Uteuzi Juni 15, 2024: Mobhare Matinyi, aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali apangiwa majukumu mengine, nafasi yake yachukuliwa na Thobias Makoba

Uteuzi Juni 15, 2024: Mobhare Matinyi, aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali apangiwa majukumu mengine, nafasi yake yachukuliwa na Thobias Makoba

Playing chess need a competent head,never out shine your master n adhore the rules once you enter the house you suppose to remove your shoes.

Mwalimu na Mwanafunzi wake are in a serious war now the last emperor vs the lord rings who will conquer the Throne?

Let wait n see
DS vs DDS🇹🇿
So the desert storm is real
 
Consistency kwenye utendaji inatoka wapi sasa kama kila siku tunateua na kutengua.

Matarijio unayotoa wapi wakati unarotate watu wale wale kutoka huku unapeleka kule.

Incompetency ni Incompetency tu hakuna namna nyingine.
Unemteua mtu ukitarajia ufanisi kiasi Fulani,dalili ya huo ufanisi hakuna,umuache tu!?..tengua,teua mwingine,huu siyo wakati wa Nyerere,mtu anakalia kiti toka uko la kwanza mpaka la Saba,akiboronga anahamishwa
 
Unemteua mtu ukitarajia ufanisi kiasi Fulani,dalili ya huo ufanisi hakuna,umuache tu!?..tengua,teua mwingine,huu siyo wakati wa Nyerere,mtu anakalia kiti toka uko la kwanza mpaka la Saba,akiboronga anahamishwa
Uteuzi siyo kucheza kamali, kama hujui. Mtu anateuliwa kwenye nafasi kutokana na vigezo vinavyojulikana, siyo kwa "matarajio".

Kwani hawa "hawahamishwi", au hata hujui unacho andika?
 
Playing chess need a competent head,never out shine your master n adhore the rules once you enter the house you suppose to remove your shoes.

Mwalimu na Mwanafunzi wake are in a serious war now the last emperor vs the lord rings who will conquer the Throne?

Let wait n see
DS vs DDS🇹🇿
Leta maneno 😁
 
View attachment 3018303
Rais Samia Suluhu Hassan

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, viongozi walioteuliwa ni kama ifuatavyo:

i Amemteua Balozi Dkt. John Stephen Simbachawene kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda na Biashara. Kabla ya uteuzi, Balozi Dkt. Simbachawene alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais - Ikulu.

ii. Amemteua Bw. Nkoba Eliezer Mabula kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii anayeshughulikia utalii. Kabla ya uteuzi, Bw. Mabula alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais - Ikulu.

Aidha, CP. Benedict Wakulyamba atakuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii anayeshughulikia maliasili.

iii. Amemteua Dkt. Habib Gallus Kambanga kuwa Balozi. Kabla ya uteuzi, Dkt. Kambanga alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais - Ikulu.

iv. Amemteua Bw. Thobias Makoba kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali. Kabla ya uteuzi, Bw. Makoba alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Msajili wa Hazina.
Bw. Makoba anachukua nafasi ya Bw. Mabhare Matinyi ambaye amepangiwa majukumu mengine.

V. Amemteua Bw. Ally Rajab Mketo kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Bukombe. Kabla ya uteuzi, Bw. Mketo alikuwa Afisa Tawala Mwandamizi, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bukombe. Bw. Mketo anachukua nafasi ya Bw. Onesmo Kisoka ambaye amestaafu.

vi. Amemteua Jaji Dkt. Mary Caroline Levira kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto. Jaji Dkt. Levira ni Jaji wa Mahakama ya Rufani. Jaji Dkt. Levira anachukua nafasi ya Jaji Dkt. Gerald Ndika ambaye amemaliza muda wake.

vii. Amemteua Dkt. Leonard Douglas Akwilapo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA). Dkt. Akwilapo ni Katibu Mkuu Mstaafu na Mhadhiri Mwandamizi, Kikuu Kikuu cha Dodoma. Dkt. Akwilapo anachukua nafasi ya Prof. Maurice Mbago ambaye amemaliza muda wake. Amemteua Dkt. Noel Eusebius Mbonde kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Utawala.

viii. ya Chuo cha Ufundi Arusha. Dkt. Mbonde ni Mkurugenzi Mstafu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.


Naona Ikulu ina pigwa deki
 
Back
Top Bottom