Utaratibu wa NHIF kumtaka mgonjwa akapate Rufaa toka Hospitali za Wilaya ni kero

Utaratibu wa NHIF kumtaka mgonjwa akapate Rufaa toka Hospitali za Wilaya ni kero

Asamwa

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2012
Posts
3,711
Reaction score
2,462
Kuna ndugu yangu amelipia kifurushi cha NHIF cha Tshs. 530,000 kwa mwaka.

Hapa karibuni amepata tatizo la maumivu ya jino. Kwa vile anaishi Oysterbay, akaamua kwenda kwenye hospitali binafsi iliyo karibu ili kupata matibabu.

Alivyofika hospitali, walimwambia kabla ya kupata matibabu inabidi aende Hospitali ya Wilaya wamwandikie rufaa ya kutibiwa katika hospitali yao!

Wote tunajua Hospitali za Wilaya zinavyokuwa na wagonjwa wengi zaidi ya uwezo wake. Kumwambia mgonjwa afunge safari hadi hospitali ya wilaya, ambayo kwa huyu ni Mwananyamala ni usumbufu ambao hauna sababu.

Kama NHIF wana makubaliano na hii hospitali binafsi, kwa nini wamsumbue mgonjwa kupoteza muda wake kwenda kutafuta rufaa?

Kama hawana imani na hospitali binafsi, kwa nini wasiweke wazi kuwa wagonjwa wao lazima watibiwe katika hospitali za serikali ili mteja aamue kama kuna sababu ya kujiunga na NHIF badala ya mifuko mingine ya Bima ya afya?

Ni vizuri NHIF wakatoa ufafanuzi kuhusu ulazima wa mgonjwa kufuata rufaa kutoka hospitali za Wilaya ambazo zimeelemewa na wagonjwa; na zinaweza kuwa mbali na eneo alilopo mgonjwa.
 
Kuna ndugu yangu amelipia kifurushi cha NHIF cha Tshs. 530,000 kwa mwaka.

Hapa karibuni amepata tatizo la maumivu ya jino. Kwa vile anaishi Oysterbay, akaamua kwenda kwenye hospitali binafsi iliyo karibu ili kupata matibabu.

Alivyofika hospitali, walimwambia kabla ya kupata matibabu inabidi aende Hospitali ya Wilaya wamwandikie rufaa ya kutibiwa katika hospitali yao!

Wote tunajua Hospitali za Wilaya zinavyokuwa na wagonjwa wengi zaidi ya uwezo wake. Kumwambia mgonjwa afunge safari hadi hospitali ya wilaya, ambayo kwa huyu ni Mwananyamala ni usumbufu ambao hauna sababu.

Kama NHIF wana makubaliano na hii hospitali binafsi, kwa nini wamsumbue mgonjwa kupoteza muda wake kwenda kutafuta rufaa?

Kama hawana imani na hospitali binafsi, kwa nini wasiweke wazi kuwa wagonjwa wao lazima watibiwe katika hospitali za serikali ili mteja aamue kama kuna sababu ya kujiunga na NHIF badala ya mifuko mingine ya Bima ya afya?

Ni vizuri NHIF wakatoa ufafanuzi kuhusu ulazima wa mgonjwa kufuata rufaa kutoka hospitali za Wilaya ambazo zimeelemewa na wagonjwa; na zinaweza kuwa mbali na eneo alilopo mgonjwa.
Hawana pesa za kulipa hizo zote ni mbinu.
 
Zingatia maelekezo acha kulialia mitandaoni ewe mkazi wa Oysterbay.
Suala si kukaa Oyster bay. Hata kama unakaa Manzese utaratibu ni huo huo. Wewe huoni usumbufu?!
 
Inasikitisha sana...


Cc: Mahondaw
Sana mkuu.
Yuko mgonjwa ambaye amekuwa akihudhuria clinic ya macho KCMC. Ana tatizo kwenye retina ya jicho, tatizo ambalo hospitali ya Mawenzi hawana uwezo wa kuishughulikia.

