UTEUZI: Jaffar Haniu ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu); amrithi Gerson Msigwa

Kwa nini msemaji mkuu wa serikali awe tofauti na mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais, Ikulu?
Wa ikulu anakuwa msemaji wa raisi pekee, wakati wa maelezo ni wa serikali. Taarifa ambazo sio za ikulu ndio zitatolewa msemaji wa serikali.
 
State house ndio government yenyewe
 
Msigwa byebye, nadhani hii ndio itakuwa taarifa yako ya mwisho kabisa kuitoa kama Mkurugenzi Wa Mawasiliano Ikulu.
Lakini ndio kapewa cheo kikubwa,kuwa msemaji wa serikali ni zaidi ya kuwa mkurugenzi wa habari ikulu mkuu. Msigwa atakuwepo sana.
 
Hawa wote ni Watanzania?? Au kuna Mrundi hapo??
 
State house ndio government yenyewe
Hapana. State house sio goverment. Sitaki kutoa lugha mbaya au kukukosea heshima mkuu ila ata watoto wa sekondari au primary wanaosoma somo la 'civics' ukienda kuwauliza tofauti ya 'ikulu' na 'serikali' watakupa majibu mujarabu.
 
Mama yenu huyo,iko siku na yeye atajitengua mwenyewe
 
Achana na civics ya sekondari, huko ni nadharia tu, Hapa Tanzania ikulu ndio serikali yenyewe.
Hapana. State house sio goverment. Sitaki kutoa lugha mbaya au kukukosea heshima mkuu ila ata watoto wa sekondari au primary wanaosoma somo la 'civics' ukienda kuwauliza tofauti ya 'ikulu' na 'serikali' watakupa majibu mujarabu.
 
Achana na civics ya sekondari, huko ni nadharia tu, Hapa Tanzania ikulu ndio serikali yenyewe.
Mwendazake aliiharibu sana hii nchi. Hakuna mgawanyo wa majukumu mpaka imefikia hatua ya watu kuona ikulu na serikali ni kitu kimoja. Siku zote aliisigina Katiba na kudai kuwa muhimili wake umejichimbia chini zaid maana yake yeye ndiye kila kitu. Angeendelea kubaki kwa miaka ya mbele zaidi watu wangeenda kusahau kama bunge na mahakama ni mihimili inayojitegemea.
Hakika huyu mama ana kazi kubwa sana ya kurudisha mambo katika uhalisia wake na kuongoza nchi katika misingi ya katiba na demokrasia maana tulikua tunaelekea pabaya sana kama taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…