UTATA: Majadiliano na DP world bado, lakini serikali yetu inajivunia faida za DP world!

UTATA: Majadiliano na DP world bado, lakini serikali yetu inajivunia faida za DP world!

Mkuu hizo faida serikali inawezaje kuzitarajia na kujivunia nazo hadharani wakati huo huo inasema hata majadiliano na DP world bado hayajafanyika?
Hizo faida hata DP world hawajazisema popote, serikali ya Tanzania inapata wapi huo ujasiri na uhakika wa kuzipata?
Sawa mkuu ila hii tathmini imefanyika upande wetu sisi watanzania sio wao .

Pia tunatakiwa kama ni kweli pawe na ufuatiliaji wa je hizo tathmini kweli zitafikiwa ?

Ndo maana hata muwekezaji akipewa tenda ya kujenga barabara katika ubora fulani ,wanafuatilia kujua je ni kweli kama makubalini na kama unakumbuka Magufuli alikuwa anavunja kabisa na nyundo kuangalia ubora.

Ishu katika nchi zetu ni ufuatilia wa "performance of contract" je muwekezaji anaweza kutimiza yale aliyoahidi maana sisi kama watanzania kwa makubaliano tushafanya tathmini yetu na kujua tutapata asilimia fulani kama ongezeko.

Kumbuka kagame alitaka bandari na alifanya tathmini na kuahidi kiasi fulani kama faida ambacho ni kikubwa zaidi ya tulichokuwa tunapata.
 
Mleta uzi na wanaokuunga mkono wote mna msongo wa mawazo! Sasa kuna shida gani waki anticipate faida?
Kama.unatarajia, unatakiwa kusema kuwa unatarajia. Na useme pia kwa nini una matarajio hayo. Zaidi ya hapo, ni dhahiri utakuwa mwongo.
 
Screenshot_20230709-130911_Instagram.jpg
 
Huenda labda ni kuchanganyikiwa au kutokujipanga kwa viongozi wa Tanzania katika kutetea mkataba wa uwekezaji wa bandari baina ya DP world na Tanzania. Kumekuwa na kauli za kukinzana na kuvuruga kutoka kwa viongozi watetezi wa sakata hili ili kujibu shutuma za Bandari yetu kutolewa bure na milele kwenda kwa muarabu wa Dubai. Watetezi wanasema kilichopitishwa bungeni sio mkataba bali ni makubaliano tu ya ushirikiano baina ya Tanzania na Dubai, yanayotengeneza msingi wa mamlaka ya bandari Tanzania kukaa chini na kujadiliana na Dp world na mwisho kutengeneza mkataba wa uwekezaji wa bandari. Maajabu ni kuwa serikali imekuwa ikijivunia faida za kitakwimu tutakazopata Tanzania kupitia uwekezaji wa Dp world hapa Tanzania wakati huo huo viongozi hao hao wanasema kuwa majadiliano bado na mkataba bado!

Maswali.
1. Wamejuaje hizo faida kabla ya majadiliano au kuwepo mkataba?

2. Hizo faida zimeandikwa wapi na zinasimamia misingi ipi ikiwa majadiliano bado na mkataba bado?

3. Nini mantiki ya kwenda kwenye majadiliano au kutengeneza mkataba tena wakati kila kitu chenye faida kwetu kipo tayari kwa kuwa serikali yetu na DP wameshapatana, kukubaliana na kupitisha bungeni?
Hakuna utata wowote ila wewe na wenzako mnafanya juhudi ili msielewe. Mkataba wa dp ni mzuri na serikali inapaswa kuongeza kasi kuwaruhusu waanze fasta.
 
Back
Top Bottom