Alipokuja clinic mara ya mwisho (anakaa Dar es Salaam) aligizwa kwenda Mawenzi kupata rufaa! Ilibidi atumie siku Moja nzima kutafuta rufaa kutoka Mawenzi Hospital. Kuna mantiki kweli?!
 
Kuna ndugu yangu amelipia kifurushi cha NHIF cha Tshs. 530,000 kwa mwaka.

Hapa karibuni amepata tatizo la maumivu ya jino. Kwa vile anaishi Oysterbay, akaamua kwenda kwenye hospitali binafsi iliyo karibu ili kupata matibabu.

Alivyofika hospitali, walimwambia kabla ya kupata matibabu inabidi aende Hospitali ya Wilaya wamwandikie rufaa ya kutibiwa katika hospitali yao!

Wote tunajua Hospitali za Wilaya zinavyokuwa na wagonjwa wengi zaidi ya uwezo wake. Kumwambia mgonjwa afunge safari hadi hospitali ya wilaya, ambayo kwa huyu ni Mwananyamala ni usumbufu ambao hauna sababu.

Kama NHIF wana makubaliano na hii hospitali binafsi, kwa nini wamsumbue mgonjwa kupoteza muda wake kwenda kutafuta rufaa?

Kama hawana imani na hospitali binafsi, kwa nini wasiweke wazi kuwa wagonjwa wao lazima watibiwe katika hospitali za serikali ili mteja aamue kama kuna sababu ya kujiunga na NHIF badala ya mifuko mingine ya Bima ya afya?

Ni vizuri NHIF wakatoa ufafanuzi kuhusu ulazima wa mgonjwa kufuata rufaa kutoka hospitali za Wilaya ambazo zimeelemewa na wagonjwa; na zinaweza kuwa mbali na eneo alilopo mgonjwa.
HUU NI UONGO NA UPOTOSHAJI.

Naomba ni-quote Masharti ya hiyo bima yake kutoka kipengere no. 6 &2 kutoka kwenye form ambayo unasaini kuomba hiyo kadi:-

"...utapata matibabu katika hospitari zote zilizosajiriwa na mfuko za dini, serikali na binafsi za MPAKA NGAZI YA MKOA, Huduma NGAZI YA KANDA NA TAIFA ZITATOLEWA KWA UTARATIBU WA RUFAA."

Sasa yeye alienda kutibiwa Hospitari gan?... Je alifata utaratibu wa rufaa??

Hakuna mtu anatakiwa kuchukua rufaa kutoka hospitari ya wilaya bali ni kutoka Hospitari ya Mkoa kwenda hospitar ya Kanda.

TATIZO WABONGO HUWA HATUSOMI MIKATABA NA WAVIVU WA KUSOMA NDO MAANA ANALETA MALALAMIKO YASIYO NA MSINGI KAMA HAYA.

Kwani wakati anasaini hiyo form ya kuomba kadi si aliambiwa kipengere namba 2 na namba 6??

Acheki hii tabia ya kuja kuichafua Taasisi ya Serikali huku.

Kwann Bima alikata mwaka jana na ana umri zaid ya miaka 35??

Ukitaka kujua umuhim wa Bima waulize wanaofanya clinic za dialysis na oncology
 
Sana mkuu.
Yuko mgonjwa ambaye amekuwa akihudhuria clinic ya macho KCMC. Ana tatizo kwenye retina ya jicho, tatizo ambalo hospitali ya Mawenzi hawana uwezo wa kuishughulikia.

Alipokuja clinic mara ya mwisho (anakaa Dar es Salaam) aligizwa kwenda Mawenzi kupata rufaa! Ilibidi atumie siku Moja nzima kutafuta rufaa kutoka Mawenzi Hospital. Kuna mantiki kweli?!
Mantiki ipo kwa hii serikari isio na kichwa..ila kwa watu wenye vichwa haina mantiki
 
HUU NI UONGO NA UPOTOSHAJI.

