Utawala wa Rais Samia tuupime kwa vigezo sawia

Utawala wa Rais Samia tuupime kwa vigezo sawia

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Bila ya kuwa na chuki na mtu yeyote, ukweli ni kwamba Mama Samia ana bahati kubwa kwenye utawala wake.

Bahati yake kubwa ni utawala uliomtangulia. Utawala uliomtangulia ulikuwa ni utawala wa chuma, ulikuwa ni utawala ulioumiza wengi. Hivyo, yeye akifanya jambo kidogo tu la kuwaletea nafuu wale walioonja machungu ya utawala uliopita, basi pongezi, furaha ja uungwaji mkono unakuwa mkubwa. Lakini laiti kama utawala wa Mama Samia ungefuata baada ya utawala wa Mkapa au Kikwete, sidhani kama angeonekana amefanya makubwa kwa haya ambayo mpaka sasa ameyafanya.

Kwa hiyo tusifurahie sana na kupongeza sana kwa mafanikio au mabadiliko kidogo.

Kiongozi makini hutumia muda mwingi kujenga mifumo imara ya uongozi na usimamizi. A good leader always creates leaders by creating collective leadership.

Kwa sasa tunafurahia sana kuona mbaazi zimezaa sana mwaka huu kwa sababu ya kuwa na mvua za kutosha ilihali hatujawa na mfumo wa kuhakikisha mbaazi zinazaa kila mwaka, kuwe kuna mvua au hakuna mvua.

Mama Samia hata atoe maelekezo mengi ya kuwaletea umafuu wananchi kiasi gani, kama hataenda kwenye msingi wa matatizo yetu, hatakuwa amelisaidia Taifa, naye atapita bila kuacha legacy yoyote ya maana, kama watangulizi wake, ukimwondoa mwanafalsafa Mwalimu Nyerere.

Kuna mambo ya msingi ambayo Rais Samia anatakiwa kuyapa muda mwingi kuliko kwenda kukagua madaraja, hospitali au barabara. Mambo hayo ya msingi:

1) Upatilanaji wa katiba bora yenye kulinda haki za kila mmoja

2) Kuondoa sheria zote gandamizi, na kwa kiasi kikubwa zinazokinzana na hata hii katiba yetu ya sasa

3) Kutengeneza sheria mpya zitakazohakikisha watu wanatendewa haki, na uhuru wao kama raia unalindwa. Kwa sasa, Tanzania unaweza kubambikiwa kesi yoyote wakati wowote, ukakosa dhamana, ukaishia hata jela bila ya kuwa na hatia

4) Kutengeneza mfumo mzuri wa utawala, na kuondokana na utitiri wa vyeo visivyokuwa na maana wala mchango wowote kwa maendeleo ya Taifa. Nafasi kama za wakuu wa Wilaya na mikoa, maRAS na maDAS, ni ufajaji wa pesa za wananchi kwa sababu kazi zao zingeweza kufanywa kwa ufanisi na wakurugenzi, OCD na RPC

5) Kuondoa mfumo wa sasa wa utawala ambao unawafanya watu wengi kujikomba na kujipendekeza kwa Rais ili wapate uteuzi. Nafasi nyingi zitegemee weledi, na ziombwe. Kuwe na chombo cha uteuzi. Rais abakie na watu wachache sana wa kuwateua, hasa kwenye ngazi ya kitaifa.
 
Mkuu umeenda sawa sehemu kubwa na mimi, nilikuwa nasubiri siku 100 rasmi za awali za huyu mama ili nitoe tathmini yangu kwake. Hadi hapa tulipofikia sioni kama mama amejipambanua kwenye upande wa kurekebisha mifumo ya kiutawala, aidha ni yeye hataki, au hajiamini kuingia kwenye upande huo, au washauri wake hasa wa upande wa chama chake, hawako tayari aguse sehemu ambayo wanajua ni ngumu kwa chama chao kuendelea kupata hii free ride ya kisiasa wanayoipata hapa nchini.

Kwa mtazamo wangu hadi sasa, ni kama mama yuko madarakani kuponya maumivu zaidi yaliyopatikana wakati wa mtangulizi wake, kuliko kufanya mageuzi makubwa ya kiutawala. Pia nilichokiona kwa huyu mama hana maono makubwa, bali ni mtu wa kutawala kwa kuangalia upepo zaidi, lakini sitarajii huyu mama kuchukua hatua ya mageuzi makubwa ya mfumo wetu wa kiutawala.
 
