Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 24,665
- 25,388
Kwanza umefanyika kimkakati, lakini pia umefanyika kwa muda muafaka kama surprise, lakini kwa kuzingatia sheria na katiba ya CCM, bila kuathiri kwa namna yoyote ile sheria na katiba ya nchi kuhusiana na masuala ya uteuzi wa wagombea uongozi na uchaguzi wenyewe.
Azimio la kumuidhinisha Dr Emmanuel Nchimbi kama mgombea mwenza wa urasi wa Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania, lilitolewa hadharani na mkutano mkuu maalumu wa CCM taifa, na kuidhinishwa kwa kauli moja za wajumbe wa mkutano mkuu huo maalumu, kwa uthibitisho wa kura za ndio za wajumbe wote wa mkutano mkuu wa Taifa waliohudhuria mkutano ule.
Aina na namna ya uteuzi wa Dr.Emanuel Nchimbi ulivyo fanyika, kwanza imedhibiti makundi ndani ya chama na kuifanya CCM kua moja, yenye nguvu na imara zaidi.
Lakini pia hili limedhihirsha umadhubuti wa CCM na thibitishia ulimwengu kwamba CCM ni jabali la siasa za Tanzania na Africa kwa ujumla.
Umadhubuti na umahiri wa Dr.Samia Suluhu Hassan kiutendaji, utampatia uzoefu na uthubutu wa kutosha Dr.Emmanuel Nchimbi kushika hatamu na dhamana ya uongozi wa kitaifa kwa wakati muafaka.
Kama ilivyo mipango ya maendeleo ya vipindi vifupi, vya kati na vipindi virefu, Chama Cha Mapinduzi CCM, kimetoa uelekeo wa uongozi wa kisiasa waTaifa letu kwa kipindi cha miaka 15 ijayo utakuaje.
Na mpango wa usimamizi wa maendeleo na mustakabali wa uongozi wa Taifa letu ni kwamba, 2025-2030 ni Dr.Samia Suluhu Hassan, na kisha kwa Neema na Baraka za Mungu 2030-2040 ni Dr. Emmanuel Nchimbi.
Una maoni gani my friends, ladies and gentlemen?π
Mungu Ibarki Tanzania
Azimio la kumuidhinisha Dr Emmanuel Nchimbi kama mgombea mwenza wa urasi wa Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania, lilitolewa hadharani na mkutano mkuu maalumu wa CCM taifa, na kuidhinishwa kwa kauli moja za wajumbe wa mkutano mkuu huo maalumu, kwa uthibitisho wa kura za ndio za wajumbe wote wa mkutano mkuu wa Taifa waliohudhuria mkutano ule.
Aina na namna ya uteuzi wa Dr.Emanuel Nchimbi ulivyo fanyika, kwanza imedhibiti makundi ndani ya chama na kuifanya CCM kua moja, yenye nguvu na imara zaidi.
Lakini pia hili limedhihirsha umadhubuti wa CCM na thibitishia ulimwengu kwamba CCM ni jabali la siasa za Tanzania na Africa kwa ujumla.
Umadhubuti na umahiri wa Dr.Samia Suluhu Hassan kiutendaji, utampatia uzoefu na uthubutu wa kutosha Dr.Emmanuel Nchimbi kushika hatamu na dhamana ya uongozi wa kitaifa kwa wakati muafaka.
Kama ilivyo mipango ya maendeleo ya vipindi vifupi, vya kati na vipindi virefu, Chama Cha Mapinduzi CCM, kimetoa uelekeo wa uongozi wa kisiasa waTaifa letu kwa kipindi cha miaka 15 ijayo utakuaje.
Na mpango wa usimamizi wa maendeleo na mustakabali wa uongozi wa Taifa letu ni kwamba, 2025-2030 ni Dr.Samia Suluhu Hassan, na kisha kwa Neema na Baraka za Mungu 2030-2040 ni Dr. Emmanuel Nchimbi.
Una maoni gani my friends, ladies and gentlemen?π
Mungu Ibarki Tanzania