Uteuzi wa Dkt. Emanuel Nchimbi kama mgombea mwenza urais wa CCM uchaguzi mkuu wa OCT.2025, ni wa kisayansi katika siasa za kisasa.

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Kwanza umefanyika kimkakati, lakini pia umefanyika kwa muda muafaka kama surprise, lakini kwa kuzingatia sheria na katiba ya CCM, bila kuathiri kwa namna yoyote ile sheria na katiba ya nchi kuhusiana na masuala ya uteuzi wa wagombea uongozi na uchaguzi wenyewe.

Azimio la kumuidhinisha Dr Emmanuel Nchimbi kama mgombea mwenza wa urasi wa Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania, lilitolewa hadharani na mkutano mkuu maalumu wa CCM taifa, na kuidhinishwa kwa kauli moja za wajumbe wa mkutano mkuu huo maalumu, kwa uthibitisho wa kura za ndio za wajumbe wote wa mkutano mkuu wa Taifa waliohudhuria mkutano ule.

Aina na namna ya uteuzi wa Dr.Emanuel Nchimbi ulivyo fanyika, kwanza imedhibiti makundi ndani ya chama na kuifanya CCM kua moja, yenye nguvu na imara zaidi.
Lakini pia hili limedhihirsha umadhubuti wa CCM na thibitishia ulimwengu kwamba CCM ni jabali la siasa za Tanzania na Africa kwa ujumla.

Umadhubuti na umahiri wa Dr.Samia Suluhu Hassan kiutendaji, utampatia uzoefu na uthubutu wa kutosha Dr.Emmanuel Nchimbi kushika hatamu na dhamana ya uongozi wa kitaifa kwa wakati muafaka.

Kama ilivyo mipango ya maendeleo ya vipindi vifupi, vya kati na vipindi virefu, Chama Cha Mapinduzi CCM, kimetoa uelekeo wa uongozi wa kisiasa waTaifa letu kwa kipindi cha miaka 15 ijayo utakuaje.

Na mpango wa usimamizi wa maendeleo na mustakabali wa uongozi wa Taifa letu ni kwamba, 2025-2030 ni Dr.Samia Suluhu Hassan, na kisha kwa Neema na Baraka za Mungu 2030-2040 ni Dr. Emmanuel Nchimbi.

Una maoni gani my friends, ladies and gentlemen?πŸ’

Mungu Ibarki Tanzania
 
TL amewashikiaa chiniiii.....haswaa...mwala huu nginja nginja kibokoooo
 
Wewe chawa kazi yako ni kupokea hela ya kula baada ya machapisho yako ya kipumbavu... uchawa ni fani ya kikumΓ— sana bora hata mtembeza mayai barabarani anaheshimika katika jamii kuliko chawa
 
Ni lzm awe kutoka CCM?
 
Hivi kina Dkt. Sheni unaweza kulinganisha na Nchimbi? Kilichobaki kwa ccm ni maziko tu..chama kimekufa! Believe t soon will see..!
 
Hivi kina Dkt. Sheni unaweza kulinganisha na Nchimbi? Kilichobaki kwa ccm ni maziko tu..chama kimekufa! Believe t soon will see..!
kikwetu kuwaza mauti kwenye mambo muhimu ya msingi tena ya kitaifa ni ushirikina gentleman πŸ’
 
Ni lzm awe kutoka CCM?
kitaalamu,
kwa hazina ya viongozi waandamizi waadilifu waliyonayo kuna kazi kubwa mno kubainisha umahiri wa walio nje ya CCM.

Hata hivyo,
wadau wa JF wako huru kuwaibua na kuwaelezea humu jukwaani πŸ’
 
Hiyo ya kumuandaa nchimbi kuwa rais umetudanganya
sina haja wala sababu hata moja kuwadanganya wadau muhimu na waheshima sana wa JF kuhusu ukweli huo mtupu na bayana dhidi ya huyo mungwana mzalendo ambae pia ni agenda ya Taifa 2030-2040πŸ’
 
Wewe chawa kazi yako ni kupokea hela ya kula baada ya machapisho yako ya kipumbavu... uchawa ni fani ya kikumΓ— sana bora hata mtembeza mayai barabarani anaheshimika katika jamii kuliko chawa
Relax gentleman,
huna haja ya kuporomosha matusi mazito mazito jukwaani mbele ya wadau makini na wa heshima sana wa JF.

na kama huna hoja kaa kimya tu na itapendeza zaidi πŸ’
 
Sukuma gang tumelia saaana,tulijua Biteko atakuwa makamu wa rais,
 
kuzungumzia mauti kikwetu ni ushirikina,
utanisamehe sana kwa hilo gentleman πŸ’
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…