Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

Kulingana na ramani uliyoiweka ndugu Zanzibar-ASP, ninkwamba ziwa hilo limegusa nchi tatu, Malawi, Mozambique na Tanzania.

Kulingana na ramani hiyo, kwenye nchi za Malawi na Tanzania, mpaka umepita kwenye ufukwe upande wa TZ. Lakini unapoambaa na mpaka huo mpaka nchini Mozambique, unagundua kwamba mpaka unarudi katikati ya ziwa, hapo mimi ndio sijaelewa aisee!!

Kwamba, kati ya Malawi na TZ mpaka upo ufukweni kwetu, ila kati ya Malawi na Mozambique mpaka upo katikati ya ziwa, inakuwaje hapo?

Pia ukiangalia mipaka kwenye maziwa mengine yanayounganisha nchi na nchi, mipaka inakuwa katikati ya ziwa!

Sasa kwanini kipande cha Tanzania na Malawi mpaka uwe ufukweni TZ ila kipande cha Malawi na Mozambique mpaka uwe katikati kama maziwa meng

Upo sahihi.
Ila nafikiri maridhiano ya mipaka yalifanyika kati ya serikali ya wakoloni wa kiingereza (Malawi) na kireno (Msumbiji).

Wakati wanaelekea kutaka kuridhiana kati ya Uingereza (Malawi) na Germany (Tanganyika), WWI ikawa imetokea na baadaye Malawi na Tanganyika zote zikawa chini ya UK, huku mpaka wa mwanzo uliotambulika na Heligolqnd treaty ukiwa haujabadilika. Ni mpaka huo ndio uliendelea kurithishwa kwenye mataifa huru na ndio unaofuatwa na google.

Ni ukweli unaouma.

Kimantiki kila mtu anatamani mpaka uwe katikati.
Katika Mipaka ya Holigoland treaty Rwanda na Burundi pamoja rasi ya Cabo Delgado zipo ndani ya Tanganyika. Kwa hiyo tuanze kudai hayo maeneo yetu yarudi ndani ya Tanganyika siyo?
 
Mkuu tunaweza kupata hiyo makala ya MH Hamza Johari
Duh, huu ni mtihani zaidi ya miaka 10 imeshapita. Ni ya mwaka 2013 iliandikwa baada ya Fatuma Karume kuilisha matango pori jamii ya Watanzania akisema kwamba mpaka ni pembeni ya Ziwa akimaanisha Ziwa lote ni mali ya Malawi.
 
Malawi ilishindwa sababu ni banana republic, siku wakipata serikali inayoeleweka hii kesi wanashinda na tunalazimika kuingia makubaliano mapya na compromise.

Status itabaki hivi endapo Nyasa hamna gesi au mafuta, siku zimetokea malighafi humo tutabishana. Ikitokea ni maji tu basi wanaweza ruhusu tutumie au tuvue samaki.

Na kisheria za kimataifa, ni marufuku kuzuia chanzo cha asili cha maji kisielekee nchi nyingine. That's an act of war.

Nigeria kwenye Niger Delta wana mabwawa ya umeme kama Kainji ambayo maji yake yanatokea nchini Niger. Nigeria ililazimika kuipa umeme Niger ili nayo isijenge bwawa kwake ambalo litazuia maji. Kwenye HEP station angalau mtazozana, sasa kwenye hamna eti Tz tuzuie maji yasiende Nyasa sijui yakalete mafuriko wapi lazima kimataifa tuonekane na makosa makubwa.

Upo sawa kabisa, sipo aware sana na international laws lakini najua fika hizo claims za malawi kuchukua ziwa nyasa zina contradiction kuanzia kwenye mkataba wa mwanzo ambao hakufuata makubaliano ya mgawanyo wa mipaka,

The same system and laws ambazo zinatumika leo hii kutafsiri mipaka ya nchi kiasi kwamba malawi kuchukua ziwa zima itakuwa ni exceptional case ambayo imetengenezwa katika udhaifu wa makubaliano ya mwanzo yasiyojali welfare au hata cultural distinctions za wakazi husika.

