UTAWALA kimajimbo una faida/madhara gani. Tuchambue ili watu waelewe

UTAWALA kimajimbo una faida/madhara gani. Tuchambue ili watu waelewe

Unafaida nyingi kuliko hasara ,yaani kuchimba Choo cha shule tusubiri amri ya mtu aliyeko MSOGA!!
Kenya na Nigeria bado hawajamaliza kuchimba machimo ya Choo japo wana hizo Serikali za Majimbo

Kenya wanapambana kutafuta mishahara ya walimu na Madaktari kila mwisho wa mwezi na wanauana kwa Ukabila mama ilivyo Nigeria

sie tunazo Halmashauri na zina autonomy kwa kiwango kikubwa sana cha kutekeleza inachoteleleza

Tutajieni hizo Nchi ukiacha Marekani zilizofanikiwa kwa kuongeza idadi ya vyeo
 
Hivi unajua kila jimbo nalo linakuwa na bunge lake dogo,
Ndio madiwani hao hao kata zinapunguzwa tu na majimbo yanapungua. Kuliko sahivi tuna bunge kubwa Bado baraza la wawakilishi Bado baraza la madiwani so unakuta gharama ni kubwa zaidi.
 
Hatuhitaji majimbo ..Sisi tuweke mabaraza ya Maendeleo kila manispaa na tuyape nguvu ya kuajiri na kufukuza wakurugenzi Tu na watu wao...the rest will be history...
Sio rahisi kiivo km unavyochukulia
 
Mzee huu mfumo una faida sana ila kwa Afrika hii hautufai kabisa, najua wanasiasa wanaupigia chapuo sababu utaongeza nafasi nyingi sana za kuchaguliwa lakini gharana kubwa ya uendeshaji itakuwa mara mbili yake. Nadhani unajua wazi wale jamaa miposho yao na mahitaji yao mengine kupitia kodi, fikiria sasa wakizidi zaidi kila jimbo wapo. Ni matumizi kiasi gani?

Achilia mbali hayo machafuko kupitia ubinafsi ambao umewajaa wengi sana kwa kutaka kuimarisha ngome zao za kisiasa na kutaka kuwa na madaraka makubwa. Nakwambia ipo siku utakuja kusikia serikali ya jimbo Morogoro imejitangazia uhuru na inataka itambulike kama nchi
Simple jeshi linabaki serikali kuu majimbo Ni ishu ya kiuchumi tu.

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Kaka Sasa hivi watu wanafikiria kujenga lami mpaka Zanzibar wakati Kuna majimbo shida juubya shida za wananchi hivyo serikali ya mjimbo Mimi naunga mkono hasa kimaamuzi ya maendeleo biashara na uchumi

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
South Africa Ina majimbo 9 na imetuzidi uchumi mara zaidi ya 5
if that is the case, Japan haina majimbo na imeizidi mbali South Africa


Utawala wa majimbo utachochea kuongezeka kwa gharama za uendeshaji wa Nchi kama inavyotokea Kenya pamoja na ku promote u maeneo, Ukanda na ukabila
 
if that is the case, Japan haina majimbo na imeizidi mbali South Africa


Utawala wa majimbo utachochea kuongezeka kwa gharama za uendeshaji wa Nchi kama inavyotokea Kenya pamoja na ku promote u maeneo, Ukanda na ukabila
Nmetolea mfano wa Sauzi sio Japan au US sababu nataka uchumi unaofanana na wa kwetu.

Kenya ilikua na GDP per Capita 1300 kipindi Kaunti ndio zinazinduluwa ila kufikia 2021 GDP per Capita ni 1700 unawezaje kusema uchumi umeporomoka? Mind you COVID iliwaathiri sana coz ya kufunga shughuli za kiuchumi.

Alafu huu ujinga wa kusema gharama ni ajabu sana sahivi tuna DC, DAS, wabunge hata wawili, Mwenyekiti wa halmashauri, wote hao wilaya Moja ila serikali za majimbo zitaondoa DCs, RCs, tunabaki na Meya na Mbunge tu huko juu yupo Governor mmoja kwa mikoa hata 4.

So devolution inapunguza gharama
 
Hatuhitaji majimbo ..Sisi tuweke mabaraza ya Maendeleo kila manispaa na tuyape nguvu ya kuajiri na kufukuza wakurugenzi Tu na watu wao...the rest will be history...
Labda kama wanaotimua wawe sio waTanzania. Unakumbuka baraza la vijana? Tuliambiwa Lita solve changamoto za vijana. Cha ajabu UVCCM ndio wamelihodhi so hakuna mjadala utafanyika bila msimamo wa Dodoma.

So Hilo baraza la maendeleo sio ajabu ukakuta ni president appointees nao wanafanya kazi kwa kuangalia maoni ya Rais. Unless hayo mabaraza yawe na security of tenure kama CAG kwamba hawatumbuliki.
 
Jamani, mimi binafsi naanza kuafiki idea ya chadema ya utawala wa kimajimbo.
Inaweza kuforce maendeleo Kwa kasi sana kulingana na ukubwa wa inchi yetu.
Lakini nimekutana na pingamizi, hacha wanaccm hawaafikiani na utawala huu.
Please tujadili faida na madhara yake humu, NAWASILISHA
bado hujajifunza kutoka kwa mwendazake?
 
Umefanya ulinganishi na wapi? Manake hili sio suala dogo ibrah, kama inavyoonekana, unavyolichukulia.

Kwa hayo majibu yako, unasema watu hawako organised......hiyo siyo kweli. Tanzania tunaanza kuwa organised kutoka nyumba kumikumi, haya nitajie Nchi yenye majimbo iliyokuwa organised kutoka nyumba kumikumi na kuridhiwa na Serikali?

