Jade_
Senior Member
- Apr 19, 2015
- 122
- 214
Habari zenu, natumai mpo salama. Mara ya mwisho nilipika pilau na leo napika white sauce inayosindikiza pilau au chakula kingine chochote kinachohitaji mchuzi.
Kama kawaida ukitaka kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.
Turudi kwenye mapishi yetu.
Nilianza kupika white sauce kwa kuyeyusha siagi kwenye sufuria ya moto jikoni. Baada ya siagi kuyeyuka kabisa nikakorogea unga wa ngano taratibu (unaweza ukatumia unga wa mahindi), halafu nikakorogea maziwa.
Siagi imeyeyuka
Nikikorogea unga wa ngano kwenye siagi
Nikikorogea maziwa
Baada ya hapo nikakorogea maji ya vuguvugu taratibu, na nikaendelea kukoroga mpaka mabonge yote yakaisha na nikaacha mchanganyiko uendelee kuchemka mpaka unga ukaiva na maji yakapungua mchuzi ukawa mzito nikauweka pembeni.
Nikikorogea maji ya vuguvugu
Nikiendelea kukoroga mabonge yaishe
Mchanganyiko ukiwa jikoni unachemka
Kwenye sufuria nyingine nilikaanga kitunguu kwenye mafuta ya mzaituni (olive oil). Vitunguu vilivyolainika niliweka pilipili manga nikaendelea kukaanga kidogo. Baada ya hapo nikakorogea ule mchanganyiko wetu wa mwanzo nikaucha uchemke kidogo.
Nikikaanga kitunguu kwenye olive oil
Nikikaangia pilipili manga kwenye vitunguu
Nikikorogea mchanganyiko wa mwanzo kwenye vitunguu
Mchanganyiko ukiwa jikoni unachemka
Kufikia hapo white sauce ilikuwa tayari na nikaiweka kwenye kibakuli kidogo ili kuila na pilau. Unaweza ukaweka viungo vingine mbalimbali kwenye white sauce ili iwe na ladha unayoipenda wewe.
Nikiweka white sauce kwenye bakuli
White sauce kwa ukaribu
Kama kawaida ukitaka kuangalia video ya haya mapishi unaweza kuangalia hapo chini. Ukipenda unaweza “kuilike” hiyo video, “kusubscribe” kwenye channel yangu na kuangalia video nyingine.
Turudi kwenye mapishi yetu.
Nilianza kupika white sauce kwa kuyeyusha siagi kwenye sufuria ya moto jikoni. Baada ya siagi kuyeyuka kabisa nikakorogea unga wa ngano taratibu (unaweza ukatumia unga wa mahindi), halafu nikakorogea maziwa.
Siagi imeyeyuka
Nikikorogea unga wa ngano kwenye siagi
Nikikorogea maziwa
Baada ya hapo nikakorogea maji ya vuguvugu taratibu, na nikaendelea kukoroga mpaka mabonge yote yakaisha na nikaacha mchanganyiko uendelee kuchemka mpaka unga ukaiva na maji yakapungua mchuzi ukawa mzito nikauweka pembeni.
Nikikorogea maji ya vuguvugu
Nikiendelea kukoroga mabonge yaishe
Mchanganyiko ukiwa jikoni unachemka
Kwenye sufuria nyingine nilikaanga kitunguu kwenye mafuta ya mzaituni (olive oil). Vitunguu vilivyolainika niliweka pilipili manga nikaendelea kukaanga kidogo. Baada ya hapo nikakorogea ule mchanganyiko wetu wa mwanzo nikaucha uchemke kidogo.
Nikikaanga kitunguu kwenye olive oil
Nikikaangia pilipili manga kwenye vitunguu
Nikikorogea mchanganyiko wa mwanzo kwenye vitunguu
Mchanganyiko ukiwa jikoni unachemka
Kufikia hapo white sauce ilikuwa tayari na nikaiweka kwenye kibakuli kidogo ili kuila na pilau. Unaweza ukaweka viungo vingine mbalimbali kwenye white sauce ili iwe na ladha unayoipenda wewe.
Nikiweka white sauce kwenye bakuli
White sauce kwa ukaribu