Upo sawa kisheria lakini malawi akipewa Ziwa usidhani kutakuwa kuna diplomatic relations nzuri and actual war haitoepukika, unless malawi ipate akili ya kutoa ushirikiano kwenye matumizi ya Ziwa ambayo nayo ni kazi kubwa.

Kuhusu kuzuia maji kuna njia nyingi ikiwemo hiyo dam kwa sababu unajua fika bwawa la Nyerere limeleta impact gani haswa kwenye drainage system nzima. Kwa hiyo Tanzania iliyojipiga kifua kutumia maji ya Ziwa Victoria ndio hiyo hiyo itatumia maji yake itakavyoona inafaa
 
Mazungumzo baina ya Tanzania na Malawi yafanyike. Au status quo ibaki hivihivi tunatumia bila shida wala ugomvi.

Ila Tanzania kulazimisha au kujiaminisha ziwa nusu liwe lake kisheria haiko na back up. Maana Malawi wala Tanganyika sio zilizogawa mipaka. Hata Kenya wangependa kuwa na eneo kubwa la ziwa Victoria ila waliambulia kaeneo kadogo 6%, Uganda 43% wakati Tanzania ina nusu nzima 51%.

Sasa Kenya waje hapa walazimishe ziwa ligawanywe kwa 33% kwa nchi tatu itakuwaje?

Ziwa Tanganyika 45% Congo, 41% Tanzania, 8% Burundi na 6% Zambia. Zambia na Burundi nazo zilalamike zitake mgawo sawa?

Tanzania kuna sehemu nyingi imependelewa kuliko kupunjwa. Thats life huwezi pata kila kitu.
Sawa ila kunamaeneo mengine kutokana na mpaka wa ki-ardhi nadhani umefanya Tanzania kuchukua eneo kubwa kiasi kwenye maziwa

Mfano muundo wa ziwa Tanganyika na nchi zilizoizunga hilo ziwa kutokana namipaka mama ya kiardhi imefanya Zambia na Burundi kupata asilimia ndogo pia Kwa Kenya mpaka wa ardhi umenyima umiliki wakupata asilimia kubwa na hivyo hivyo Tanzania pia ingepata asilimia ndogo kwenye ziwa Nyasa kutokana na mpaka wa ardhi.

Ila tukisema tubaki hivi hivi kuwa mpaka wa ziwa Nyasa huishie pwani ya Tanzania lakini tulitumie ziwa hilo pasipo kutanabaisha mipaka hapo tunakuwa tunawasikilizia Wamalawi kuamua upepo wamatumizi ya ziwa uende vipi nahisi kama tutakuwa watumwa hivi na wanyonge kwenye maamuzi.

Mimi naona mipaka inayohusu maji tukiichukulia kuanzia kwenye mipaka ya ardhi tukafanyia makadirio ya kuiingiza kwenye ziwa au mto unagusa nchi zaidi ya moja,tunaweza tukaitatua migogoro tukandoe vinyongo.
 
Siyo wanyasa tu.. Kuna Wanyakyusa wa Malawi na Wanyakyusa wa Tanzania...
Kuanzia Songwe, Iponga,Kaporo, Pusi, Mwanitete, Ngerenge,pote huko wanaoishi ni Wanyakyusa tu....,siyo Wanyakyusa wahamiaji,ni Wanyakyusa ambao walikuwe kabla hata ya uhuru wa Malawi na Tanganyika.
Na Wangoni pia wapi pande zote za Tanzania na Malawi.
 