Naomba ni-quote Masharti ya hiyo bima yake kutoka kipengere no. 6 &2 kutoka kwenye form ambayo unasaini kuomba hiyo kadi:-

"...utapata matibabu katika hospitari zote zilizosajiriwa na mfuko za dini, serikali na binafsi za MPAKA NGAZI YA MKOA, Huduma NGAZI YA KANDA NA TAIFA ZITATOLEWA KWA UTARATIBU WA RUFAA."

Sasa yeye alienda kutibiwa Hospitari gan?... Je alifata utaratibu wa rufaa??

Hakuna mtu anatakiwa kuchukua rufaa kutoka hospitari ya wilaya bali ni kutoka Hospitari ya Mkoa kwenda hospitar ya Kanda.

TATIZO WABONGO HUWA HATUSOMI MIKATABA NA WAVIVU WA KUSOMA NDO MAANA ANALETA MALALAMIKO YASIYO NA MSINGI KAMA HAYA.

Kwani wakati anasaini hiyo form ya kuomba kadi si aliambiwa kipengere namba 2 na namba 6??

Acheki hii tabia ya kuja kuichafua Taasisi ya Serikali huku.

Kwann Bima alikata mwaka jana na ana umri zaid ya miaka 35??

Ukitaka kujua umuhim wa Bima waulize wanaofanya clinic za dialysis na oncology
Aliyekuambia alienda hosptali ambayo haikusajiliwa na NHF nani? Hiyo hspitali imesajilwa na NHIFna alishawahi kutibiwa hapo.

Nakupa mfano wa mgonjwa mwingine ambayae anahudhuria clinic ya macho KCMC. Mara ya mwisho alipokuja clinic alilazimika kwenda Hospitali ya Wilaya Mawenzi kupata rufaa ya tatizo ambalo Mawenzi hawana uwezo wa kulishughulikia! Hii siyo hadithi, bali ni ukweli.
Usiwe unakurupuka kujadili mambo ambayo huyaelewi.
 
Mantiki ipo kwa hii serikari isio na kichwa..ila kwa watu wenye vichwa haina mantiki
Uko sahihi mkuu.
Unamtuma mgonjwa ambaye ana faili na anatibiwa KCMC kwenda kupata rufaa Mawenzi hospital! Kama SI upuuzi tutaita hii kitu gani?!
 
Aliyekuambia alienda hosptali ambayo haikusajiliwa na NHF nani? Hiyo hspitali imesajilwa na NHIFna alishawahi kutibiwa hapo.

Nakupa mfano wa mgonjwa mwingine ambayae anahudhuria clinic ya macho KCMC. Mara ya mwisho alipokuja clinic alilazimika kwenda Hospitali ya Wilaya Mawenzi kupata rufaa ya tatizo ambalo Mawenzi hawana uwezo wa kulishughulikia! Hii siyo hadithi, bali ni ukweli.
Usiwe unakurupuka kujadili mambo ambayo huyaelewi.
Hospital zenye ngazi Sawa na hospital za kanda kuna utaratibu wa kufata , unless uwe na kifurushi cha Bima cha VVP , Ila hvyo vifurushi vingine Mzee inabd uanzie health center huko wakishindwa ndo wakupe referral
 
Aliyekuambia alienda hosptali ambayo haikusajiliwa na NHF nani? Hiyo hspitali imesajilwa na NHIFna alishawahi kutibiwa hapo.

Nakupa mfano wa mgonjwa mwingine ambayae anahudhuria clinic ya macho KCMC. Mara ya mwisho alipokuja clinic alilazimika kwenda Hospitali ya Wilaya Mawenzi kupata rufaa ya tatizo ambalo Mawenzi hawana uwezo wa kulishughulikia! Hii siyo hadithi, bali ni ukweli.
Usiwe unakurupuka kujadili mambo ambayo huyaelewi.
Kuna shida mahali.
Either watumishi wa kcmc hawajui taratibu au ni uongo.
Kwanza kabisa kila hospital kubwa siku hizi kuna mtu toka nhif anaesimamia mambo yote ya wagonjwa wa nhif.
 
Aliyekuambia alienda hosptali ambayo haikusajiliwa na NHF nani? Hiyo hspitali imesajilwa na NHIFna alishawahi kutibiwa hapo.

