Utengenezaji "White Sauce"

Utengenezaji "White Sauce"

Jade_

Senior Member
Joined
Apr 19, 2015
Posts
122
Reaction score
214
Habari zenu, natumai mpo salama. Mara ya mwisho nilipika pilau na leo napika white sauce inayosindikiza pilau au chakula kingine chochote kinachohitaji mchuzi.

Kama kawaida ukitaka kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.



Turudi kwenye mapishi yetu.

Nilianza kupika white sauce kwa kuyeyusha siagi kwenye sufuria ya moto jikoni. Baada ya siagi kuyeyuka kabisa nikakorogea unga wa ngano taratibu (unaweza ukatumia unga wa mahindi), halafu nikakorogea maziwa.

Pic 01.jpg

Siagi imeyeyuka

Pic 02.jpg

Nikikorogea unga wa ngano kwenye siagi

Pic 03.jpg

Nikikorogea maziwa

Baada ya hapo nikakorogea maji ya vuguvugu taratibu, na nikaendelea kukoroga mpaka mabonge yote yakaisha na nikaacha mchanganyiko uendelee kuchemka mpaka unga ukaiva na maji yakapungua mchuzi ukawa mzito nikauweka pembeni.

Pic 04.jpg

Nikikorogea maji ya vuguvugu

Pic 05.jpg

Nikiendelea kukoroga mabonge yaishe

Pic 06.jpg

Mchanganyiko ukiwa jikoni unachemka

Kwenye sufuria nyingine nilikaanga kitunguu kwenye mafuta ya mzaituni (olive oil). Vitunguu vilivyolainika niliweka pilipili manga nikaendelea kukaanga kidogo. Baada ya hapo nikakorogea ule mchanganyiko wetu wa mwanzo nikaucha uchemke kidogo.

Pic 07.jpg

Nikikaanga kitunguu kwenye olive oil

Pic 08.jpg

Nikikaangia pilipili manga kwenye vitunguu

Pic 09.jpg

Nikikorogea mchanganyiko wa mwanzo kwenye vitunguu

Pic 10.jpg

Mchanganyiko ukiwa jikoni unachemka

Kufikia hapo white sauce ilikuwa tayari na nikaiweka kwenye kibakuli kidogo ili kuila na pilau. Unaweza ukaweka viungo vingine mbalimbali kwenye white sauce ili iwe na ladha unayoipenda wewe.

Pic 11.jpg

Nikiweka white sauce kwenye bakuli

Pic 12.jpg

White sauce kwa ukaribu
 
Habari zenu, natumai mpo salama. Mara ya mwisho nilipika pilau na leo napika white sauce inayosindikiza pilau au chakula kingine chochote kinachohitaji mchuzi.


White sauce kwa ukaribu
Naonaga kwenye picha insta, nimeongeza kitu.
 
Kuna Mgahawa niliwekewa sijui walitia viungo vingi, nilipoteza funguo siku 3 🥲
 
Kuna Mgahawa niliwekewa sijui walitia viungo vingi, nilipoteza funguo siku 3 🥲
Nimecheka mpaka nimepaliwa. Pole sana mkuu. Migahawa mingi vyakula vyao... mhmmm...Mungu anajua.
 
Back
Top Bottom