Utatu wa Dkt. Magufuli, Eng. Kijazi na Eng. Mfugale katika ujenzi wa barabara nchi nzima tutaukumbuka milele

Magufuli alikuwa mbinafsi sana, kila kitu akivutia kwake. waliopo tofauti ni ndogo, na kuzima mwenye chato unaenda kutangazwa rasmi kuwa mkoa.
 

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni jamaa wamefanya kazi nzuri sana ya usimamizi wa matumizi ya kodi za wananchi
 
We JPM alikuwa ni habari nyingine, miradi mingi ilikuwa inajengwa kwa pamoja ukijumuisha miradi mikubwa Kama Sgr na Bwawa la umeme. Barabara kila wilaya, masoko ya kisasa mikoa yote, stendi mikoa yote, vituo vya afya zaidi ya 400, zahanati zaidi ya 800, hospitali za wilaya zaidi ya 70, Hospitali za kanda 3, ujenzi wa meli mpya ziwa Victoria na ziwa Nyasa. Madaraja makubwa Kama Ubungo interchange, daraja la Salender na daraja la Busisi. Miradi ya maji mfano mradi wa maji toka ziwa Victoria kwenda Tabora. Kuhamisha makao makuu ya serikali na wizara zake kwenda Dodoma ndani ya mwaka 1.

JPM alikuwa genius katika utekelezaji wa miradi, katika miaka mitano amefanya mengi kuzidi awamu yeyote ya watangulizi wake. Tumseme kwa mengine lakini siyo swala la miradi.

Sent from my itel W6004 using JamiiForums mobile app
 
Unajua DINI la TAIFA hadi anakufa lilikuwa limefika kiasi gani? na alilikuta kiasi gani?na hiyo MIRADI yote mikubwa unayo msifia kaiwacha ktk stage gani au asilimia ngapi imefika ?

Na kuhakikishia angekuwapo HAI na angemaliza vipinde vyake viwili TANZANIA [emoji1241] inge Collapse completely ktk zana nzima ya UCHUMI na alikuwa hana intention yeyote ya kuachia MADARAKA watu wenye akili walishaliona alikuwa ana philosophy zilizopitwa na wakati.
 
Dah nafikiria kwa kina sana juu ya ubishani wa nani kafanya mini kumzidi nani na mwishowe naomba niseme kila mtu aheshimiwe kwa kile alichokitenda katika Awamu yake na Itoshe kusema Shukrani kwa yote mazuri waliyotufanyia hawa viongozi wetu.

Kila mmoja ametumia uwezo wake kadri alivyoweza kuleta maendeleo kwa hii nchi. Tusibishane kwamba nani hakufanya pakubwa nani pakubwa sio tija kwa sasa ila Cha Msingi zaidi ndugu zangu tujitahidi kuchagua Viongozi wenye Upeo Mkubwa wenye Maono na Utashi wa kuleta maendeleo thabiti kwa nchi yetu maana bado tuko nyuma sana kimaendeleo ukilinganisha na Umri wa nchi yetu toka tupate Uhuru.
 
Mpuuzi wewe,uwe una adabu wakati unamtetea huyo mtu wako.
 
Unauliza miradi imefikia asilimia ngapi?!! Upo Tanzania hii kweli? Ukiacha miradi 2 ya muda mrefu (Sgr na bwawa la umeme) miradi mingi ilikuwa aidha imekamilika au inaelekea kukamilika.

JPM alikuwa na nia njema ya kujenga nchi, hata Kama alikopa lakini kulikuwa na uhakika wa kurejesha mikopo hiyo kwa sababu aliwekeza kwenye miudo mbinu ambayo ingesisimua ukuaji wa uchumi. Awamu zilizopita mikopo haikuwa na tija hatukuona matokeo kwa sababu pesa ziliishia mifukoni mwa wajanja wachache.

Nikwambie ukweli Watanzania wengi walitamani aongezewe muda wa kuiongoza Tanzania baada ya muda wake kuisha. Ni watu wachache tu (Mafisadi na wapiga dili) walihofia hilo.


Sent from my itel W6004 using JamiiForums mobile app
 
Na Mungu amesikia kilio cha Watanzania sasa atakuwa Rais wa milele.
 
Na Mungu amesikia kilio cha Watanzania sasa atakuwa Rais wa milele.
Legacy yake itadumu milele, JPM hatunaye kimwili lakini ameacha ametengeneza akina JPM wengi Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Tutaenzi yote mazuri Kama hulka yake ya kusema ukweli na kutokuwa mnafiki, uwezo wa kufanya maamuzi na kuyasimamia bila kuyumba, uwezo wake wa kuchapa kazi usiku na mchana, uzalendo katika kusimamia rasimali za nchi na kupambana na ufisadi na rushwa.

Sent from my itel W6004 using JamiiForums mobile app
 
Mpuuzi wewe,uwe una adabu wakati unamtetea huyo mtu wako.
Limekugonga utosini jiwe...Pole! Acha hasiara Tanzania ni ya watanzania siyo ya makundi fulani. Mwelewe Mh. Rais yeye hana hizo tabia kutwa kucha kumchonganisha kwasababu zenu binafsi!
 
Walitoa pesa zao mifukoni??

Nitajie yoyote kati yao aliyekua kajipunguzia hata msahara wao kwa walau laki moja kutoka kwa watangulizi wao!

Kama hakuna just zip your mouth.
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Basi!
 
Trio Majes, hatunao.
Ujenzi wa barabara ulipata kasi kuanzia utawala wa Raisi Mkapa, na ukakolezwa moto wakati wa Raisi Kikwete. Trio Majes walikuwepo awamu zote hizo.
Japo wamesimamia ujenzi wa barabara nyingi je zinakidhi viwango?
 
Trio Majes, hatunao.
Ujenzi wa barabara ulipata kasi kuanzia utawala wa Raisi Mkapa, na ukakolezwa moto wakati wa Raisi Kikwete. Trio Majes walikuwepo awamu zote hizo.
Japo wamesimamia ujenzi wa barabara nyingi je zinakidhi viwango?
Nyingi za awamu ya tano ziko kwenye ubora wa kuaminika. Hazikuchakachuliwa. Angalia Moroco Mwenge na bamaga Shekilango.
 
Barabara ya Jet corner hadi Davis corner na ile ya kutoka Mbezi hadi Goba zote zilijengwa wakati wa Kikwete tafuteni barabara nyingine alizojenga sio kumpa sifa za mwingine.
Eneo kubwa la barabara ulizosema zimejengwa kuanzia wakati hao wote wakiwa wizara ya Ujenzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…