Mkuu umeenda sawa sehemu kubwa na mimi, nilikuwa nasubiri siku 100 rasmi za awali za huyu mama ili nitoe tathmini yangu kwake. Hadi hapa tulipofikia sioni kama mama amejipambanua kwenye upande wa kurekebisha mifumo ya kiutawala, aidha ni yeye hataki, au hajiamini kuingia kwenye upande huo, au washauri wake hasa wa upande wa chama chake, hawako tayari aguse sehemu ambayo wanajua ni ngumu kwa chama chao kuendelea kupata hii free ride ya kisiasa wanayoipata hapa nchini.

Kwa mtazamo wangu hadi sasa, ni kama mama yuko madarakani kuponya maumivu zaidi yaliyopatikana wakati wa mtangulizi wake, kuliko kufanya mageuzi makubwa ya kiutawala. Pia nilichokiona kwa huyu mama hana maono makubwa, bali ni mtu wa kutawala kwa kuangalia upepo zaidi, lakini sitarajii huyu mama kuchukua hatua ya mageuzi makubwa ya mfumo wetu wa kiutawala.
Mmenyooka baada ya kuona haendi na matakwa yenu?

Si tukiwambia ile ni ccm mkaendelea kudemka kwamba hoo yule siyo mwenda zake?

Na bado
 
Mmenyooka baada ya kuona haendi na matakwa yenu?

Si tukiwambia ile ni ccm mkaendelea kudemka kwamba hoo yule siyo mwenda zake?

Na bado

Huwa unanichekesha ile mbaya, hisia zako ndio kulazimisha kuwa ni mitazamo yangu. Kimsingi huyo mama hana siasa za kishenzi kama za dhalimu aliyeko motoni, sasa sijui unalazimisha wafanane kwenye angle ipi.
 
Huwa unanichekesha ile mbaya, hisia zako ndio kulazimisha kuwa ni mitazamo yangu. Kimsingi huyo mama hana siasa za kishenzi kama za dhalimu aliyeko motoni, sasa sijui unalazimisha wafanane kwenye angle ipi.
Ongea kilichopo hapa we pumbavu,hata ukimchukia vp jiwe alikua rais hasa.
Hivi nyie mafala mlijuaje kuna JF.
Zamani tunajadili mada haswa hapa zinazoeleweka.
Nyie ngedere sijui mmetoka wapi mnaongea upuuzi tu
 
Ongea kilichopo hapa we pumbavu,hata ukimchukia vp jiwe alikua rais hasa.
Hivi nyie mafala mlijuaje kuna JF.
Zamani tunajadili mada haswa hapa zinazoeleweka.
Nyie ngedere sijui mmetoka wapi mnaongea upuuzi tu

Yaani mtu akimjibu mume wako una panic hivi! Dhalimu alikuwa rais hasa kwako, kwangu alikuwa ni kiongozi muovu na katili kama makatili wengine. Anzisha jukwaa lako muwe mnajadili mambo ya jiwe, na logo ya huo mtandao wako iwe ni kaburi la jiwe, na motto yake iwe ni hapa kazi tu.
 
Kinachowaponza wengi wenu ni kuwa na matumaini makubwa kupitiliza kwa mtu ambaye alikuwa ndio kwanza anafungua ukurasa wa awamu yake, kwa sababu ya zile hotuba zake tamu, binafsi sikutaka hata kusubiri hizo siku 100 baada ya kuona Katiba Mpya imemshinda pale aliposema isubiri kwanza.

Hilo kwangu ndio lilikuwa hitaji la kwanza na la msingi zaidi ya yote, wakati huo mkimshangilia ametumbua msiowapenda na kumpa kila aina ya sifa mpaka mkasahaulika kama nyie ni wapinzani.

Huku mkiwa na matumaini nae makubwa kwa kutaka apewe muda zaidi mkiamini atafanya kila mtakalo, na kuwalaumu wale walioanza kuonesha kutomuamini.

Sasa kwasababu ameanza kwenda kinyume na yale matarajio yenu ya awali, ndio mmeanza kumgeuka, kimsingi mlichokuwa mnakitegemea toka kwa kiongozi wa CCM ilikuwa ni ndoto tu, sasa naona wengi wenu ndio mnaanza kuamka, mnamlaumu mpaka kwa uteuzi wa ma-DC aliofanya kama vile hizo nafasi zimewahi kuwa na manufaa kwa upinzani.
 
Bila ya kuwa na chuki na mtu yeyote, ukweli ni kwamba Mama Samia ana bahati kubwa kwenye utawala wake.