Narudia, umefanya ulinganishi na wapi? ili niweze kujadili hizo faida za "forced' Development kama ulivyowasilisha.
A: Katika mfumo huu, kutakuwa na;

1. Serikali kuu (Central Government).

2. Serikali za majimbo (Profince/States Government)..

===Serikali za Majimbo zitakuwa na mamlaka kamili katika baadhi ya mambo kwa kadiri itakavyokubaliwa na kuanishwa na katiba..

===Muhimu ni kuwa, serikali za majimbo zinapaswa kuachwa na kupewa mamlaka kamili ya kikatiba kujiamulia na kujisimamia zenyewe juu ya shughuli za maendeleo yao na kuweka/kujichagulia viongozi wao..

===================================

✓ On the other hand, ukitazama kwa makini ni kuwa, sera ya utawala wa majimbo ya CHADEMA haina tofauti na sera ya utawala ya CCM inayotumika sasa chini ya mfumo wa serikali za mitaa (local governments).

✓ Na dhana ya serikali za mitaa maana yake ni kuwa na serikali za mitaa zenye mamlaka kamili ya kujiamulia mambo yao kwa 100%

✓ Kasoro kubwa iliyopo kwa mfumo huu uliopo sasa chini ya CCM ni kuwa, serikali hizi za mitaa chini ya mwavuli wa vijiji/mtaa, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa ni kukosa mamlaka ya kujiamulia mambo ya maendeleo yao na namna ya kujichagulia viongozi wao

===================================

✓ Ziko nchi nyingi zinazotumia mfumo huu wa utawala Afrika na duniani kote kwingine...

✓ Kwa Afrika ziko nchi kama Kenya, Africa Kusini, Nigeria, Swaziland, Lesotho, Namibia nk nk..

✓ Huko ktk Dunia nyingine ziko nchi kama Marekani, Ubelgiji, Uingreza, China, Japan nk nk
 
Labda kama wanaotimua wawe sio waTanzania. Unakumbuka baraza la vijana? Tuliambiwa Lita solve changamoto za vijana. Cha ajabu UVCCM ndio wamelihodhi so hakuna mjadala utafanyika bila msimamo wa Dodoma.

So Hilo baraza la maendeleo sio ajabu ukakuta ni president appointees nao wanafanya kazi kwa kuangalia maoni ya Rais. Unless hayo mabaraza yawe na security of tenure kama CAG kwamba hawatumbuliki.
Actually kama Rais ana akili utapata mabaraza independent...yataondoa kabisa mzigo Kwa Rais wa kufukuza na kuangalia Mkurugenzi yupi kaiba hela ... wananchi wenyewe wataaajir ..sifa zitakuwepo ..watafata miongozo na kuajiri wanaemtaka na kumfukuza wakiamua
 
Hapa ndio pazuri yaan ataeiba Mali za Jimbo tunamalizana nae wenyewe sisi wananchi ndio tunasimama mahakamani tukishindwa mahakamani tutajua cha kumfanya

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Katika mfumo huu, kutakuwa na;
Natumaini Umejaa Uzima.
Mkuu Tele hujajibu maswali yangu. Naomba ulitafakari hilo kwani yalikuwa ni maswali ya Makusudi.

Hatahivyo nitakujibu hivi...

Kwanza;
Nataka niamini kuwa unazungumzia mfumo ulioridhiwa na CHADEMA na kuwa mfumo huo ndio utakaotumiwa na CHADEMA pindi wakishika DOLA au tutakuwa tunajadiliana hewa. Pata potea. na Upotoshaji mkubwa. Tusijikite kwenye upotoshaji wa suala hili kwa manufaa mafupi ya hapa Jamvini, bali kwa mustakabhali wa Nchi.
 
1. Serikali kuu (Central Government).
Sawa Serikali Kuu itakuwa imewakilishwa. Itakuwa na wajibu upi...Unafikiri CHADEMA Wanataka Wajibu wa Serikali kuu uwe na mamalaka gani na Kwa vyombo vipi?
Mfano-Mahakama, Ulinzi, na Mambo ya Nje?
 
2. Serikali za majimbo (Profince/States Government)..
Provincial Governments zipo, tatizo? Mamlaka?👇
Muhimu ni kuwa, serikali za majimbo zinapaswa kuachwa na kupewa mamlaka kamili ya kikatiba kujiamulia na kujisimamia zenyewe juu ya shughuli za maendeleo yao na kuweka/kujichagulia vi
Mbona Wananchi wanajichagulia Madiwani? Mbona Wananchi wanajichagulia wabunge hali kadhalika Wajumbe wa Nyumba kumikumi...n.k n.k.

serikali za mitaa zenye mamlaka kamili ya kujiamulia mambo yao kwa 100%
Kuna mfano wowote ule wa majimbo (nchi yeyote ile)yenye mamlaka yao kujiamlia 100% Je hii ndiyo CHADEMA wanachotaka au ni matamanio yako?

Kasoro kubwa iliyopo kwa mfumo huu uliopo sasa chini ya CCM ni kuwa, serikali hizi za mitaa chini ya mwavuli wa vijiji/mtaa, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa ni kukosa mamlaka ya kujiamulia mambo ya maendeleo yao na namna ya kujichagulia viongozi wao
Aha, kama kweli CHADEMA wanaafiki ninanukuu
utawala wa majimbo ya CHADEMA haina tofauti na sera ya utawala ya CCM inayotumika sasa chini ya mfumo wa serikali za mitaa (local governments).
....huoni tatizo ni la kisheria au kikaanuni tu? Majimbo ya nini kama Sheria au Kanuni zinaweza tatuta kasoro za kujiamlia n.k?
 
Back
Top Bottom