Tatizo ni wazungu kwenye heligoland treaty ndo walifuta huo mpk ambao walisema malawi wachukue jurisdiction ya ziwa lote ambapo mwaka 1967 ndo ugomvi ulianza wakashindwa kupatana ila ugomvi ulipamba moto 2012 malawi walivyoanza uchimbaji wa mafuta ambapo serikali ya Tanzania wakasema isitishwe mpk ugomvi uishe wangekuwa na busara wangekubaliana ila sasa ziwa lina faida sana ndo.maana ugomvi ila kwa mozambique hawana ugomvi walieka border 1954 katika mkataba wa uingereza na wareno.
Cha kuongezea ziwa likiwa malawi.linaitwa lake malawi,tanzania.lake nyasa na likiwa msumbiji linaitwa lake niassa
 
Serikali ya Tanzania imetoa tamko la marufuku ya kuzuia matumizi ya google map yenye kuonyesha mpaka wa Tanzania na Malawi kwenye ziwa Nyasa ulipo kutumika kufundishia mashuleni. Kwenye ramani hiyo ya google inaonyesha mpaka wa kisheria uko pwani ya Ziwa Nyasa upande wa Tanzania na hapo hapo kuonyesha mpaka ambao Tanzania inadai ambao uko katikati ya Ziwa Nyasa. Kimsingi google map wako sahihi kwa 100%. Huo ndio ukweli ambao umekuwepo siku zote kabla hata ya kupata Uhuru na baada ya kupata uhuru.

Mpaka leo hii Tanzania tunadai kupata haki ya kumiliki karibu nusu ya Ziwa Nyasa lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa Malawi bado wana umiliki wa Ziwa Nyasa lote katika mpaka wake na Tanzania. Ni ukweli mchungu dhidi ya Tanzania na ukweli usio wa haki. Lakini ndio ukweli halisi. Tuna haki ya kudai ubadilishwe lakini hatuna haki ya kuupotosha.

Zama za kuwadanganya watu kielimu na kuwatisha wasijifunze kujua nini dunia inasema na kutambua (tofauti na vile walivyoaminishwa awali) kuhusu jeografia, historia na sayansi zimepitwa na wakati.
Mbona hujatoa/onyesha uthibitisho wa hoja yako? lete chanzo/support cha hoja yako na siyo maneno yako tu.
 
U
Serikali ya Tanzania imetoa tamko la marufuku ya kuzuia matumizi ya google map yenye kuonyesha mpaka wa Tanzania na Malawi kwenye ziwa Nyasa ulipo kutumika kufundishia mashuleni. Kwenye ramani hiyo ya google inaonyesha mpaka wa kisheria uko pwani ya Ziwa Nyasa upande wa Tanzania na hapo hapo kuonyesha mpaka ambao Tanzania inadai ambao uko katikati ya Ziwa Nyasa. Kimsingi google map wako sahihi kwa 100%. Huo ndio ukweli ambao umekuwepo siku zote kabla hata ya kupata Uhuru na baada ya kupata uhuru.

Mpaka leo hii Tanzania tunadai kupata haki ya kumiliki karibu nusu ya Ziwa Nyasa lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa Malawi bado wana umiliki wa Ziwa Nyasa lote katika mpaka wake na Tanzania. Ni ukweli mchungu dhidi ya Tanzania na ukweli usio wa haki. Lakini ndio ukweli halisi. Tuna haki ya kudai ubadilishwe lakini hatuna haki ya kuupotosha.

Zama za kuwadanganya watu kielimu na kuwatisha wasijifunze kujua nini dunia inasema na kutambua (tofauti na vile walivyoaminishwa awali) kuhusu jeografia, historia na sayansi zimepitwa na wakati.
Mipaka yote ya bara la Afrika iliwekwa na wakoloni, na hiyo ndio tuliweza kurithi baada ya uhuru na sheria za UN zinatamka wazi, mipaka ya kikoloni ya kisheria ndio mipaka rasmi baada ya uhuru. Mpaka wa kikoloni unatamka wazi kuwa Ziwa Nyasa lote ni mali ya Malawi japokuwa lilikuwa linapakana na nchi tatu (Malawi, Tanzania, Msumbiji), leo hii Msumbiji ana umiliki pia wa sehemu ya ziwa Nyasa baada ya kuridhiana na Malawi kumpa sehemu ya ardhi yake yenye milima ili yeye (Msumbiji) apate sehemu ya ziwa hivyo mpaka wa Malawi na Msumbiji ukabadilishwa kisheria. Tanzania tumekataa kuridhiana na Malawi ili nasi tupate sehemu ya ziwa kisheria.

