Utatambuaje timu zinazocheza kwenye league ya Serie A

BANDOKITITA

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2022
Posts
1,484
Reaction score
2,852
Nimekuwa napata shida sana kutambua timu zinapokuwa zinacheza kwenye hii League ya Serie A hasa ukiwa haujui wachezaji wa timu hizo na km hautaona line-up. Tumezoea kutambua timu kwa rangi zao kwenye runinga kwa juu kushoto lakini hawa jamaa hizo rangi za kutofautisha hazipo, ni rangi moja tu ya blue.

Mwenye kujua jinsi ya kuzitambua anisaidie. Mfano hapa utajuaj hii ni NAPOLI na hii ni JUVENTUS
 
Mkuu ukiwa mtu wa mpira hata uamshwe usiku wa matisa uonyeshwe hiyo screenshot unajua hizo ni timu gani
 
Yenye wachezaji vipara wawili na rasi rasi wengi ni napoli
 
Hiyo dosari nilishaiona hata mimi kwa Seria A. Kwenye ligi nyingine wanaweka rangi kwenye kila upande wa matokeo katika timu
 
Mkuu ukiwa mtu wa mpira hata uamshwe usiku wa matisa uonyeshwe hiyo screenshot unajua hizo ni timu gani
Hamaanishi vifupisho vya majina. Anamaanisha ligi zingine wanatofautisha kwa rangi ya jezi walizo vaa wachezaji siku hiyo kwa kuweka rangi hizo chini ya maneno au maneno yenyewd yanakuwa rangi tofauti au maneno yanazungukwa na rangi tofauti ili hata kama sio mtu wa mpira unatambua kwa urahisi.

HUU NI UDHAIFU WA SERIE A. wabadilike

 
Kwenye scoreboard hapo juu kawaida timu iliyopo upande wa kushoto ni home timu

Kuhusu kuyatambua majina ya timu husika unapaswa kuwa mkamaria mashuhuri.
Sisi wakamaria tumekariri majina ya timu karibia zote Duniani 😂
 
Chini ya ayo majina kuna vidoti vina rangi rangi, izo ndoo jezi walizo vaa.

Au angalia anaepoteza muda uwanjani ndio mshindi.
Hivyo vidoti doti sio alama ya jezi. Jana Juve walivaa jezi ya rangi nyeupe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…