Bahati yake kubwa ni utawala uliomtangulia. Utawala uliomtangulia ulikuwa ni utawala wa chuma, ulikuwa ni utawala ulioumiza wengi. Hivyo, yeye akifanya jambo kidogo tu la kuwaletea nafuu wale walioonja machungu ya utawala uliopita, basi pongezi, furaha ja uungwaji mkono unakuwa mkubwa. Lakini laiti kama utawala wa Mama Samia ungefuata baada ya utawala wa Mkapa au Kikwete, sidhani kama angeonekana amefanya makubwa kwa haya ambayo mpaka sasa ameyafanya.

Kwa hiyo tusifurahie sana na kupongeza sana kwa mafanikio au mabadiliko kidogo.

Kiongozi makini hutumia muda mwingi kujenga mifumo imara ya uongozi na usimamizi. A good leader always creates leaders by creating collective leadership.

Kwa sasa tunafurahia sana kuona mbaazi zimezaa sana mwaka huu kwa sababu ya kuwa na mvua za kutosha ilihali hatujawa na mfumo wa kuhakikisha mbaazi zinazaa kila mwaka, kuwe kuna mvua au hakuna mvua.

Mama Samia hata atoe maelekezo mengi ya kuwaletea umafuu wananchi kiasi gani, kama hataenda kwenye msingi wa matatizo yetu, hatakuwa amelisaidia Taifa, naye atapita bila kuacha legacy yoyote ya maana, kama watangulizi wake, ukimwondoa mwanafalsafa Mwalimu Nyerere.

Kuna mambo ya msingi ambayo Rais Samia anatakiwa kuyapa muda mwingi kuliko kwenda kukagua madaraja, hospitali au barabara. Mambo hayo ya msingi:

1) Upatilanaji wa katiba bora yenye kulinda haki za kila mmoja

2) Kuondoa sheria zote gandamizi, na kwa kiasi kikubwa zinazokinzana na hata hii katiba yetu ya sasa

3) Kutengeneza sheria mpya zitakazohakikisha watu wanatendewa haki, na uhuru wao kama raia unalindwa. Kwa sasa, Tanzania unaweza kubambikiwa kesi yoyote wakati wowote, ukakosa dhamana, ukaishia hata jela bila ya kuwa na hatia

4) Kutengeneza mfumo mzuri wa utawala, na kuondokana na utitiri wa vyeo visivyokuwa na maana wala mchango wowote kwa maendeleo ya Taifa. Nafasi kama za wakuu wa Wilaya na mikoa, maRAS na maDAS, ni ufajaji wa pesa za wananchi kwa sababu kazi zao zingeweza kufanywa kwa ufanisi na wakurugenzi, OCD na RPC

5) Kuondoa mfumo wa sasa wa utawala ambao unawafanya watu wengi kujikomba na kujipendekeza kwa Rais ili wapate uteuzi. Nafasi nyingi zitegemee weledi, na ziombwe. Kuwe na chombo cha uteuzi. Rais abakie na watu wachache sana wa kuwateua, hasa kwenye ngazi ya kitaifa.
Mimi mtu akiongelea katiba hua aiamini chochote maana katiba ni sheria,na watu ni mamilion,ukibadirisha katiba siyo wote wataikubali hata kidogo,kila mtu ana hulka yake,matakwa na mapendekezo anayoona yeye ndiyo sawa kwake,hivyo basi katiba si chochote kukibadirisha labda kukiheshimu kilichopo, waTanzania wengi sana hua wanafuata uvumi tu kama uvumi wa wanasiasa na wana harakati,mTanzania akisikia neno kijiwe kimoja ananyanyuka na hilo neno anaenda nalo kijiwe kingine bila kua na uhakika nalo wala kulithibitisha,swala la katiba kila mTanzania utamsikia anasema katiba haifai,ukimuuliza mtu katiba unataka uweje na ya sasa ina mapungufu gani,yaani mTanzania anayeweza kuelezea hilo ni wachache sana,wengi utamsikia tu anaanza kua mkali na anaanza kukuita wewe ni CCM[emoji16][emoji16]...katiba kuifanya kua nyingine sioni sababu ya msingi maana inaweza kuumiza wengine pia na kisha kuanza kulalamika tu tena maana mi nawajua sana waTanzania.
 
Yaani mtu akimjibu mume wako una panic hivi! Dhalimu alikuwa rais hasa kwako, kwangu alikuwa ni kiongozi muovu na katili kama makatili wengine. Anzisha jukwaa lako muwe mnajadili mambo ya jiwe, na logo ya huo mtandao wako iwe ni kaburi la jiwe, na motto yake iwe ni hapa kazi tu.
We kenge tu unaongea sana bwege wewe
 
Kinachowaponza wengi wenu ni kuwa na matumaini makubwa kupitiliza kwa mtu ambaye alikuwa ndio kwanza anafungua ukurasa wa awamu yake, kwa sababu ya zile hotuba zake tamu, binafsi sikutaka hata kusubiri hizo siku 100 baada ya kuona Katiba Mpya imemshinda pale aliposema isubiri kwanza.

