UTATA: Majadiliano na DP world bado, lakini serikali yetu inajivunia faida za DP world!

UTATA: Majadiliano na DP world bado, lakini serikali yetu inajivunia faida za DP world!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Huenda labda ni kuchanganyikiwa au kutokujipanga kwa viongozi wa Tanzania katika kutetea mkataba wa uwekezaji wa bandari baina ya DP world na Tanzania. Kumekuwa na kauli za kukinzana na kuvuruga kutoka kwa viongozi watetezi wa sakata hili ili kujibu shutuma za Bandari yetu kutolewa bure na milele kwenda kwa muarabu wa Dubai. Watetezi wanasema kilichopitishwa bungeni sio mkataba bali ni makubaliano tu ya ushirikiano baina ya Tanzania na Dubai, yanayotengeneza msingi wa mamlaka ya bandari Tanzania kukaa chini na kujadiliana na Dp world na mwisho kutengeneza mkataba wa uwekezaji wa bandari. Maajabu ni kuwa serikali imekuwa ikijivunia faida za kitakwimu tutakazopata Tanzania kupitia uwekezaji wa Dp world hapa Tanzania wakati huo huo viongozi hao hao wanasema kuwa majadiliano bado na mkataba bado!

Maswali.
1. Wamejuaje hizo faida kabla ya majadiliano au kuwepo mkataba?

2. Hizo faida zimeandikwa wapi na zinasimamia misingi ipi ikiwa majadiliano bado na mkataba bado?

3. Nini mantiki ya kwenda kwenye majadiliano au kutengeneza mkataba tena wakati kila kitu chenye faida kwetu kipo tayari kwa kuwa serikali yetu na DP wameshapatana, kukubaliana na kupitisha bungeni?
 
Wamechanganyikiwa, hawajui washike lipi na waache lipi, sasa wapo wapo tu kama popo.
 
MTU akijinyea kamwe hawezi kusimama mbele za watu kwa kujiamini.
 
Faida zinafanywa kwa tathmini ya "Performance of contract".


Kwamba hizo ndo performance criteria ambazo wanakuwa wanatathmini kwa kupigia mahesabu ,yeye kama mwekezaji amekija na ombi lake ila nchi nayo inafanya tathmini za kiuchumi incase yatakuja tofauti basi kama TICTS vile wanaweza kumuondoa .

Mikataba yenye mlengo wa kiuchumi lazima watu wafanye tathmini ya awali kwa kuangalia ufanisi Mfano kwa tathmini ya awali labda palikuwa na upotevu wa mapato kwa njia fulani ,je anayekuja anaweza vipi kuzuia hilo na kama akiuzia kwamba yale mapato yatarudi kwa serikali basi wanayapigia mahesabu yataongezeka .

Hata miradi mengi kabla ya kuanza utasikia huu utazalisha ajira idadi fulani .

Sasa kwa serikali makini hizo performance agreements ndo za kufuatilia katika utendaji kazi wa huyo muwekezaji ..
 
Mleta uzi na wanaokuunga mkono wote mna msongo wa mawazo! Sasa kuna shida gani waki anticipate faida?
 
Kuna ugumu gani kuuacha kabisa huo mkataba??
 
Huenda labda ni kuchanganyikiwa au kutokujipanga kwa viongozi wa Tanzania katika kutetea mkataba wa uwekezaji wa bandari baina ya DP world na Tanzania. Kumekuwa na kauli za kukinzana na kuvuruga kutoka kwa viongozi watetezi wa sakata hili ili kujibu shutuma za Bandari yetu kutolewa bure na milele kwenda kwa muarabu wa Dubai. Watetezi wanasema kilichopitishwa bungeni sio mkataba bali ni makubaliano tu ya ushirikiano baina ya Tanzania na Dubai, yanayotengeneza msingi wa mamlaka ya bandari Tanzania kukaa chini na kujadiliana na Dp world na mwisho kutengeneza mkataba wa uwekezaji wa bandari. Maajabu ni kuwa serikali imekuwa ikijivunia faida za kitakwimu tutakazopata Tanzania kupitia uwekezaji wa Dp world hapa Tanzania wakati huo huo viongozi hao hao wanasema kuwa majadiliano bado na mkataba bado!

Maswali.
1. Wamejuaje hizo faida kabla ya majadiliano au kuwepo mkataba?