Hoja ya Tanzania ni moja tu, mkataba wa kikoloni ulioipa Malawi umiliki wote wa Ziwa haukuwa wa haki, hivyo haupaswi kurithiwa, upigwe chini. Hayo sasa ndio mambo ya kisheria, siku moja tutajadili upya hapa JF japokuwa ilishajadiliwa sana humu.
Universal law inasema " mpaka wa kwenye maji ziwani ni KATIKATI ya ziwa husika.
 
Hakuna nchi inayojimilikisha. Nani alikupa mipaka ya Tanganyika unayotumia leo, nani alikupa 51% ya ziwa Victoria na akawapa Kenya 6%?
Huyohuyo ndio aliipa Malawi ziwa lote.

Ukisema wanajimilikisha basi na Kenya iseme tunajimilikisha mlima Kilimanjaro na Uganda iseme tunajimilikisha bandari nyingi wakati yenyewe haina.
Mlima Kilimanjaro ni ardhi hiyo sio maji

Ila tukisema tufumue mipaka mpaka ya ardhi mambo yatakuwa mengi na itabidi tufuate makabila yaliyo mipakani ya nayo ingia nchi zaidi ya moja ili yakae kwenye nchi moja,maana hapo tutakuwa hatuitaki kabisa mipaka ya kikoloni tutakuwa tunaitakamipaka yetu sisi wenyewe tutayoiweka.
 
Ukweli usemwe na sio kupotoshwa.
Ziwa Nyasa ni mali ya Malawi kisheria, Tanzania mpaka leo tunaendelea kudai haki ya kudhurumiwa kupata sehemu ya ziwa. Hicho ndio google map wamefanya.
Toa sababu za msingi za kisheria kuonyesha mpaka ulioonyeshwa na Google map ni sahihi kuliko ule ulioonyeshwa na JMT.
 
Mtu sahihi alikuwa Nyerere (kwa sababu alikuwa na ushawishi), na labda Kikwete (alikuwa ni mwanadiplomasia mzuri), tofauti na hapo tupate rais mwenye kujua sheria za kimataifa vizuri (hapa nadhani Lissu atatufaa zaidi). Magufuli angeishia kutumia nguvu (jeshi), Ziwa tungelipata lakini tungeshindwa kulitumia, lingeishia kuwa kambi ya wanajeshi wa majini.
Ni kweli kabisa ila hapo mwishoni nitakupinga sasa una train navy kwa ajili ya air force??
 
Mazungumzo baina ya Tanzania na Malawi yafanyike. Au status quo ibaki hivihivi tunatumia bila shida wala ugomvi.

Ila Tanzania kulazimisha au kujiaminisha ziwa nusu liwe lake kisheria haiko na back up. Maana Malawi wala Tanganyika sio zilizogawa mipaka. Hata Kenya wangependa kuwa na eneo kubwa la ziwa Victoria ila waliambulia kaeneo kadogo 6%, Uganda 43% wakati Tanzania ina nusu nzima 51%.

Sasa Kenya waje hapa walazimishe ziwa ligawanywe kwa 33% kwa nchi tatu itakuwaje?

Ziwa Tanganyika 45% Congo, 41% Tanzania, 8% Burundi na 6% Zambia. Zambia na Burundi nazo zilalamike zitake mgawo sawa?

Tanzania kuna sehemu nyingi imependelewa kuliko kupunjwa. Thats life huwezi pata kila kitu.
Mnavyobwabwaja huku kama vile nyie ndo mmepewa mamlaka na Mungu ya kuamuliwa wazawa walikuwa wakitumia hayo maji tangu Asili
 
Serikali ya Tanzania imetoa tamko la marufuku ya kuzuia matumizi ya google map yenye kuonyesha mpaka wa Tanzania na Malawi kwenye ziwa Nyasa ulipo kutumika kufundishia mashuleni. Kwenye ramani hiyo ya google inaonyesha mpaka wa kisheria uko pwani ya Ziwa Nyasa upande wa Tanzania na hapo hapo kuonyesha mpaka ambao Tanzania inadai ambao uko katikati ya Ziwa Nyasa. Kimsingi google map wako sahihi kwa 100%. Huo ndio ukweli ambao umekuwepo siku zote kabla hata ya kupata Uhuru na baada ya kupata uhuru.

