Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

Sisi tunashikilia ya UN kwamba endapo nchi ni majirani na wanashare water bodies hivyo inatakiwa mpaka uwe katikati na si vinginevyo..
Pia kipindi Cha mvua your so called Lake Malawi linaongezeka ukubwa, maji ya ziwani yanakuja Hadi Kijiji Cha Isanga na ngonga hivyo,mpaka wa ziwa unakuwa ndani ya hivyo vijiji...kwahiyo kwa mantiki Yako ni kwamba kumbe kipindi Cha masika Mpaka wa Malawi Unaingia hadi vijiji vilivyopo pembezoni mwa ziwa hilo!
Nenda kyela,tembelea vijiji vya kata ya ngonga,Mwaya hadi Matema..halafu uje uelewe Mantiki iliyowekwa na UN uifananishe na huo UROJO wako uliouandika.
 
Hamna mwenye haki ya umiliki wa hilo ziwa asilimia 100.

Mipaka ya kikoloni haiwezi kutuondolea haki yetu.
Unajua kwamba OAU walikubaliana kuwa mipaka ya kikoloni ndio iendelee kutumika baada ya uhuru?

Yani unataka kusema kwamba nchi za Afrika tuna busara sana kwahiyo tuanze kuchora upya mipaka. Unazijua akili za Mwafrika kweli mkuu?

Yani turudie kuchora, Uganda wapendekeze kupata Kagera salient, Kenya wapendekeze kupata mlima Kilimanjaro pale ambapo ramani ilipindishwa ili mlima uwe Tanzania, Zanzibar wadai pwani ya bara maana kuna Sultan aliwahi sema anaimiliki na akiwapa Wajerumani sijui, Tanzania tudai sehemu ya Masai Mara ya Kenya ili Wamasai wote wawe Tanzania, Kenya wapendekeze waongezewe sehemu ya ziwa Victoria wawe nayo nyingi maana Tanzania imechukua kipande kikubwa zaidi, Burundi nao waombe sehemu kubwa zaidi ya ziwa Tanganyika. Hapo ni sisi tu, bado sehemu nyingine za Afrika.

Kiuhalisia ukisoma Helligoland treaty na mkataba mwingine, hakuna ushahidi unaoonyesha Tanzania tunamiliki nusu ya ziwa Nyasa. Hata Wajerumani waliokuwa wanatawaka Tanganyika ramani yao inaonyesha Nyasa nzima ni ya Malawi.

Sisi Tanzania tunakuwa na claim kuwa wazungu walikubaliana kama kuna chanzo cha maji mpakani basi kigawanywe kila nchi inayopakana ipate kiasi chake. But that wasn't the case kwa ziwa Nyasa. Tukienda mahakama ya usuluhishi, zikaletwa mikataba na mashahidi wakoloni Tanzania tunashindwa asubuhi na mapema kabisa.
 
View attachment 3183727
Ukimaliza kuzungumzia Malawi anza kuzungumzia ID yako na mikapa yako
Hivi unajua Zanzibar tuna eneo letu rasmi kisheria huko Tanganyika maeneo ya Bagamoyo. Ni maelfu ya ekari, eneo kubwa huenda zaidi ya nchi ya Vatican. Hivyo wazanzibar wote tunaweza kuja hapo Tanganyika, tukaanzisha taifa letu jipya dogo ndani ya taifa lenu huku tukila mema ya Tanganyika huku mazombi ya kitanganyika yakieendelea kulia lia.
Tanganyika ni shamba fulani la bibi mzee sana.
Hivyo ukae utulie tu.


Niishie hapo.
 
Kwahiyo watu wa Kyela waachaje kutumia hayo maji!??
Huyu ana siasa ya kuwagawa watu,yaani wengine wanahangaika watu waungane,yeye anafanya juu chini kutugawa..
Vijiji vyote vilivyopo pembezoni mwa ziwa nyasa kwa upande wa kyela ,kwa kipindi Cha masika,mpaka wa ziwa Unaingia ndani kabisa ya vijiji hivyo,kwahiyo tuseme kipindi Cha masika Malawi inakuwa kubwa hadi kuingia kwenye vijiji vyetu?
Hili jambo siyo la kulichukulia juu juu watuulize tuliowahi kufika huko na kujionea.
 
Naendelea kuzoom hii ramani..najaribu kupitia pia comments za uzi huu ntapata kitu hapa japo nilisoma tangu msingi kuwa Nyasa ipo Tanzania na Malawi, japo landmark ya Tz ni pembezoni mwa ziwa..ila haiwezekani nchi ipakane na maji halafu asimiliki hata kidogo..ndio mana kuna comment humu za UN nazielewa,
 
Nakumbuka tulikuwa na kesi na malawi kuhudu hilo ziwa sijui iliishaje, marehemu Membe, alituambia tulishinda ile kesi.

Maana google sijui wao wanatumia vipimo gani, au tulidanganywa?
Tulifungua kesi kihuni na kimihemko, tukaishia kwenye usuluhishi baada ya kunusa kuwa tutapigwa kama kawaida yetu kwenye kesi za kimataifa. Majadiliano ya usuluhishi ni janja janja ya kuvuta muda, kupiga pesa nk.

Baada ya Membe kuukosa urais, uliwahi kumsikia akizungumzia hiyo kitu?
 
Japo umeandika Kwa kebehi Sana 😂😂 lakini umesema kitu cha maana Sana ...
 
Duh hapo ndio naonaga muungano hauna tija..why uwepo? Faida zake ni za..kisiasa au kiuchumi au Kiusalama?
 
nilende kukupinga. mipaka inapoangukia kwenye maj.bas lazma iwe nusu kwa nusu. kwa raman hio kipi kijustify malawa aje mpaka tanzania? bas kama ndio hivyo hata tanganyika uwaambie ko ngo kuwa ziwa ni lettu lote .hapa umepotosha
 

Tunakuvuta kwenye 18 tu
 
nilende kukupinga. mipaka inapoangukia kwenye maj.bas lazma iwe nusu kwa nusu. kwa raman hio kipi kijustify malawa aje mpaka tanzania? bas kama ndio hivyo hata tanganyika uwaambie ko ngo kuwa ziwa ni lettu lote .hapa umepotosha
Aende akaangalie ya ziwa Tanganyika au ziwa Victoria halafu aje na mlinganyo/utofauti.
 
Vyovyote iwavyo, usuruhishi au kesi, maamuzi yalikuwaje, au tulikubaliana nini kuhusu huo mpaka?

Nakumbuka Marehemu Membe alisema tulishinda, sasa sijui maamuzi ya hiyo arbitration yalikuwaje.

Unaweza kutuletea hapa?
 
Your very genius man..
Mpo wachache sana jf hapa mkuu
🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…