2. Hizo faida zimeandikwa wapi na zinasimamia misingi ipi ikiwa majadiliano bado na mkataba bado?

3. Nini mantiki ya kwenda kwenye majadiliano au kutengeneza mkataba tena wakati kila kitu chenye faida kwetu kipo tayari kwa kuwa serikali yetu na DP wameshapatana, kukubaliana na kupitisha bungeni?
Tatizo ni akili ndogo kupewa dhamana ya uongozi na mamlaka ya kufanya maamuzi yenye kugusa maslahi mapana ya nchi yetu. Badala kuangalia undani wa kiitu kabla ya kufanya maamuzi, wao hudanganyika na ahadi za zitokanazo na ghiliba, rushwa, na vizawadi vya kipuuzi.
 
Faida zinafanywa kwa tathmini ya "Performance of contract".


Kwamba hizo ndo performance criteria ambazo wanakuwa wanatathmini kwa kupigia mahesabu ,yeye kama mwekezaji amekija na ombi lake ila nchi nayo inafanya tathmini za kiuchumi incase yatakuja tofauti basi kama TICTS vile wanaweza kumuondoa .

Mikataba yenye mlengo wa kiuchumi lazima watu wafanye tathmini ya awali kwa kuangalia ufanisi Mfano kwa tathmini ya awali labda palikuwa na upotevu wa mapato kwa njia fulani ,je anayekuja anaweza vipi kuzuia hilo na kama akiuzia kwamba yale mapato yatarudi kwa serikali basi wanayapigia mahesabu yataongezeka .

Hata miradi mengi kabla ya kuanza utasikia huu utazalisha ajira idadi fulani .

Sasa kwa serikali makini hizo performance agreements ndo za kufuatilia katika utendaji kazi wa huyo muwekezaji ..
Nini kilitakiwa kuanza? Majadiliano na mwekezaji au Azimio la Bunge?
 
Huenda labda ni kuchanganyikiwa au kutokujipanga kwa viongozi wa Tanzania katika kutetea mkataba wa uwekezaji wa bandari baina ya DP world na Tanzania. Kumekuwa na kauli za kukinzana na kuvuruga kutoka kwa viongozi watetezi wa sakata hili ili kujibu shutuma za Bandari yetu kutolewa bure na milele kwenda kwa muarabu wa Dubai. Watetezi wanasema kilichopitishwa bungeni sio mkataba bali ni makubaliano tu ya ushirikiano baina ya Tanzania na Dubai, yanayotengeneza msingi wa mamlaka ya bandari Tanzania kukaa chini na kujadiliana na Dp world na mwisho kutengeneza mkataba wa uwekezaji wa bandari. Maajabu ni kuwa serikali imekuwa ikijivunia faida za kitakwimu tutakazopata Tanzania kupitia uwekezaji wa Dp world hapa Tanzania wakati huo huo viongozi hao hao wanasema kuwa majadiliano bado na mkataba bado!

Maswali.
1. Wamejuaje hizo faida kabla ya majadiliano au kuwepo mkataba?

2. Hizo faida zimeandikwa wapi na zinasimamia misingi ipi ikiwa majadiliano bado na mkataba bado?

3. Nini mantiki ya kwenda kwenye majadiliano au kutengeneza mkataba tena wakati kila kitu chenye faida kwetu kipo tayari kwa kuwa serikali yetu na DP wameshapatana, kukubaliana na kupitisha bungeni?
Yaani inashangaza, mara mapato yata shoot toka 7 trillions to 24 trillions unabaki kujiuliza namba hizi wanazitoa wapi ili hali IGA bado? Kumbe kila kitu kiliisha wamekuja bungeni kuzuga tu. Ila hili haliwaachi salama baadhi yao.
 
Mleta uzi na wanaokuunga mkono wote mna msongo wa mawazo! Sasa kuna shida gani waki anticipate faida?
Sasa mmekuwa waongo kupitiliza! Hivi unaweza sema duka hili litanipa faidi milioni kumi kwa mwaka wakati bado hujui litakuwa wapi na utauza nini!?
Njia bora hapo ungesema natamani biashara ya duka ya kunipa milioni kumi faida.
 
Nini kilitakiwa kuanza? Majadiliano na mwekezaji au Azimio la Bunge?
Azimioa la bunge hata kushirikisha wadau kama wasomi , wanasheria then ndo waende kujadili na muwekezaji, kwa sababu draft ya makubaliano ipo wanaweza wasilisha bungeni Kwanza na kushirikisha wasomi wote .

Hapa watapata mwanga na maoni ya kwenda kuwasilisha kama kuna mapungufu pia ni vizuri kwa vile watu muhimu wote watakuwa wametoa maoni yao ,kweny udhaifu patajulikana .
 
