Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

My apologies if this just so happens to be an incorrect prejudice, ila username yako inasadifu uzi wako. Ama ni kutokujua sheria za kimataifa za mipaka? Ikitokea nchi zinapakana kwenye chanzo cha maji (isipokuwa bahari), mpaka ni nusu ya chanzo hicho. Hivyo ndivyo nijuavyo. Nadhani mambo ya Tanganyika ungetuachia waTanganyika tu kiongozi.
 
Wamalawi waliingia mitini waliikacha kesi mahakamani. Mpaka ni katikati ya Ziwa, hizi habari nyingine zichukulie kuwa ni za uzushi.
 
Mtoa Mada naona unawathamini sana Wakoloni na kuona maamuzi yao ndio sahihi.

Kama ni hivyo warudishie Waarabu kisiwa chao cha Zanzibar na muendelee kuwa Watumwa kama walivyo amua Waarabu.
Wewe bado una fikra ya kuwa Mtumwa.

Wanyasa wa Tanganyika walikuwa wanalitumia Ziwa Nyasa kama raslimali yao halari ya asili bila bugdha yoyote ile kabla hata ya kuja huyo Mkoloni wako, na Kabla ya kuja kwa yule anaye kujaza ujinga mwingi kichwani na kukabwa na kupigwa kule Pangoni na Ibirisi.
 
Malawi ilishindwa sababu ni banana republic, siku wakipata serikali inayoeleweka hii kesi wanashinda na tunalazimika kuingia makubaliano mapya na compromise.

Status itabaki hivi endapo Nyasa hamna gesi au mafuta, siku zimetokea malighafi humo tutabishana. Ikitokea ni maji tu basi wanaweza ruhusu tutumie au tuvue samaki.

Na kisheria za kimataifa, ni marufuku kuzuia chanzo cha asili cha maji kisielekee nchi nyingine. That's an act of war.

Nigeria kwenye Niger Delta wana mabwawa ya umeme kama Kainji ambayo maji yake yanatokea nchini Niger. Nigeria ililazimika kuipa umeme Niger ili nayo isijenge bwawa kwake ambalo litazuia maji. Kwenye HEP station angalau mtazozana, sasa kwenye hamna eti Tz tuzuie maji yasiende Nyasa sijui yakalete mafuriko wapi lazima kimataifa tuonekane na makosa makubwa.
 
Wakamfufue Mwalimu Julius Nyerere na Kamuzu Banda kama mashahidi mahususi waliochukua nchi zetu kutoka kwa wakoloni ili kesi iishe,porojo porojo za google map hazitusaidii chochote zaidi ya magomvi.
Mwalimu Nyerere na mzee Banda waliikuta mikataba ambayo hadi leo ipo, hakuna haja ya kuwafufua.

Iddi Amin alikuwa na sababu hafifu za kuidai Kagera salient, mipaka ya nchi kitaratibu inagawanywa kwenye natural obstacle. Na pale obstacle ni mto Kagera, na sehemu ile inaingiliana na Uganda zaidi kuliko Tanzania. Ila kimkataba wa kikoloni wao walichora mstari kwa rula. Basi iko hivyo anayebisha analeta ugomvi.

Ni makosa yalifanyika na wakoloni, na founding fathers wa OAU waliyajua makosa hayo ila wakaona muda utakaotumika kupigana na kubishana hauna manufaa. Kila nchi ina claim, na zipo nchi zaidi ya 50.
 
Mkuu tunaweza kupata hiyo makala ya MH Hamza Johari
 
Sisi tunachojua mpaka uko kati kati ya ziwa hizo porojo zako za Google maps wapelekee wachambawima wenzako
Hicho unachojua umeambiwa na nani?
Kama uliambiwa na serikali ya CCM kupitia matamko yao au shuleni ulipokuwa ukisoma, basi piga piga kifua chako kwa kujiamini huku ukijisemea mwenyewe wewe ni mjinga kabisa!

Google map ni sehemu tu ya kupata taarifa za kiramani, na taarifa zao wanazitafuta kutoka vyanzo rasmi mbali mbali vyenye kueleweka na kukubalika na mamlaka za kiulimwengu.
 
😆😆😆😆😆
 
Mazungumzo baina ya Tanzania na Malawi yafanyike. Au status quo ibaki hivihivi tunatumia bila shida wala ugomvi.

Ila Tanzania kulazimisha au kujiaminisha ziwa nusu liwe lake kisheria haiko na back up. Maana Malawi wala Tanganyika sio zilizogawa mipaka. Hata Kenya wangependa kuwa na eneo kubwa la ziwa Victoria ila waliambulia kaeneo kadogo 6%, Uganda 43% wakati Tanzania ina nusu nzima 51%.

Sasa Kenya waje hapa walazimishe ziwa ligawanywe kwa 33% kwa nchi tatu itakuwaje?

Ziwa Tanganyika 45% Congo, 41% Tanzania, 8% Burundi na 6% Zambia. Zambia na Burundi nazo zilalamike zitake mgawo sawa?

Tanzania kuna sehemu nyingi imependelewa kuliko kupunjwa. Thats life huwezi pata kila kitu.
 
Hilo ziwa haiwezekani nchi moja kujimilikisha lote ilihali na raia wetu wanalitumia kwa sababu za kiuchumi na kimaisha...eti kisa mkataba wa mkoloni....
Hakuna nchi inayojimilikisha. Nani alikupa mipaka ya Tanganyika unayotumia leo, nani alikupa 51% ya ziwa Victoria na akawapa Kenya 6%?
Huyohuyo ndio aliipa Malawi ziwa lote.

Ukisema wanajimilikisha basi na Kenya iseme tunajimilikisha mlima Kilimanjaro na Uganda iseme tunajimilikisha bandari nyingi wakati yenyewe haina.
 
Unadhani kwanini makambi ya wakimbizi ya Congo yapo Tanzania?
Asa nawe jamaa una akili gani, watu wanakimbia Congo sababu ya machafuko afu unataka na kambi za wakimbizi ziwepo hapo Congo, kwann Kambi za wakimbizi wa Syria zilikuwepo kusini mwa Turkiye

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
 
Dunia imechangamka currently,Mara ukraine,Mara Palestina,Mara congo,Sudan, Syria n.k
Na sisi kupitia lake nyasa dispute "tuwachangamshe" wamalawi.
 
We mkim
We mkimbizi rudini kwenu NYASA mmezamia Zanzibar
 
Mada ni kubwa kuliko mtoa mada, ni wa kumpuuza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…