Utekaji na uuaji unaofanyika Tanzania ni sawa na kilichofanywa na vyombo vya dola Uganda dhidi ya wananchi wakati wa Idd Amin Dada

Utekaji na uuaji unaofanyika Tanzania ni sawa na kilichofanywa na vyombo vya dola Uganda dhidi ya wananchi wakati wa Idd Amin Dada

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kwa wale wanaojua historia ya Uganda, watakuambia wazi kwamba utekaji na uuaji unaofanyika hivi sasa nchini Tanzania ni sawa kabisa na vyombo vya dola na usalama vilivyowafanyia wananchi wa Uganda wakati wa utawala wa dikteta Idd Amin Dada wa Uganda.

Polisi na chombo kilichoitwa State Research Bureau (SRB) of Uganda, ambacho kilikuwa ni sawa na TISS ya Tanzania, walifanya utekaji na uuaji wa wananchi wa Uganda walioonekana kupinga hadharani au kisiri utawala wa dhalimu Idd Amin Dada. Mara nyingi waliwavamia wananchi wakiwa ofisini, mitaani na hata nyumbani, kuwaingiza kwenye magari kwa nguvu na kutokomea nao. Waliwaua na kuwatupa msituni au mitoni, pamoja na Mto Kagera.

Polisi na SRB wa Uganda walifanya haya mbele za watu, na wananchi walikuwa wameingiwa uoga hawakuweza kufanya kitu wala kutoa msaada wowote pale ambapo waliona wananchi wenzao wakitekwa, japo walijua wanaenda kuuawa!

Kama inavyofanyika Tanzania, Polisi wa Uganda wakati huo walitoa matamko ya juu juu tu kuhusu watu kutekwa, na Raisi Idd Amin aliwasifu SBR na Polisi kwa kazi nzuri ya kusimamia amani na utulivu nchini Uganda, kama vile tu ambavyo hapa Tanzania tumesikia jeshi letu la Polisi likisifiwa kwa kazi nzuri katika kipindi hiki kigumu cha utekaji na uuaji.

Na utekaji na uuaji nchini Uganda ulianza taratibu, lakini kadiri muda ulivyozidi kwenda, Polisi watekaji na SRB (sawa na TISS) hawakuogopa tena. Walifanya utekaji huu waziwazi kabisa. Kumekuwa na kila dalili kwamba hata hapa Tanzania tunaona watekaji wakizidi kuwa na ujasiri wa kuteka watu bila kuogopa, hata mchana kweupe!

Ilifikia mahali ambapo waliotekwa na kuuawa nchini Uganda walitia ndani raia, wanasiasa waliopinga utawala wa Idd Amin, viongozi wa dini, viongozi wa taasisi za serikali nk.

Utekaji na uuaji Uganda ulikuja kukoma baada ya vita vya Kagera pale ambapo majeshi ya Tanzania yalimwondoa Idd Amin Uganda. Ndio maana hata sasa hapa nchini wananchi wameanza kuona kwamba pengine tunahitaji nguvu kama hiyo ili kukomesha utekaji na uuaji ambao asilimia kubwa sana ya wananchi nchini wanauhusisha na vyombo vya dola dhidi ya watu wanaoonekana kuwa na upinzani dhidi ya utawala serikali iliyopo madarakani
 
The State Research Bureau (SRB), initially the State Research Centre (SRC), was a Ugandan intelligence agency. Active from 1971 until 1979, it served as a secret police organisation for President Idi Amin's regime. The SRB retained numerous agents and maintained a wide network of informants.

The SRB recruited a substantial number of Rwandan immigrants, and attractive Rwandan Tutsi women were used as undercover operatives as well as stationed at airports, banks, hotels, restaurants, government offices, hospitals, and locations near Uganda's borders. Empowered by a sweeping February 1971 decree which gave state agents wide latitude to act, the SRB tortured and executed many suspected dissidents, provoking international outrage. Agents frequently abducted people by forcing them into the trunk of a car and driving off. For its role in state repression and killings, the SRB came to be derisively known among the Ugandan population as the "State Research Butchery".

In June 1974, in response to criticism of his regime and specifically accusations of numerous "disappearances" of persons in Uganda, Amin established a commission of inquiry to investigate abuses of state authority. The commission concluded that the SRB and another state security agency, the Public Safety Unit, were responsible for most of the disappearances. The abuses committed by the SRB was known among personnel of various international embassies in Kampala, though they generally did not publicly criticise it.

SRB agents frequently abducted people by forcing them into the trunk of a car and driving off. The SRB headquarters became notorious for the human rights abuses committed within its walls; Venter described it as "one-way trip to hell" and ex-rebel Paul Oryema Opobo called it a "place of no return". Prisoners were "flayed, beaten, suffocated, tortured or electrocuted for hours at a stretch" before being executed. Venter referenced one prisoner who had "his eyes gouged out with a screwdriver and his genitals removed with a pair of garden shears." Dead prisoners were mostly dumped in a forest near Kampala.

The question is, are we witnessing copycats in Tanzania? Coincidentally, President Samia has been heard to form a commission of inquiry over the abduction and killing of a senior opposition leader. Its report was never made public.
 
Namkumbuka marehemu Anglican Archi bishop Luwuum wa Uganda alivyouawa na Amin huko Uganda
 
Namkumbuka marehemu Anglican Archi bishop Luwuum wa Uganda alivyouawa na Amin huko Uganda
Waliteka na kuua wengi sana. Tunaenda huko pia, kama hili litaruhusiwa kuendelea
 
Mimi nawaomba wenye mamlaka kuhakikisha nchi yetu haielekei huko. Kwa wale walioshuhudia kipindi hiki kibaya sana kwenye historia ya Uganda, nadhani kwa sasa ni watu wazima sana, ni mashahidi kuwa nchi yetu haistahili hata kidogo haya tunayoyashuhudia.

Wasisahau kuwa mamlaka haya wamepewa na wananchi ambao ni lazima walinde maisha yao na mali zao, hata kama kuna manung'uniko kuwa mahali pengine mamlaka haya yameporwa kutoka mikononi mwa wananchi, ni ukweli usiopingika kuwa wenye mamlaka wanayo nafasi ya kuchukua hatua kuzuia nchi yetu isielekee huko. Jamani siasa usiwe uadui.

Tuulinde uhai wa kila mmoja wetu.
 
Back
Top Bottom