Uteuzi wa Afande Ramadhani Kingai kuwa DCI (Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai). Je, Rais Samia amepotoshwa?

Uteuzi wa Afande Ramadhani Kingai kuwa DCI (Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai). Je, Rais Samia amepotoshwa?

seedfarm

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2020
Posts
260
Reaction score
2,655
Kwanini kama Taifa tunarudia makosa ya kuteua watu wenye makando kando kama Afande Ramadhani Kingai? Huyu mtu kwa sasa anafahamika na kila Raia kwa matendo yake yaliyojidhihirisha pale Mahakamani wakati wa kesi ya Mbowe

Je, tunasubiri afanye ukatili na unyama wa kiasi gani kwenye hili Taifa?

Tulishajifunza wakati wa JPM umuhimu wa vetting ya viongozi kwa yaliyotokea. Je, bado tunaendelea kujifunza.

Afande Kingai hakupaswa kupewa nafasi ya DCI hata kidogo, Imani ya Raia kwa huyu mtu ni ndogo sana, Wakati wa kesi ya Mbowe huyu alihusishwa na utesaji na utekaji, Na hata majibu yake mahakamani alijichanganya sana kuhusu kuwahamisha watuhumiwa tokea kituo kimoja cha polisi kwenda kingine na malengo yake kuhusu utesaji

Uteuzi wa Afande Ramadhani Kingai kuwa Mkurugenzi wa makosa ya jinai unaligawa Taifa ambalo Rais Samia alikuwa anafanya jitihada za kuliunganisha kwa maridhiano

Kwenye kesi ya Mbowe pale mahakamani, Afande Kingai alikuwa shahidi mkuu upande wa jamhuri na ushahidi wake alioutoa pale mahakamani wa kuwanunulia watuhumiwa Mo energy ikawa mwanzo wa watu kuamini huyu Bwana ameshiriki Katika kesi ya mchongo kuanzia kudraft mpaka kupeleka mahakamani.

Afande Kingai alishindwa kujibu maswali ya mawakili wa utetezi hata moja na hata maswali yaliyohusiana na kitendea kazi chake ya General Orders of police (PGO) alionekana haelewi pale Mahakama ya uhujumu Uchumi.

Ushahidi wa Afande Kingai ambaye alikuwa Shahidi mkuu ulileta mkanganyiko pale Mahakama ya Uhujumu Uchumi na ndio ukawa mwanzo wa watu kufahamu siri ya kesi ya akina Mbowe pamoja na Kikosi kazi maalum kilichojumuisha Afande Goodluck

Maswali ya kujiuliza sisi kama Raia wa nchi hii:

Unawezaje kumpa mtu nafasi ya DCI wakati umma wa Watanzania wanafahamu huyu mtu amechafuka?

Je, huu ndio mwanzo wa watu kubambikiwa kesi za mauaji hapa nchini?

Je, uteuzi huu Bwana Kingai sio ni mwanzo wa kufumua madonda ambayo Rais Samia alishaanza kuyaponya?

Moja ya watu kuzidi kudai Katiba Mpya ni kutokana na uteuzi wa watu aina ya Afande Kingai, Tungekuwa na tume maalum ya kuchuja na kuteua aina ya watu kama Afande Kingai kama Rasimu ya Jaji Warioba alivyopendekeza tusingekuwa na utata.
 
MH Rais mama yetu Samia Suluhu Hassan kwakweli japo jeshi Zima la polisi limekuwa bovu Sanaa lakini Kuna wachache ambao Wana hofu ya Mungu, na Taasisi kubwa na ya muhimu kama hili jeshi halitakiwi kuwa na kiongozi asiyetoa Haki au Mwongo.

Kama mama una nia kweli ya kulirekebisha watu kama KINGAI hawakupaswa kupewa ofisi kubwa maana kwa UONGO na uonevu aliowafanyia watu akiwa ngazi za chini akiwa Ngazi uliyompa atakuwa mbaya zaidi.

Sio polisi mwenye maadili hasa msingiziaji mporaji wa haki za watu mtesaji ana damu kwenye vganja vyake.

Jiepushe nae, HAWEZI kutenda Haki tunakuomba Unda na kulisuka upya Hili jeshi lililopoteza maana ya jeshi la kusimamia Haki.

Kwa hili nasema WAMBURA SAWA LAKINI SIO KINGAI, HAPANA.
 
Yaani Wankyo Chali Tena Anakwenda Bila Cheo
 
Moja ya watu kuzidi kudai katiba mpya ni kutokana na uteuzi wa watu aina ya Afande Kingai, Tungekuwa na tume maalum ya kuchuja na kuteua aina ya watu kama Afande Kingai kama Rasimu ya Jaji warioba alivyopendekeza tusingekuwa na utata
Uzuri wa Afande Kingai ali rahisisha kesi ya Mbowe kuwa nyepesi.

Ila kwa zile harakati za Kingai, Azizi, Mahita, minja na wengine utamkubali Kingai alikuwa Staring hatari🤣🤣
 
Afande Kingai hakupaswa kupewa nafasi ya DCI hata kidogo, Imani ya Raia kwa huyu mtu ni ndogo sana, Wakati wa kesi ya Mbowe huyu alihusishwa na utesaji na utekaji, Na hata majibu yake mahakamani alijichanganya sana kuhusu kuwahamisha watuhumiwa tokea kituo kimoja cha polisi kwenda kingine na malengo yake kuhusu utesaji

*ndio maana shavu. No smart people allowed!
 
Sasa kama Kiongozi anateua wasaifixi wake, na hao wasaifixi wanampotosha, Bado tu hauoni tatizo liko wapi? Kumbuka anavitendea kazi na Kila kitu anachohitaji kufanya vetting. Isitoshe anauwezo hata kutengua uteuzi wake skibaini Kuna dosari, Kwa baadhi ya mambo, nafikiri si sawa kusingizia wasaifixi.

Mwisho, viongozi wameshatujilia, likitokea jambo, tutalalamikaa Kisha tunanyamaza maisha yanaendelea. Kelele zetu ni kama wameshazixoea " upepo tu utapita" ( Ze Kwere)
 
Afande Kingai hakupaswa kupewa nafasi ya DCI hata kidogo, Imani ya Raia kwa huyu mtu ni ndogo sana, Wakati wa kesi ya Mbowe huyu alihusishwa na utesaji na utekaji, Na hata majibu yake mahakamani alijichanganya sana kuhusu kuwahamisha watuhumiwa tokea kituo kimoja cha polisi kwenda kingine na malengo yake kuhusu utesaji

*ndio maana shavu.. No smart people allowed!
Kwa uteuzi huu Hangaya kapuyanga sana
 
Afande Kingai hakupaswa kupewa nafasi ya DCI hata kidogo, Imani ya Raia kwa huyu mtu ni ndogo sana, Wakati wa kesi ya Mbowe huyu alihusishwa na utesaji na utekaji, Na hata majibu yake mahakamani alijichanganya sana kuhusu kuwahamisha watuhumiwa tokea kituo kimoja cha polisi kwenda kingine na malengo yake kuhusu utesaji

*ndio maana shavu.. No smart people allowed!
Mama hana makuu huenda hajui asubuhi anaenda kumuapisha nani.
 
Back
Top Bottom