Nakupa mfano wa mgonjwa mwingine ambayae anahudhuria clinic ya macho KCMC. Mara ya mwisho alipokuja clinic alilazimika kwenda Hospitali ya Wilaya Mawenzi kupata rufaa ya tatizo ambalo Mawenzi hawana uwezo wa kulishughulikia! Hii siyo hadithi, bali ni ukweli.
Usiwe unakurupuka kujadili mambo ambayo huyaelewi.
Ni kweli ku mtu alienda kutibiwa mloganzila ambapo kuna dr wa tatizo lake lkn akalazimika kwenda hospitali X kupata refferral ndio arudi MNH. Ni kautaratibu fulani kana usumbufu hata kama kuna sababu nyuma yake.
 
Kuna shida mahali.
Either watumishi wa kcmc hawajui taratibu au ni uongo.
Kwanza kabisa kila hospital kubwa siku hizi kuna mtu toka nhif anaesimamia mambo yote ya wagonjwa wa nhif.
Kinachofanyika na mfuko ni kuwa wewe mgonjwa huwezi tu kuamua umuone daktari fulani, inawezekana unaumwa malaria unataka ukamuone specialist wa moyo.. haiwezekana sasa ndio wanataka utibiwe kwanza kawaida ndipo daktari aseme hii case yako inabidi uende kumwona specialist fulani.

Ikitokea kila mgonjwa akapewa uhuru wa kupata matibabu wote watakimbilia kwa specialist hawataenda kwa CO au GP.

Hii ni moja ya kulinda mapato ya mfuko maana kila level ya qualifications ina gharama zake
 
Aliyekuambia alienda hosptali ambayo haikusajiliwa na NHF nani? Hiyo hspitali imesajilwa na NHIFna alishawahi kutibiwa hapo.

Nakupa mfano wa mgonjwa mwingine ambayae anahudhuria clinic ya macho KCMC. Mara ya mwisho alipokuja clinic alilazimika kwenda Hospitali ya Wilaya Mawenzi kupata rufaa ya tatizo ambalo Mawenzi hawana uwezo wa kulishughulikia! Hii siyo hadithi, bali ni ukweli.
Usiwe unakurupuka kujadili mambo ambayo huyaelewi.
Sasa mm na ww nani kakurupuka?

KCMC ina level gan? Ni Hospitari ya kanda ile... So lazima urud hospitar ya Mawenzi ambayo ni RRH Kupata rufaa kulingana na masharti ya hizo bima za vifurushi zinavyotaka.

Swala la kuwa na file KCMC sio sababu ya msingi, Unajua maana ya rufaa?... Uko kwenye sekta ya afya?...

Narudia tena acheni kukurupuka na muwe mnasoma masharti ya vitu kabla ya kusaini.

All in all HIZO BIMA WANAKATA KWA HIARI, Kama unaona haikufai si unaacha kwani umelazimishwa ukate??

Wanasheria wanasema "VOLENT NON FIT INJURIA"
 
Mpuuzi ni anayekata bima bila kusoma masharti yake na kuja kutafuta huruma huku mtandaoni.

Si kuna makampuni kibao huko mkakate bima kwan lazima NHIF??
Uko sahihi mkuu.
Unamtuma mgonjwa ambaye ana faili na anatibiwa KCMC kwenda kupata rufaa Mawenzi hospital! Kama SI upuuzi tutaita hii kitu gani?!
 
Kuna shida mahali.
Either watumishi wa kcmc hawajui taratibu au ni uongo.
Kwanza kabisa kila hospital kubwa siku hizi kuna mtu toka nhif anaesimamia mambo yote ya wagonjwa wa nhif.
Hiyo niliyoandika ni habari halisi. Huyo mgonjwa alishatibiwa KCMC Kwa muda mrefu, lakini ghafla utaratibu ukabadilika.

Wewe unalaumu KCMC kwamba hawajui utaratibu. Unadhani wao wanafurahi kusumbua wagonjwa wao?!

NHIF ndiyo wameanza huu utaratibu kwa sababu ambazo wanazijua wenyewe.
 
Back
Top Bottom