sawa.
 
Tena ukikuta anayejua kuhonga ngono akamambisha hakimu utajuta aisee, utakuta kwenye doc ya hukumu kamuandikia maelezo yote ambayo demu hakuongea hata moja ila hakimu kayachonga yanlenga point za kisheria tupu huku maelezo yako uloyatoa mwenyewe yakigeuzwa na kuchomekwa vitu ambavyo hata hukuongea alafu zile point muhimu zoote amezileft out! Mahakama ni bora zingeboresha namna ya kuchukua maelezo ya mlalamikaji na mlalamikiwa ikibidi yarekodiwe pia katika video kuepusha rushwa na uchakachuaji!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…