Hilo kwangu ndio lilikuwa hitaji la kwanza na la msingi zaidi ya yote, wakati huo mkimshangilia ametumbua msiowapenda na kumpa kila aina ya sifa mpaka mkasahaulika kama nyie ni wapinzani.

Huku mkiwa na matumaini nae makubwa kwa kutaka apewe muda zaidi mkiamini atafanya kila mtakalo, na kuwalaumu wale walioanza kuonesha kutomuamini.

Sasa kwasababu ameanza kwenda kinyume na yale matarajio yenu ya awali, ndio mmeanza kumgeuka, kimsingi mlichokuwa mnakitegemea toka kwa kiongozi wa CCM ilikuwa ni ndoto tu, sasa naona wengi wenu ndio mnaanza kuamka, mnamlaumu mpaka kwa uteuzi wa ma-DC aliofanya kama vile hizo nafasi zimewahi kuwa na manufaa kwa upinzani.

Mmmhh, imebidi nicheke tu. Lawama kwamba huyo mama anasifiwa naona ni too general. Ni kweli kuna baadhi ya watu wanamsifia kwenye baadhi ya maeneo na wala sio kwa ubora. Sehemu kadhaa anazosifiwa ni zile za wazi kabisa alizokuwa anafanya vibaya Magufuli kama kuzuia shughuli za kisiasa, watu kutekwa hovyo hovyo kwa sababu za kisiasa, kuchukua hatua kwa watu waovu hata kama sio wote mfano Sabaya. Sisi wengine tunangoja siku 100 tutoe tathmini ya awali ya awali ya utawala wake, ambapo tathmini yetu itakuwa ni kwenye uga wa kisiasa, kiuchumi, kijamii nk. Hili umeshindwa kulielewa?
 
Mimi mtu akiongelea katiba hua aiamini chochote maana katiba ni sheria,na watu ni mamilion,ukibadirisha katiba siyo wote wataikubali hata kidogo,kila mtu ana hulka yake,matakwa na mapendekezo anayoona yeye ndiyo sawa kwake,hivyo basi katiba si chochote kukibadirisha labda kukiheshimu kilichopo, waTanzania wengi sana hua wanafuata uvumi tu kama uvumi wa wanasiasa na wana harakati,mTanzania akisikia neno kijiwe kimoja ananyanyuka na hilo neno anaenda nalo kijiwe kingine bila kua na uhakika nalo wala kulithibitisha,swala la katiba kila mTanzania utamsikia anasema katiba haifai,ukimuuliza mtu katiba unataka uweje na ya sasa ina mapungufu gani,yaani mTanzania anayeweza kuelezea hilo ni wachache sana,wengi utamsikia tu anaanza kua mkali na anaanza kukuita wewe ni CCM[emoji16][emoji16]...katiba kuifanya kua nyingine sioni sababu ya msingi maana inaweza kuumiza wengine pia na kisha kuanza kulalamika tu tena maana mi nawajua sana waTanzania.

Daaa Mkuu maelezo yako ni mengi na mazuri, ila nimecheka hapo uliposema watanzania wengi wanafuata mkumbo kuhusu katiba mpya, na wala hawawezi kudhibitishamapungufu ya katiba ya sasa. Kwahiyo kwa mtazamo wako unataka watu wote wanaotaka katiba mpya waufahamu udhaifu wa katiba hii, ndio watake hiyo nyingine? Yaani ubovu wa katiba hii ni mpaka watu wote waione. Unaposema kuwa hiyo katiba nyingine inaweza kuja na kuwaumiza wengine, unaweza kusema kifungu chochote kilichoko kwenye rasimu ya Warioba ambacho kimewekwa kwa ajili ya kuwaumiza wengine? Kwani ukikosa hoja za utetezi wa jambo ni lazima upotoshe?
 
Bams na tindo ahsanteni sana. Hotuba ya Mama siku ya kuapishwa kwake ilinipa matumaini makubwa sana na nakuamini sasa tutakuwa na Demokrasi ya kweli. Baada ya hapo kauli na matendo yake mbali mbali ikiwemo "Mtasubiri sana kuhusu Katiba mpya" na "Mimi na mwendazake ni KITU KIMOJA" pia ukimya kuhusu uwepo wa wale COVID-19 kule Bungeni. Yapo aliyoyafanya ambayo nayafurahia lakini anayafanya nusu nusu na kubwa kuliko lote ambalo ndiyo tunalitaka sana la kuoata Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wa Octover 26, 2025 sioni nia yake ya kutimiza hilo. Kwa hiyo mimi sina imani naye tena katika kuiongiza nchi kwenye demokeasia ya kweli.
 