Mpaka leo hii Tanzania tunadai kupata haki ya kumiliki karibu nusu ya Ziwa Nyasa lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa Malawi bado wana umiliki wa Ziwa Nyasa lote katika mpaka wake na Tanzania. Ni ukweli mchungu dhidi ya Tanzania na ukweli usio wa haki. Lakini ndio ukweli halisi. Tuna haki ya kudai ubadilishwe lakini hatuna haki ya kuupotosha.

Zama za kuwadanganya watu kielimu na kuwatisha wasijifunze kujua nini dunia inasema na kutambua (tofauti na vile walivyoaminishwa awali) kuhusu jeografia, historia na sayansi zimepitwa na wakati.
Wewe ni Mjinga wa mwisho Popoma mkubwa, usiyejitambua.

Sheria za kimataifa, International territorial water,b

When countries separated with water bodies, mpaka wake ni katikati.

Kwa sababu maji ni uhai!!, kama akili zako za kuvukia barabara zingetosha ungejiuliza kwanini ziwa nyasa upande wa msumbiji
Unajua kwamba OAU walikubaliana kuwa mipaka ya kikoloni ndio iendelee kutumika baada ya uhuru?

Yani unataka kusema kwamba nchi za Afrika tuna busara sana kwahiyo tuanze kuchora upya mipaka. Unazijua akili za Mwafrika kweli mkuu?

Yani turudie kuchora, Uganda wapendekeze kupata Kagera salient, Kenya wapendekeze kupata mlima Kilimanjaro pale ambapo ramani ilipindishwa ili mlima uwe Tanzania, Zanzibar wadai pwani ya bara maana kuna Sultan aliwahi sema anaimiliki na akiwapa Wajerumani sijui, Tanzania tudai sehemu ya Masai Mara ya Kenya ili Wamasai wote wawe Tanzania, Kenya wapendekeze waongezewe sehemu ya ziwa Victoria wawe nayo nyingi maana Tanzania imechukua kipande kikubwa zaidi, Burundi nao waombe sehemu kubwa zaidi ya ziwa Tanganyika. Hapo ni sisi tu, bado sehemu nyingine za Afrika.

Kiuhalisia ukisoma Helligoland treaty na mkataba mwingine, hakuna ushahidi unaoonyesha Tanzania tunamiliki nusu ya ziwa Nyasa. Hata Wajerumani waliokuwa wanatawaka Tanganyika ramani yao inaonyesha Nyasa nzima ni ya Malawi.

Sisi Tanzania tunakuwa na claim kuwa wazungu walikubaliana kama kuna chanzo cha maji mpakani basi kigawanywe kila nchi inayopakana ipate kiasi chake. But that wasn't the case kwa ziwa Nyasa. Tukienda mahakama ya usuluhishi, zikaletwa mikataba na mashahidi wakoloni Tanzania tunashindwa asubuhi na mapema kabisa.
Wewe unafikiri KIJINGA!! wakati wa kuabudu Sheria za wakoloni zimepita!!


Unafikiri Ethiopia ni wajinga waliojenga Hydro Electric power kubwa sana, kwa maji ya mto Nile??
Angetaka kufuata Sheria za wakoloni kwa ajili ya Matumizi ya maji ya moto Nile unafikiri angejenga???

Lowasa alikuwa Mjinga alipofanya project kubwa ya maji Toka ziwa Victoria to KAHAMA??? alipokuwa waziri wa maji?

think big, acha kuabudu Sheria za mizimu ya kikoloni!
 
Hivi Nyerere alipopewa nchi na Waingereza mwaka 1961 hawakumpa documents zinazoonyesha mipaka ya nchi wanayompa? Maana Tz imepata uhuru 1961. Malawi 1964. Wakati wanatupa uhuru walitupa nchi gani? Maana kesho Zanzibar watadai km 16 za pwani ya Tz. Pengine ndiyo anachotaka ASP😂
 
Back
Top Bottom