Tatizo ni akili ndogo kupewa dhamana ya uongozi na mamlaka ya kufanya maamuzi yenye kugusa maslahi mapana ya nchi yetu. Badala kuangalia undani wa kiitu kabla ya kufanya maamuzi, wao hudanganyika na ahadi za zitokanazo na ghiliba, rushwa, na vizawadi vya kipuuzi.
Wewe mtu anakuambia hata akikosea au kutotimiza ahadi huruhusiwi kuuvunja mkataba. Sasa hizo faida zisipopatkana au ajira asitoe kwa wazawa utamdhibiti vipi ilihali amekufunga???

Wasipotusikia humu twendeni Magogoni watatuelewa
 
Faida zinafanywa kwa tathmini ya "Performance of contract".


Kwamba hizo ndo performance criteria ambazo wanakuwa wanatathmini kwa kupigia mahesabu ,yeye kama mwekezaji amekija na ombi lake ila nchi nayo inafanya tathmini za kiuchumi incase yatakuja tofauti basi kama TICTS vile wanaweza kumuondoa .

Mikataba yenye mlengo wa kiuchumi lazima watu wafanye tathmini ya awali kwa kuangalia ufanisi Mfano kwa tathmini ya awali labda palikuwa na upotevu wa mapato kwa njia fulani ,je anayekuja anaweza vipi kuzuia hilo na kama akiuzia kwamba yale mapato yatarudi kwa serikali basi wanayapigia mahesabu yataongezeka .

Hata miradi mengi kabla ya kuanza utasikia huu utazalisha ajira idadi fulani .

Sasa kwa serikali makini hizo performance agreements ndo za kufuatilia katika utendaji kazi wa huyo muwekezaji ..
Mbona unatuchanganya. Hizo zinaoneshwa wapi? Serious? Do we have any written promises?
 
Ni kama zile porojo za gesi tu tulipoambiwa gesi itabadilisha kabisa taswira ya hali ya uchumi ya kusini.
 
Faida zinafanywa kwa tathmini ya "Performance of contract".


Kwamba hizo ndo performance criteria ambazo wanakuwa wanatathmini kwa kupigia mahesabu ,yeye kama mwekezaji amekija na ombi lake ila nchi nayo inafanya tathmini za kiuchumi incase yatakuja tofauti basi kama TICTS vile wanaweza kumuondoa .

Mikataba yenye mlengo wa kiuchumi lazima watu wafanye tathmini ya awali kwa kuangalia ufanisi Mfano kwa tathmini ya awali labda palikuwa na upotevu wa mapato kwa njia fulani ,je anayekuja anaweza vipi kuzuia hilo na kama akiuzia kwamba yale mapato yatarudi kwa serikali basi wanayapigia mahesabu yataongezeka .

Hata miradi mengi kabla ya kuanza utasikia huu utazalisha ajira idadi fulani .

Sasa kwa serikali makini hizo performance agreements ndo za kufuatilia katika utendaji kazi wa huyo muwekezaji ..
Mkuu hizo faida serikali inawezaje kuzitarajia na kujivunia nazo hadharani wakati huo huo inasema hata majadiliano na DP world bado hayajafanyika?
Hizo faida hata DP world hawajazisema popote, serikali ya Tanzania inapata wapi huo ujasiri na uhakika wa kuzipata?
 
Mbona unatuchanganya. Hizo zinaoneshwa wapi? Serious? Do we have any written promises?
Ndo maana ninakuambia ni tathmini.

Tathmini ndo wametaja kwa aslimia je umeona wapi wamesema ni kiasi gani cha fedha ?

Na tathmini wamefanya Tanzania sio wao DP World.


Elewa kitu kinachoitwa tathmini ni .makadirio ya awali katika utekelezaji wa mkataba kwa manufaa ,hata wana uchumi wanakadiria labda uwekezaji utakuwa kwa kiwango fulani kwa kuangalia trends fulani ya ufanisi na uwekezaji.

Hakuna sehemu imesema itatoa shlling kadhaa ila itachangia kwa asalimi fulani ,ili lengo liweze kutimia ni lazima pawe na "performance " kama alivyoahidi atakuwa ana-serving meli kadhaa kwa mda mfupi ili kupunguza msongamano basi ndo jambo la kufuatilia ndani ya mda aliosema atakuwa akifanya hivyo je ni kweli.
 
Back
Top Bottom