Bams na tindo ahsanteni sana. Hotuba ya Mama siku ya kuapishwa kwake ilinipa matumaini makubwa sana na nakuamini sasa tutakuwa na Demokrasi ya kweli. Baada ya hapo kauli na matendo yake mbali mbali ikiwemo "Mtasubiri sana kuhusu Katiba mpya" na "Mimi na mwendazake ni KITU KIMOJA" pia ukimya kuhusu uwepo wa wale COVID-19 kule Bungeni. Yapo aliyoyafanya ambayo nayafurahia lakini anayafanya nusu nusu na kubwa kuliko lote ambalo ndiyo tunalitaka sana la kuoata Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wa Octover 26, 2025 sioni nia yake ya kutimiza hilo. Kwa hiyo mimi sina imani naye tena katika kuiongiza nchi kwenye demokeasia ya kweli.

Asante mkuu, mimi pia ukiacha kuwa hana siasa za kidhalimu kama za mtangulizi wake, sioni nguvu yake kwenye suala la mageuzi ya mifumo ya utawala. Kwenye maeneo mengine namuona ni wa kawaida sana.
 
Mmmhh, imebidi nicheke tu. Lawama kwamba huyo mama anasifiwa naona ni too general. Ni kweli kuna baadhi ya watu wanamsifia kwenye baadhi ya maeneo na wala sio kwa ubora. Sehemu kadhaa anazosifiwa ni zile za wazi kabisa alizokuwa anafanya vibaya Magufuli kama kuzuia shughuli za kisiasa, watu kutekwa hovyo hovyo kwa sababu za kisiasa, kuchukua hatua kwa watu waovu hata kama sio wote mfano Sabaya. Sisi wengine tunangoja siku 100 tutoe tathmini ya awali ya awali ya utawala wake, ambapo tathmini yetu itakuwa ni kwenye uga wa kisiasa, kiuchumi, kijamii nk. Hili umeshindwa kulielewa?
Wale maafisa wawili waliokuwa wanapigania Katiba Mpya walitekwa chini ya huu utawala mpya, na sijui kama lile tukio ndio litakuwa la mwisho au litamhusu kila atakaefungua mdomo kuidai Katiba ambayo bosi wa nchi keshasema isubiri kwanza.

Kwa muktadha huu, kwangu sikuona sababu ya kusubiri siku mia moja, kila ovu lazima lilaaniwe instantly, hakuna sababu ya kusubiri siku 100 zifike huku wengine wakiwa wanaumia.
 
Wale maafisa wawili waliokuwa wanapigania Katiba Mpya walitekwa chini ya huu utawala mpya, na sijui kama lile tukio ndio litakuwa la mwisho au litamhusu kila atakaefungua mdomo kuidai Katiba ambayo bosi wa nchi keshasema isubiri kwanza.

Kwa muktadha huu, kwangu sikuona sababu ya kusubiri siku mia moja, kila ovu lazima lilaaniwe instantly, hakuna sababu ya kusubiri siku 100 zifike huku wengine wakiwa wanaumia.

Siku 100 ni standard, sio lazima ziwe kapimo cha kila mtu. Ndani ya siku 100 sio kipimo, bali ni kutoa mwenendo halisi wa utawala wake kwa ujumla, kwa kuangalia mwanzo wake. Ama huo utawala wake ni eneo moja tu la katiba mpya?
 
Pole mjane,utapata mwingne ucjal
Ongea kilichopo hapa we pumbavu,hata ukimchukia vp jiwe alikua rais hasa.
Hivi nyie mafala mlijuaje kuna JF.
Zamani tunajadili mada haswa hapa zinazoeleweka.
Nyie ngedere sijui mmetoka wapi mnaongea upuuzi tu
 
Suala la katiba co jepesi kama tunavyofikiria,hili suala akilianzisha anaweza jikuta hata nafac aliyokuwepo anatolewa,tukumbuke mzee wa msoga kilichomkuta,kwa upande wangu suala kubwa sasa hv ni kudai tume huru.
Asante mkuu, mimi pia ukiacha kuwa hana siasa za kidhalimu kama za mtangulizi wake, sioni nguvu yake kwenye suala la mageuzi ya mifumo ya utawala. Kwenye maeneo mengine namuona ni wa kawaida sana.
 
Back
Top Bottom